Mhaya
JF-Expert Member
- Aug 20, 2023
- 1,669
- 4,919
Tupeane elimu kidogo, kuna watu wanachanganya mambo. Hapa tufundishane jambo moja. Kitu cha kwanza kabisa watu wanachokichanganya ni kuhusu Ibrahim, wengi wanasema Ibrahim alikuwa Mwarabu, ndugu yangu, nikwambie tu kwamba jamaa hakuwa Mwarabu.
Ibrahim baada ya kuzaa na kijakazi ambaye alikuwa Mwarabu, inamaanisha damu yake ilichanganyika na ya Kiarabu na ndiyo maana tunasema Ishmael ni baba wa Waarabu kwa sababu mama yake alikuwa Mwarabu.
Nchi za Kiarabu ambazo zipo kwenye umoja ni hizi, Algeria, Bahrain, Iraq, Jordan, Kuwait, Djibout, Saudi Arabia, Tunisia, United Arab Emirates, Yemen, Somalia, Sudan, Syria, Comoros, Misri, Maurtania, Qatar na Palestina.
Kwa nini Waarabu wanamchukia Israel? Ni kwa sababu si Mwarabu mwenzao. Na hao ndiyo wa kizazi cha Ibrahim. Kwa hiyo kama ulikuwa unahisi Ibrahim alikuwa Mwarabu, futa hiyo akilini mwako.
Hata Iran sio Waarabu, najua wengine mtakuwa hamlijui hili kwa undani. Miongoni mwa nchi za Kiarabu, Iran hayupo kwa sababu yeye si Mwarabu.
So Israel na Waarabu ni baba mmoja ila mama tofauti. Ibrahim alizaa na Muisrael mwenzake kwa kipindi hicho ilikuwa bado haijaitwa Israel na mtoto wake kuitwa Isaka ila yule aliyezaa na kijakazi ambaye ni Mwarabu anaitwa Ishmael. Tatizo kubwa la vita baina ya Mwarabu na Israel ni hapa.
Kama Israel angekuwa Mwarabu, leo usingesikia vita vinavyoendelea huko. Na mara zote Israel anawaambiaga kwamba nchi zote za Uarabuni ni mali ya Israel na ndiyo maana kila anapokwenda kupiga, anachukua ardhi na kutanua nchi yake.
Israel walipewa nchi ndogo sana wakae baada ya kutawanywa na Adolf Hitler, baada ya kuanza kurudi, wakaitaka nchi yao, lakini kwa bahati mbaya waliwaona Waarabu washajigawia ardhi yao. Walichokifanya ni kuanza kupigana nao.
Kama unakumbuka Umoja wa Mataifa uliingilia kati, ulichukizwa na kitendo cha Israel kuwapiga Waarabu, walichokifanya, wakawapelekea Biblia ambayo kwa nyuma kuna ramani ya Israel tangu enzi za Musa. Wakawaonyesha na kuwaambia kwamba nchi zote za Uarabuni ni Israel, tutakapokuwa wengi, tutaendelea kupiga na kuirudisha nchi yetu.
So jua hili. Ibrahim hakuwa Mwarabu. Musa hakuwa Mwarabu. Suleimani mtoto wa Daudi na baba yake huyo hawakuwa Waarabu. Ni Waisrael ambao bado wanaendelea kupigana na Waarabu ili wachukue nchi yao iliyowafanya waondoke Misri.
Uzao wa Ibrahim ndiyo uliomleta Yusufu ambaye akawachukua Waisrael kwenda kuishi Misri. Maisha yalikuwa ya raha sana, watu waliionjoi maisha lakini baada ya mfalme huyo kufa, ndipo akaja mfalme mwingine ambaye sasa hakuwataka Waisrael, akawafanya watumwa wake.
Wakafanyishwa kazi. Baadaye ndipo Musa akazaliwa ndani ya ardhi ya Kiarabu. Akapewa jukumu la kuwatoa Israel kutoka hapo Misri kwenda kwao. Wakati huo ndio ambao nao Waarabu walikuwa wamejinyakulia nchi, tena walikuwa ni watu wakubwa kimuonekano.
Musa akaanza mchakato wa kuwatoa Israel Uarabuni na kuwapelekea Israel. Waliishi Misri kwa miaka 400. Wakaondoka na kwenda Misri, na walitumia miaka 40.
Musa hakuingia Israel, alikufa jangwani na Mungu kumzika. Wale waliofanikiwa kuingia huko Israel ndio walioendelea kuipambania ardhi yao mpaka leo hii.
Hapa kuna jambo moja.
Vita ya Israel na Waarabu itapamba moto hapo baadaye. Itapigwa vita kali sana. Sasa kwa kuwa Israel ataonekana kuwa kiburi na mwenye nguvu sana, dunia nzima itaanza kumcharaza. Huyu Marekani anayeonekana kuwa karibu na Israel naye atamgeuka, kila nchi duniani itamgeuka na kumpiga.
Mwisho wa siku baada ya kuona wanapigwa sana, watakimbilia mpaka kwenye mlima ule aliopaa Yesu, wataomboleza na kulia, hapo ndipo Yesu atashuka kuimaliza vita hiyo, na huo ndiyo utakuwa mwisho wa kila kitu.
Ibrahim baada ya kuzaa na kijakazi ambaye alikuwa Mwarabu, inamaanisha damu yake ilichanganyika na ya Kiarabu na ndiyo maana tunasema Ishmael ni baba wa Waarabu kwa sababu mama yake alikuwa Mwarabu.
Nchi za Kiarabu ambazo zipo kwenye umoja ni hizi, Algeria, Bahrain, Iraq, Jordan, Kuwait, Djibout, Saudi Arabia, Tunisia, United Arab Emirates, Yemen, Somalia, Sudan, Syria, Comoros, Misri, Maurtania, Qatar na Palestina.
Kwa nini Waarabu wanamchukia Israel? Ni kwa sababu si Mwarabu mwenzao. Na hao ndiyo wa kizazi cha Ibrahim. Kwa hiyo kama ulikuwa unahisi Ibrahim alikuwa Mwarabu, futa hiyo akilini mwako.
Hata Iran sio Waarabu, najua wengine mtakuwa hamlijui hili kwa undani. Miongoni mwa nchi za Kiarabu, Iran hayupo kwa sababu yeye si Mwarabu.
So Israel na Waarabu ni baba mmoja ila mama tofauti. Ibrahim alizaa na Muisrael mwenzake kwa kipindi hicho ilikuwa bado haijaitwa Israel na mtoto wake kuitwa Isaka ila yule aliyezaa na kijakazi ambaye ni Mwarabu anaitwa Ishmael. Tatizo kubwa la vita baina ya Mwarabu na Israel ni hapa.
Kama Israel angekuwa Mwarabu, leo usingesikia vita vinavyoendelea huko. Na mara zote Israel anawaambiaga kwamba nchi zote za Uarabuni ni mali ya Israel na ndiyo maana kila anapokwenda kupiga, anachukua ardhi na kutanua nchi yake.
Israel walipewa nchi ndogo sana wakae baada ya kutawanywa na Adolf Hitler, baada ya kuanza kurudi, wakaitaka nchi yao, lakini kwa bahati mbaya waliwaona Waarabu washajigawia ardhi yao. Walichokifanya ni kuanza kupigana nao.
Kama unakumbuka Umoja wa Mataifa uliingilia kati, ulichukizwa na kitendo cha Israel kuwapiga Waarabu, walichokifanya, wakawapelekea Biblia ambayo kwa nyuma kuna ramani ya Israel tangu enzi za Musa. Wakawaonyesha na kuwaambia kwamba nchi zote za Uarabuni ni Israel, tutakapokuwa wengi, tutaendelea kupiga na kuirudisha nchi yetu.
So jua hili. Ibrahim hakuwa Mwarabu. Musa hakuwa Mwarabu. Suleimani mtoto wa Daudi na baba yake huyo hawakuwa Waarabu. Ni Waisrael ambao bado wanaendelea kupigana na Waarabu ili wachukue nchi yao iliyowafanya waondoke Misri.
Uzao wa Ibrahim ndiyo uliomleta Yusufu ambaye akawachukua Waisrael kwenda kuishi Misri. Maisha yalikuwa ya raha sana, watu waliionjoi maisha lakini baada ya mfalme huyo kufa, ndipo akaja mfalme mwingine ambaye sasa hakuwataka Waisrael, akawafanya watumwa wake.
Wakafanyishwa kazi. Baadaye ndipo Musa akazaliwa ndani ya ardhi ya Kiarabu. Akapewa jukumu la kuwatoa Israel kutoka hapo Misri kwenda kwao. Wakati huo ndio ambao nao Waarabu walikuwa wamejinyakulia nchi, tena walikuwa ni watu wakubwa kimuonekano.
Musa akaanza mchakato wa kuwatoa Israel Uarabuni na kuwapelekea Israel. Waliishi Misri kwa miaka 400. Wakaondoka na kwenda Misri, na walitumia miaka 40.
Musa hakuingia Israel, alikufa jangwani na Mungu kumzika. Wale waliofanikiwa kuingia huko Israel ndio walioendelea kuipambania ardhi yao mpaka leo hii.
Hapa kuna jambo moja.
Vita ya Israel na Waarabu itapamba moto hapo baadaye. Itapigwa vita kali sana. Sasa kwa kuwa Israel ataonekana kuwa kiburi na mwenye nguvu sana, dunia nzima itaanza kumcharaza. Huyu Marekani anayeonekana kuwa karibu na Israel naye atamgeuka, kila nchi duniani itamgeuka na kumpiga.
Mwisho wa siku baada ya kuona wanapigwa sana, watakimbilia mpaka kwenye mlima ule aliopaa Yesu, wataomboleza na kulia, hapo ndipo Yesu atashuka kuimaliza vita hiyo, na huo ndiyo utakuwa mwisho wa kila kitu.