Ukweli kuhusu ishu ya Stephen Masele

Ukweli kuhusu ishu ya Stephen Masele

Maskini Ndugai hata watu wa nje wamemtambua ni wa jazba na ana mambo ya hovyo wameanza kumshirikisha kwenye mambo yao ya hovyo, nae kwa vile ni wa hovyo hajatambua anatumika hovyo na anaendelea kujipambanua ulimwenguni jinsi alivyo wa hovyo..
Masele ameponzwa na tamaa ya kuwa Rais wa PAP kwa maana nyingine Ngamia anataka kuingia mzima mzima kwenye hema!
 
Kuna kitu sijaelewa, yaani mtanzania Job Ndugai ameamua kumhujumu mtanzania mwenzie ili kumtetea mkameruni katika bunge la Afrika?

Ana bifu gani hilo na Masele?

Yaani kwamba amehongwa na mkameruni? Spika wa bunge la Tanzania ana njaa kiasi cha kuhongwa na mtu wa nje ili kumhujumu mbunge mwenzie ili kumtetea mtu wa nje? Mkuu nakuamini haya mambo una uelewa nayo sana, wewe unahisi kuna nini hapa?
Vita yaUspika 2020

Eti kosa lake Umbea, tangu lini umbea umekuwa kosa la kisheria ?
 
Masele ameponzwa na tamaa ya kuwa Rais wa PAP kwa maana nyingine Ngamia anataka kuingia mzima mzima kwenye hema!
Masele hana tamaa ya urais mkuu, rais wa PAP mwenyewe amekiri kuwa ana tuhuma na wabunge wote wametaka apishe kiti, masele hawezi kunyamaza kwa kuwa ataonekana ameona hizo tuhuma si chochote.. Hofu ya Ndugai ni kuwa Masele akiwa rais wa PAP kama atamzidi vile, jamaa ni jazba na kibri kichwani mtupu.
 
Kwa hisani ya Malisa GJ

Kwa wasioelewa yanayoendelea kuhusu Masele. Ni kwamba Masele ni Makamu wa kwanza Rais wa bunge la Afrika (PAP). Hivi karibuni ameingia kwenye mgogoro na Rais wa bunge hilo Bw.Roger Nkodo Dang raia wa Cameroon. Masele anamtuhumu Dang kwa ubadhirifu wa pesa za bunge hilo, hivyo ameunda kamati ya kumchunguza.

Dang amekasirishwa na uamuzi huo na anaona Masele anafanya mbinu za kumuondoa ili yeye akalie kiti cha Urais wa bunge hilo. Kwahiyo Dang ameamua kumng'oa Masele kwenye nafasi yake ili yeye aweze kuwa 'safe'.
_
Dang amempigia Spika Ndugai kumuomba amuite Masele nchini ili yeye aweze kusurvive. Na Spika Ndugai leo kwa jazba amemsimamisha Masele ubunge wake na kuagiza arudi nchini haraka kwa kile alichokiita mambo ya hovyo. Lengo la Spika ni kumuokoa Rais 'fisadi' wa bunge la Afrika, Roger Dang. Yani Ndugai anatumika kwenye mgogoro usiomhusu.

Leo Masele ameliambia bunge la Afrika kwamba hatarudi nchini kwa agizo la Spika kama alivyoamriwa. Amesema Waziri Mkuu Mhe.Kassim Majaliwa amemruhusu aendelee na shughuli zake za bunge la Afrika (PAP).
_
Amesema Rais wa bunge hilo Roger Nkodo Dang hataweza kumng'oa kwenye nafasi yake ya Umakamu wa Rais kwa sababu hakuteuliwa, bali alichaguliwa na wabunge wa bunge hilo. Amesema na kushangiliwa na wabunge hao.

Nafikiri mmeelewa sasa. Maana wengine mlishaanza kumuwazia jiwe.!View attachment 1100051
Safi mkuu kwa kuniongezea taaluma. Mimi nilisikia mgogoro wao Masele & Dung ni huyu rais kudhalilisha wafanyakazi wa kike kingono. Waafrika tunakwama hapohapo kila siku ila bado hatupagundui.
 
Mkuu kuna uzi mwingine wa Spika wa PAP uangalie
Safi mkuu kwa kuniongezea taaluma. Mimi nilisikia mgogoro wao Masele & Dung ni huyu rais kudhalilisha wafanyakazi wa kike kingono. Waafrika tunakwama hapohapo kila siku ila bado hatupagundui.
 
Ile cklip ya masele akihutubia bunge na wabunge kumpigia kofi,,,, kwamba yeye kachaguliwa na wabunge !!!! Ingemfanya Jobu kutathmini uamuzi wa kumsitisha kwake
 
Kuna kitu sijaelewa, yaani mtanzania Job Ndugai ameamua kumhujumu mtanzania mwenzie ili kumtetea mkameruni katika bunge la Afrika?

Ana bifu gani hilo na Masele?

Yaani kwamba amehongwa na mkameruni? Spika wa bunge la Tanzania ana njaa kiasi cha kuhongwa na mtu wa nje ili kumhujumu mbunge mwenzie ili kumtetea mtu wa nje? Mkuu nakuamini haya mambo una uelewa nayo sana, wewe unahisi kuna nini hapa?
Birds of a feather
 
Zile tweets za Mh. Masele zikisema "Mr. President siwezi kufanya yale unayotaka kusikia tu..." wananchi walizihusisha moja kwa moja na mr. Jiwe kuwa 'KAMCHANA LIVE!'

Kumbe aliyekuwa anaongelewa ni President wa PAP. Kwa hili, inabidi Jiwe ajitafakali kukubalika kwake.

Heko PM kumruhusu jamaa aendelee na majukumu yake (japo naona kama ni mgongano wa mihimili) lakini supika kwanini amrejeshe kwa lengo la kulindana? Rais ameshakiri makosa, Supika utajificha wapi?

Je, anaendelea kuthibitidha ile kauli ya CAG? Au ndo masna ameamua kumkagua na CAG ili kuendelea kuipa nguvu ile kauli? Binafsi naona wangeshughulikia kasoro zilizoibuliwa kuliko kulindana.


Mnamuundia zengwe CAG ili mumuondoe???
 
Masele hana tamaa ya urais mkuu, rais wa PAP mwenyewe amekiri kuwa ana tuhuma na wabunge wote wametaka apishe kiti, masele hawezi kunyamaza kwa kuwa ataonekana ameona hizo tuhuma si chochote.. Hofu ya Ndugai ni kuwa Masele akiwa rais wa PAP kama atamzidi vile, jamaa ni jazba na kibri kichwani mtupu.
Hekima na busara havijatumika katika ku-handle hiyo issue na baadhi ya ma-Rais wa nchi za Africa wamelalamika, hivyo kijana anatakiwa kurudi tz ASAP na kwa swala la PM huo ulikuwa mtego wa kumnasa kirahisi.

Inasemekana Masele akiwa Rais wa PAP ata-pose a threat to.......
 
Hivi inawezekana kuutafuta ubora au u weledi wa SPIKA wetu kwa kuwatumia wananchi wapige kura kusema ANAFAA au HAFAI
Tuweni kama wale wengi bungeni hata mmoja tu akisema Ndiyoooo anawawakilisha wooote.
 
Back
Top Bottom