Ukweli Kuhusu Edward Lowassa na Urais 2015

Ukweli Kuhusu Edward Lowassa na Urais 2015

Mimi ni Chadena ila Lowassa namkubali sana kwa kuwa na maamuzi ya kiume. Nchi hakuna mwizi wengine humu mpo vitengo vya serikari mkiwa mmeajiriwa na ni wezi tu hukoo sehemu ya kazi Tanzania kila mtu anapiga Dili tusidanganyane Ila kwa Lowasa hata kama ni Fisadi basi huyo Anajali jamii pia kuna mafisadi jamanii khaaa ya wanaaiba kweupeee na hawaogopiii. LOWASSA AKIWA PRESIDENT YAANI MWAKYEMBE SITTA MEMBE WATAFUTE KAZI NYINGINE
 
Watanzania tuwe makini kuelekea mwaka 2015, vinginevyo tutaendelea kupangisha mafisadi pale ikulu ya magogoni!
 
NI NANI KAMA LOWASSA
1. Kalamu ninakushika, ili nipate andika,
Habari zipate fika, kwa watu wa kila rika,
Jambo moja mi nataka, ya moyoni kuanika,
Ni nani kama lowassa, kwa mema lotutendea.

2. Sifa alijizolea, utumishi ‘lotukuka,
Ofisi kaiachia, nchi nzima kazunguka,
Roho zetu kaokoa, baa njaa kutimka,
Ni nani kama lowassa, kwa mema lotutendea.

3. Pia uwajibikaji, kasimamia nchini,
Ripoti za utendaji, katilia maanani,
Kwenye miji na vijiji, misaada kila dini,
Ni nani kama lowassa, kwa mema lotutendea.

4. Hakika Edo jasiri, Mola kampa kipaji,
Kawazima wamisri, kwenye mradi wa maji,
Kilimo kinashamiri, kisa umwagiliaji,
Ni nani kama lowassa, kwa mema lotutendea.

5. Kajenga kwa umahiri, umoja wa kitaifa,
Kafanya kazi vizuri, kwa juhudi maarifa,
Kwa matendo kahubiri, naitaja yake sifa,
Ni nani kama lowassa, kwa mema lotutendea.

6. Kazi mbele aliweka, kuleta maendeleo,
Nchi ikaimarika, ikapata mwelekeo,
Kweli tulinufaika, kwa mazuri matokeo,
Ni nani kama lowassa, kwa mema lotutendea.

7. Ni mzalendo shupavu, thabiti asiyeyumba,
Si kiongozi mabavu, na sio wa kujigamba,
Mtii mnyenyekevu, hakika Edo ni mwamba,
Ni nani kama lowassa, kwa mema lotutendea.

8. Kumbuka aliyofanya, na mema aliyotenda,
Usije ukatawanya, yale aliyoyapanda,
Jaribu kuyakusanya, hakika utampenda,
Ni nani kama lowassa, kwa mema lotutendea.

9.Sekondari kila kata, ‘lijenga kote nchini,
Zahanati zikafata, mijini na vijijini,
Kwa juhudi katafuta, masoko nje na ndani.
Ni nani kama lowassa, kwa mema lotutendea.

10. Walimu tunakusifu, twasema wewe ni namba,
Aliokoa maelfu, kwa kutujengea nyumba,
Ni kwa wako ubunifu, bado amani yatamba,
Ni nani kama lowassa, kwa mema lotutendea.

11. Hata shule za msingi, sasa hawakai chini,
Madawati yako mengi, alosambaza nchini,
Heri ikawa kwa wengi, karo ikushushwa chini,
Ni nani kama lowassa, kwa mema lotutendea.

12. Tamati nimefikia, kwa yale niliyowaza,
Nilosema zingatia, kweli Edo anaweza,
Ni mengi katufanyia, machache nimeeleza,
Ni nani kama lowassa, kwa mema ulio tutendea watanzania
 
umeahidiwa cheo gani?

Mkuu sija ahidiwa cheo chochote
Namkubali sna mzee wa maamuzi magumu na ndiye kiongoz tuliyebakiwa naye tz wengine wote ni wababaishaji tu,namuomba sna Mungu aniweke salama nije nimpigie kura yangu akatuongoze watanzania kwenye nchi ya asali na maziwa
 
Kila kona ya nchi jina linalovuma masikioni mwa watanzania wengi ni lowassa.duh safar bado inaendelea
 
Hawezi mikikimikiki ya urais hasa ya kampeni afya yake ni mgogoro
 
...haya maradhi uchachamaa kwa wale wagonjwa wakati mwezi unapokuwa mchanga,sijui ni kwa nini huya ameharibikia kwa kipindi hiki!!!???...
 
NI NANI KAMA LOWASSA
1. Kalamu ninakushika, ili nipate andika,
Habari zipate fika, kwa watu wa kila rika,
Jambo moja mi nataka, ya moyoni kuanika,
Ni nani kama lowassa, kwa mema lotutendea.

2. Sifa alijizolea, utumishi ‘lotukuka,
Ofisi kaiachia, nchi nzima kazunguka,
Roho zetu kaokoa, baa njaa kutimka,
Ni nani kama lowassa, kwa mema lotutendea.

3. Pia uwajibikaji, kasimamia nchini,
Ripoti za utendaji, katilia maanani,
Kwenye miji na vijiji, misaada kila dini,
Ni nani kama lowassa, kwa mema lotutendea.

4. Hakika Edo jasiri, Mola kampa kipaji,
Kawazima wamisri, kwenye mradi wa maji,
Kilimo kinashamiri, kisa umwagiliaji,
Ni nani kama lowassa, kwa mema lotutendea.

5. Kajenga kwa umahiri, umoja wa kitaifa,
Kafanya kazi vizuri, kwa juhudi maarifa,
Kwa matendo kahubiri, naitaja yake sifa,
Ni nani kama lowassa, kwa mema lotutendea.

6. Kazi mbele aliweka, kuleta maendeleo,
Nchi ikaimarika, ikapata mwelekeo,
Kweli tulinufaika, kwa mazuri matokeo,
Ni nani kama lowassa, kwa mema lotutendea.

7. Ni mzalendo shupavu, thabiti asiyeyumba,
Si kiongozi mabavu, na sio wa kujigamba,
Mtii mnyenyekevu, hakika Edo ni mwamba,
Ni nani kama lowassa, kwa mema lotutendea.

8. Kumbuka aliyofanya, na mema aliyotenda,
Usije ukatawanya, yale aliyoyapanda,
Jaribu kuyakusanya, hakika utampenda,
Ni nani kama lowassa, kwa mema lotutendea.

9.Sekondari kila kata, ‘lijenga kote nchini,
Zahanati zikafata, mijini na vijijini,
Kwa juhudi katafuta, masoko nje na ndani.
Ni nani kama lowassa, kwa mema lotutendea.

10. Walimu tunakusifu, twasema wewe ni namba,
Aliokoa maelfu, kwa kutujengea nyumba,
Ni kwa wako ubunifu, bado amani yatamba,
Ni nani kama lowassa, kwa mema lotutendea.

11. Hata shule za msingi, sasa hawakai chini,
Madawati yako mengi, alosambaza nchini,
Heri ikawa kwa wengi, karo ikushushwa chini,
Ni nani kama lowassa, kwa mema lotutendea.

12. Tamati nimefikia, kwa yale niliyowaza,
Nilosema zingatia, kweli Edo anaweza,
Ni mengi katufanyia, machache nimeeleza,
Ni nani kama lowassa, kwa mema ulio tutendea watanzania

Hivi unamzungumzia lowasa huyuhuyu? au tusubili lowasa mwingine ambae umemuandikia kwa mfano wa shairi maana huyu ninaemfahamu mimi tangu miaka ya 90 sifa hizo hana labda kama amefanya hayo kwenye familia yenu si kwa nchi zaidi ya hapo ni kuganga njaa kwako ndo kunakusumbua
 
Hivi unamzungumzia lowasa huyuhuyu? au tusubili lowasa mwingine ambae umemuandikia kwa mfano wa shairi maana huyu ninaemfahamu mimi tangu miaka ya 90 sifa hizo hana labda kama amefanya hayo kwenye familia yenu si kwa nchi zaidi ya hapo ni kuganga njaa kwako ndo kunakusumbua

Unaushaidi??kama unao kamshtaki au peleka TAKUKURU,usiwe mlalamisi kama Mzee SITA.
 
Hivi unamzungumzia lowasa huyuhuyu? au tusubili lowasa mwingine ambae umemuandikia kwa mfano wa shairi maana huyu ninaemfahamu mimi tangu miaka ya 90 sifa hizo hana labda kama amefanya hayo kwenye familia yenu si kwa nchi zaidi ya hapo ni kuganga njaa kwako ndo kunakusumbua

mkuu una chuki na wivu kama wa mke mwenza!!ndio hvyo lakin lowassa hashiki tena
 
Back
Top Bottom