Ukweli kuhusu bahati nasibu za Simu za Mkononi

Ukweli kuhusu bahati nasibu za Simu za Mkononi

Mbunge

Senior Member
Joined
Aug 7, 2008
Posts
104
Reaction score
10
KWA HESABU za haraka haraka tuseme kila mchezo wa bahati nasibu iwe Jivulie au Mkopo au Mwanakuliwa au Mjingahajui na kadhalika inayoendesha na makampuni ya simu za mkononi kwenye televisheni inapata washiriki 300,000 tu ambayo ni idadi ya chini mno, kisha kwa kila mmoja wao anacheza mara 10 tu kitu ambacho sio rahisi lazima acheze zaidi kutokana na uroho wa kutaka kuukata; halafu kila mmoja anakatwa shilingi 1,000 tu kwa ujumbe mfupu. Piga hesabu : jumla hii ya chini inatupa hesabu ya shilingi bilioni tatu- safi kabisa na sijui hata kama zinalipiwa kodi wala ushuru wowote. Na hata wakikata theluthi ya hapo wakatoa bilioni moja hivi bado wana faida pale wasipopanda lakini wanavuna kama vile vichaa. Mtu akinunua magari ya mtumba 100 kwa bei ya shilingi milioni 10 kila gari anakuwa ametumia shilingi bilioni moja tu. Wapi na wapi ? Nani kaliwa kama sio mtumiaji simu za mkononi mlalahoi. Kwa hiyo kaa ukitambua kwamba michezo hiyo ya kamari na hasa kwa wewe unayestahili kuiogopa dini yako na yule aliyekuumba inazidi kukufanya wewe uwe masikini zaidi na zaidi na haikupi nafuu yoyote.

Kuna wasiwasi kuwa michezo hii yote ya bahati nasibu kupitia simu za mkononi ina nia ya kufadhili vyama fulani vya siasa, yaani, mapato yatakuwa yakigawiwa kati ya kampuni ya simu mkononi na chama shirika cha kisiasa. Je, ni kweli ?
 
Huenda ni kweli -- haswa kwa kampuni kama ya Vodacom amb ayo nanihii bado ana hisa nyingi.
 
Hii kweli kabisa na sisi kwa ujinga wetu ndio tunawatajirisha wao na sisi tunazidi kuwa masikini.
 
Marksmanhuyo Mirambo anazo 30% tu, jamani what is the logic behind lottery aka bahati nasibu?
 
Marksmanhuyo Mirambo anazo 30% tu, jamani what is the logic behind lottery aka bahati nasibu?

Unaandaliwa mkakati wa kuja kuwaengua hawa washenzi (makaburu) na wenzao kwenye soko. Ni wakati wa kuwa na kampuni ya simu za mikononi ya WAZAWA wakimiliki asilimia 70 ya hisa, na 30 za wawekezaji wa nje, si kinyume chake!
 
hata siku moja kwa hii sidanganyi.
kama juzi mtu wa mkoko 4:30 usiku anasema tusuburie mwezi kama utaandama wakati taarifa ya habari ya saa 2:00 walishasema mwezi umeandama. pale ilikuwa recorded wanarusha usiku lkn kwenye advertisement zao wanakuambia cheza then sikiliza TBC1 4:30 ucku. sidanganyikiiiiiiiiii!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
hata siku moja kwa hii sidanganyi.
kama juzi mtu wa mkoko 4:30 usiku anasema tusuburie mwezi kama utaandama wakati taarifa ya habari ya saa 2:00 walishasema mwezi umeandama. pale ilikuwa recorded wanarusha usiku lkn kwenye advertisement zao wanakuambia cheza then sikiliza TBC1 4:30 ucku. sidanganyikiiiiiiiiii!!!!!!!!!!!!!!!!!
Aiseeeeeeeeeee hata mimi nimewasitukia. Hii ni danganya toto kabisa? Watatuibia mpaka damu ituishie
 
Lakini kama umecheza michezo mi4 kuna ubaya gani? Na wengine si wamechangia? All in all, siamini katika bahati nasibu
 
ooooooooooooooooooooops!

sasa ndio napata ufahamu
kumbe zile siku 100 za VODACOM i10 miamoja ni za kampeni??????????????????????????????


Nisameheni sikujua.
 
Mmeliwa kweupeee? Nilisema ktk thread fulani kama hii niliyoanzisha last month kuwa wanawaibia watu. CCM inashiriki haya madudu maana serikali yake inajua kila uozo wa hizi nasibu bahati lakini hakuna wanachofanya. Endeleeni kucheza huku vigezo na masharti vikizingatiwa. dawa ni kutocheza hizi bahati nasibu
 
makampuni ya simu ni utapeli wa hali ya juu. Au pengine wanatafuta pesa za kampeni kwa ajili ya mtoto wa mrisho.
 
Mbaya zaidi ni kuwa ukishinda milioni kama 40, haupewi. Nyingi zinagawanwa na wao wenyewe ndani kidogo tu anapewa yule aliyetangazwa. Haya yamewatokea rafiki zangu wawili hapa Dar. Mmoja aliambiwa ameshinda 10M akapewa 2M na mwingine a mwingine (Yeye aliomba dili hilo) akaambiwa asihofu, kisha akatangazwa ameshinda 40M akapewa 3.5M. Zingine zinaishie katiuka msululu wa wao wenyewe!!!!!! Wizi huu?
 
hii ya vodacom nimeishtukia, lakini angalia hata yule dada wa jikoki wa milioni 100, anapigiwa simu wala hata hashtuki sio siri huu ni wizi wa mchana kweupeeeeeee, sichezi tena madudu haya,
 
kwa jinc wanavyovuna...hawana hata haja ya kupanga..maana wanapata mahela kwelikweli...especially vijijini huko...maana watu wananunua vocha na kujibu maswali..wana meseji zao wanazokutumia ambazo zinakutia ujinga na kuona kama unashinda vile...kubwa zaidi ninataka kujua..leseni yao ni kutoa mawasiliano, au kufanya biashara ya bahati nasibu...?
 
kwa jinc wanavyovuna...hawana hata haja ya kupanga..maana wanapata mahela kwelikweli...especially vijijini huko...maana watu wananunua vocha na kujibu maswali..wana meseji zao wanazokutumia ambazo zinakutia ujinga na kuona kama unashinda vile...kubwa zaidi ninataka kujua..leseni yao ni kutoa mawasiliano, au kufanya biashara ya bahati nasibu...?

Hawa jamaa karibu watageuka kuwa kama matapeli wa Nigeria. Naombeni muache kunitumia ujumbe kuwa jina langu limeshinda kushiriki katika bahati nasibu. mimi sijawahi na sitokaa nishiriki huo ujinga. wajinga ndio waliwao.
Nashangaa siku mnazindua ile promosheni ya hyundai i10 mlisema kusudio ni kurudishe faida kwa watumiaji, halafu hapo hapo mnamkata m2 550/= Hapo mmerudishia faida au ndio mnazidi kumkamua?

 
kabla ya uchaguzi wa mwaka 2005 walikuja na janja ya kubalisha namba za magari na kila gari ilikuwa TZS 50000 kama sikosei, wakavuna pesa baadae tuliambiwa ilikuwa pesa ya kampeni...leo driving licence na bahati nasibu za Simu za Mkononi...
 
Back
Top Bottom