Ukuta katika machimbo ya Mererani wazua utata

Ukuta katika machimbo ya Mererani wazua utata

Mimi niliwahi kuchimba madini huko mererani, nilikuwa najaribu kujiuliza ukuta utasaidiaje? nikawa sipati picha. Labda kama huo ukuta unaweza kupunguza wizi. Sikushangaa sana kwani rais wetu anapenda kudhibiti au kulinda kwa mtazamo wake. Lakini anakosa mbinu sahihi au wanaomshauri wanamshauri anachowashauri wao.

Nilishangaa ili siku aliposema kesho jeshi likaingia na mkwara mkubwa utafakiri ni jambo lenye tija sana. Nimewahi kushauri mara nyingi humu, badala ya jeshi kukaa tu bila kuzalisha mali wakati huu wa amani, ni bora lipewe mashamba makubwa ya kulima kwa kupewa pembejeo kama tractors, combine harvestors, mbolea nk. wazalishe kwa wingi kisha wananchi tunaolima kwa nguvu zetu tuachwe tuuze tunapotaka. Hayo ya jeshi ndio yakajazwe kwenye maghala ya serekali kwa ajili ya njaa na kutunza bei elekezi. Lakini nimeona jeshi limeenda kama roketi kujenga ukuta wakati kama ni madini ndio yako ukingoni. Usishangae ndani ya mwaka huo ukuta ukaanza kuweka ufa kwani sidhani hata kama feasibility study imefanyika. Anyway ndio rais wetu huyo nia njema lakini hana mbinu.
Nchi za wenzetu wanajeshi wao wako busy na technology innovations sie tuko busy tunajenga UKUTA na kutumiana manissan meupe.
 
Kwa uelewa wangu eneo linawekewa mitambo ya gprs ukivuka eneo la uzio hata ukiwa kilometer tano chini ya ardhi inajulikana so kwa hili kuiba ni ngumu, japo huyu sizonje simpendi hata
GPRS?? Unajua ulichokiandika?
 
Habari wana jamvi,

Kama kichwa kisemavyo,

Huu ukuta wa mererani ulioagizwa na mh Magu umezua utata kwa namna ulivgopokelewa hasa na washikadau wa shughuli usika za madini,

Kwanza wameshangaa kutolewa maamuzi ya namna ile ambayo kwayo wamesikitika kwamba kwann nguvu hio na gharama hizo wasingejenga barabara sehemu zenye uhitaji.

Wakaenda mbali zaaidi juu ya washauri wa mh. Magu kana kwamba elimu yao ni yakinadharia tuu imewanyima ujuzi wa uhalisia kufikia maamuzi yasiyo na tija au wanaamua kumpotisha tuu mh. Magu.

Wanasema kama mh. Magu hawajui wachimba madini na wadau wake atakuja shtuka shimo linachimbwa mererani wanapolo wanatokea Arusha au hata chumbani kwa mtu na hapo ndo hasara ya kamera itakapo onekana, pia patakua na njia nyingi tuu za kufanikisha wizi kwa serikali kama serikali haitokuja na sera rafiki, shirikishi katika ukusanyaji kodi.

Mimi ni mzalando!!
Big point. Ukuta ni kupoteza maboya. Kodi na miundo mbinu ndilo majibu
 
Kama low mind wameelewa basi,ndio hicho kinachotafutwa. Kama kuna wimbi la watu wameshangilia inatosha...

Daa nimechoka kabisa, nikasema au mimi sielewi labda kwa kuwa sio mzalendo au ni vipi. Anyway ngoja tuone bora uzima.
 
Kwa hiyo hata ule ukuta wa Berlin wa kuwatenganisha wajerumani baada ya vita kuu ya pili haukusaidia? Yaani wanapolo wa ujerumani walikuwa wana pita tu underground na kuibukia watakavyo? Ina maana hata huo ukuta anaoujenga Trump kwenye mpaka na Mexico hauna maana yo yote maana wanaapolo watapita tu? Hicho kitu hawataweza. Tanzanite iko tele eneo hilo la Merarani. Hadi sasa uchimbaji unaofanyika ni wa kupapasa tu -- less than 9 metres depth. Mali iko hadi kilometers 500 deep.
 
Mimi niliwahi kuchimba madini huko mererani, nilikuwa najaribu kujiuliza ukuta utasaidiaje? nikawa sipati picha. Labda kama huo ukuta unaweza kupunguza wizi. Sikushangaa sana kwani rais wetu anapenda kudhibiti au kulinda kwa mtazamo wake. Lakini anakosa mbinu sahihi au wanaomshauri wanamshauri anachowashauri wao.

Nilishangaa ili siku aliposema kesho jeshi likaingia na mkwara mkubwa utafakiri ni jambo lenye tija sana. Nimewahi kushauri mara nyingi humu, badala ya jeshi kukaa tu bila kuzalisha mali wakati huu wa amani, ni bora lipewe mashamba makubwa ya kulima kwa kupewa pembejeo kama tractors, combine harvestors, mbolea nk. wazalishe kwa wingi kisha wananchi tunaolima kwa nguvu zetu tuachwe tuuze tunapotaka. Hayo ya jeshi ndio yakajazwe kwenye maghala ya serekali kwa ajili ya njaa na kutunza bei elekezi. Lakini nimeona jeshi limeenda kama roketi kujenga ukuta wakati kama ni madini ndio yako ukingoni. Usishangae ndani ya mwaka huo ukuta ukaanza kuweka ufa kwani sidhani hata kama feasibility study imefanyika. Anyway ndio rais wetu huyo nia njema lakini hana mbinu.
Mi nilishawahi kusema VETA wapige practical za kujenga madawati?
 
Huyu jamaa kakaa muda mrefu wizara ya ujenzi. Anajua kutumia miradi ya ujenzi kupiga pesa. Tena anamtumia nduguye kumpa contract.
 
Ukuta utazuiaje uchumbaji na utorishaji wa madini?

Kikawaida, wanapolo safari zao ni chini kwa chini. Ndo maana wengi tulitaka more details kuhusiana na huo ukuta.

Kama ni kuzuia wauzaji wasitoroshe, ukuta peke yake hautasaidia.
Ni kichekesho! kwa mchimba madini yeyote ukimwambia ukuta atakucheka kwa kweli..umepata jiwe la 1bln na zaidi ushindwe kulitoa..akawaulize wamarekani wanavyohangaika na wamexico kuzuia madawa kuingizwa USA ndo atajua pesa ni nn!
 
PIGA UKUTA KURUKARUKA KWA MAHARAGE NDO KUIVA KWAKE
 
MENGI.jpg
 
Nyie keng..e msiwe Wapuu..zi kiasi hicho, msipinge kila kitu maana hata migodi ya wazungu ina fence
Wewe ndiye ulikuwa umeandaliwa kuongea pale Arusha, ukaingia mitini dakika ya mwisho? Hadi ukasababisha mh rais akaweka KIBWAGIZO.
 
hii kali machimbo kuwekewa ukuta juu ya ardhi? Ni sawa Shimo la Panya kuzibwa kwa Mkate
 
Wasomi wa kitanzania vichekesho vitupu. Huwa wanaibuka linapotokea jambo na wanaongea sentensi nyiiingi zenye nge....wange, tunge, ninge, ukishaweka nge tu, tayari maana nzima imeshapotea.

Tuna wasomi reactive badala ya kuwa proactive. Tuna wasomi wenye bei, kama walivyo wanasiasa wetu. Price tag yao inaonekana hata mtu akiwa umbali wa kilomita moja kutoka mahali waliposimama!!.
 
.....
.....GPS haishiki huko chini mkuu

Mkuu, nimesoma nimenyamaza kwa sababu huwezi kujibu kila post kwani JF imejaa vilaza hasa washabiki wa upande uleeeeee.

Jama hata hiyo GPS unayomrekebisha umehisi tu lakini mwenzako hajui hata GPS ni nini, yeye anadani ni GPSR?

Hao wana apollo tutawafungia gprs tracker, halafu watu wasiojulikana watawafatilia hukohuko chini,
 
Back
Top Bottom