Ukuta katika machimbo ya Mererani wazua utata

Ukuta katika machimbo ya Mererani wazua utata

Kwa uelewa wangu eneo linawekewa mitambo ya gprs ukivuka eneo la uzio hata ukiwa kilometer tano chini ya ardhi inajulikana so kwa hili kuiba ni ngumu, japo huyu sizonje simpendi hata
Ye mwenyewe hataki mapenzi, ni kazi tu. Umpende usimpende haiongezi wala kupunguza kitu
 
ngoja tupime manyokaa/ wana apolo na wazee wa mabaka nani mkali
Mabaka hawawezi fua dafu kwa apolo kwenye hizo anga, nakumbuka miaka ya nyuma migodi ilipofurika maji waliletwa wajeda kusaidia shughuli za uokoaji wakachemka ikabidi apolo waingie mzigoni wakafanya yao.
 
Hamna wema nyie hv ukijenga nyumba yako ukiweka ukuta unakuea na maana gani?ni moja ya njia za ulinzi,njia nyingine zinafuata badae ...Tuko pamoja Mh Rais 100%
HUJIELEWI.. kWENYE UKUTA WA NYUMBA YAKO, nani anafanya shughuri za kuchimba ardhini? MUWE MNATOA MIFANO HALISI ...
 
Mimi niliwahi kuchimba madini huko mererani, nilikuwa najaribu kujiuliza ukuta utasaidiaje? nikawa sipati picha. Labda kama huo ukuta unaweza kupunguza wizi. Sikushangaa sana kwani rais wetu anapenda kudhibiti au kulinda kwa mtazamo wake. Lakini anakosa mbinu sahihi au wanaomshauri wanamshauri anachowashauri wao.

Nilishangaa ili siku aliposema kesho jeshi likaingia na mkwara mkubwa utafakiri ni jambo lenye tija sana. Nimewahi kushauri mara nyingi humu, badala ya jeshi kukaa tu bila kuzalisha mali wakati huu wa amani, ni bora lipewe mashamba makubwa ya kulima kwa kupewa pembejeo kama tractors, combine harvestors, mbolea nk. wazalishe kwa wingi kisha wananchi tunaolima kwa nguvu zetu tuachwe tuuze tunapotaka. Hayo ya jeshi ndio yakajazwe kwenye maghala ya serekali kwa ajili ya njaa na kutunza bei elekezi. Lakini nimeona jeshi limeenda kama roketi kujenga ukuta wakati kama ni madini ndio yako ukingoni. Usishangae ndani ya mwaka huo ukuta ukaanza kuweka ufa kwani sidhani hata kama feasibility study imefanyika. Anyway ndio rais wetu huyo nia njema lakini hana mbinu.
Hivi hili wazo la ukuta kalianzisha Magufuli? Hili si ni pendekezo la kamati za bunge tukufu, na yeye kaamua kutekeleza tu!!! Tuwe fair kwake hata kama kmhatumpendi! Kama huo ukuta ni useless, basi kamati ya Bunge imemshauri vibaya, na inabidi ilaumiwe kwa hilo!
Lakini nikonacho humu ni mikwara ya wanaojiita mabilionea wa arusha, wameanza kuona mirija yao inazibwa sasa wanamtisha Rais. Sababu nasoma comments humu, sioni hata mmoja anayetoa suluhisho zaidi ya kutoa kejeli Na matusi
 
Hata siku moja huwezi kumzuia binadamu mwenye akili zake kufanya anachotaka huo UKUTA ni bora ule wa CDM aliouzuia
 
Hii inanikumbusha wapalestina walivyochimba mahandaki chini kwa chini katika mpaka wake na Egypt. Hawa wachimbaji wadogo watachimba chini ya huo ukuta kutafuta Tanzanite.
Mradi huu ni upotevu wa pesa. Cha msingi serikali ingeanza kuwatoza kodi wachimbaji wote kutokana na eneo la vitalu vyao
Waulize Guzmann alitorokaje jela Mexico ndo wajue. Mbona hiyo ni kawaida. Ukuta tena? Wamexico wengi hawatumii ukuta wa US wanapita chini wanatokea upande wa US mbugani. Sema walishastukiwa.
 
Kwa hiyo hata ule ukuta wa Berlin wa kuwatenganisha wajerumani baada ya vita kuu ya pili haukusaidia? Yaani wanapolo wa ujerumani walikuwa wana pita tu underground na kuibukia watakavyo? Ina maana hata huo ukuta anaoujenga Trump kwenye mpaka na Mexico hauna maana yo yote maana wanaapolo watapita tu? Hicho kitu hawataweza. Tanzanite iko tele eneo hilo la Merarani. Hadi sasa uchimbaji unaofanyika ni wa kupapasa tu -- less than 9 metres depth. Mali iko hadi kilometers 500 deep.
Ukuta wa Berlin ulihusika ktk kulinda migodi?! Huo kwenye mpaka wa Mexico unalinda mgodi?!
Mifano yako haina uhusiano na hili la Mererani kabisa.
 
kumbuka hata kwenye hao wana apolo kuna usalama wa taifa wanafanya kazi kama wana apolo
 
Hamna wema nyie hv ukijenga nyumba yako ukiweka ukuta unakuea na maana gani?ni moja ya njia za ulinzi,njia nyingine zinafuata badae ...Tuko pamoja Mh Rais 100%
Hizi ndizo akili za ki-sisiem. Huo mfano wako hauna hata tbs kabisa!
 
Phd feki hua hazijifichi, kama ile ya Bashite.
Ukuta uzuie uibaji wa madini? Hehehe. Yanachimbwa chini ya ardhi we unaziba ukuta pembeni. Siamini dini ila kweli hapa albadri haijamuacha mtu. Haiwezekani mtu amedata kiasi hiki.

😀😛
 
Ukuta hauzuii chochote hapo, watu wabadilike labda wamweke malaika getini .

Ndiyo maana nikasema tunahitaji UKUTA wa Sheria zinazotekelezeka,Sheria zisizofumba macho pale cheo cha mtu kinapotajwa kuwa sababu ya kuachiwa huru,tunahitaji RAIA watanzania kuijua KATIBA yao na sheria za nchi,mlinzi wa arslimali za TAIFA ni RAIA wa Taifa husika si ASKARI,RAIS,WAZIRI wala mkuu wa mkoa.
 
Back
Top Bottom