Ujenzi wa ukuta na ulinzi Mirerani, Tanzanite italindwa?

MTAZAMO

JF-Expert Member
Feb 8, 2011
19,643
33,439
Mirerani.jpg

Wakuu,

Rais wetu Magufuli amekuwa akikosolewa mno na wapinzani hata anapofanya mambo ambayo ni historia kwa nchi hii.

Pamoja na madai ya msingi wakati mwingine lakini ni vizuri kumtia moyo kwenye issues za msingi ambazo ni kwa faida ya Taifa hili.

Ujenzi wa ukuta kuzunguka machimbo ya madini ya Tanzanite na kuandaa mpango wa soko kuwa pale pale ni kitu kikubwa mno! Historia itamkumbuka kwa hili na hata kama sisi tutabeza vipo vizazi vitamuelewa.

Rais Magufuli amekuwa champion wa kulinda rasilimali zetu kwa vitendo ingawa kwasasa tunaumia na matokeo ya "sabotage" against juhudi hizi kutoka kwa "wakubwa" waliokuwa wakijichotea sawa na bure.

Mbona hatusikii "wazalendo" wetu wakipongeza hatua hii ngumu na muhimu kwa kelele zile zile tunazopiga akikosea jambo. Kitu kimoja ambacho ni hakika, Rais Magufuli anaweka historia na Africa itajifunza kwake mbinu za ulinzi wa rasilimali za nchi.

Kwa hili la kujenga ukuta, kuhusisha majeshi moja kwa moja kulinda rasilimali na mkakati wa madini kuuzwa pale pale ni moja ya maamuzi ambayo Rais John Pombe Magufuli utakumbukwa na vizazi vyote.

Uwe humpendi au humuungi mkono Rais Magufuli lakini anaweka historia na mlio kinyume chake kwa hili kumbukumbu zitabaki hivyo vizazi vyote.

Ushauri kwa mh Rais Magufuli;

Vitu vidogo kama kijana Abdul kuhojiwa uraia wake vinachafua mambo makubwa na mazuri unayofanya. Hivi hatuna magenius wa kushughulika na hali ya kisiasa inayoendelea ili nchi ibaki na mshikamano kwenye mambo ya msingi unayofanya kama haya?

Mambo mengine mnayakuza wenyewe. Tunapaswa kuwa na mshikamano against mabeberu walioitafuna hii nchi kwa muda mrefu. Kelele lazima zitakuwepo lakini nyingi zinakuzwa na wenyewe.

Kumuhoji uraia kijana Abdul kipindi hiki inajenga taswira gani? Sehemu kubwa ya wananchi wakiwemo wanafunzi wenzake wanaichukuliaje hii?

Hongera sana Rais Magufuli kwa hatua hizi za kulinda rasilimali zetu ambazo zinaenda kuweka alama ya kukumbukwa nchi hii. Napendekeza swala la majeshi kulinda rasilimali zetu moja kwa moja iwe kisheria badala ya kutegemea wanasiasa wenye objectives zao kulingana na nyakati.

Sasa Tanzanite italindwa!

Soma: Raw Tanzanite exports hurting local economy

Soma: Rais Magufuli kuzindua ukuta katika migodi ya Tanzanite Mirerani

Soma: Kujenga ukuta Mererani haitaweza kutatua tatizo la utoroshaji wa madini
 
MTAZAMO subiri kejeli, matusi na dharau za kila aina, Mbowe na ruzuku ya mabilioni kwa mwaka wameshindwa hata kujenga ofisi tu ya makao makuu, ruzuka yote inaishia kwenye kujilipa “ madeni” yao na recurrent expenditures. Ila kwa hili wao watatoa kejeli tu.
 
MTAZAMO subiri kejeli, matusi na dharau za kila aina, Mbowe na ruzuku ya mabilioni kwa mwaka wameshindwa hata kujenga ofisi tu ya makao makuu, ruzuka yote inaishia kwenye kujilipa “ madeni” yao na recurrent expenditures. Ila kwa hili wao watatoa kejeli tu, kweli nyumbxxx ni nyumbxxx tu.
Makamanda watajibu hii ....
 
Rais anafanaya vizuri sana kulinda rasilimali za nchi hasa madini. Ujenzi wa ukuta huo ni mojawapo ya jitihada za utekelezaji wa ulinzi huo.

Hata hivyo, kuna wachimbaji wadogo wadogo, walalahoi watakaoathirika na ujenzi huo kama utaratibu wa kuwaruhusu kuingia hautakuwa mzuri.

Udhibiti uimarishwe zaidi kwenye makampuni makubwa ambayo tayari yana uzio ndani ya ukuta kwani hayo ndiyo yanayotoa madini mengi yanayoweza kutoroshwa nje ya nchi.
Pia ni muhimu kuangalia gharama za ulinzi na udhibiti zisiwe kubwa kuliko kitakachopatikana.
 
Tunapaswa kuwa na mshikamano against mabeberu walioitafuna hii nchi kwa muda mrefu. Kelele lazima zitakuwepo lakini nyingi zinakuzwa na wenyewe.
Mabeberu ni TANU/CCM ambao wamekuwa madarakani tangu nchi hii ipate uhuru, kuitafuna/kuiharibu nchi wao ndio wamefanya na bado wanaendelea kufanya kwa kasi kubwa kipindi hiki.
 
Magufuli anafanya makubwa mno yenye faida na kimsingi ilipaswa ndio yawe yakiongelewa zaidi, lakini watu uzalendo hawana, wamekaa kushikiwa akili na kubeza tu bila kujali damage wanayoijenga kwa taifa hili.

Jongera JPM, nchi inakuhitaji sana tu...
 
Tatizo utawala na democracy bora tu vingine ni 100 yuko sawa%
Hakunaga democracy popote pale, ila kuna kuvumiliana tu, hapa Tanzanian watu wanaongea sana, na hawaishi kuongea, JPM uvumilivu huo hana... Yeye anapiga kazi tu, tena iko wazi kuwa ana maadui wengi, akiwapa uhuru sana, hatofanya kazi.... Wamuache afanye yake kwa manufaa ya taifa....
 
Magufuli anafanya makubwa mno yenye faida na kimsingi ilipaswa ndio yawe yakiongelewa zaidi, lakini watu uzalendo hawana, wamekaa kushikiwa akili na kubeza tu bila kujali damage wanayoijenga kwa taifa hili.

Jongera JPM, nchi inakuhitaji sana tu...
Unaweza ukatuelezea japo kwa ufupi kuwa huo ukuta unazuia vipi madini kupotea?

Karibu
 
Magufuli anafanya makubwa mno yenye faida na kimsingi ilipaswa ndio yawe yakiongelewa zaidi, lakini watu uzalendo hawana, wamekaa kushikiwa akili na kubeza tu bila kujali damage wanayoijenga kwa taifa hili.

Jongera JPM, nchi inakuhitaji sana tu...

Mimi naisubiria kwa hamu sana 2020, naamini wabunge wengi wa upinzani watadondoka sababu ya unafiki wao. Na hawajui kabisa nini wananchi wanataka, wananchi wanataka mtu anayeongelea inshu za maendeleo na sio porojo za uhuru wa kuropoka kwa wanasiasa.
 
Magufuli anafanya makubwa mno yenye faida na kimsingi ilipaswa ndio yawe yakiongelewa zaidi, lakini watu uzalendo hawana, wamekaa kushikiwa akili na kubeza tu bila kujali damage wanayoijenga kwa taifa hili.

Jongera JPM, nchi inakuhitaji sana tu...
You can build castles in the air...but they are useless with no FREEDOM..
 
Naunga mkono uwekwaji wa physical security systems kulinda madini yetu....twende mbali zaidi kuweka mfumo wa ulinzi kupitia uzalendo wa watakaosimamia uchimbaji nk.
 
Back
Top Bottom