Mshambuliaji
Senior Member
- Jul 9, 2017
- 132
- 79
Ametukanwa nani?! Mbona uelewa watu tunatofautiana hivi?!Wapinzani please tubadilike. Siyo mpaka tutume lugha za matusi kumkosoa mtu.
Sent using Jamii Forums mobile app
Mheshmiwa Mpendazoe, shikamoo!! Kwa sasa nitajikita katika maana ya uzalendo.
Pengine baadae nitarudi kujibu hoja zako zingine. Nimeona msingi wa hoja yako ipo kwenye neno "uzalendo" hadi umehoji uzalendo wa Tundu Lissu (TL) uko wapi.
Nijuavyo mimi uzalendo ni mapenzi ya kujitoa, kuunga mkono na kuilinda nchi yako;utii kwa taifa lako (i.e devoted love, support, and defense of one's country; national loyalty). Hapa hakuna maneno mawili "rais" na "chama cha siasa".
Kwa sababu binfasi, sababu za kisiasa, sababu za kutetea maslahi binafsi, watanzania wengi tena wengi wao ni wasomi wamekuwa wakipotosha maana ya neno "uzalendo". Wao kwenye neon "taifa" au "nchi" wanaweka neon "rais" kwenye definition ya neon uzalendo.
Mark Twain alipata kusema "patriotism is supporting your country all the time, and your government when it deserves it". Pia Edward Abbey alipata kusema "A patriot must always be ready to defend his country against his government".
Hapa utaona utofauti kati ya nini mzalendo anapaswa kutetea; Je ni serikali (including rais) au Je ni nchi/taifa?
Serikali ni watu ambao wapo wema na wabaya lakini nchi/taifa lina misingi na miiko yake ikiwemo demokrasia, utawala wa sheria, umoja, huduma bora za kijamii, amani nk. Je, anayoyafanya TL hata kuhoji uzalendo wake ana-defend nini? Unachofanya wewe Mpendazoe, JPM nk mna-defend nini?
Uzalendo ni "NDIYOOOOO" kwa kila afanyalo Rais hata kama linavunja msingi na mwiko wa taifa letu?
Uzalendo ni kuunga mkono chochote kilicho chema kwa taifa regardless kimefamywa na nani? Kinachopaswa kuungwa mkono ni MTU au KITENDO?
Wewe ni mjuvi wa kiwango cha lami. Umesoma ukaelimika.Mheshmiwa Mpendazoe, shikamoo!! Kwa sasa nitajikita katika maana ya uzalendo.
Pengine baadae nitarudi kujibu hoja zako zingine. Nimeona msingi wa hoja yako ipo kwenye neno "uzalendo" hadi umehoji uzalendo wa Tundu Lissu (TL) uko wapi.
Nijuavyo mimi uzalendo ni mapenzi ya kujitoa, kuunga mkono na kuilinda nchi yako;utii kwa taifa lako (i.e devoted love, support, and defense of one's country; national loyalty). Hapa hakuna maneno mawili "rais" na "chama cha siasa".
Kwa sababu binfasi, sababu za kisiasa, sababu za kutetea maslahi binafsi, watanzania wengi tena wengi wao ni wasomi wamekuwa wakipotosha maana ya neno "uzalendo". Wao kwenye neon "taifa" au "nchi" wanaweka neon "rais" kwenye definition ya neon uzalendo.
Mark Twain alipata kusema "patriotism is supporting your country all the time, and your government when it deserves it". Pia Edward Abbey alipata kusema "A patriot must always be ready to defend his country against his government".
Hapa utaona utofauti kati ya nini mzalendo anapaswa kutetea; Je ni serikali (including rais) au Je ni nchi/taifa?
Serikali ni watu ambao wapo wema na wabaya lakini nchi/taifa lina misingi na miiko yake ikiwemo demokrasia, utawala wa sheria, umoja, huduma bora za kijamii, amani nk. Je, anayoyafanya TL hata kuhoji uzalendo wake ana-defend nini? Unachofanya wewe Mpendazoe, JPM nk mna-defend nini?
Uzalendo ni "NDIYOOOOO" kwa kila afanyalo Rais hata kama linavunja msingi na mwiko wa taifa letu?
Uzalendo ni kuunga mkono chochote kilicho chema kwa taifa regardless kimefamywa na nani? Kinachopaswa kuungwa mkono ni MTU au KITENDO?
Sitegemei wa kanda ya ziwa aandike tofautu ni ulivyoandika mheshimiwa...Nilisikiliza hotuba ya Mh Tundu Lissu aliyoitoa huko jimboni kwake akimshambulia Mh Rais wa Jamhuri Ya Muungano wa Tanzania JPM kwamba ni dikteta uchwara, ni mkabila na anaendesha nchi kwa upendeleo.
Ameomba Jumuiya ya Kimataifa iinyime misaada Tanzania na waizomee Tanzania kutokana na uongozi mbaya wa JPM unaogandamiza demokrasia nchini. Mh.Tundu Lissu alionyesha hasira na dharau kubwa kwa Rais wakati akitoa hotuba hiyo.
Kwanza nianze na masuali ya jumla :
Mimi ninajiuliza, je Mh Lissu na viongozi wengine wa upinzani hawawezi kabisa kuikosoa Serikali bila kutumia matusi na kejeli ? Je hawawezi kabisa kutoa maoni yao bila kutoa matusi na kejeli kwa viongozi waliopo madarakani?
Pamoja na Elimu aliyonayo Mh Tundu Lissu haelewi kwamba Mh John P Magufuli amechaguliwa na wa Tanzania na ni kiongozi wa Nchi na lugha anayoitumia dhidi yake inalidhalilisha Taifa ?
Naomba nitazame hoja za Mh Lissu.
1. Madai kuhusu demokrasia kuminywa na haki na Uhuru wa kutoa maoni. Wakati Mh Lissu anadai haya kwa Serikali iliyopo madarakani angewatetea wanachadema kuhusu haki na Uhuru wa kutoa maoni na demokrasia ndani ya Chadema. Mfano Lowassa alishindanishwa na nani wakati wa kugombea urais 2015.
Sikumsikia Mh Lissu akimuijia juu Mbowe wakati alipobadilisha gia angani. Wengi watakumbuka uchaguzi wa viongozi wa jumuia za Chama ndani ya Chadema ulivyokuwa umegubigwa na ubabe kwa kisingizio cha maslahi mapana ya Chama. Mh Lissu alikaa kimya.
Dk Slaa aliondolewa kwenye kugombea urais ndani ya Chadema kibabe, Mh Lissu alitetea ujio wa Lowassa. Mh Lissu na Chadema haiwezi ikawa msemaji wa kudai demokrasia nchini wakati ndani ya Chadema kuna udikiteta ulipitiliza.
2. Kuhusu haki na Uhuru wa kutoa maoni. Uhuru na haki hiyo haijazuiwa isipokuwa lipo tatizo kubwa upande wa Lissu na wengine kwenye upinzani. Wakijenga hoja na kutoa maoni yao bila matusi sidhani kama watakatazwa.
Hakuna jambo linalokera na kuudhi kama lugha zinazotumiwa Mh Lissu na baadhi ya wapinzani. Watambue pia kama wao walivyo na haki ya kutoa maoni pia Rais nae ana haki zake kama kiongozi wa Nchi. Haikubaliki mtu atumie lugha ya kejeli, dharau, na matusi kwa Rais na kiongozi wa Nchi kwa kisingizio cha haki na Uhuru wa kutoa maoni. Hapana.
3. Lissu amezungumzia suala la ukabila na upendeleo wa kiukoo. Inasikitisha na ni hatari sana kwa kuanza kuleta hoja za ukabila na ukoo au undugu au udini. Ni kweli JPM analo Kabila lake, ukoo wake wa kuzaliwa na dini yake. Lakini JPM kama Rais, ni baba wa Tanzania wote.
Na koo zote ni zake, watumishi wote ni wake, na wanajeshi wote ni wake. Hivyo, Mh Rais anayo haki ya kumchagua yeyote katika nafasi yoyote anayemwona ataweza kumsaidia katika kutekeleza majukumu yake bila kujali alikotoka au dini au kabila au ukoo au hata Chama.
Hivyo, hoja alizozitoa Mh Lissu kuhusu ukabila au ukanda ni matatizo yake ya kifikra. Wengine hawaoni kama anavyoona yeye Mh Lissu. Mh Lissu ndiye mwenye ukabila, udini, na ukanda. Watanzania wengi wameondokana na fikra hasi alizonazo Mh Lissu. Inawezekana, hoja za ukabila, ukanda, udini na ukoo bado zipo Chadema.
4. Mh Lissu ameiomba Jumuiya ya Kimataifa iinyime misaada Tanzania. Ni jambo La kushangaza kweli! Moja ya viongozi wanaozungumzwa duniani kuhusu uongozi bora ni Rais JPM. Jitihada za Rais JPM katika kupiga vita rushwa na ufisadi zinaonyesha matunda.
Kama Chadema ilikuwa imedhamiria kweli kupiga vita rushwa na ufisadi inatakiwa imuunge mkono Rais JPM. Lakini cha kushagaza kabisa Mh Lissu kuhusu suala la ufisadi amekuwa kimya tangu Chadema wampokee Lowassa. Mh Lissu tangu wakati huo alibadilika.Mh Lissu aligeka jiwe.
Mh JPM anapigania kwa dhati utajiri wa Nchi yetu ili uweze kuwanufaisha watanzania wote. Mh Lissu na hili limemkera mpaka anaombea Tanzania ishitakiwe na makampuni yanayochimba madini nchini !
Mh Rais JPM anapambana kwa dhati na uzembe na ubadhirifu kwenye mashirika ya umma na Serikali, Mh Lissu na hili linamkera kwani alishasema atawatetea wale wote wanaotumbuliwa ! Very sad. Kwa juhudi hizi zinazofanywa na Serikali ya awamu ya 5 bado Mh Lissu anashawishi nchi na Jumuiya ya Kimataifa ziisusie Tanzania na kuinyima misaada! Inasikitisha sana.
Uko wapi Uzalendo wa Mh Lissu kwa Nchi yake ?
Mimi ninaamini Mh Rais anastahili kuungwa mkono kwani ameonyesha kwa dhati anatetea wanyonge.
Sent using Jamii Forums mobile app