Nawashangaa sana wananchi, wachumi, viongozi wa dini na wanasiasa wa Tanzania. Naomba tutafakari pamoja yafuatayo na kisha, pamoja na maoni yangu, tujibu maswali yatakayofuata:
Section A (Sehemu ya kwanza)
Phase I (Awamu ya kwanza) (November 2015-June 2017)
Rais: Haiingii akilini kwa nchin yetu kutegemea misaada. Sisi tuna kila kitu, hatupaswi kuendesha nchi yetu kwa kutegemea
misaada. Kwanza hii misaada ina masharti mengi, na masharti mengine yanakwenda kinyume na utamaduni wetu.
Katika kipindi changu cha uongozi sitategemea misaada. Tunatakiwa sisi tukopeshe na kusaidia mataifa mengine na
siyo kusaidiwa. Misaada inatweza utu wetu.
Itikio la wasomi, wachumi, wananchi na wanasiasa: Tanzania tumempata Rais tuliyemhitaji tangu zamani. Tumechoka
na uhuru wa bendera. Tunatakiwa kujitegemea maana tuna kila kitu. Hatuwezi kuendelea kwa kutegemea misaada
ambayo wakati mwingine inatweza utu wetu. Hakuna nchi iliyoendelea duniani kwa kutegemea misaada. Huyu
anayekataa kuongoza nchi kwa kutegemea misaada anatufaa sana! Tumuunge mkono. Tanzania tuna kila raslimali na
ni aibu kutegemea misaada.
Phase II (Awamu ya pili) (July 2017)
Lissu: Nchi inaongozwa kinyume na Katiba. Kuna ukandamizaji mkubwa wa demokrasia nchini. Nchi haifuati mfumo wa vyama vingi. Vyama vya upinzani vinazuiwa kufanya shughuli za siasa. Viongozi wa upinzani wanakamatwa ovyo bila sababu maalumu. Jeshi la polisi, wakuu wa wilaya na mikoa wanatumika kukandamiza demokrasia ya vyama vingi. Mihimili mingine ya dola inadharaulika na kunyimwa uhuru wao. Uhuru wa kutoa maoni nchini umekosekana. Serikali inatumia fedha za kodi zetu na misaada kukandamiza demokrasia. Kwa hali hii tutaomba jumuiya za kimataifa ziinyime Tanzania misaada kwani inatumika vibaya kuminya demokrasia nchini.
Itikio la wasomi, wachumi, wananchi na wanasiasa: Huyu Lissu haitakii mema nchi. Hatuwezi kuendesha nchi na kuwahudumia watu wetu bila misaada toka nje. Mtu anayetaka kukwamisha misaada hatufai, apuuzwe kabisa. Msaada ndio nguzo ya maendeleo yetu. Hivi tukinyimwa misaada ataumia Lissu au Rais? Watakaoumia ni wananchi. Nchi haiwezi kwenda bila misaada.
Swali: Unapata picha gani ya wasomi, wananchi, wanasiasa na wachumi wa Tanzania?
My take: Kinachoungwa mkono Tanzania siyo nguvu ya hoja bali nani katoa hoja.
Section B (Sehemu ya pili)
Phase I (Awamu ya kwanza) (Julai 2015-Juni 2017)
Mkapa: Watanzania acheni kulialia. Watanzania ni wapumbavu na malofa.
Itikio la viongozi wa dini: Kimyaaaaaaaaa
Phase II (Awamu ya pili) (Julai 2017)
Lissu: Nchi inaongozwa kidikteta. Huyu kiongozi wetu ni udikteta. Udikteta uchwara umetamalaki nchini. Tuupinge kwa nguvu zote, viongozi wa dini wapinge na kila mtu kwa nafasi yake apinge maana hakuna aliye salama.
Itikio la viongozi wa dini (hasa kupitia msiba wa mke wa Mwakyembe): Hatutaki lugha za kuudhi na kuwakejeli viongozi wetu. Hatutamuunga mkono anayempinga Rais wetu na kumtolea lugha za kuudhi au matusi. Hiyo tabia ikome.
Swali: Unapata picha gani ya viongozi wa dini nchini?
My take: Tangu enzi na enzi viongozi wa dini (mafarisayo na masadukayo) wamekuwa upande wa tabaka tawala. hawajawahi kuwa upande wa wanyonge. Pia watu hawa hawakemei ubaya wa dhambi bali huangalia nani kafanya dhambi ndipo wakemee.