Tundu Lissu: Watoto wangu ni raia wa Marekani kwa kuzaliwa kwao

GUSSIE

JF-Expert Member
Dec 2, 2014
3,866
11,100
Makamu mwenyekiti wa chadema mh Tundu Lissu akiongea na diaspora wa Tanzania waishio Marekani kwenye suala la uraia pacha amegusia kuhusu maisha ya watoto wake wawili wanaosoma vyuo vikuu vya Marekani

Mosi, Tundu Lissu anasema watoto wake wawili walizaliwa Marekani katika hospitali ya George Town University miaka ishirini na moja iliyopita na hivyo wana haki za kugombea Urais wa Marekani na watoto wake hawahitaji visa kama yeye na mkewe kuingia Marekani kwani watoto ni Raia wa Marekani

Tundu Lissu amesema kwa sasa watoto wake mmoja anasoma George Town University Atalanta Marekani na mwngine anasoma Kenneth State University Marieta Georgia Marekani

Pili, Tundu Lissu amesisitiza watoto wake hawana haki yoyote ya kurithi mali zake za Tanzania kwa mujibu wa sheria za Tanzania hususani suala la ardhi kutokana ni Raia wa Marekani

Tatu,Tundu Lissu amesisitiza ni lazima suala la uraia likafikiliwa upya kwani watanzania wapo wengi wenye elimu bora lakini wanashindwa kusaidia nyumbani kutokana na sheria za Tanzania zinazominya uraia pacha

Nne, Tundu Lissu amesisitiza pia kuwa watoto hawakuwa na maamuzi ya kuzaliwa Marekani bali ni maamuzi ya wazazi, Lakini kwa sheria za Tanzania masuala ya wazazi yanawaathiri watoto ambao hawakuwa na maamuzi wazaliwe nchi gani.
 
Makamu mwenyekiti wa chadema mh Tundu Lissu akiongea na diaspora wa Tanzania waishio Marekani kwenye suala la uraia pacha amegusia kuhusu maisha ya watoto wake wawili wanaosoma vyuo vikuu vya marekani

Mosi,Tundu lissu anasema watoto wake wawili walizaliwa marekani katika hospital ya George town university miaka ishirini na moja iliyopita na hivyo wana haki za kugombea uraisi wa Marekani na watoto wake hawahitaji visa kama yeye na mkewe kuingia marekani kwani watoto ni Raia wa marekani

Tundu lissu amesema kwa sasa watoto wake mmoja anasoma George town university Atalanta na mungine anasoma kenneth state university Marieta Georgia

Pili,Tundu lissu amesisitiza watoto wake hawana haki yeyote ya kurithi mali zake za Tanzania kwa mujibu wa sheria za Tanzania hususani suala la ardhi kutokana ni Raia wa Marekani

Tatu,Tundu lissu amesisitiza ni lazima suala la uraia likafikiliwa upya kwani watanzania wapo wengi wenye elimu bora lakini wanashindwa kusaidia nyumbani kutokana na sheria za Tanzania zinazominya uraia pacha

Nne,Tundu lissu amesisitiza pia kuwa watoto hawakuwa na maamuzi ya kuzaliwa marekani bali ni maamuzi ya wazazi,Lakini kwa sheria za Tanzania masuala ya wazazi yanawaathiri watoto ambao hawakuwa na maamuzi wazaliwe nchi gani?
Jamaa kwa kudandia sera za watu ni mjanaja sana.

Hayo mbona tayari yameshafanyiwa kazi na diaspora "special status" inangoja wakati muafaka ipelekwe bungeni ikawe sheria.
 
Ni exposure tu mkuu,

Sasa wewe watoto wako wote wamezaliwa nanjilinji na somanga tunaweza pata mawazo mapya kama Taifa kweli?

Hao watoto wa Lissu hawafundishwi binadamu alitokana na nyani kama watoto wa kitanzania wanavyodanganywa

Tanzania Baba alidanganywa binadamu anatokana na nyani mwaka 1972 ,anazaa mtoto naye mtoto mwaka 1992 anafundishwa binadamu ametokana na nyani
Hawa ni marekani bado wale wa ubelgiji, utagundua ndiyo maana hupenda kweli kinuke! Mbakie mkiuana ovyo!
Watanzania hawapendi kabisa kusikia mambo ya kujisifia matoto yako ni raia wa nje, that mean wewe hatupo pamoja, heri mbowe kuliko huyu jamaa, ishi kitanzania ishi kizalendo, onyesha utanzania na kujali Tanzania.
 
Lissu The Greatest!
F6xfq_lXcAAF1vV.jpeg
 
Ni kutumia akili tu
Halafu mtoto anasoma shule ya kata unataka akafanye kazi UNESCO,UNICEF ,WB kwa kiingereza cha ugoko

Ni ngumu kuwaweka kapu moja watoto wa Lisu na watoto wa watanzania wengi kwenye uelewa na competition za ajira

Bongo elimu ilijifia miaka ya 2000 kurudi nyuma

Kweli ni kutumia akili tu,Maamuzi yake ya miaka ishirini sasa anakula maisha
 
Jamaa kwa kudandia sera za watu ni mjanaja sana.

Hayo mbona tayari yameshafanyiwa kazi na diaspora "special status" inangoj awakati muafaka ipelekwe bingeni ikawe sheria.
Punguza pupa kidogo ukiwa katika uandishi mama. Lakini pia nadhani lissu amefanya nao mazungumzo kama kuwaunga mkono katika walilolianzisha hao diaspora
 
Back
Top Bottom