Jamani nauliza hivi kwa sababu nimeangalia kesi inayoendelea kati ya Winshear Gold Corp na Tanzania ARBN 20/25 kwa kweli inasikitisha. Profesa hana majibu yoyote yanayoweza kuishawishi Tribunal kuamua in favor of Tanzania. Kwa sababu hiyo, ninasikitika sana kuona wasomi na walimu wakongwe wa vyuo vikuu hawafanyi yanayostahili kufanywa na wao kwa maslahi mapana ya nchi.
Prof. Mbarawa, yeye amesaini mkataba bila kujua ni mkataba, bali akijua ni makubaliano. Prof. Sospeter Muhongo, naye kafanya yake wakati akiwa waziri wakati ule. sasa jamani Uprofesa usio argue kabla ya kutenda jambo ni uprofesa gani? hasa jambo lenye maslahi ya kitaifa.
Mikataba hii imeendelea kuiletea nchi madhila makubwa sana kimataifa na hata kitaifa. Tutaendelea kuwa na watu wa ajabu ambao kila kukicha wanaliingizia taifa hasara ya kukamatwa kwa rasilimali zetu ama kulazimika kulipa uzembe alioufanya mtu anayejiita Profesa na nguli wa mambo fulani. Jamani hili Taifa linamwitaji Mungu sana kuliko kawaida.
Prof. Mbarawa, yeye amesaini mkataba bila kujua ni mkataba, bali akijua ni makubaliano. Prof. Sospeter Muhongo, naye kafanya yake wakati akiwa waziri wakati ule. sasa jamani Uprofesa usio argue kabla ya kutenda jambo ni uprofesa gani? hasa jambo lenye maslahi ya kitaifa.
Mikataba hii imeendelea kuiletea nchi madhila makubwa sana kimataifa na hata kitaifa. Tutaendelea kuwa na watu wa ajabu ambao kila kukicha wanaliingizia taifa hasara ya kukamatwa kwa rasilimali zetu ama kulazimika kulipa uzembe alioufanya mtu anayejiita Profesa na nguli wa mambo fulani. Jamani hili Taifa linamwitaji Mungu sana kuliko kawaida.