Ukiumiza watu kwa kudhani wewe ni mzalendo sana kumbuka ukiondoka Nchi ina baki palepale wanachukua wengine

Rasterman

JF-Expert Member
Feb 24, 2015
33,905
44,017
Ndugu wanajamii naungana na Paul Mayalla ktk makala zake za Kwa Maslahi ya taifa.

Tukiwa ktk wikendi hii ni vema tukatafakari jambo hili. Kumbe cheo ni dhamana. Siasa ni swala la kitaifa sio la mtu binafsi na kwamba usijimilikishe michakato ya kitaifa kufika hatua ya kuumiza watu wengine ili kujionesha wewe ndio mzalendo sana.

Kumbuka ukifanya hivyo sana sana unafurashisha na kunufaisha wapambe wako lakini ukiondoka nafasi hiyo hiyo atachukua mwingine na nchi itasonga mbele. So kama ulikuwa unadhani bila wewe nchi haisongi mbele unajidanganya.

Mfano tunao sasa, Mh Rais Samia Nchi inasonga vizuri tu. waliodhani bila wao hatuwezi kusonga mbele wajiulize tena na tena. Kukuru kakara zote pengine hazikuwa maana sana kwao bali kwa wapambe wao.

Tujiulize tena je Jiji la Dar es salaam limesinama? Si linasonga mbele bila Paul Makonda? Sasa yale maugomvi yalikuwa ya nini?

Leo nani angeamini kuwa Uhuru Kenyata iko siku ataungana na Raila Odinga wawe na wazo moja na maono mamoja?

Kama wewe unaweka swala la siasa kama jambo binafsi kiasi cha kuanza kuwinda na kutesa watu sababu ya siasa, kutukana na kukera watu sababu ya siasa now you must have learned.

Ipo siku Kiongozi mkubwa wa CCM tena yamkini Mwenyekiti ataungana na Mpinzani; sijui utakuwa upande gani ndugu yangu . Linapokuja swala la Maslahi ya Taifa watu makini huwa wanakuwa kitu kimoja kama Uhuru Kenyata na Raila Odinga.

Je Kwa sababu IGP ni mwingine ndio kusema polisi yetu haitafanya kazi? La hasha itasonga ktk majukumu yake pengine kwa ubora zaidi. Sasa kubambikia kesi watu kwa nini?

Wilaya ya Hai hawana Maji kwa sababu Sabaya hayupo? Au kuna hospitali imefungwa kwa sababu hayupo Mzalendo General Sabaya?

Vipi Chama tawala ccm hakisongi mbele sababu Mangula hayupo? Sasa walishindwa nini kushauri mambo mema yakupendeza Mungu na wanadamu?

Vipi Bunge nalo limefungwa kwa sababu Ndugai hayupo? Linasonga mbele tena likiwa Live. Sasa majivuno na makasiriko yalikuwa ya nini kwa Mr Job?

Mwisho: Huu ndio muda mwafaka pekee kwa Rais Samia kuhakikisha Nchi inatawalika kwa misingi ya sheria bora na Katiba bora.
Ipo siku ataihitaji na kama atafata huu ushauri huko mbeleni atanishukuru.

Nakutakia Kazi njema Mh Rais Samia Suluhu ktk ujenzi wa Taifa.
 
Ndugu wanajamii naungana na Paul Mayalla ktk makala zake za Kwa Maslahi ya taifa.

Tukiwa ktk wikendi hii ni vema tukatafakaei jambo hili. Kumbe cheo ni dhamana. Siasa ni swala la kitaifa sio la mtu binafsi na kwamba usijimilikishe michakato ya kotaifa kufika hatua ya kuumiza watu wengine ili kujionesha wewe ndio Mjanja sana...
Katiba Mpya ni kwa faida ya wananchi wote, wenye vyama na wasio na vyama. Ni chachu ya maendeleo ya taifa.
 
Ndugu wanajamii naungana na Paul Mayalla ktk makala zake za Kwa Maslahi ya taifa.

Tukiwa ktk wikendi hii ni vema tukatafakari jambo hili. Kumbe cheo ni dhamana. Siasa ni swala la kitaifa sio la mtu binafsi na kwamba usijimilikishe michakato ya kitaifa kufika hatua ya kuumiza watu wengine ili kujionesha wewe ndio mzalendo sana.

Kumbuka ukifanya hivyo sana sana unafurashisha na kunufaisha wapambe wako lakini ukiondoka nafasi hiyo hiyo atachukua mwingine na nchi itasonga mbele. So kama ulikuwa unadhani bila wewe nchi haisongi mbele unajidanganya.

Mfano tunao sasa, Mh Rais Samia Nchi inasonga vizuri tu. waliodhani bila wao hatuwezi kusonga mbele wajiulize tena na tena. Kukuru kakara zote pengine hazikuwa maana sana kwao bali kwa wapambe wao.

Tujiulize tena je Jiji la Dar es salaam limesinama? Si linasonga mbele bila Paul Makonda? Sasa yale maugomvi yalikuwa ya nini?

Leo nani angeamini kuwa Uhuru Kenyata iko siku ataungana na Raila Odinga wawe na wazo moja na maono mamoja?

Kama wewe unaweka swala la siasa kama jambo binafsi kiasi cha kuanza kuwinda na kutesa watu sababu ya siasa, kutukana na kukera watu sababu ya siasa now you must have learned.

Ipo siku Kiongozi mkubwa wa CCM tena yamkini Mwenyekiti ataungana na Mpinzani; sijui utakuwa upande gani ndugu yangu . Linapokuja swala la Maslahi ya Taifa watu makini huwa wanakuwa kitu kimoja kama Uhuru Kenyata na Raila Odinga.

Je Kwa sababu IGP ni mwingine ndio kusema polisi yetu haitafanya kazi? La hasha itasonga ktk majukumu yake pengine kwa ubora zaidi. Sasa kubambikia kesi watu kwa nini?

Wilaya ya Hai hawana Maji kwa sababu Sabaya hayupo? Au kuna hospitali imefungwa kwa sababu hayupo Mzalendo General Sabaya?

Vipi Chama tawala ccm hakisongi mbele sababu Mangula hayupo? Sasa walishindwa nini kushauri mambo mema yakupendeza Mungu na wanadamu?

Vipi Bunge nalo limefungwa kwa sababu Ndugai hayupo? Linasonga mbele tena likiwa Live. Sasa majivuno na makasiriko yalikuwa ya nini kwa Mr Job?

Mwisho: Huu ndio muda mwafaka pekee kwa Rais Samia kuhakikisha Nchi inatawalika kwa misingi ya sheria bora na Katiba bora.
Ipo siku ataihitaji na kama atafata huu ushauri huko mbeleni atanishukuru.

Nakutakia Kazi njema Mh Rais Samia Suluhu ktk ujenzi wa Taifa.
Ni aibu kwa mtu mwenye akili timamu kutojua kuwa Taifa halisongi mbele!

Watu wanaendelea na maisha yao, Ila Taifa limesimama!

Ni aibu kwa mtu mwenye akili zake timamu, kutojua kuwa mifumo ya usimamizi na uongozi wa Taifa Ni mibovu hivyo Taifa haliwezi kusonga mbele

Mpumbavu Ni Nani?

Mpumbavu Ni yule anayesifia Taifa linasonga mbele, Kisha anaanza kudai katiba mpya!

Asali Ni tamu sana!!

Kama Taifa linasonga mbele, Sasa madai ya katiba ya Nini?

Hao wanaokataa kuandaa katiba mpya, Wana hoja Kama yako, kuwa Taifa linasonga mbele, kwa amani na utulivu, kwa maendeleo endelevu!

Walamba asali wote Kama wewe mtoa mada, wanajisaulisha kuwa katiba Ni ingini ya kulifanya Taifa lisonge mbele!

Wenye akili timamu tunawaza kwamba maono ya wazalendo yaingizwe kwenye katiba ili kuondoa tatizo linalotokea la Taifa kusimama na kulala pale mzalendo anapoondoka madarakani!
 
Kila nikikumbuka urais wa magufuri naumia sana najitaidi kusamehe nashindwa.

Kilikuwa kipindi kibaya sana uhuru wa kutoa maoni 0%.

Tumshukuru mungu Kwa kumuuwa mapema, maana angemaliza miaka Kumi magereza yangekuwa yamejaa wafungwa was kesi za kubambikiwa na akina kingai.

Imagine mpaka jeshini watu walikuwa wanabambikiwa kesi za kumtukana huyo mbwa marehemu.

Kila sehemu kulikuwa na wapambe wake wanabambikia TU watu kesi.

Tumshukuru Mungu Sasa nchi inaamani na utulivu.

Tujitaidi kupigania katiba mpya Ili asijetokea kichaa mwingine kama magufuri, hakika tutaangamia.
 
Unaweza kujiuliza

1. Je rais Samia Suluhu Hassan hasemwi?
2. Je hakuna wanao mbeza?
3. Hakuna wanao mponda?

Sasa mbona kesi za kubambikiwa hakuna?

Imagine wanajeshi wanakamata mwanajeshi na kumpa KESI ya kumtukana rais.

Watanzania tulifika pabaya sana.

Malipo ni hapahapa. Mungu ni mwema sana. Akamuuwa haraka baada ya kuona hata Wana wa Mungu wanabambikiwa kesi. Miezi ilipita SITA TU baada ya kubambikiwa kesi maombi yakakolea tarehe Saba mwezi march jamaa akavuta. Wakaacha kutoa taarifa wakachanganyikiwa. Jamaa alikufa tarehe 7 sio 17. Alikufa haraka sana Ili kuliponya Taifa.
 
Kila nikikumbuka urais wa magufuri naumia sana najitaidi kusamehe nashindwa.

Kilikuwa kipindi kibaya sana uhuru wa kutoa maoni 0%.

Tumshukuru mungu Kwa kumuuwa mapema, maana angemaliza miaka Kumi magereza yangekuwa yamejaa wafungwa was kesi za kubambikiwa na akina kingai.

Imagine mpaka jeshini watu walikuwa wanabambikiwa kesi za kumtukana huyo mbwa marehemu.

Kila sehemu kulikuwa na wapambe wake wanabambikia TU watu kesi.

Tumshukuru Mungu Sasa nchi inaamani na utulivu.

Tujitaidi kupigania katiba mpya Ili asijetokea kichaa mwingine kama magufuri, hakika tutaangamia.
Unaonekana bado una hasira nae sana mkuu, msamehe bure hayupo tena
 
Ni aibu kwa mtu mwenye akili timamu kutojua kuwa Taifa halisongi mbele!

Watu wanaendelea na maisha yao, Ila Taifa limesimama!

Ni aibu kwa mtu mwenye akili zake timamu, kutojua kuwa mifumo ya usimamizi na uongozi wa Taifa Ni mibovu hivyo Taifa haliwezi kusonga mbele

Mpumbavu Ni Nani?

Mpumbavu Ni yule anayesifia Taifa linasonga mbele, Kisha anaanza kudai katiba mpya!

Asali Ni tamu sana!!

Kama Taifa linasonga mbele, Sasa madai ya katiba ya Nini?

Hao wanaokataa kuandaa katiba mpya, Wana hoja Kama yako, kuwa Taifa linasonga mbele, kwa amani na utulivu, kwa maendeleo endelevu!

Walamba asali wote Kama wewe mtoa mada, wanajisaulisha kuwa katiba Ni ingini ya kulifanya Taifa lisonge mbele!

Wenye akili timamu tunawaza kwamba maono ya wazalendo yaingizwe kwenye katiba ili kuondoa tatizo linalotokea la Taifa kusimama na kulala pale mzalendo anapoondoka madarakani!
Madai ya katiba Mpya ni ili Taifa lisonge mbele zaidi kwa misingi ya haki zaidi.
 
Ndugu wanajamii naungana na Paul Mayalla ktk makala zake za Kwa Maslahi ya taifa.

Tukiwa ktk wikendi hii ni vema tukatafakari jambo hili. Kumbe cheo ni dhamana. Siasa ni swala la kitaifa sio la mtu binafsi na kwamba usijimilikishe michakato ya kitaifa kufika hatua ya kuumiza watu wengine ili kujionesha wewe ndio mzalendo sana.

Kumbuka ukifanya hivyo sana sana unafurashisha na kunufaisha wapambe wako lakini ukiondoka nafasi hiyo hiyo atachukua mwingine na nchi itasonga mbele. So kama ulikuwa unadhani bila wewe nchi haisongi mbele unajidanganya.

Mfano tunao sasa, Mh Rais Samia Nchi inasonga vizuri tu. waliodhani bila wao hatuwezi kusonga mbele wajiulize tena na tena. Kukuru kakara zote pengine hazikuwa maana sana kwao bali kwa wapambe wao.

Tujiulize tena je Jiji la Dar es salaam limesinama? Si linasonga mbele bila Paul Makonda? Sasa yale maugomvi yalikuwa ya nini?

Leo nani angeamini kuwa Uhuru Kenyata iko siku ataungana na Raila Odinga wawe na wazo moja na maono mamoja?

Kama wewe unaweka swala la siasa kama jambo binafsi kiasi cha kuanza kuwinda na kutesa watu sababu ya siasa, kutukana na kukera watu sababu ya siasa now you must have learned.

Ipo siku Kiongozi mkubwa wa CCM tena yamkini Mwenyekiti ataungana na Mpinzani; sijui utakuwa upande gani ndugu yangu . Linapokuja swala la Maslahi ya Taifa watu makini huwa wanakuwa kitu kimoja kama Uhuru Kenyata na Raila Odinga.

Je Kwa sababu IGP ni mwingine ndio kusema polisi yetu haitafanya kazi? La hasha itasonga ktk majukumu yake pengine kwa ubora zaidi. Sasa kubambikia kesi watu kwa nini?

Wilaya ya Hai hawana Maji kwa sababu Sabaya hayupo? Au kuna hospitali imefungwa kwa sababu hayupo Mzalendo General Sabaya?

Vipi Chama tawala ccm hakisongi mbele sababu Mangula hayupo? Sasa walishindwa nini kushauri mambo mema yakupendeza Mungu na wanadamu?

Vipi Bunge nalo limefungwa kwa sababu Ndugai hayupo? Linasonga mbele tena likiwa Live. Sasa majivuno na makasiriko yalikuwa ya nini kwa Mr Job?

Mwisho: Huu ndio muda mwafaka pekee kwa Rais Samia kuhakikisha Nchi inatawalika kwa misingi ya sheria bora na Katiba bora.
Ipo siku ataihitaji na kama atafata huu ushauri huko mbeleni atanishukuru.

Nakutakia Kazi njema Mh Rais Samia Suluhu ktk ujenzi wa Taifa.
Magufuli alijua bila yeye Nchi itasimama labda
 
1.Kuna yule aliyetangulia 'kule'
2.Kuna huyu aliyekuwa mtawala wa dsm mwizi, jambawazi, katili, dhulumati wa 'maisha ya watu'
3. kuna lile jambawazi lingine la kimasai lililofikia hadi kupora wake za watu na kukata watu wasikio!
4. Kuna yule mwingine mburuza miguu aliyeona yeye 'mjengoni' atakaa milele
Haya maisha ni ya kupita jamani acheni uhayawani
 
Katiba mpya ni suala la lazima la si hivyo kuna siku nchi itarudi kuwa mateka kama ilivyokuwa miaka 6 iliyopita.
 
Katiba mpya ni suala la lazima la si hivyo kuna siku nchi itarudi kuwa mateka kama ilivyokuwa miaka 6 iliyopita.
Bila katiba mpya huyu mama ni Hatari kwa nchi hii ubaya anafanya kutumia TAKUKURU, CAG na DPP kujifanya anapambana na wamwendazake hao jamaa zake marehemu Jiwe wakichukua nchi Tena mama amekwisha
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom