Ukitapeliwa usifanye haya. Ni janga!

Ukitapeliwa usifanye haya. Ni janga!

miaka ya 1990 hivi, baada ya kumaliza manunuzi yangu mitaa ya Kariakoo nikawa nakatiza mitaa kuelekea kituo cha Kongo nichukue daladala kurudi nyumbani. Katikati ya hiyo mitaa nikakutana na machinga ameshika blausi mkononi akaniambia elfu nne, kiukweli blausi niliipenda maana fasheni yake ndio ilikuwa imeingia ila mkononi nilibakiwa na shilingi elf 2 na mia tano tuu. Nikaanza kuondoka nikijua siwezi inunua, akaniambia kwani una shilingi ngapi, nikamwambia elf 2 akasema lete nikuuzie. Haraka nikampa hela na kujua kuna kufungiwa kanyaboya nikamwambia usinifungie naondoka nayo mkononi ile nageuka nashikwa bega na kijana mwingine, sista hiyo blausi umeuziwa shilingi ngapi nikamwambia kwani vipi akasema hiyo hela haitoshi ongeza hela au rudisha balusi urudishiwe pesa yako. Nikasema isiwe tabu nipeni elfu 2 yangu niondoke. Kama Mungu ile napewa elfu 2 nikaiangalia kwa macho kumbe nashikishwa kikaratasi cha majaladio yale ya khaki.

Nikapata ujasiri ghafla wa kumshika shati yule jamaa nipe hela yangu nakuitia mwizi sasa hivi, akamwambia jamaa mwingine lete hiyo hela na matusi juu kuwa ulifikiri utapata nguo nzuri kwa bei rahisi hivyo. Niliishika hela yangu mkononi huku naondoka haraka kuelekea kituoni na kila dakika naiangalia ni ela kweli au itageuka kuwa karatasi looh.

Nilipenya tundu la sindano.
 
miaka ya 1990 hivi, baada ya kumaliza manunuzi yangu mitaa ya Kariakoo nikawa nakatiza mitaa kuelekea kituo cha Kongo nichukue daladala kurudi nyumbani. Katikati ya hiyo mitaa nikakutana na machinga ameshika blausi mkononi akaniambia elfu nne, kiukweli blausi niliipenda maana fasheni yake ndo ilikuwa imeingia ila mkononi nilibakiwa na shilingi elf 2 na mia tano tuu. Nikaanza kuondoka nikijua siwezi inunua, akaniambia kwani una shilingi ngapi, nikamwambia elf 2 akasema lete nikuuzie. Haraka nikampa hela na kujua kuna kufungiwa kanyaboya nikamwambia usinifungie naondoka nayo mkononi ile nageuka nashikwa bega na kijana mwingine, sista hiyo blausi umeuziwa shilingi ngapi nikamwambia kwani vipi akasema hiyo hela haitoshi ongeza hela au rudisha balusi urudishiwe pesa yako. Nikasema isiwe tabu nipeni elfu 2 yangu niondoke. Kama Mungu ile napewa elfu 2 nikaiangalia kwa macho kumbe nashikishwa kikaratasi cha majaladio yale ya khaki.

Nikapata ujasiri ghafla wa kumshika shati yule jamaa nipe hela yangu nakuitia mwizi sasa hivi, akamwambia jamaa mwingine lete hiyo hela na matusi juu kuwa ulifikiri utapata nguo nzuri kwa bei rahisi hivyo. Niliishika hela yangu mkononi huku naondoka haraka kuelekea kituoni na kila dakika naiangalia ni ela kweli au itageuka kuwa karatasi looh.

Nilipenya tundu la sindano.
Miaka ya 90 elfu 2 za noti zilikuwepo ?au mia 2 ya noti.
 
Narudia tena kusema binafsi nawakubali sana matapeli,hswstumii nguvu wao ni akili tu
Nalog off
 
Niliuziwa sabuni badala ya simu pale Kariakoo...huo ndo utapeli naoukumbuka
 
Na kwakuongezea hapo, ukishagundua umetapeliwa usianze kulia kwa sauti kubwa, kupiga mayowe na kugalagala chini. Sanasana hapo utawapa faida watu wengine watakaokua wanakuangalia na kufa mbavu kwa vicheko.

Mwisho kabisa ukitapeliwa usipoteze muda wako KWENDA POLISI!
Yaani polisi wa Tanzania sijui wapo vipi, ukitapeliwa wao wanaungana na tapeli tena unakuta hamna kinachofanyika! Unaweza lipwa kidogo au ikawa ndio basi tena...!

Sent from my STK-L21 using JamiiForums mobile app
 
Hii ya mwanao anaumwa niliwahi kutumiwa wakati mwenyewe sina mtoto nikaishia kuwasikitikia tu.

Siku nyingine nilitumiwa sms ninadaiwa hela ya kodi na mwenye nyumba nikaishia kucheka tu, wale watu wapuuzi kweli.

Utapeli niliofanyiwa ni kutolipwa hela yangu baada ya kuwakopesha panya fulani.
Mimi nilimwambia " Asante sana kwa taarifa, Mimi ni RPC Niko kwenye kikao, nitakupigia baadae tukimaliza kikao. Namba yako nimeisevu"
 
Wanawake dada zetu na mama zetu ni wahanga sana wa matapeli. Wana weakness ndogo sana wakikutana na mpiga saundi kiwango cha juu, kilaini hutoa kila kituuuu
 
wanawake dada zetu na mama zetu ni wahanga sana wa matapeli.wana weakness ndogo sana wakikutana na mpiga saundi kiwango cha juu.kilaini hutoa kila kituuuu
Hata mabrazamen kibao ni majanga! Wanalizwa tu deile!
 
Back
Top Bottom