Miaka ya nyuma nikiwa bado bwana mdogo ndio naanza maisha nilijikuta naiuza pikipiki yangu (niliyoipata kwa urithi na sikuwa na uwezo wa kuinunua) kwa Ml 1.2 na zote kumpatia tapeli wa mambo ya rupia! Nilifadhaika sana na kuingia unyonge haswa kwa kuwa ilikuwa ndio kitu pekee ninachokitegemea na cha thamani nilichonacho, maneno ya malawama ya mama mzazi na mke wangu yalizidi kuniumiza moyo haswa kwa kuwa walinikanya hapo kabla lakini sikuwaelewa.
Nilijikaza kiume nikajipa moyo na kuanza upya kwani hadi kazi nilishaacha nikajikuta nipo vijijini takribani miezi miwili nikiwawinda wabaya wangu na nikaambulia patupu, nilianza moja na kujipanga nikiwa na ghadhabu za maisha hatimae kazi zikakaa sawa nikanunua kwa jasho langu machine kubwa na yenye thamani kuliko ile na pia kufikia malengo kadhaa ya kimaisha kwani tukio lile kila nilipolikumbuka lilinifanya niamini zaidi kazi za mikono yangu ndio zitakazo nisogeza niongeze bidii kwani hakuna njia ya mkato.
Baadae nikahamia kwenye magari na hapo akatokea mtu ambae nilimuamini sana na kumtumia pesa mara nyingi na kunitumia spare na muda mwengine kuniletea yeye mwenyewe ila ghafla akaja kunitapeli laki nne za gear box na kubadilisha line! Maisha yana mambo mengi na mengine huja kama funzo na kukukomaza ki fikra hivyo huyu nae nilimuombea Mungu tu....baada ya miezi kadhaa nikapita mahali nikasikia vurugu kuna mtu anapigwa kufika ni yule jamaa kamtapeli mtu karibu ml 3 za mazao!!
Matukio hayo japo yalikuwa ni mabaya na kwa ambae hayajamkuta huona ni ya kizembe ila kwangu niliyageuza kuwa chachu ya mafanikio na leo hii ukisogea karibu tu nimeshakusoma ubongo wako kabla hujatoa kauli [emoji2][emoji2][emoji2]