Drone Camera
JF-Expert Member
- Jul 25, 2017
- 14,121
- 14,032
Usipende kukopa kopa.... Hasa kama ni kiasi kikubwa cha fedha
Yeah! Ila kwa kuwa umeshawajua mapema, itakusaidia kujua unaweza wapi kupata kwa uhakika msaada.Kweli mkuu,nilijiuliza swali moja...ndio mtu uko mgonjwa mahututi na inahitajika fedha ya dharura kutoka kwa mtu wa karibu unayemuamini...hapo si ndio itakuwa shida zaidi.
Kweli mkuu,sema ilitokea kutokana na malighafi kuhitajika zaidi saiti na muda unavyozidi kuongezeka na garama pia zinaongezeka.Usipende kukopa kopa.... Hasa kama ni kiasi kikubwa cha fedha
Kweli mkuu,kwenye shida ndio utajua mtu sahihiYeah! Ila kwa kuwa umeshawajua mapema, itakusaidia kujua unaweza wapi kupata kwa uhakika msaada.
Tatizo lenu hamlipi.Mnajifanya wapole sana muda wa kukopa.Time ya kurejesha mnakimbia.


kabisa, tena wakat wa kukopa anakuwa mpole balaa awaweza taka hadi kukuogesha.


aliahidi kitu kisichotekelezeka tena kwa mbwembwe.Kweli mkuu,ndio nimejifunza;na imebidi kuwatoa kwenye database yangu.Vinginevyo unaweza kujiaminisha nina marafiki,kumbe ni watu wa kula na kunywa tu.Sioni umuhimu wa kuwa na marafiki ambao amsaidiani.Yani wewe ukiwa unashida ,utafute mtu wa mbali wakati karibu yupo na uwezo anao.Au unarafiki Ila matatizo yake yanaishia Kwa watu wengine huko.
Rafiki zangu tunasaidiana kwa kweli ,na ndo wakwanza kuwacheki napo kwama.Nao pia wakikwama wananicheki
Sent using Jamii Forums mobile app
Tatizo mtu akuambii kama anayo ama hana...bali anakuahidi baadaye ukimpigia simu hapokeikabisa, tena wakat wa kukopa anakuwa mpole balaa awaweza taka hadi kukuogesha.
Sent using Jamii Forums mobile app
Ukitaka ukosane na rafiki omba akukopeshe fedha..
Siku mbili tatu zilizopita nilipata changamoto kidogo za kiuchumi,kutokana na mambo ya ujenzi....wajuzi wanasema zege hali lali,nikajishauri nikaona ngoja niombe fedha ya dharura kwa marafiki zangu.Majadiliano yakawa hivi:-
Mimi: mambo vipi mkuu?naomba unisaidie kiasi fulani cha dharura by alhamisi nitakurudishia hata kwa riba.
Rafiki 1: Sawa haina shida kaka nitakucheki baadaye
Baada ya hapo kimya,ukimpigia simu hapokei
Rafiki 2: Ok nitakupatia kesho
Kesho inafika kimya,ukimpigia simu hapokei
Rafiki 3: Siko vizuri kiuchumi,biashara zimesimama kaka
Bora huyu alikuwa muwazi na nilimuelewa
Rafiki 4 : Siko vizuri kaka,nitakupatia nusu yake
Mimi: Nashukuru nilikuwa naitaji full
Kutokana na hali hiyo,nilichoweza kujifunza ili usikosane na rafiki yako inabidi mahusiano yenu yasihusu mambo ya fedha.
Ha ha ha ha,binadamu tuishi nao kwa akiliMimi:Inakuaje kiongozi uko poa?
Rafiki:Fresh mwanangu,niambie kaka.
Mimi:Vipi michakato?
Rafiki:dah michakato iko poa mambo yako vizuri.
Mimi:aisee na hali hii kaka?
Rafiki:kaka pesa ukiitafuta mbona itakufuata,now mtaji umekua si unaona mwenyewe.
Mimi😛oa kaka hongera na jambo la kumshukuru Mungu,sasa Mkuu nimekwama hapa na huu mguu wako ,nina shida na elfu 10 hebu naomba unisaidie kesho kutwa jioni nitakupa sina hata mia ukicheki familia inahitaji kula.
Rafiki:Aisee pole sana ndugu yangu najisikia vibaya sana ,sasa umechelewa kidogo yaani nimetoa sasa hivi laki 8 kununua mzigo hapa nimebakiwa na elfu 5 kama nauli ila usijali kuna mtu hapa analeta pesa yangu laki 4 saa 11 jioni kama vipi pitia.
Mimi:sawa kaka nitashukuru
Saa 11 jioni
Mimi:Kaka umeshindaje?
Rafiki😀ah acha tu ndugu yangu.
Mimi:kuna usalama kweli?
Rafiki😀ah utoke wapi si unakumbuka nilikuambia kuna mtu ana pesa yangu laki 4 ana ileta leo ndo nikakwambia uje?
Mimi:Ndio nakumbuka kaka
Rafiki:Sasa yule mtu kafariki dah roho inaniuma kweli peaa yangu nishaikosa na hapa biashara leo ngumu sijui itakuaje ndugu yangu nilitamani kukusaidia ila nimekwama pia.
Hapo giza lishaingia ushafeli huna pa kwenda maana alikupa matumaini ukaweka kwake hukutaka kutafuta kwingine.
Watu wa namna hii ni hovyo sana mfano hai wiki mbili zilizopita tulikua na kikao cha harusi sista anataka kuolewa february 23 tukakubaliana tufanye sherehe ndogo kila mtu atoe laki moja,lakini Kaka yetu wa pili akagoma akasema tutoe laki mbili kila mmoja tulimgomea kwa kua uchumi mgumu lakini akashinda kwa kua aliungwa mkono na mama .Leo ndo siku ya kuwasilisha mchango tangu jana kazima simu zote hapatikanialiahidi kitu kisichotekelezeka tena kwa mbwembwe.
Sent using Jamii Forums mobile app
Inawezekana ikawa sababu mkuu,lakini si bora mtu akuambie ukweli...kuliko kukupa matumaini,baadaye ukimpigia simu muda aliokuahidi...hapokei simu.
Ha ha ha haHizi sio zama za kukopesha hovyo hovyo maana mambo ni mengi ikiwemo corona virus na vifo vya kuanguka bafuni
That's is itUsimkope rafiki yako mwambie naomba kiasi fulani sio kwa mkopo.
Na wala usimkopeshe rafiki yako inabidi umpe tu usimdai na kama huna sema huna.
Na hata Ndugu akikuomba umkopeshe muambie sina hela labda nikupe kiasi kidogo ufabye na mipango mingine upate kujazilia.
Na hata wewe ndugu Muombe hela usimkope.
Mimi kama unanikopa unaniambia utanirudishia kesho si bora usubiri hiyo kesho tu utumie pesa yako.omba bwana.
Sasa mfano wewe mtoa mada sijui kwa nini hukusubiri hiyo alhamisi tu ukatumia pesa yako.
Mkopo wa uhakika uende kwa watu ambao wapo kwa ajili ya kutoa huduma hiyo.
Saikolojia zetu sisi watu hatupendi kuombwa Mungu ndo hupenda watu wakimuomba.kwa hyo hakuna mtu atafurahi ukienda kumuomba kitu.
Fuata hii principle kisha rudi hapa
Sent using Jamii Forums mobile app
Wapo wa namna hiyo pia mkuuKuna rafiki yangu nilimkopesha alisema ana shida kubwa atanirudishia weekend,weekend ya mwaka juzi hadi leo haifiki,kila siku hana wakati bata anayokula si mchezo
Sent using Jamii Forums mobile app
Kwanini hataki kulipa deni?Nina machungu hapa kuna mtu namdai kaingia mitini nna hasira balaa
Sent using Jamii Forums mobile app