Ukitaka kujua kama unapendwa kweli ugua

Ukitaka kujua kama unapendwa kweli ugua

Oa mwanamke anayekupenda,
Wanaume wengi wanawashawishi kwa mali, wadhifa n.k ili kuwawin wanwake waingie nao kwenye ndoa na kuwamiliki pasipo kutengeneza mazingira ya kumfanya mwanamke akupende
Hilo ni la msingi sana, vizuri kwa huona hilo.
 
Hii yote n matokeo ya upendo wa upande mmoja, unakuta mwanaume ndye anampenda mwanamke mnoo wakat mwanamke hana habar nae......vivyo hivyo kwa mwanamke hutukia pndi mwanamke atakuwa ndye anapenda zaid ya mwanaume.

Upendo yapasa uwepo kwa mwanamke na mwanaume, mkipendana haya yote hayatatokea.
 
Hali gani? Wanawake wengi wa kitanzania wana unafiki na ubinafsi wa hali ya juu ndani yao. Hili nimelithibitisha yapata miaka 3 sasa. Wengi wakiumwa wao wanataka kuhudumiwa na kupewa attention na care, ila akiumwa mwanaume hata kukopa hela hataki.

Kuna jamaa yangu alikuwa anaumwa nimem save juzi tu hapa. Alikuwa na mke wake, mke alikuwa mfanyakazi mwenye kipato kizuri. Jamaa alikuws anahitaji 500K kwa ajili ya operation. Mke alikana kata kata kuwa na hela.

Imagine jamaa usiku halali ni kuugulia maumivu tu, analia wakati mwingine kama mtoto. Mbaya zaidi huyu mwanamke aliwahi kuumwa mwaka mzima, aliwahi kulazwa miezi miwili, jamaa alitoa jumla ya 5M ya matibabu. Hapo mke alipata hela special kazini ya likizo ya matibabu ila akaficha.

Huyu jamaa alimpigia ndugu yake amsaidie, ila mke wa huyo ndugu yake naye kamuambia mumewe wana majukumu mengi hivyo asitoe hiyo hela. Imagine mtu anateseka halafu wanapigiana mipira hivi.

Mwisho ikabidi anitafute. Nami bila hiyana nikam save jamaa yangu.

Funzo: mwanaume jijali, jipe raha na ujipende mwenyewe KWANZA. Potelea mbali hata wakikuona mbinafsi. 90+% ya mnaowaita wake zenu ni wabinafsi and they are money oriented.

Inasikitisha. Mke wake amenipigia simu ananishukuru(unafiki tu), jamaa kesho anakwenda kufanya OP.

Nimejifunza hapa. Huyu ni mmoja tu, je, wapo wangapi wanakufa kabisa kutokana na ubinafsi na uchoyo wa wanaowaita wake zao? Jibu unalo.!

Sasa unataka mwanamke akukopee hela? Hilo neno limenikata kuendelea kusoma! Tafuten hela Vijana maisha Ni matamu Sana!
 
Aisee hiyo ni roho ngumu mno, yaani mume aumwe niwe na pesa nisimpe ili atibiwe mmh , utakua na furaha gani na pesa zako huku babe,mpenzi,mkata kiu wako akiugulia maumivu?😒. Yanauzwaga hadi mashamba ili mgonjwa atibiwe akipona tutatafuta vingine.

Note: ni tabia ya mtu tu haina uhusiano na ke wote, do not generalize.
 
: mwanaume jijali, jipe raha na ujipende mwenyewe KWANZA. Potelea mbali hata wakikuona mbinafsi. 90+% ya mnaowaita wake zenu ni wabinafsi and they are money oriented.

Hii statement nimeielewa sana na ninaiishi kuanzia mwaka jana.
Heri yako kwa kugundua, umechelewa kugundua SIRI hii ila bado hakijaharibika kitu. Hakika umepona na utakuwa salama, karibu sasa kilingeni. Karibu kijana!
 
Aisee hiyo ni roho ngumu mno, yaani mume aumwe niwe na pesa nisimpe ili atibiwe mmh , utakua na furaha gani na pesa zako huku babe,mpenzi,mkata kiu wako akiugulia maumivu?[emoji19]. Yanauzwaga hadi mashamba ili mgonjwa atibiwe akipona tutatafuta vingine.

Note: ni tabia ya mtu tu haina uhusiano na ke wote, do not generalize.
Most of ke
 
Back
Top Bottom