Ukisikia habari ya Kambona, ukimuangalia Warioba, ukiona walivyofanyiwa na Chama cha Mapinduzi na Serikali zake utaelewa kwanini Tanzania ni masikini

Ukisikia habari ya Kambona, ukimuangalia Warioba, ukiona walivyofanyiwa na Chama cha Mapinduzi na Serikali zake utaelewa kwanini Tanzania ni masikini

Lord Denning

JF-Expert Member
Joined
Jun 3, 2015
Posts
23,494
Reaction score
57,869
Mkwamo wa Tanzania tangu kuanzishwa kwake umetokana na sababu kuu mbili.

1. Kuwapa kipaumbele zaidi wajinga na ujinga kuliko akili na wenye akili.

2. Rushwa na Ubinafsi.


Kuhusu kuwapa kipaumbele wajinga na ujinga kuliko akili na wenye akili.

Kabla ya kifo chake. Aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mzee Mark Bomani alikuwa rafiki yangu sana. Mara nyingi nikitoka kwenye kazi zangu mitaa ya kisutu, Posta nilikuwa napitia zilipokuwepo Ofisi zake, nakaa nae na ananielezea mengi sana kuhusu historia ya Taifa letu.

Mark Bomani aliyepata kuwa DPP na baadae Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Waziri wa Sheria wakati wa Nyerere alinihadithia kisa cha ugomvi wa Nyerere na Oscar Kambona vizuri sana.

Kwa mujibu wa Marehemu Mark Bomani, Kambona alitofautiana na Nyerere kuhusu namna ya kutekeleza sera ya Ujamaa na Kujitegemea. Kwa mawazo yake aliona sio sawa kuwanyang'anya watu mali zao kama mashamba, matrekta, nyumba na kuwalazimisha kwenda kuishi vijiji vya ujamaa kulipokuwa hakuna chochote. Kambona aliona ile kama dalili ya kwanza ya udikteta na kijiua kiuchumi ( Economical suicide).

Kwa mawazo ya Kambona hatua ile ilikuwa ni kuharibu uchumi wa Taifa uliokuwa unaendelea vizuri sana ikumbukwe kabla ya sera ya Ujamaa na Kujitegemea Tanganyika na baadae Tanzania ilikuwa na uzalishaji mkubwa sana wa chakula uliokuwa ukifanywa na Wazawa pamoja na wakulima wachache wa kigeni. Wakulima hawa walikuwa wanazalisha chakula kwa wingi sana mikoa ya Mbeya, Iringa, Tanga, Morogoro, Lindi, Kilimanjaro, Arusha, Mara, Mwanza na Dodoma. Mawazo ya Kambona ilikuwa akili kubwa.

Kambona hakukubaliana na kuwanyang'anya watu uwezo wao na nguvu kazi zao. Matokeo yake alikuja kutangazwa kuwa Mhaini ila ukweli ulibaki palepale kuwa Sera ya Ujamaa na Kujitegemea hasa vijiji vya Ujamaa ilikuja kuzalisha umaskini wa kutisha kwa Watanzania hadi kuleta mabalaa ya Njaa hadi kusababisha kuletewa vyakula vya msaada.

Sio hivyo tu Sera hii ilikuja kusababisha kuanguka kwa uchumi wa nchi hadi kupelekea wananchi kuvaa nguo zenye viraka.

Kwa upande wa Mzee Warioba huyu uzuri historia yake wengi tunaifahamu.

Inasemwa tangu alipokuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali alikuwa na misimamo thabiti yenye akili na wakati mwingi aliweza kutofautiana hadi na Waziri Mkuu Edward Sokoine na kutishia kujiuzuru. Siku zote amekuwa mtetezi mkubwa wa mifumo imara, utawala wa sheria na haki.

Kwenye moja ya visa vinavyosemwa sana inasemwa Sokoine kwenye kutekeleza Sera ya Uhujumu Uchumi alilazimisha kutungwa kwa Sheria zinazolazimisha watu kuadhibiwa nje ya utaratibu wa Kimahakama na Warioba alipingana nae waziwazi kuwa hatuwezi kutunga Sheria ya namna hiyo. Suala hili lilifanya Warioba atake kujiuzuru hadi Nyerere akaingilia kati na kusema vifungu hivyo visiwekwe kwenye Sheria.

Sio hivyo tu. Inasemwa akiwa Waziri Mkuu alipingana na Rais Mwinyi mara kadhaa wakati Mwinyi alipotaka kufanya mambo kinyume na utaratibu wa Kisheria hadi kumlazimisha Mwinyi kuvunja Baraza la Mawaziri na Warioba akaishia kutupwa nje ya Baraza la Mawaziri.

Akiwa Waziri Mkuu Mstaafu Mzee Warioba aliongoza mchakato wa Katiba Mpya iliyopendekezwa kupunguza madaraka ya Rais na kutengeneza mifumo imara kwa uimara wa Taifa.

Ukiangalia kwa umakini namna Kambona na Warioba walivyotendewa na Serikali ya CCM kusema kweli lazima utaelewa tu kuwa kansa kuu inayoliangamiza Taifa letu ni namna Serikali ya CCM wasivyopenda watu wenye akili na matumizi sahihi ya akili kwa maendeleo ya binadamu hasa Watanzania.

Kote duniani, Mataifa yaliyoendelea na yanayoendelea vizuri ni yale yanayojali matumizi sahihi ya akili kwa maendeleo ya binadamu. Akili ni pamoja na kusema ukweli, kushauri ukweli na kuupa ukweli huo kipaumbele katika kutatua matatizo yanayokukabili.

Kutopenda matumizi sahihi ya akili ndipo kumekuja kusababisha kutokuwepo kwa mifumo imara ya kuliendesha Taifa letu na hatimaye Rushwa imekuja kushamiri na kuliimarisha zaidi kundi la Watu wachache wanaoishi kwa kutumia vibaya kodi na rasilimali zetu huku wakitukandamiza kwa nguvu kwa mtutu wa bunduki.
 
Ni vile hatukuwa na mitandao ya kijamii kama saivi uwenda nyerere na kundi lake la kna sokoine walifanya maujinga mengi sn kwny taifa hli. Ila cha kumsifu ni hakuwa na tamaa ya kubnafisisha madini na rasilimali zngne ni kama naona kambona angeshka taifa hli tungekwenda mbali sn kiuchumi.
 
Mkwamo wa Tanzania tangu kuanzishwa kwake umetokana na sababu kuu mbili.

1. Kuwapa kipaumbele zaidi wajinga na ujinga kuliko akili na wenyewe akili.

2. Rushwa na Ubinafsi.


Kuhusu kuwapa kipaumbele wajinga na ujinga kuliko akili na wenye akili.

Kabla ya kifo chake. Aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mzee Mark Bomani alikuwa rafiki yangu sana. Mara nyingi nikitoka kwenye kazi zangu mitaa ya kisutu, Posta nilikuwa napitia zilipokuwepo Ofisi zake, nakaa nae na ananielezea mengi sana kuhusu historia ya Taifa letu.

Mark Bomani aliyepata kuwa DPP na baadae Mwanasheria Mkuu wa Serikali wakati wa Nyerere alinihadithia kisa cha ugomvi wa Nyerere na Oscar Kambona vizuri sana.

Kwa mujibu wa Marehemu Mark Bomani, Kambona alitofautiana na Nyerere kuhusu namna ya kutekeleza sera ya Ujamaa na Kujitegemea. Kwa mawazo yake aliona sio sawa kuwanyang'anya watu mali zao kama mashamba, matrekta, nyumba na kuwalazimisha kwenda kuishi vijiji vya ujamaa kulipokuwa hakuna chochote.

Kwa mawazo ya Kambona hatua ile ilikuwa ni kuharibu uchumi wa Taifa uliokuwa unaendelea vizuri sana ikumbukwe kabla ya sera ya Ujamaa na Kujitegemea Tanganyika na baadae Tanzania ilikuwa na uzalishaji mkubwa sana wa chakula uliokuwa ukifanywa na Wazawa pamoja na wakulima wachache wa kigeni. Mawazo ya Kambona ilikuwa akili kubwa.

Kambona hakukubaliana na kuwanyang'anya watu uwezo wao na nguvu kazi zao. Matokeo yake alikuja kutangazwa kuwa Mhaini ila ukweli ulibaki palepale kuwa Sera ya Ujamaa na Kujitegemea hasa vijiji vya Ujamaa ilikuja kuzalisha umaskini wa kutisha kwa Watanzania hadi kuleta mabalaa ya Njaa hadi kusababisha kuletewa vyakula vya msaada.

Sio hivyo tu Sera hii ilikuja kusababisha kuanguka kwa uchumi wa nchi hadi kupelekea wananchi kuvaa nguo zenye viraka.

Kwa upande wa Mzee Warioba huyu uzuri historia yake wengi tunaifahamu.

Inasemwa tangu alipokuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali alikuwa na misimamo thabiti yenye akili na wakati mwingi aliweza kutofautiana hadi na Waziri Mkuu Edward Sokoine na kutishia kujiuzuru. Siku zote amekuwa mtetezi mkubwa wa mifumo imara, utawala wa sheria na haki.

Kwenye moja ya visa vinavyosemwa sana inasemwa Sokoine kwenye kutekeleza Sera ya Uhujumu Uchumi alilazimisha kutungwa kwa Sheria zinazolazimisha watu kuadhibiwa nje ya utaratibu wa Kimahakama na Warioba alipingana nae waziwazi kuwa hatuwezi kutunga Sheria ya namna hiyo. Suala hili lilifanya Warioba take kujiuzuru hadi Nyerere akaingilia kati na kusema vifungu hivyo visited kwenye Sheria.

Sio hivyo tu. Inasemwa akiwa Waziri Mkuu alipingana na Rais Mwinyi mara kadhaa wakati Mwinyi alipotaka kufanya mambo kinyume na utaratibu wa Kisheria hadi kumlazimisha Mwinyi kuvunja Baraza la Mawaziri.

Akiwa Waziri Mkuu Mstaafu Mzee Warioba aliongoza mchakato wa Katiba Mpya iliyopendekezwa kupunguza madaraka ya Rais na kutengeneza mifumo imara kwa uimara wa Taifa.

Ukiangalia kwa umakini namna Kambona na Warioba walivyotendewa na Serikali ya CCM kusema kweli lazima utaelewa tu kuwa kansa kuu inayoliangamiza Taifa letu ni namna Serikali ya CCM wasivyopenda watu wenye akili na matumizi sahihi ya akili kwa maendeleo ya binadamu hasa Watanzania.

Kote duniani, Mataifa yaliyoendelea na yanayoendelea vizuri ni yale yanayojali matumizi sahihi ya akili kwa maendeleo ya binadamu. Akili ni pamoja na kusema ukweli, kushauri ukweli na kuupa ukweli huo kipaumbele katika kutatua matatizo yanayokukabili.

Kutopenda matumizi sahihi ya akili ndipo kumekuja kusababisha kutokuwepo kwa mifumo imara ya kuliendesha Taifa letu na hatimaye Rushwa imekuja kushamiri na kuliimarisha zaidi kundi la Watu wachache wanaoishi kwa kutumia vibaya kodi na rasilimali zetu huku wakitukandamiza kwa nguvu kwa mtutu wa bunduki.
kwahio kambona ndo alikua anakuja kufanya uwe tajiri 🤣
 
Mkwamo wa Tanzania tangu kuanzishwa kwake umetokana na sababu kuu mbili.

1. Kuwapa kipaumbele zaidi wajinga na ujinga kuliko akili na wenyewe akili.

2. Rushwa na Ubinafsi.


Kuhusu kuwapa kipaumbele wajinga na ujinga kuliko akili na wenye akili.

Kabla ya kifo chake. Aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mzee Mark Bomani alikuwa rafiki yangu sana. Mara nyingi nikitoka kwenye kazi zangu mitaa ya kisutu, Posta nilikuwa napitia zilipokuwepo Ofisi zake, nakaa nae na ananielezea mengi sana kuhusu historia ya Taifa letu.

Mark Bomani aliyepata kuwa DPP na baadae Mwanasheria Mkuu wa Serikali wakati wa Nyerere alinihadithia kisa cha ugomvi wa Nyerere na Oscar Kambona vizuri sana.

Kwa mujibu wa Marehemu Mark Bomani, Kambona alitofautiana na Nyerere kuhusu namna ya kutekeleza sera ya Ujamaa na Kujitegemea. Kwa mawazo yake aliona sio sawa kuwanyang'anya watu mali zao kama mashamba, matrekta, nyumba na kuwalazimisha kwenda kuishi vijiji vya ujamaa kulipokuwa hakuna chochote.

Kwa mawazo ya Kambona hatua ile ilikuwa ni kuharibu uchumi wa Taifa uliokuwa unaendelea vizuri sana ikumbukwe kabla ya sera ya Ujamaa na Kujitegemea Tanganyika na baadae Tanzania ilikuwa na uzalishaji mkubwa sana wa chakula uliokuwa ukifanywa na Wazawa pamoja na wakulima wachache wa kigeni. Mawazo ya Kambona ilikuwa akili kubwa.

Kambona hakukubaliana na kuwanyang'anya watu uwezo wao na nguvu kazi zao. Matokeo yake alikuja kutangazwa kuwa Mhaini ila ukweli ulibaki palepale kuwa Sera ya Ujamaa na Kujitegemea hasa vijiji vya Ujamaa ilikuja kuzalisha umaskini wa kutisha kwa Watanzania hadi kuleta mabalaa ya Njaa hadi kusababisha kuletewa vyakula vya msaada.

Sio hivyo tu Sera hii ilikuja kusababisha kuanguka kwa uchumi wa nchi hadi kupelekea wananchi kuvaa nguo zenye viraka.

Kwa upande wa Mzee Warioba huyu uzuri historia yake wengi tunaifahamu.

Inasemwa tangu alipokuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali alikuwa na misimamo thabiti yenye akili na wakati mwingi aliweza kutofautiana hadi na Waziri Mkuu Edward Sokoine na kutishia kujiuzuru. Siku zote amekuwa mtetezi mkubwa wa mifumo imara, utawala wa sheria na haki.

Kwenye moja ya visa vinavyosemwa sana inasemwa Sokoine kwenye kutekeleza Sera ya Uhujumu Uchumi alilazimisha kutungwa kwa Sheria zinazolazimisha watu kuadhibiwa nje ya utaratibu wa Kimahakama na Warioba alipingana nae waziwazi kuwa hatuwezi kutunga Sheria ya namna hiyo. Suala hili lilifanya Warioba take kujiuzuru hadi Nyerere akaingilia kati na kusema vifungu hivyo visited kwenye Sheria.

Sio hivyo tu. Inasemwa akiwa Waziri Mkuu alipingana na Rais Mwinyi mara kadhaa wakati Mwinyi alipotaka kufanya mambo kinyume na utaratibu wa Kisheria hadi kumlazimisha Mwinyi kuvunja Baraza la Mawaziri.

Akiwa Waziri Mkuu Mstaafu Mzee Warioba aliongoza mchakato wa Katiba Mpya iliyopendekezwa kupunguza madaraka ya Rais na kutengeneza mifumo imara kwa uimara wa Taifa.

Ukiangalia kwa umakini namna Kambona na Warioba walivyotendewa na Serikali ya CCM kusema kweli lazima utaelewa tu kuwa kansa kuu inayoliangamiza Taifa letu ni namna Serikali ya CCM wasivyopenda watu wenye akili na matumizi sahihi ya akili kwa maendeleo ya binadamu hasa Watanzania.

Kote duniani, Mataifa yaliyoendelea na yanayoendelea vizuri ni yale yanayojali matumizi sahihi ya akili kwa maendeleo ya binadamu. Akili ni pamoja na kusema ukweli, kushauri ukweli na kuupa ukweli huo kipaumbele katika kutatua matatizo yanayokukabili.

Kutopenda matumizi sahihi ya akili ndipo kumekuja kusababisha kutokuwepo kwa mifumo imara ya kuliendesha Taifa letu na hatimaye Rushwa imekuja kushamiri na kuliimarisha zaidi kundi la Watu wachache wanaoishi kwa kutumia vibaya kodi na rasilimali zetu huku wakitukandamiza kwa nguvu kwa mtutu wa bunduki.
Yanzania ni masikini kuliko nchi gani? Au unasema tz ipi, hiihii yenye treni ya umeme na madaraja ya baharini kama ulaya?. Bro, ni kweli tz pia kuna shida lakini sio kubwa kuliko za nchi nyingine Afrika. Mfano, Kenya kuna nini cha maana kutuzidi sisi? Msidanganywe aloo, matatizo ya Afrika yanafanana kote, nayo ni ukosefu wa nguvu za kuchimba na kuchakata madini yetu mpaka tupate wazungu(wezi) waje watusaidie kuyachimba kwa mashariti yao. Pili hatuna masoko huru ya kuuza bidhaa zetu, masoko yote na bei vimehodhiwa na mabeberu. Kaka bila Afrika yote kusimama na kuwa kitu kimoja hakuna kitu cha maana hata chadema ikiingia Ikulu.
 
Yanzania ni masikini kuliko nchi gani? Au unasema tz ipi, hiihii yenye treni ya umeme na madaraja ya baharini kama ulaya?. Bro, ni kweli tz pia kuna shida lakini sio kubwa kuliko za nchi nyingine Afrika. Mfano, Kenya kuna nini cha maana kutuzidi sisi? Msidanganywe aloo, matatizo ya Afrika yanafanana kote, nayo ni ukosefu wa nguvu za kuchimba na kuchakata madini yetu mpaka tupate wazungu(wezi) waje watusaidie kuyachimba kwa mashariti yao. Pili hatuna masoko huru ya kuuza bidhaa zetu, masoko yote na bei vimehodhiwa na mabeberu. Kaka bila Afrika yote kusimama na kuwa kitu kimoja hakuna kitu cha maana hata chadema ikiingia Ikulu.
Kwa hiyo unakataa Tanzania sio masikini?

Unaishi Tanzania wewe? Treni za umeme ni nini? Umeishi vijijini? Umeona shida za watu kwenye maji, miundombinu na madawa?

Hujui kuna jamii nyingi sana hapa nchini hata uhakika wa matibabu hawana? Uhakika wa chakula hawana? Makazi bora na salama hawana?
 
Yanzania ni masikini kuliko nchi gani? Au unasema tz ipi, hiihii yenye treni ya umeme na madaraja ya baharini kama ulaya?. Bro, ni kweli tz pia kuna shida lakini sio kubwa kuliko za nchi nyingine Afrika. Mfano, Kenya kuna nini cha maana kutuzidi sisi? Msidanganywe aloo, matatizo ya Afrika yanafanana kote, nayo ni ukosefu wa nguvu za kuchimba na kuchakata madini yetu mpaka tupate wazungu(wezi) waje watusaidie kuyachimba kwa mashariti yao. Pili hatuna masoko huru ya kuuza bidhaa zetu, masoko yote na bei vimehodhiwa na mabeberu. Kaka bila Afrika yote kusimama na kuwa kitu kimoja hakuna kitu cha maana hata chadema ikiingia Ikulu.
Kwanini unajilinganisha na Kenya wakati una madini adimu na uranium mpaka mabeberu wanatuonea wivu kulingana na madelu??
 
Yanzania ni masikini kuliko nchi gani? Au unasema tz ipi, hiihii yenye treni ya umeme na madaraja ya baharini kama ulaya?. Bro, ni kweli tz pia kuna shida lakini sio kubwa kuliko za nchi nyingine Afrika. Mfano, Kenya kuna nini cha maana kutuzidi sisi? Msidanganywe aloo, matatizo ya Afrika yanafanana kote, nayo ni ukosefu wa nguvu za kuchimba na kuchakata madini yetu mpaka tupate wazungu(wezi) waje watusaidie kuyachimba kwa mashariti yao. Pili hatuna masoko huru ya kuuza bidhaa zetu, masoko yote na bei vimehodhiwa na mabeberu. Kaka bila Afrika yote kusimama na kuwa kitu kimoja hakuna kitu cha maana hata chadema ikiingia Ikulu.
Jikite kwenye hoja. Hakuna mahali mtoa mada ameifananisha Tanzania na nchi nyingine. Yeye amejikita kuelezea ni kwa namna gani mifumo na maamuzi ya hivyo kutoka kwa viongozi wetu, imetufikisha hapa tulipo.
 
Mwingine aliyefanyiwa figisu na wanamtandao ni Salim Ahmed Salim, sasa hivi familia nzima ya Mkwere wanajipakulia minyama tu huku raia wengi wakishindia dagaa na mihogo.
Huko Serikalini unaambiwa ndo kunasikitisha. Wenye akili na mawazo mazuri ya kulijenga vizuri Taifa wanatengwa, hawasikilizwi, wanaitwa wajuaji, wana kiburi na hawaheshimu Viongozi.

Wanaopewa safari ni machawa, wasioweza kushauri na kusema ukweli nyeusi ni nyeusi na nyeupe ni nyeupe. Wenye elimu zenye mashaka na kuunga unga wasiojiamini.

Matokeo yake ndo tupo hapa miaka 64 baada ya uhuru tunategemea maji ya mvua mikoa ya Morogoro, Pwani na Dar.
 
Na jinsi mambo yanavyoendeleq tanzania tutakuwa maskini daima.
Itabaki historia tu, tulikuwa na madini, tulikuwa na gesi..
Tunakoelekea ni kubaya zaidi na kunatisha zaidi.

N hili ongezeko la watu ndo itakuwa balaa zaidi maana wingi wa rasilimali sio chochote kwenye ongezeko la watu. Umadhubuti wa akili ndo kila kitu.
 
Moja ya majanga makubwa tulionayo kama Taifa ni hii katiba sifa muhimu ya kuwa kiongozi ni kujua kusoma na kuandika. Sifa nyingine hatari iliyozaliwa nchini ni uchawa ukitaka kuwa kiongozi au kuteuliwa nafasi ama kupanda cheo ni kufanya jambo la ukatili kuteka na hata kuua. Kwa watu wanaokataa ama kuhoji hasa wapinzani wako kisiasa.
 

Attachments

  • Ey_hdJMXAAIfziz.jpeg
    Ey_hdJMXAAIfziz.jpeg
    107.3 KB · Views: 10
  • WIMBO MPYA WA CHADEMA - WARAKA.mp4
    13 MB
Back
Top Bottom