Fanfa
JF-Expert Member
- Sep 25, 2009
- 2,388
- 3,710
Sarakasi za polepole tumeziona.
Hebu tujikumbushe kidogo ni nani aliyetengeneza precedent ya uchafu wote huu unaolalamikiwa na Polepole????
1. Nani aliyeacha precedent ya kuteka, kupoteza, kutesa na kuua watu wanaokosoa watawala???
2. Nani aliyeanzisha upuuzi huu wa kuvuruga chaguzi kuanzia 2019, 2020, 2024 .....
3. Nani aliyeanzisha utawala wa kidikteta ndani ya chama na ndani ya serikali?
4. Nani aliyeanzisha uminywaji wa Demokrasia hadi kufikia vyama kuzuiwa kufanya siasa?
5. Nani aliyeasisi utaratibu wa fomu moja ndani ya chama?
6. Nani aliyeasisi utaratibu wa uchawa na ukunguni na kutaka yeye tu asifiwe ndani ya chama, serikali na nchi kwa ujumla?
7. Nani aliyessisi uminywaji wa uhuru wa vyombo vya habari, uhuru wa watu kujieleza, uvunjwaji wa haki za watu nk.??
8. Nani asiyeasisi uvurugwaji wa mifumo ya kitaasisi (Serikali, Bunge, mahakama) kwa kuingilia na muhimili uliojichimbia???
9. Na mengine mengi.
Mambo haya yote yalifanyika Ponjoro Polepole akiwa kwenye inner cycle na msemaji wa chama.
Swali: mbona hayo yote yalifanyika akiwa mjumbe wa vikao vyote vya chama na pia msemaji wa chama lakini hatukusikia akilalamika au kukemea maovu yote yale????
Iweje leo Ponjoro Polepole aonekane Shujaa na mzalendo wa kweli ili hali ni mmoja wa waasisi wa mambo yote ya kishenzi niliyoyataja hapo juu!!!!!!
Au ndo kusema kuwa Taifa hili limejaa watu wajinga kwa zaidi ya 90%.??? Kwamba unaweza ukatengeneza tatizo au kuwa sehemu ya tatizo lakini watanzania wale wale ukiwajia kwa mlango wa nyuma wanakushangilia kama mazuzu. Vilee!!!
Kwa ujinga huu itatuchukua miaka zaidi ya 200 kuuondoa ujinga na umasikini wa kifikra. Taifa limejaa wajinga na wapumbavu wengi sana.
Sitashangaa akifanya mwanaccm mwingine sarakasi za polepole tukaendelea kurukaruka kama mazuzu. Nimeona hata wapinzani wanashangilia kweli kweli na kumwona Polepole shujaa wao.
Ama kweli unyani bado umetukaaa.
Hebu tujikumbushe kidogo ni nani aliyetengeneza precedent ya uchafu wote huu unaolalamikiwa na Polepole????
1. Nani aliyeacha precedent ya kuteka, kupoteza, kutesa na kuua watu wanaokosoa watawala???
2. Nani aliyeanzisha upuuzi huu wa kuvuruga chaguzi kuanzia 2019, 2020, 2024 .....
3. Nani aliyeanzisha utawala wa kidikteta ndani ya chama na ndani ya serikali?
4. Nani aliyeanzisha uminywaji wa Demokrasia hadi kufikia vyama kuzuiwa kufanya siasa?
5. Nani aliyeasisi utaratibu wa fomu moja ndani ya chama?
6. Nani aliyeasisi utaratibu wa uchawa na ukunguni na kutaka yeye tu asifiwe ndani ya chama, serikali na nchi kwa ujumla?
7. Nani aliyessisi uminywaji wa uhuru wa vyombo vya habari, uhuru wa watu kujieleza, uvunjwaji wa haki za watu nk.??
8. Nani asiyeasisi uvurugwaji wa mifumo ya kitaasisi (Serikali, Bunge, mahakama) kwa kuingilia na muhimili uliojichimbia???
9. Na mengine mengi.
Mambo haya yote yalifanyika Ponjoro Polepole akiwa kwenye inner cycle na msemaji wa chama.
Swali: mbona hayo yote yalifanyika akiwa mjumbe wa vikao vyote vya chama na pia msemaji wa chama lakini hatukusikia akilalamika au kukemea maovu yote yale????
Iweje leo Ponjoro Polepole aonekane Shujaa na mzalendo wa kweli ili hali ni mmoja wa waasisi wa mambo yote ya kishenzi niliyoyataja hapo juu!!!!!!
Au ndo kusema kuwa Taifa hili limejaa watu wajinga kwa zaidi ya 90%.??? Kwamba unaweza ukatengeneza tatizo au kuwa sehemu ya tatizo lakini watanzania wale wale ukiwajia kwa mlango wa nyuma wanakushangilia kama mazuzu. Vilee!!!
Kwa ujinga huu itatuchukua miaka zaidi ya 200 kuuondoa ujinga na umasikini wa kifikra. Taifa limejaa wajinga na wapumbavu wengi sana.
Sitashangaa akifanya mwanaccm mwingine sarakasi za polepole tukaendelea kurukaruka kama mazuzu. Nimeona hata wapinzani wanashangilia kweli kweli na kumwona Polepole shujaa wao.
Ama kweli unyani bado umetukaaa.