Ukipata msaada katika maisha jiongeze kidogo usijibweteke.

Sky Eclat

JF-Expert Member
Oct 17, 2012
57,595
215,280
Swaiba alipata kiwanja Kigamboni, enzi zile bado mapori mengi. Kwa kifupi aliuziwa shamba la ekari mbili. Kwakua haishi Tanzania aliamua kujenga ili asipoteze kiwanja. Alijenga nyumba yake nzuri na swimming pool. Kwakua kiwanja ni kikubwa alijenga na guest wing ya vyumba vitatu yenye master’s bedroom.

Alizingusha uzio na kuweka gate. Furniture ya ndani na kila kitu nyumba ilikamilika. Alimuweka binamu yake kule kwenye guest wingi na nyumba yake alifunga ila mara moja kwa mwezi kuna mtu anafanya usafi, anafungua madirisha asubuhi na kuyaacha wazi mpaka jioni ili hewa iingie.

Binamu alipokabidhiwa nyumba alikua bwana mdogo ndiyo amemaliza chuo. Alitafuta kazi mpaka anaoa yuko katika nyumba ile. Halipi chochote zaidi ya kulipaia umeme, na gas anayotumia maji jamaa alichimba kisima wakati anajenga.

Katika mazungumzo siku moja aliniambia, mtoto wa binamu yake ambae amezaliwa pale amemaliza form six, kama utani alisema hawa watoto watajua nyumba ile ni ya kwao maana maisha yao yote wameishi pale. Tulicheka lakini swaiba alidhamiria. Alimpa notice binamu.

Hata hivyo alipata shirika linataka nyumba zote mbili kwa wafanya kazi wao. Tangu ametoa notice sasa amekua adui wa familia, shangazi yake ambae ni mama wa binamu analalamika wanaua undugu atamtoaje ndugu yake kwenye nyumba ilhali hata yeye akienda Dar kwa matibabu anafikia hapo.

Shangazi haoni kabisa kuwa kwa miaka zaidi ya 15 mtoto wake alipaswa kuwa na nyumba hata kama alipenda kukaa pale basi yake angepangisha. Binamu alipaswa ajiongeze kimaisha.
 
Madame kumpa ndugu kitu sijui kwanini inaleta ugomvi.

Mimi nilitoka Dar nikahamia mkoani bro akaniomba TV nikampa.

Amekaa nayo mwaka mzima. Sasa nimerudi namuomba TV akanuna maneno yakafika hadi kwa wazee. Ananiuliza sasa nikichukua mkewe ataangalia nini chumbani.

Na hiyo ni Star X tu 32 inches.
 
Hii ipo sana, kuna jamaa yangu alipewa nyumba na uncle wake, jamaa kaishi vizuri tu, nyumba ilikuwa na wapangaji. Uncle wake akavuta, yule jamaa sasa ilibidi awe anawasiliana na mke wa uncle, mke wa uncle akasema inabidi jamaa aanze kulipa kodi maana ndio kipato chake huyo aunt

Familia ikaanza kumnunia aunt, mbona uncle alivyokuwepo hakunifanyia hivi, inakuwaje leo amekufa aunt anifanyie hivi, imagine kidume kipo 50 kinalalamika namna hiyo.
 
Nina nyumba huko huko sipangishi wala kuweka mtu wa kulinda!

Funguo nimeacha mahali salama, nikiihitaji huwa tunamwambia anapeleka mtu wa usafi, inasafishwa weeh, tukienda tunakaa siku2-3. Tukiwa tumechoshwa na kilimo.

Zamani simu zilikuwa nyingi, sasa pale ndugu yangu unipe nikae Mimi, maana watoto tunahangaika, sijui blah blah blah, jibu langu siku zote lilikuwa moja, sipangishi wala siweki mtu! Ooh nyumba inaharibika mara inahitaji joto! Misemo mingi!

Wacha uwe na roho mbaya, kabla ya kujenga nyumba kubwa kulikuwa na kibanda kidogo, alikaa mwenyeji pale, kumuondoa ili nibomoe nijenge nyumba kubwa, ilinisumbua Sana, pamoja na kumpa hela ya Kodi akapange kwingineko.

Sitorudia Hilo kosa.

Huyo bwege atakuwa anaendesha gari kubwa hajawahi kuwaza kujenga! Akapange ahame akajenge!
 
Nina nyumba huko huko sipangishi wala kuweka mtu wa kulinda!

Funguo nimeacha mahali salama, nikiihitaji huwa tunamwambia anapeleka mtu wa usafi, inasafishwa weeh, tukienda tunakaa siku2-3. Tukiwa tumechoshwa na kilimo.

Zamani simu zilikuwa nyingi, sasa pale ndugu yangu unipe nikae Mimi, maana watoto tunahangaika, sijui blah blah blah, jibu langu siku zote lilikuwa moja, sipangishi wala siweki mtu! Ooh nyumba inaharibika mara inahitaji joto! Misemo mingi!

Wacha uwe na roho mbaya, kabla ya kujenga nyumba kubwa kulikuwa na kibanda kidogo, alikaa mwenyeji pale, kumuondoa ili nibomoe nijenge nyumba kubwa, ilinisumbua Sana, pamoja na kumpa hela ya Kodi akapange kwingineko.

Sitorudia Hilo kosa.

Huyo bwege atakuwa anaendesha gari kubwa hajawahi kuwaza kujenga! Akapange ahame akajenge!
Anaendesha gari kubwa na kila anakoulizia kiwanja anaonyeshwa kando zaidi wakati pale pamechangamka akifungua tu gate kuna butcher ya nyama, kuna genge, kuna bar na nyama choma.
 
Nina nyumba huko huko sipangishi wala kuweka mtu wa kulinda!

Funguo nimeacha mahali salama, nikiihitaji huwa tunamwambia anapeleka mtu wa usafi, inasafishwa weeh, tukienda tunakaa siku2-3. Tukiwa tumechoshwa na kilimo.

Zamani simu zilikuwa nyingi, sasa pale ndugu yangu unipe nikae Mimi, maana watoto tunahangaika, sijui blah blah blah, jibu langu siku zote lilikuwa moja, sipangishi wala siweki mtu! Ooh nyumba inaharibika mara inahitaji joto! Misemo mingi!

Wacha uwe na roho mbaya, kabla ya kujenga nyumba kubwa kulikuwa na kibanda kidogo, alikaa mwenyeji pale, kumuondoa ili nibomoe nijenge nyumba kubwa, ilinisumbua Sana, pamoja na kumpa hela ya Kodi akapange kwingineko.

Sitorudia Hilo kosa.

Huyo bwege atakuwa anaendesha gari kubwa hajawahi kuwaza kujenga! Akapange ahame akajenge!
Toa funguo hiyo 😂 nyumba inahitaji joto na kelele za hapa na pale.
 
Mwambie huyo jamaa aje huku Mombasa tumpe nyumba bure akae tumlee na yeye atulee kifupi tuleane.
 
Mwafrica akipata mteremko sehemu ni kuserereka tu hadi mwisho juzi juzi tu hapa shishi baby kanuniwa na baba levo kisa kula kujigaragaza bure
 
Amekaa nayo mwaka mzima. Sasa nimerudi namuomba TV akanuna maneno yakafika hadi kwa wazee. Ananiuliza sasa nikichukua mkewe ataangalia nini chumbani.
Ndugu Lawama na Lawama ni Mzigo Mkubwa sana japo hajaumbiwa Mbuzi.

Bi Mkubwa wangu yeye ndiyo 1st born kwahiyo kajitahidi akaja Mjini miaka hiyo akaskuti na kuhustle sana mpaka akapata Mjengo, akaolewa na sisi tukazaliwa tukawa tunaishi.

Maza akawa kila mwaka lazima ahakikishe ndugu wawili; 1 upande wake na wa2 upande wa Mzee awe anakwenda kuwachukua na kuja kuwafundisha na kuwatafutia Maisha mixer Koneksheni wakitoboa wanajitegemea.

Mpk majuzi hapa nahesabu ndugu 12 sasa Bi Mkubwa Afya imezingua kidogo tu, tunawacheki pamoja na wengine kuwafuata kabisa mpaka home kwao hata wadogo zake ambao ni Wajomba Blood kabisa... Wamechomoa Betri! Niliumia!!

Maza akaniambia; "Mwanangu, Tizama na Ujifunze. Tenda Wema kisha nenda zako".
 
Back
Top Bottom