IPECACUANHA
JF-Expert Member
- Feb 19, 2011
- 3,216
- 1,906
Ni vyema ukatambua kwamba kujitabanaisha na wenye nguvu na kujitenga na wanyonge ni dalili ya kwanza ya udhaifu na unafiki. Pia utambue vyama vya siasa vipo kisheria na ni sehemu ihalalishayo matumizi ya demokrasia katika utawala wa kisiasa nchini. Ujue kuwa mwanachama au mpenzi wa chama chochote cha kisiasa sio kosa na ni dalili ya kwanza ya watu waliopevuka kisiasa. Ni ujinga kufikiria kwamba upinzani wa kisiasa ni uadui. Ni ujinga zaidi kufifisha uwepo utaratibu wa kidemokrasia za kutoa mawazo tofauti na yale ya waliomadarakani. Mfumo wa kidemokrasia tunaoutumia upo baada ya mifumo ya kiimla kushindwa kuendelea kuwepo. Historia inaonyesha nchi na wananchi wake huondoa mifumo ya kiimla kama ya akina Kagame ni suala la muda tu.Mtu huyo Lazima atakuwa na tabia za Kichadema, Tabia za kutaka Taifa liharibikiwe tu, kutaka Serikali iliyoko madarakani iharibikiwe, kutaka CCM iharibikiwe, Mijitu hii ni Rahisi mno kuijua. Kwa kupitia comments mitandaoni