Ukiona ishara hizi 12 ujue mwanamke anataka mrudiane lakini bado anasitasita

Infinite_Kiumeni

JF-Expert Member
Jan 23, 2023
382
661
Si rahisi kujua kama mwanamke anataka mrudiane.

Hasa pale unapokua humwelewi kwa vitu vinavyotokea.

Kutokana na wanaume nliowasaidia kuwarudisha ma ex wao.

Wakiachwa wampe muda huyo mwanamke bila kumtafuta. Na baadae mwanamke anaanza kujirudi tena, nimeona hivi vitu vinajirudia rudia. Nawe ukiona ishara kadhaa ujue anataka mrudiane. Pia uangalie ishara nyingi zaidi, sio uangalie moja tu na useme anataka kurudiana nawe.

Ni muhimu umpe nafasi ajidhihirishe kwako tena kama anafaa.

Sio lazima urudiane naye, hasa kama umekua kimaisha. Ukirudiana naye lakini yeye yupo palepale atakurudisha nyuma badala ya kusonga mbele.

Ni muhimu ujue kuwa hata kama anataka mrudiane, haina maana mahusiano yenu ndo yatakua mazuri muda huu.

Hivyo, ukiona ishara hizi usikimbilie kurudiana naye.

Anakuomba msamaha kwa kuvunja mahusiano
Ukiona ivi ujue amekubali kujishusha kuona makosa yake. Ujue kuna kitu anajutia kwa kuvunja mahusiano yenu.
Akikuomba msamaha usianze tena kumwagia hasira zako za kwanini alikuacha. Bali msamehe na kuwa mpole. Kuonesha hasira maana yake bado anakuumiza moyoni sababu alikuacha.

Anajiweka karibu na uwepo wako
Anajiweka sehemu ambazo mtaonana tu.
Anakuja karibu na kazini kwako, au unapofanyia mazoezi au unapoendaga kupumzika au popote ili mradi muonane tena.

Atatafuta njia kukuonesha anajali
Anaweza kukutumia sms za motisha. Au,

Anaweza anaweza kukusaidia kufanya kitu, au chochote cha kuonesha anajali.

Ujue anatafuta sababu muongee zaidi au muwe karibu.

Atakusifia bila sababu wala kutegemea
Sio sifa za juu juu, hapana.

Atakusifia kwa kitu kuhusu wewe au matendo yako.

Nayo ni njia ya kukuonesha “nilikosea, saivi naona kitu”.

Pia ukiona anakushukuru kwa moyo, ujue nayo ni sifa na anatamani ayarudie tena hayo.
.
Atajifanya amekupotezea
Ili asioneshe kuwa ameumizwa na kuachana kwenu.

Atajifanya ameshakusahau na anaendelea na maisha bila wewe.

Utajuaje sasa anakutaka bado?

Atataka ajue kuwa amekupotezea.

Atatumia nguvu nyingi kukuonesha hilo.

Ili aone utafanyaje. We cha kufanya mwache afanye ivo akichoka atajirudi.
.
Atakushirikisha malengo yake.
Na utaona pia anataka kujua kuhusu wewe.

Ujue ni njia ya kutaka mrudiane.

Wapenzi huwa wanashirikishana malengo. Huwafanya waaminiane zaidi.

Anakutafuta lakini anaondoka tena ukimlazimisha
Mwanamke akiwa anakurudia nenda naye taratibu.

Ila ukiwa na haraka ya kurudi penzini ataondoka tena.

Kisha baada ya muda atakutafuta tena. Usiharakishe ukiona anarudi kwako.

Pia atakupotezea tena ukionesha kumtaka sana.
.
Anakubali mkutane lakini haongelei kurudiana.
Kwanini haongelei kurudiana?

Sababu anaogopa mahusiano yenu yatakua kama yalivyokua mwanzo.

Japo bado anapenda kuwa nawe lakini hajisikii amani kurudi kwenye mahusiano.

Hivyo, kama kawaida, usilazimishe we nenda naye taratibu.
.
Atakukasirikia.
Sababu hataki kujishusha lakini bado anakukubali.

Muda mwingine mwanamke anatumia hasira kuonesha hisia zake za upendo.

We usiingie kwenye hasira zake. Wala usibishane naye kwa lolote maana hauna cha kumshawishi.

Lakini kama hasira yake ni juu ya kitu kinachoeleweka kama vile ulikua humtimizii ahadi ujue ili mrudiane lazima ubadilike.
.
Haeleweki.
Kuna muda atakurudia.

Muda mwingine anafanya kama hajawahi kukujua.

Ukiona hivyo ujue bado hajajiamini na uamuzi wa kurudiana.

We endelea kuenda naye taratibu.
.
Ana wivu ukiwa na mwanamke mwingine.
Sababu anaogopa kusahauliwa na wewe.

Na bado anatamani awe katika iyo nafasi.

Hata kama akikukasirikia, usiache kuwa na mwanamke mwingine sababu ya mwanamke aliyekuacha.
Na kama akitaka kurudiana, uangalie mwenyewe ni mwanamke yupi anakufaa kuendeleza naye maisha.
.
Atakujaribu
Ataijaribu mipaka yako ili ajue kama bado anakuendesha au la.

Mfano, atakupigia usiku aone kama utapokea, atakuomba umsaidie kitu, atakuambia kitu kama “we ndo nnaye kuamini katika hili”, atakualika kufanya kitu pamoja, atakuuliza kuhusu mahusiano yako ya sasa.

Yote ayo ili ajue bado unamfikiria kiasi gani.

We onesha kutojali. Usimamie mipaka yako.

Lakini ni muhimu zaidi kuangalia vitendo vyake. Je, yupo tayari mkutane kwako au anakuzungusha na anataka mchati tu? Je, kweli anaonesha kujutia au anakuchukulia poa tu?
 
Hapo ndo ukiambiwa ukisimama nchale ukikimbia nchale

Inawezekana kumalizana kwa amani, yaani baada ya makasiriko ya mpito ukakubali mapenzi huisha na maisha mengine yakaendelea kwa kushirikiana ama vinginevyo.
 
Si rahisi kujua kama mwanamke anataka mrudiane.
Hasa pale unapokua humwelewi kwa vitu vinavyotokea.
Kutokana na wanaume nliowasaidia kuwarudisha ma ex wao.
Wakiachwa wampe muda huyo mwanamke bila kumtafuta. Na baadae mwanamke anaanza kujirudi tena, nimeona hivi vitu vinajirudia rudia. Nawe ukiona ishara kadhaa ujue anataka mrudiane. Pia uangalie ishara nyingi zaidi, sio uangalie moja tu na useme anataka kurudiana nawe.
Ni muhimu umpe nafasi ajidhihirishe kwako tena kama anafaa.
Sio lazima urudiane naye, hasa kama umekua kimaisha. Ukirudiana naye lakini yeye yupo palepale atakurudisha nyuma badala ya kusonga mbele.
Ni muhimu ujue kuwa hata kama anataka mrudiane, haina maana mahusiano yenu ndo yatakua mazuri muda huu.
Hivyo, ukiona ishara hizi usikimbilie kurudiana naye.
.
Anakuomba msamaha kwa kuvunja mahusiano.
Ukiona ivi ujue amekubali kujishusha kuona makosa yake.
Ujue kuna kitu anajutia kwa kuvunja mahusiano yenu.
Akikuomba msamaha usianze tena kumwagia hasira zako za kwanini alikuacha. Bali msamehe na kuwa mpole. Kuonesha hasira maana yake bado anakuumiza moyoni sababu alikuacha.
.
Anajiweka karibu na uwepo wako.
Anajiweka sehemu ambazo mtaonana tu.
Anakuja karibu na kazini kwako, au unapofanyia mazoezi au unapoendaga kupumzika au popote ili mradi muonane tena.
.
Atatafuta njia kukuonesha anajali.
Anaweza kukutumia sms za motisha. Au,
Anaweza anaweza kukusaidia kufanya kitu, au chochote cha kuonesha anajali.
Ujue anatafuta sababu muongee zaidi au muwe karibu.
.
Atakusifia bila sababu wala kutegemea.
Sio sifa za juu juu, hapana.
Atakusifia kwa kitu kuhusu wewe au matendo yako.
Nayo ni njia ya kukuonesha “nilikosea, saivi naona kitu”.
Pia ukiona anakushukuru kwa moyo, ujue nayo ni sifa na anatamani ayarudie tena hayo.
.
Atajifanya amekupotezea.
Ili asioneshe kuwa ameumizwa na kuachana kwenu.
Atajifanya ameshakusahau na anaendelea na maisha bila wewe.
Utajuaje sasa anakutaka bado?
Atataka ajue kuwa amekupotezea.
Atatumia nguvu nyingi kukuonesha hilo.
Ili aone utafanyaje. We cha kufanya mwache afanye ivo akichoka atajirudi.
.
Atakushirikisha malengo yake.
Na utaona pia anataka kujua kuhusu wewe.
Ujue ni njia ya kutaka mrudiane.
Wapenzi huwa wanashirikishana malengo. Huwafanya waaminiane zaidi.
.
Anakutafuta lakini anaondoka tena ukimlazimisha.
Mwanamke akiwa anakurudia nenda naye taratibu.
Ila ukiwa na haraka ya kurudi penzini ataondoka tena.
Kisha baada ya muda atakutafuta tena. Usiharakishe ukiona anarudi kwako.
Pia atakupotezea tena ukionesha kumtaka sana.
.
Anakubali mkutane lakini haongelei kurudiana.
Kwanini haongelei kurudiana?
Sababu anaogopa mahusiano yenu yatakua kama yalivyokua mwanzo
Japo bado anapenda kuwa nawe lakini hajisikii amani kurudi kwenye mahusiano.
Hivyo, kama kawaida, usilazimishe we nenda naye taratibu.
.
Atakukasirikia.
Sababu hataki kujishusha lakini bado anakukubali.
Muda mwingine mwanamke anatumia hasira kuonesha hisia zake za upendo.
We usiingie kwenye hasira zake. Wala usibishane naye kwa lolote maana hauna cha kumshawishi.
Lakini kama hasira yake ni juu ya kitu kinachoeleweka kama vile ulikua humtimizii ahadi ujue ili mrudiane lazima ubadilike.
.
Haeleweki.
Kuna muda atakurudia.
Muda mwingine anafanya kama hajawahi kukujua.
Ukiona hivyo ujue bado hajajiamini na uamuzi wa kurudiana.
We endelea kuenda naye taratibu.
.
Ana wivu ukiwa na mwanamke mwingine.
Sababu anaogopa kusahauliwa na wewe.
Na bado anatamani awe katika iyo nafasi.
Hata kama akikukasirikia, usiache kuwa na mwanamke mwingine sababu ya mwanamke aliyekuacha.
Na kama akitaka kurudiana, uangalie mwenyewe ni mwanamke yupi anakufaa kuendeleza naye maisha.
.
Atakujaribu.
Ataijaribu mipaka yako ili ajue kama bado anakuendesha au la.
Mfano, atakupigia usiku aone kama utapokea, atakuomba umsaidie kitu, atakuambia kitu kama “we ndo nnaye kuamini katika hili”, atakualika kufanya kitu pamoja, atakuuliza kuhusu mahusiano yako ya sasa.
Yote ayo ili ajue bado unamfikiria kiasi gani.
We onesha kutojali. Usimamie mipaka yako.

Lakini ni muhimu zaidi kuangalia vitendo vyake. Je, yupo tayari mkutane kwako au anakuzungusha na anataka mchati tu? Je, kweli anaonesha kujutia au anakuchukulia poa tu?
Ila we jamaa akili yako inawazaga mapenzi tu
 
Back
Top Bottom