Ukimya uliokuwepo Ikulu umenistua!!

Ukimya uliokuwepo Ikulu umenistua!!

Mie nimemuona Prof Ndalichako yuko pale Kimwili tu si kifikra na kiakili!

Seriously Sehemu ya Pili ya Wimbo wetu wa Taifa tunapoombea Taifa letu Mwenyezimungu haipokei Tangu Awamu ya Tano imeingia
Watu wamechoka ........... Badala ya kukaa nyumabni wapumzike na familia zao kila second week lazima wakutanishwe Jumapili Ikulu kuapishwa kwa mteule/wateule fulani!!
 
Anzieni msoga kwa mstaafu ndio alituletea janga hili kwa kuogopa chama kisifie mikononi mwake, yeye alijichumia pesa ya kutosha anakula nchi ughaibuni shida zetu katuachia wenyewe tunateseka peke yetu.

Anzia msoga mstaafu awaeleze alikuwa na nia ya kujenga nchi au ni ubinafsi ulikuwa unamtuma kutuletea janga hili?!

Anzia msoga kwa mstaafu awaeleze huyu aliyekuwa waziri wake hakumjua kama Hana aiba ya uongozi au alifanya hivyo kutukomoa watanzania halisi wenzie?!

Anzia msoga tena anzia msoga nasema, anzia msoga mstaafua awaeleze furaha aliyo nayo kwa Tanzania na watanzania wenye njaa, wenye kiu, wenye magonjwa, wasiomudu elimu bure ya msingi mpaka sekondari, wenye kufungwa na kuwekwa vizuizini ili wenye madaraka wafurahi!
ANZIA MSOGA.
[emoji122] [emoji122] [emoji122] nimekuelewa mkuu!waanzie hapo maana wengine kichwa tikiti Maji!
 
Akiwepo Mwigulu Nchemba, Nape Nnauye na mawaziri kadhaa wa serikali ambao ni makada nguli wa CCM kwenye kuapishwa kwa viongozi waliokuwa wameteuliwa na Mheshimiwa Rais, nimeona kuna ukimya wa kutisha sana hadi nimejiuliza kulikoni?

Hata Makonda alipopewa Pongezi zake sikuona kama kuna mwitikio toka kwa viongozi wengine wa serikali walipokuwemo mle ndani. utulivu hata wakati Mheshimiwa Rais akijaribu kuwa mcheshi kwa wageni wake makofi yaliyokuwa yanapigwa yalikuwa haba sana. Hii hali imenifikirisha sana. Au kwa kuwa leo ni Week-end watu wana uchovu wa jana?
Ukiona hivyo ujue Betri ya kiheherere cha madaraka imeanza kuisha charge ... wasiwasi wangu umeme unaashiria kukatika sasa sijui watacharge na nini ...
 
Mkuu kwani wewe unaona? Kama kweli unaona mbona unabishana na asiyeona? Utawala huu sidhani kama utapata chchte kwa kutoa povu utadhani umemfumania mkeo.
Unajifurahisha. Ni haki yako. Endelea.
 
Mimi nimekumbuka tu ile hekaya ya Mfalme J.u.h.a, hata sijui kwa nini!
 
Back
Top Bottom