Ukimya ni usaliti

Ukimya ni usaliti

Nyani Ngabu

Platinum Member
Joined
May 15, 2006
Posts
97,070
Reaction score
136,458
Labda ni mimi tu. Labda mimi ndo tatizo. Labda nina uwezo mdogo wa kuelewa mambo.

Labda ni hivi au labda ni vile.

Labda nategemea mambo flani flani toka kwa watu ambao sipaswi kutegemea chochote au lolote toka kwao.

Kuna ukimya wa ajabu sana kutoka kwa baadhi ya watu na taasisi ambazo mtu ungedhani ziko mstari wa mbele katika kutetea haki za kibinadamu.

Kwa uwazi tu, sitegemei chochote toka kwa muuaji na kiongozi haramu.

Ataanzia wapi kukemea kilichotokea na kutoa pole kwa wahanga?

Lakini wengine nao je?

Wako wapi wale viongozi wa dini ambao huwa wanakemea utekaji?

Wako wapi wale viongozi wa zamani ambao wamestaafu kukemea kilichotokea?

Watu wamejikausha tu kama vile hakuna chochote kilichotokea!

Kuna mambo mtu mwenye akili timamu hupaswi kuyakalia kimya.

Zaidi ya wiki sasa na watu hawasemi chochote.

Ukimya mbele ya ukiukwaji wa makusudi wa haki za kibinadamu ni usaliti.

Waendelee kupumzika kwa amani wazalendo wote waliopoteza maisha yao na wale walioumizwa.

Kwa nyie wasaliti, kama mnadhani kila kitu ni upepo tu na lililotokea nalo litapita tu kama upepo, subirini muone.
 
Labda ni mimi tu. Labda mimi ndo tatizo. Labda nina uwezo mdogo wa kuelewa mambo.

Labda ni hivi au labda ni vile.

Labda nategemea mambo flani flani toka kwa watu ambao sipaswi kutegemea chochote au lolote toka kwao.

Kuna ukimya wa ajabu sana kutoka kwa baadhi ya watu na taasisi ambazo mtu ungedhani ziko mstari wa mbele katika kutetea haki za kibinadamu.

Kwa uwazi tu, sitegemei chochote toka kwa muuaji na kiongozi haramu.

Ataanzia wapi kukemea kilichotokea na kutoa pole kwa wahanga?

Lakini wengine nao je?

Wako wapi wale viongozi wa dini ambao huwa wanakemea utekaji?

Wako wapi wale viongozi wa zamani ambao wamestaafu kukemea kilichotokea?

Watu wamejikausha tu kama vile hakuna chochote kilichotokea!

Kuna mambo mtu mwenye akili timamu hupaswi kuyakalia kimya.

Zaidi ya wiki sasa na watu hawasemi chochote.

Ukimya mbele ya ukiukwaji wa makusudi wa haki za kibinadamu ni usaliti.

Waendelee kupumzika kwa amani wazalendo wote waliopoteza maisha yao na wale walioumizwa.

Kwa nyie wasaliti, kama mnadhani kila kitu ni upepo tu na lililotokea nalo litapita tu kama upepo, subirini muone.
Ni kweli huu ni Usaliti hata vyombo vyetu vya habari wamejifanya hawajui kilichotokea!!!
 
Kilichotokea kinahitaji uthibitisho gani?
Uharibifu wa mali za watu na miundombinu ulifanywa na vijana wavuta bangi hauonekani??
Alaaniwe roma na mange kijambio kwa kuhamasisha hiki kilichotokea
Mali za watu na Miundombinu tunaweza kuzirejesha wakati wowote ule Je maisha ya watu mtayarejesha lini? Toka lini adhabu ya mtu kuandamana ni kumuua?
 
Labda ni mimi tu. Labda mimi ndo tatizo. Labda nina uwezo mdogo wa kuelewa mambo.

Labda ni hivi au labda ni vile.

Labda nategemea mambo flani flani toka kwa watu ambao sipaswi kutegemea chochote au lolote toka kwao.

Kuna ukimya wa ajabu sana kutoka kwa baadhi ya watu na taasisi ambazo mtu ungedhani ziko mstari wa mbele katika kutetea haki za kibinadamu.

Kwa uwazi tu, sitegemei chochote toka kwa muuaji na kiongozi haramu.

Ataanzia wapi kukemea kilichotokea na kutoa pole kwa wahanga?

Lakini wengine nao je?

Wako wapi wale viongozi wa dini ambao huwa wanakemea utekaji?

Wako wapi wale viongozi wa zamani ambao wamestaafu kukemea kilichotokea?

Watu wamejikausha tu kama vile hakuna chochote kilichotokea!

Kuna mambo mtu mwenye akili timamu hupaswi kuyakalia kimya.

Zaidi ya wiki sasa na watu hawasemi chochote.

Ukimya mbele ya ukiukwaji wa makusudi wa haki za kibinadamu ni usaliti.

Waendelee kupumzika kwa amani wazalendo wote waliopoteza maisha yao na wale walioumizwa.

Kwa nyie wasaliti, kama mnadhani kila kitu ni upepo tu na lililotokea nalo litapita tu kama upepo, subirini muone.
Tumevunjiwa maduka na kuibiwa,ndugu zetu wamekatwa vidole kisa walikua na wino wa kupiga kura,sasa tunapanda daladala mbezi kwenda city center miundombinu ya mwendokasi imechomwa na wahalifu
 
Kilichotokea kinahitaji uthibitisho gani?
Uharibifu wa mali za watu na miundombinu ulifanywa na vijana wavuta bangi hauonekani??
Alaaniwe roma na mange kijambio kwa kuhamasisha hiki kilichotokea

C.C.M tumewapa dhamana ya kutulinda wananchi na mali zetu, kilichotokea ni kuwa CCM imeshindwa kuwalinda Watanganyika na mali zao!
Misiba iliyopo mtaani si ya wanaCHADEMA au wanaCCM pekee bali ni ya WATANGANYIKA!
IF WE MUST DIE..............................
#TUTAKUWEPO
 
Kwa baadhi ya maeneo duniani true free speech ni illusion kutokana na kitakachotokea baada ya kutumia 'haki' hiyo ya true free speech!

Mleta mada, naomba uwaelewe unaowalalamikia.
Mtu aliye muoga kukemea maovu yayokeayo kwenye jamii hana tofauti na hao watenda uovu.

Akina Mandela wangekuwa ni waoga kama ulivyoelezea hapo basi utawala wa makaburu ungekuwa bado upo.

Mbele ya uovu mimi sitokaa kimya.
 
Ni kweli huu ni Usaliti hata vyombo vyetu vya habari wamejifanya hawajui kilichotokea!!!
FB_IMG_17624363654153733.jpg
 
C.C.M tumewapa dhamana ya kutulinda wananchi na mali zetu, kilichotokea ni kuwa CCM imeshindwa kuwalinda Watanganyika na mali zao!
Misiba iliyopo mtaani si ya wanaCHADEMA au wanaCCM pekee bali ni ya WATANGANYIKA!
IF WE MUST DIE..............................
#TUTAKUWEPO
CCM ndo imevunja vituo vya mwendokasi? CCM ndo imechoma maduka na sehemu za biashara za watu? Huna akili wewe hata ukiishiwa unga ndani utailaumu CCM
 
Tumevunjiwa maduka na kuibiwa,ndugu zetu wamekatwa vidole kisa walikua na wino wa kupiga kura,sasa tunapanda daladala mbezi kwenda city center miundombinu ya mwendokasi imechomwa na wahalifu
Hayo Maduka na miundombinu inaweza kurudishwa na kutengenezwa!! Fikiria maisha ya maelfu ya watu waliouliwa kinyama na polisi uhai wao mtaurudisha?
 
Tengeneza bango andika ujumbe wako kesho ingia nalo mtaani ukiwa umelinyanyua juu
 
Labda ni mimi tu. Labda mimi ndo tatizo. Labda nina uwezo mdogo wa kuelewa mambo.

Labda ni hivi au labda ni vile.

Labda nategemea mambo flani flani toka kwa watu ambao sipaswi kutegemea chochote au lolote toka kwao.

Kuna ukimya wa ajabu sana kutoka kwa baadhi ya watu na taasisi ambazo mtu ungedhani ziko mstari wa mbele katika kutetea haki za kibinadamu.

Kwa uwazi tu, sitegemei chochote toka kwa muuaji na kiongozi haramu.

Ataanzia wapi kukemea kilichotokea na kutoa pole kwa wahanga?

Lakini wengine nao je?

Wako wapi wale viongozi wa dini ambao huwa wanakemea utekaji?

Wako wapi wale viongozi wa zamani ambao wamestaafu kukemea kilichotokea?

Watu wamejikausha tu kama vile hakuna chochote kilichotokea!

Kuna mambo mtu mwenye akili timamu hupaswi kuyakalia kimya.

Zaidi ya wiki sasa na watu hawasemi chochote.

Ukimya mbele ya ukiukwaji wa makusudi wa haki za kibinadamu ni usaliti.

Waendelee kupumzika kwa amani wazalendo wote waliopoteza maisha yao na wale walioumizwa.

Kwa nyie wasaliti, kama mnadhani kila kitu ni upepo tu na lililotokea nalo litapita tu kama upepo, subirini muone.
Nimemsikia Prof Tibaijuka na Kanisa katoliki...yaani safari hii hadi mzee Warioba kakausha?
 
Mali za watu na Miundombinu tunaweza kuzirejesha wakati wowote ule Je maisha ya watu mtayarejesha lini? Toka lini adhabu ya mtu kuandamana ni kumuua?
Echolima1 a.k.a choo cha kulima kimoja(1). Mkuu niseme tu kule jukwaa la international hapakufai uwezo wako mkubwa wa kujenga hoja upo hapa kwenye jukwaa la siasa.
 
Back
Top Bottom