PROF. ENG
Senior Member
- Nov 15, 2011
- 122
- 34
Mume wangu nakupenda sana, ujilinde, mimi siwezi kukulinda au kukuchunga kila uendapo, unaweza ukawa kuna mambo unayafanya ambayo mimi hutaki niyajue na wala sitaki nijue, Tafadhali sana lolote lile utakalofanya jua kuna ukimwi, Angalau ukumbuke kutumia kinga, kwakweli sitakusamehe wala kukuhudumia siku ukipatwa na ukimwi. Hayo ni maneno ambayo mke alikuwa anamwambia mumewe. Lakini baada ya miaka kadhaa ya ndoa kama nane hivi mke ikajulikana yeye ndio amepata ukimwi bahati nzuri mume alipoenda kucheki yeye alikuwa bado hajaathirika. Mbaya zaidi jamaa hajawahi kusikia wala kuhisi kama mkewe anatoka nje ya ndoa mpaka alipogundua dalili za ukimwi kwa mkewe.
Kweli ndoa ngumu. Kupata mtu muaminifu ni ndoto.
Kweli ndoa ngumu. Kupata mtu muaminifu ni ndoto.