Uke wenza (najua wanawake mtachukia hili)

Uke wenza (najua wanawake mtachukia hili)

Mohamedex121

JF-Expert Member
Joined
Jan 27, 2022
Posts
1,734
Reaction score
3,310
Wanawake hata wakiwa wacha Mungu namna gani wanashindwa kukubali rukhsa moja iliyotolewa na Allah aliyetukuka, nayo ni mume kuoa mke wa pili. Allah Aliyetukuka kwa hekma yake ametoa ruhusa hii pale aliposema:

"Basi oeni mnaowapenda katika wanawake wawili, au watatu au wanne, na mkiogopa kuwa hamuwezi kufanya uadilifu, basi oeni mmoja tu' (Qur'an 4:3).

Kitu muhimu cha mke kufanya ni kumsaidia mumewe kuchagua mke mwenye dini na maadili ya Kiislamu. Usiwe ndio sababu ya kuharibu uhusiano na wewe na kumpelekea kufanya zinaa kwa ajili yako kuifanya hali yake kuwa ngumu katika suala hilo.

Kisheria mume hahitaji idhini au ruhusa ya mke katika kuoa mke mwengine. La kufanya ni kumsaidia aweze kutimiza haki zako na za mke mpya na wala usiwe ndio sababu ya uhasama na kutolewa talaka.

Ukimruhusu mumeo kuoa mke qa pili utapata faida zifuatazo:

(1) Utapata thawabu kwa kumzuia mumeo na zinaa.

(2) Mumeo atazidi kukupenda na kukuthamini, kinyume na utakapomfanyia matatizo huenda akachukizwa na wewe na huenda apoteze mapenzi yote kwako.

(3) Utakuwa miongoni kwa waumini wanaopokea na kukubali sheria za dini. Utapata thawabu za kuwa na subra kwa jambo zito kama hili.

(4) Utakuwa mfano mzuri kwa wanawake wengine na utapata thawabu kwa kila mwanamke atakaekuiga mfano wako kwa kukubali waume zao kuongeza mke

Allah awatangulie hili dada zangu muwe wenye kuridhia kwa moyo msafi, Amin.

IMG_20231029_131529.jpg
 
Ngumu kumeza hii naona itanikaba kabisa. Ningekua muislam kwa mfano, siku ambayo mume angenambia anamleta mke mwenzangu asubuhi sana ningetafuta utaratibu wa kusepa.
Kwanini hutaki uke wenza??
 
Napambana inshaAllah nataka kuoa wake wawili Kwa harusi Moja .
Hii ni kuondoa Ile ya mke mkubwa na mdogo.
Mwanamke anakua mke pindi unapo lala nae haijalishi mmefunga ndoa au lah asha na agano la ndoa linatimizwa kwa damu kama binti atakua Bikra, ndoa ni tendo kiroho na kimwili linakamilishwa kwa kukutana kimwili jinsia ya kike na kiume na siyo kwa harusi wala ibada na swala kama tujuavyo wanadamu .


Sasa nikuulize swali kama ifuatavyo;-


Je, utaondoaje dhana ya mke mkubwa na mke mdogo kwa mujibu wa kuzingatia tendo la ndoa, ni vipi basi utazingatia dhana hii kuondoa mtazamo wa mke mkubwa na mdogo ukizingatia yule wa kwanza kumuingia ndiye wa kwanza na ndiye atakaye kua mke mkubwa kwa wa mwisho kumuingilia ambaye atakua mdogo?
 
[QUOTE="Loading failed, post: 48274531, member: 727
Je, utaondoaje dhana ya mke mkubwa na mke mdogo kwa mujibu wa kuzingatia tendo la ndoa, ni vipi basi utazingatia dhana hii kuondoa mtazamo wa mke mkubwa na mdogo ukizingatia yule wa kwanza kumuingia ndiye wa kwanza na ndiye atakaye kua mke mkubwa kwa wa mwisho kumuingilia ambaye atakua mdogo?
[/QUOTE]
Kama wote nimeona siku Moja huwezi epuka Kwamba mmoja ndio atakuwa wa kwanza kuingiliwa lakini point na Lengo langu si kuoa mmoja Kisha baada ya miaka au miezi au siku baada uoe mwingine , basi yule wa kwanza hujiweka status ya mi-mke mkubwa.
Pia unaweza kuwadanganya ila ukweli unaujua.Kumdanganya mmke Kwa kuepuka Shari au kuongeza mapenzi hakuna tatizo.
 
Back
Top Bottom