UKAWA wamchokoza Rais Magufuli

UKAWA wamchokoza Rais Magufuli

Mimi nilishangazwa sana na swala la posho kutolewa muongozo mara mbili hapo ndio niliamini bunge linaongozwa na baba j.eska
 
Source ndo ya kipumbavu..... eti mwanahalisi...

Ikifika karibia na uchaguzi watapinga maandishi yao
 
Husirudie kuwahusisha wabunge wa ukawa na ccm,wabunge wa ccm ni wafia matumbo yao wakati wabunge wa ukawa wao ni mwananchi kwanza mengine baadae
wewe unawasemea,lakini wao tayari wamethibitisha kwa kauli ya mbatia...................
 
Halafu cha kustaajabisha akikosolewa yeye, anadai wanaomkosoa wanamchonganisha na Watanzania.

Naona matendo anayo ruhusu kufanywa na serikali yake ni sawa na kuichonganisha na watanzania
 
Halafu cha kustaajabisha akikosolewa yeye, anadai wanaomkosoa wanamchonganisha na Watanzania.
Mkuu hiyo ni tabia ya kawaida kwani mtenda akitendewa?
 
  • Thanks
Reactions: BAK
wenye akili za kuku ni nyinyi magamba maana hamchelewi kusahau,leo hii watu wanapata futali bila sukari alafu mnakuwa kama mazuzu
Kwa mwendo huu basi wewe una akili kama Ngiri kwa kusahau CCM imeshinda uchaguzi mkuu majuzi tu na inawaburuza UKAWA kama inavyotaka hadi mjifunze siasa siyo matusi na vurugu. Na LAZIMA MJIFUNZE MPENDE MSIPENDE.
 
Kwa mwendo huu basi wewe una akili kama Ngiri kwa kusahau CCM imeshinda uchaguzi mkuu majuzi tu na inawaburuza UKAWA kama inavyotaka hadi mjifunze siasa siyo matusi na vurugu. Na LAZIMA MJIFUNZE MPENDE MSIPENDE.
Huo ndio upeo wa akili yako na nyoka daima hawezi kumzaa paka,matusi ni jadi ya wana ccm
 
  • Thanks
Reactions: BAK
UKAWA wamchokoza Rais Magufuli


Rais John Magufuli

WABUNGE walio katika Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) jana walimtuhumu Rais John Magufuli kuwa analiendesha Bunge kutokea Ikulu kwa kumtumia Naibu Spika, Dk. Tulia Ackson.

Wakizungumza na waandishi wa habari katika ofisi ya habari ya Bunge, wabunge hao walisema wanachokiona bungeni ni Rais Magufuli akiwa kama Spika wa Bunge huku viongozi wengine wa Bunge wakiwa ni matawi yake.

Wa kwanza kutoa tuhuma hizo katika mkutano huo uliohudhuriwa na wabunge wengi wa Ukawa alikuwa Mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara ambaye alisema Bunge la 11 haliko huru kwa sababu maamuzi yake yanatolewa na Rais Magufuli kutoka Ikulu kupitia Naibu Spika, Dk. Ackson.

“Bunge linaongozwa na Magufuli (Rais John) kutoka Ikulu moja kwa moja kupitia Dk. Tulia, Rais ndiye Spika wengine ni matawi tu, mfano tukiangalia mwongozo wa posho za wabunge wa upinzani uliotolewa juzi, umetolewa uamuzi mara mbili, haiwezekani kitu kimoja kikatolewa maelezo mawili tofauti ni wazi kuwa anafuata maagizo kutoka juu,” alisema Waitara.

Alisema hivi sasa kuna mhimili mmoja wa dola ambao ni Serikali Kuu kwa sababu maamuzi yote yanatolewa na chombo hicho huku akilitaja Bunge kuwa tawi la Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Alisema Naibu Spika, Dk. Tulia hakupaswa kutoa uamuzi wa wabunge wa Ukawa kutolipwa posho kwa sababu ni mtuhumiwa wa jambo hilo.

“Kutomwita mheshimiwa tunamaanisha na tungekuwa na jina baya zaidi tungemwita, nina wasiwasi na PhD yake ya sheria, sijawahi kuona mtu anayelalamikiwa anatoa hukumu sijawahi kuona, yeye ni mtuhumiwa anatoaje uamuzi. Bora Spika Job Ndugai arudi,” alisema Waitara.

Katika mwendelezo wa tuhuma zake hizo, alisema Naibu Spika, Dk. Tulia aliteuliwa kimkakati na Rais Magufuli na amekuwa akiongoza matukio mbalimbali yanayogharimu wananchi.

“Naibu Spika ni Mbunge wa ‘Voda Faster’, aligombea uspika CCM wakamkataa, baada ya kuona amekataliwa Rais akaamua kumpa ubunge ili aje kugombea nafasi ya Naibu Spika ambayo nayo ameilazimisha hata CCM walikuwa hawamtaki,” alituhumu Waitara.

Waitara alienda mbali zaidi kwa kumtuhumu Dk. Tulia kuwa miongoni mwa watu waliovuruga mchakato wa upatikanaji wa Katiba Mpya kwa kushiriki kukata maoni ya wananchi na kubakiza yaliyotolewa na CCM.


Katika mlolongo huo wa tuhuma, Waitara aliendelea kutuhumu kuwa Dk. Tulia alishiriki kuwanyima haki ya kulinda matokeo ya kura kwa kuwataka wananchi kukaa umbali wa mita 200 kutoka kituo cha kupigia kura wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka jana.

Aliendelea kusema kuwa pia alishiriki kurudisha Sh bilioni 12 Ikulu bila kumshirikisha Spika Ndugai.

Kwa upande wa Mbunge wa Vunjo, James Mbatia, alisema Serikali haiheshimu maamuzi wabunge na kwa mara kadhaa Rais Magufuli amekuwa akitoa uamuzi bila kuwashirikisha.

“Bunge linakaa na kujadili bajeti na kupitisha lakini Serikali haiheshimu na haitekelezi, kuna haja gani ya kuwa na mhimili wa Bunge? Dk. Magufuli (Rais John) amekuwa akifanya maamuzi yake mwenyewe ya kuchukua fedha na kuzigawa katika taasisi mbalimbali bila kupitishwa na Bunge jambo ambalo ni kinyume cha sheria.

“Kinachotushangaza ni fedha zinazobaki katika taasisi mbalimbali kupelekwa Ikulu wakati zinapaswa kurudi Hazina, anapelekewa yeye ndiye Hazina? Rais hapaswi kuzipangia fedha kazi kabla ya kupitishwa na Bunge, hakuna haja ya kuwa na huu mhimili kama unaingiliwa kiasi hiki,” alisema Mbatia.

Mbatia alisema msimamo wa Ukawa ni kufutwa kwa posho na endapo Serikali itapitisha hoja ya kukatwa kwa kodi mafao ya wabunge inapaswa iwakate viongozi wa ngazi zote waliotajwa katika sheria hiyo.

“Sheria mafao ya wabunge inahusu viongozi wote wa kisiasa, pia inaenda sambamba na pensheni ya Rais, Makamu wa Rais, mawaziri, Spika, Naibu Spika, wakuu wa mikoa na wilaya, iweje wachague wabunge tu kuwakata kodi kama ni hivyo wawakate viongozi wote waliotajwa ndiyo watakuwa wametenda haki,” alisema Mbatia.

SOURCE: Mwanahalisi
UKAWA wamchokoza Rais Magufuli


Rais John Magufuli

WABUNGE walio katika Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) jana walimtuhumu Rais John Magufuli kuwa analiendesha Bunge kutokea Ikulu kwa kumtumia Naibu Spika, Dk. Tulia Ackson.

Wakizungumza na waandishi wa habari katika ofisi ya habari ya Bunge, wabunge hao walisema wanachokiona bungeni ni Rais Magufuli akiwa kama Spika wa Bunge huku viongozi wengine wa Bunge wakiwa ni matawi yake.

Wa kwanza kutoa tuhuma hizo katika mkutano huo uliohudhuriwa na wabunge wengi wa Ukawa alikuwa Mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara ambaye alisema Bunge la 11 haliko huru kwa sababu maamuzi yake yanatolewa na Rais Magufuli kutoka Ikulu kupitia Naibu Spika, Dk. Ackson.

“Bunge linaongozwa na Magufuli (Rais John) kutoka Ikulu moja kwa moja kupitia Dk. Tulia, Rais ndiye Spika wengine ni matawi tu, mfano tukiangalia mwongozo wa posho za wabunge wa upinzani uliotolewa juzi, umetolewa uamuzi mara mbili, haiwezekani kitu kimoja kikatolewa maelezo mawili tofauti ni wazi kuwa anafuata maagizo kutoka juu,” alisema Waitara.

Alisema hivi sasa kuna mhimili mmoja wa dola ambao ni Serikali Kuu kwa sababu maamuzi yote yanatolewa na chombo hicho huku akilitaja Bunge kuwa tawi la Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Alisema Naibu Spika, Dk. Tulia hakupaswa kutoa uamuzi wa wabunge wa Ukawa kutolipwa posho kwa sababu ni mtuhumiwa wa jambo hilo.

“Kutomwita mheshimiwa tunamaanisha na tungekuwa na jina baya zaidi tungemwita, nina wasiwasi na PhD yake ya sheria, sijawahi kuona mtu anayelalamikiwa anatoa hukumu sijawahi kuona, yeye ni mtuhumiwa anatoaje uamuzi. Bora Spika Job Ndugai arudi,” alisema Waitara.

Katika mwendelezo wa tuhuma zake hizo, alisema Naibu Spika, Dk. Tulia aliteuliwa kimkakati na Rais Magufuli na amekuwa akiongoza matukio mbalimbali yanayogharimu wananchi.

“Naibu Spika ni Mbunge wa ‘Voda Faster’, aligombea uspika CCM wakamkataa, baada ya kuona amekataliwa Rais akaamua kumpa ubunge ili aje kugombea nafasi ya Naibu Spika ambayo nayo ameilazimisha hata CCM walikuwa hawamtaki,” alituhumu Waitara.

Waitara alienda mbali zaidi kwa kumtuhumu Dk. Tulia kuwa miongoni mwa watu waliovuruga mchakato wa upatikanaji wa Katiba Mpya kwa kushiriki kukata maoni ya wananchi na kubakiza yaliyotolewa na CCM.


Katika mlolongo huo wa tuhuma, Waitara aliendelea kutuhumu kuwa Dk. Tulia alishiriki kuwanyima haki ya kulinda matokeo ya kura kwa kuwataka wananchi kukaa umbali wa mita 200 kutoka kituo cha kupigia kura wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka jana.

Aliendelea kusema kuwa pia alishiriki kurudisha Sh bilioni 12 Ikulu bila kumshirikisha Spika Ndugai.

Kwa upande wa Mbunge wa Vunjo, James Mbatia, alisema Serikali haiheshimu maamuzi wabunge na kwa mara kadhaa Rais Magufuli amekuwa akitoa uamuzi bila kuwashirikisha.

“Bunge linakaa na kujadili bajeti na kupitisha lakini Serikali haiheshimu na haitekelezi, kuna haja gani ya kuwa na mhimili wa Bunge? Dk. Magufuli (Rais John) amekuwa akifanya maamuzi yake mwenyewe ya kuchukua fedha na kuzigawa katika taasisi mbalimbali bila kupitishwa na Bunge jambo ambalo ni kinyume cha sheria.

“Kinachotushangaza ni fedha zinazobaki katika taasisi mbalimbali kupelekwa Ikulu wakati zinapaswa kurudi Hazina, anapelekewa yeye ndiye Hazina? Rais hapaswi kuzipangia fedha kazi kabla ya kupitishwa na Bunge, hakuna haja ya kuwa na huu mhimili kama unaingiliwa kiasi hiki,” alisema Mbatia.

Mbatia alisema msimamo wa Ukawa ni kufutwa kwa posho na endapo Serikali itapitisha hoja ya kukatwa kwa kodi mafao ya wabunge inapaswa iwakate viongozi wa ngazi zote waliotajwa katika sheria hiyo.

“Sheria mafao ya wabunge inahusu viongozi wote wa kisiasa, pia inaenda sambamba na pensheni ya Rais, Makamu wa Rais, mawaziri, Spika, Naibu Spika, wakuu wa mikoa na wilaya, iweje wachague wabunge tu kuwakata kodi kama ni hivyo wawakate viongozi wote waliotajwa ndiyo watakuwa wametenda haki,” alisema Mbatia.

SOURCE: Mwanahalisi

Sioni kama ni tatizo kwa raisi kiasi cha kushangaza kwani nikisheria bado rais ni sehemu ya bunge na pia ikumbukwe rais ni mwakilishi wa watanzania wote na dhamana yake ni kubwa kuliko mfano haswa juu ya usimamizi wa raslimali za nchi, na kwa hali ya tanzania tulipofika na kwa aina ya wabunge tunaowachagua baada ya kupewa buku saba tukiwaachia maamuzi ya jumla juu ya nchi hii tumekwisha kwani leo hii wabunge ndiyo wakwepa kodi wakubwa, wakiukaji wa sheria za nchi, wapo juu ya sheria, wananchi wanatakiwa wawasikilize wao na si wao wachukue maoni kwa wananchi. wabunge wetu leo ni wafanyabiashara wakubwa na wadanganyifu. tumeona leo wabunge wakidai na wakitetea makampuni kama ya simu yapunguziwe kodi, na si hivyo tu ni pamoja na kuwatetea mafisadi kwa maslahi binafsi
 
UKAWA wamchokoza Rais Magufuli


Rais John Magufuli

WABUNGE walio katika Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) jana walimtuhumu Rais John Magufuli kuwa analiendesha Bunge kutokea Ikulu kwa kumtumia Naibu Spika, Dk. Tulia Ackson.

Wakizungumza na waandishi wa habari katika ofisi ya habari ya Bunge, wabunge hao walisema wanachokiona bungeni ni Rais Magufuli akiwa kama Spika wa Bunge huku viongozi wengine wa Bunge wakiwa ni matawi yake.

Wa kwanza kutoa tuhuma hizo katika mkutano huo uliohudhuriwa na wabunge wengi wa Ukawa alikuwa Mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara ambaye alisema Bunge la 11 haliko huru kwa sababu maamuzi yake yanatolewa na Rais Magufuli kutoka Ikulu kupitia Naibu Spika, Dk. Ackson.

“Bunge linaongozwa na Magufuli (Rais John) kutoka Ikulu moja kwa moja kupitia Dk. Tulia, Rais ndiye Spika wengine ni matawi tu, mfano tukiangalia mwongozo wa posho za wabunge wa upinzani uliotolewa juzi, umetolewa uamuzi mara mbili, haiwezekani kitu kimoja kikatolewa maelezo mawili tofauti ni wazi kuwa anafuata maagizo kutoka juu,” alisema Waitara.

Alisema hivi sasa kuna mhimili mmoja wa dola ambao ni Serikali Kuu kwa sababu maamuzi yote yanatolewa na chombo hicho huku akilitaja Bunge kuwa tawi la Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Alisema Naibu Spika, Dk. Tulia hakupaswa kutoa uamuzi wa wabunge wa Ukawa kutolipwa posho kwa sababu ni mtuhumiwa wa jambo hilo.

“Kutomwita mheshimiwa tunamaanisha na tungekuwa na jina baya zaidi tungemwita, nina wasiwasi na PhD yake ya sheria, sijawahi kuona mtu anayelalamikiwa anatoa hukumu sijawahi kuona, yeye ni mtuhumiwa anatoaje uamuzi. Bora Spika Job Ndugai arudi,” alisema Waitara.

Katika mwendelezo wa tuhuma zake hizo, alisema Naibu Spika, Dk. Tulia aliteuliwa kimkakati na Rais Magufuli na amekuwa akiongoza matukio mbalimbali yanayogharimu wananchi.

“Naibu Spika ni Mbunge wa ‘Voda Faster’, aligombea uspika CCM wakamkataa, baada ya kuona amekataliwa Rais akaamua kumpa ubunge ili aje kugombea nafasi ya Naibu Spika ambayo nayo ameilazimisha hata CCM walikuwa hawamtaki,” alituhumu Waitara.

Waitara alienda mbali zaidi kwa kumtuhumu Dk. Tulia kuwa miongoni mwa watu waliovuruga mchakato wa upatikanaji wa Katiba Mpya kwa kushiriki kukata maoni ya wananchi na kubakiza yaliyotolewa na CCM.


Katika mlolongo huo wa tuhuma, Waitara aliendelea kutuhumu kuwa Dk. Tulia alishiriki kuwanyima haki ya kulinda matokeo ya kura kwa kuwataka wananchi kukaa umbali wa mita 200 kutoka kituo cha kupigia kura wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka jana.

Aliendelea kusema kuwa pia alishiriki kurudisha Sh bilioni 12 Ikulu bila kumshirikisha Spika Ndugai.

Kwa upande wa Mbunge wa Vunjo, James Mbatia, alisema Serikali haiheshimu maamuzi wabunge na kwa mara kadhaa Rais Magufuli amekuwa akitoa uamuzi bila kuwashirikisha.

“Bunge linakaa na kujadili bajeti na kupitisha lakini Serikali haiheshimu na haitekelezi, kuna haja gani ya kuwa na mhimili wa Bunge? Dk. Magufuli (Rais John) amekuwa akifanya maamuzi yake mwenyewe ya kuchukua fedha na kuzigawa katika taasisi mbalimbali bila kupitishwa na Bunge jambo ambalo ni kinyume cha sheria.

“Kinachotushangaza ni fedha zinazobaki katika taasisi mbalimbali kupelekwa Ikulu wakati zinapaswa kurudi Hazina, anapelekewa yeye ndiye Hazina? Rais hapaswi kuzipangia fedha kazi kabla ya kupitishwa na Bunge, hakuna haja ya kuwa na huu mhimili kama unaingiliwa kiasi hiki,” alisema Mbatia.

Mbatia alisema msimamo wa Ukawa ni kufutwa kwa posho na endapo Serikali itapitisha hoja ya kukatwa kwa kodi mafao ya wabunge inapaswa iwakate viongozi wa ngazi zote waliotajwa katika sheria hiyo.

“Sheria mafao ya wabunge inahusu viongozi wote wa kisiasa, pia inaenda sambamba na pensheni ya Rais, Makamu wa Rais, mawaziri, Spika, Naibu Spika, wakuu wa mikoa na wilaya, iweje wachague wabunge tu kuwakata kodi kama ni hivyo wawakate viongozi wote waliotajwa ndiyo watakuwa wametenda haki,” alisema Mbatia.

SOURCE: Mwanahalisi
Bado natafakari Ntatoa JIPU Baaada ya muda hivi Punde........... Please Wait........
 
Acha kukurupuka wewe, nani alikudanganya kama Rais ni sehemu ya Bunge!?

Sioni kama ni tatizo kwa raisi kiasi cha kushangaza kwani nikisheria bado rais ni sehemu ya bunge na pia ikumbukwe rais ni mwakilishi wa watanzania wote na dhamana yake ni kubwa kuliko mfano haswa juu ya usimamizi wa raslimali za nchi, na kwa hali ya tanzania tulipofika na kwa aina ya wabunge tunaowachagua baada ya kupewa buku saba tukiwaachia maamuzi ya jumla juu ya nchi hii tumekwisha kwani leo hii wabunge ndiyo wakwepa kodi wakubwa, wakiukaji wa sheria za nchi, wapo juu ya sheria, wananchi wanatakiwa wawasikilize wao na si wao wachukue maoni kwa wananchi. wabunge wetu leo ni wafanyabiashara wakubwa na wadanganyifu. tumeona leo wabunge wakidai na wakitetea makampuni kama ya simu yapunguziwe kodi, na si hivyo tu ni pamoja na kuwatetea mafisadi kwa maslahi binafsi
 
Ngoja tuone kama Magufuli ataingia na mahakamani kuwaamuru majaji na mahakimu kuamua against vyama vya upinzani vilivyoenda mahakamani kupinga amri ya polisi ya kupiga marufuku harakati za vyama vya siasa kujijenga kwa njia ya mikutano na maandamano!!

Kisisingizio ni "sababu za kiintelejensia ya usalama" kwamba katika mikutano hiyo wameambiwa vyama vitahamasisha wananchi kutokutii serikali yao (civil disobidience)!

Kisingizizio kingine ni eti kuna vyama vingine navyo vimetangaza kupitia njia hii kupinga kitakachokuwa kinasemwa na vyama vya upinzani. Sasa polisi wameona ni sbb na wameogopa kuwa kutakuwa na uvunjifu wa amani!!

Sijui wataishawishi kwa namna gani mahakama nayo iamini hiki wanachokiamini wao!!

Tunamkaribisha Tulia mahakamani!!
 
Back
Top Bottom