UKAWA nendeni Mahakamani kesho 15/10/2015

UKAWA nendeni Mahakamani kesho 15/10/2015

Wanajamvi,

Hili suala la kubaki vituoni baada ya kupiga kura linaanza leta ukakasi sasa, leo Mh. Raisi kaliongelea na kusisitiza watakaobaki vituoni watashughulikiwa. Nimemsikia mhe. Kinana na IGP pia wakiliongelea na mbaya zaidi kwenye magroup yote wana CCM wamefurahia sana tamko la leo la mh. Raisi ambae pia ni Amiri jeshi mkuu katika nchi ambayo Tume ya Uchaguzi haiko huru, tumeona wakurugenzi wa tume wakibadilishwa chini ya mwezi mmoja kabla ya uchaguzi kwa sababu za kikatiba/kisheria maana mhe. Raisi ana uwezo huo.

Lakini pia tuna kumbukumbu za chaguzi zilizo pita ambapo bila wananchi kuwepo eneo la tukio, sina uhakika kama mh. Wenje angepata ushindi zaidi ya mh. Masha aliye kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani.

Hii yote inaleta Sintofahamu na kuonyesha kama ule usemi wa Nape unatimizwa kwa njia hii.

Pia nimemuona Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC akiiweka kama issue ya kubaki kwenye vituo haiko kisheria.

Je, kama suala la kubaki vituoni kwa umbali usiopungua mita 100 liko kisheria, ni kwa nini UKAWA wasiende mahakamani kesho kwa hati ya dharula kuweza pata ufafanuzi na order ya mahakama kwenye jambo hili?

Nia ni kuepusha damu za Watanzania kumwagika maana ninavyoona, tunakoelekea sio kuzuri ifikapo tarehe 25 Oktoba.

Nawakilisha.


Mimi naona CCM imeshaona hawashindi uchaguzi na mbinu za magoli ya mikono zimekuwa ni ngumu , iliyobaki watumie goli la hockey , wazushe vurugu hii ndio turufu yao .

Wanataka kulitoboa jahazi tuzame sote
 
Lowassa atatimkia nyumbani kwake Uingereza,Mbowe Dubai.Wengine watakapokuwa wanapelekwa ICC wewe utakuwa KABURINI MUDA HUO.Wazazi na wako watakuwa wanahangaika ukimbizini.

Unadhani wazazi wako wewe au wazazi wa wakati wanaotumiwa na Rais JK kuleta vurugu dhidi ya raia watakuwa wapi?
 
tulia sindano ikuingie wewe gamba

wao ndio wanataka kuiba kura za ccm.
Nina wasiwasi kuwa nia ya kubaki vituoni ni kufanya fujo endapo watashindwa kwa namna yoyote ile.
Ni aibu sana kwa kiongozi kama lowassa kushauri kuwepo kwa mzingira ambayo yatahatarisha usalama kwa ajili yake binafsi

lowassa siyo wa thamani kuliko tanzania. Kuna mfumo wa kisheria wa kufuata endapo mtu hakuridhika na matokeo - sioni kwanini lowassa na matajiri wenzake ambao wanataka ikulu hata kwa damu ya watu wengine wanaogopa kufuata mfumo huu.

Tanzania kwanza, lowassa na maghufuli baadae!!!!!
 
Wakati upigaji kura unaendelea kwa nini wabaki vituoni? Mwaka 2010 ilikuwa hivi: tulipiga kura tukarudi nyumbani. Saa 10 au saa 11 tukarudi vituoni na tukakesha hata siku 3 ilipotakiwa. Hawa viongozi wanaotaka hata wakati wa upigaji kura wabaki wanafanya VOTER INTIMIDATION na hakuna panapokubalika hilo duniani. Ukimaliza kupiga kura nenda nyumbani na urudi kupata matokeo.
Hakuna anayeng'ang'ania kubaki kituonu baada ya kupiga kura hali ya kuwa hana sababu muafaka.
1. Ndani ya vyumba vya kupigia kura kazi ya mawakala ni pamoja na kuhakiki uhalali wa mpiga kura kabla hajapiga kura. wakati wakala anatekeleza wajibu wake huo hatakiwi kubabaishwa kimkakati na mtu au kikundi cha watu kutaka kulazimisha wapige kura au kuyakaribia masanduku ya kura.
2. ikitokea hali niliyoielezea hapo juu wapiga kura halali wakishirikiana na polisi ndio wanapaswa kushirikiana kuweka mambo sawa ikiwa na maana ya kutafsiri kanuni za upigaji kura ili kuondoa rabsha.
3. baada ya zoezi la kupiga kura kukamilika vyumba vya kupigia kura hugeuka kuwa vyumba vya kuhesabia kura, kanuni zinaelekeza kuwa kipindi cha kuhesabu kura ukiondoa wasimamizi wa uchaguzi ni watu wawili tu ndio wanaruhusa ya kuingia kwa lengo la kuangalia tu zoezi linavyoenda kwenye vyumba vya kuhesabia kura, watu hao ni mgombea na mwenyekiti wa kamati ya ulinzi wa wilaya.

Dhana ya ulinzi wa kura inakuja pale watu wasiohusika kisheria kutaka kuingia kwenye vyumba vya kuhesabia kura. Ndipo wapiga kura walioweka kambi mita 100 au zaidi wanapochukua hatua ya kuwazuia watu hao (mwenyekiti wa kamati ya siasa, katibu mwenezi, kampeni meneja, mpambe wa mgombea N.K)
polisi peke yao hawana weledi wa kutosha kusimamia jambo hili, hapa ndipo ulinzi shirikishi unapohusika.
Kujilinda na kulinda mali yangu ni haki yangu ya kikatiba.
 
Unalinda nini nje ya kituo cha kura?

Huamini mawakala wa ukawa waliopo ndani ya vituo? Huamini wasimamizi wa Kimataifa? Huwaamini NEC waliopo ndani ya vituo?

Hawa watu wanataka kuleta fujo tu, washughulikiwe ipasavyo.


Very well said!

Tanzania kwanza, Lowassa baadae!!
 
Vijana tusiwe kama Wajinga kutumiwa na wanasiasa vibaya.
Jiulize ukikaa hizo mita 200 utaweza kuona kinachoendelea ndani? Maana mita 200 ni viwanja viwili vya mpira.
Au mtakuwa na darubini?

Tutumie akili Vijana. Sisi bado hatujtimiza malengo yetu mengi kama hao tunaowapigania.
 
Who is ICC toa ujinga wako, mahakama hazikuwekwa kwa ajili ya wanyama au miti. Serikali haiwezi kuacha wajinga wacyhache walithiri taifa kisa kuogopa ICC. Kupigwa mtapigwa na kuvunjwa vyunjwa na ICC kama kuna wa kwenda ataenda lkn nyie mtabaki walemavu maisha yenu yote, maana hakuna namna tena, tumechoka na kutishiwa na nyau wa ICC.

Hapa hujashirikisha ufahamu wako na huenda unauelewa mdogo, je anayevunja vunja wengine na yeye yakimpata hayo. Mkuu vita haina macho acha kushabikia upumbavu.
 
Sheria hii ya kuwa umbl wa mt 100 au 200 bado hata tume ynyewe haijaitafsiri ipasavo,lkn ukwl sheria inataka pasiwepo na shughuli yyte iwe ya kisiasa au nyngnezo ktk umbali huo

Na nje ya umbali huo unaweza endelea na shuhuli za kawaida tu za kila siku bila kuathiri shughuli zitakazokuwa znaendelea ktk kituo cha kupigia kura.

Fikiri km kituo kitakuwa karibu na makazi ya watu.Mi nadhani c kosa kulingana na sheria hii watu kuwepo umbali huo wa mita 100,wacwac wao mi naona ni Hilo neno "kukaa"hili linatafsiri ya kungoja au kusubiri,

Lkn km watu watasubiri kwa nia ya kujua matokeo c kosa kwa mujibu wa sheria hii,lkn pia km ni kwa ajili ya kulinda kura,hapo cna uhakika sn kwmba zinalindwaje,ila pia c kosa km hawatathiri shughuli zitakazokuwa zikiendelea ktk kituo cha kupiga kura.

Mm pia ni mwanamabadiliko,kwa kauli ya Kikwete ni yakutilia mashaka,kwn watakuwa wanaingilia kaz za tume,na yy hakupaswa kuongelea maswala yanayoihusu tume,aiache tume iangalie sheria zake za uchaguzi,then tume yenyewe itoe tamko lake.
 
Si kila mtu atabaki kituoni lakini wanaotaka kubaki waachwe wabaki kwa mujibu wa Sheria. By the way, wapiga kura wote wakiondoka vituoni, msimamizi wa uchaguzi atamtangazia nani matokeo? Au watapiga kengele kuita Watu? Kama suala la kusubiri matokeo lipo kisheria, kwa nini. NEC, IGP na hata Rais wanaliongelea kama ni jambo linalofanywa kinyume cha Sheria? Sheria hiyo kwa nini hawakuifuta 'kisheria' kama wanaona hawaipendi. Nami nashauri wanasheria wa CHADEMA/UKAWA wakatafute ufafanuzi mahakamani.
Watanzania wengi ni wavivu wa kufanya kazi.Komaeni kupiga kelele huko vituoni halafu Mbowe atawaletea KIROBA CHA SEMBE Nyumbani.
 
Mkiambiwa watu Wana uzoefu hamuelewi, mnapiga kelele... Ni kwamba mawakala wengi si WAZALENDO sana, wanahongwa pesa ndefu aka wananunuliwa, na ndio maana Tume wamekataa UKAWA wa we na mawakala wa vyama vyao, stuka toroka uje
1. Sasa tatizo la mawakala ni la chama husika au Taifa??!! Unashindwa kupata watu wa kulinda kura kwa uzalendo unataka nchi??!!! Huu ni utetezi au unajizamisha zaidi?!!!
2. Tume imekataa mawakala unamaanisha nini kwa mfano????
 
Wangejua wanaaandaa watu na maji, itakuwa wananchi vs serikali
 
wao ndio wanataka kuiba kura za ccm.

Nina wasiwasi kuwa nia ya kubaki vituoni ni kufanya fujo endapo watashindwa kwa namna yoyote ile.

Ni aibu sana kwa kiongozi kama lowassa kushauri kuwepo kwa mzingira ambayo yatahatarisha usalama kwa ajili yake binafsi



lowassa siyo wa thamani kuliko tanzania. Kuna mfumo wa kisheria wa kufuata endapo mtu hakuridhika na matokeo - sioni kwanini lowassa na matajiri wenzake ambao wanataka ikulu hata kwa damu ya watu wengine wanaogopa kufuata mfumo huu.



Tanzania kwanza, lowassa na maghufuli baadae!!!!!


Wewe ni mgeni Tanzania?
Kuna sehemu mahakama imetenda haki?
Tena kuhusu wapinzani kwenye maswala ya uchaguzi.
 
Acheni uhuni wenu.kila mtu akibaki kituoni itakuwa fujo.wewe huelewi nini!

acha upimbi wewe,hayo matokeo wanamtangazia nani? kupiga kura tutapiga na kulinda tutalinda kulingana na sheria ilivo wazi kwa umbali ulioelezewa...chagua Lowassa,chagua ukawa=Tanzania mpya
 
Vijana tusiwe kama Wajinga kutumiwa na wanasiasa vibaya.
Jiulize ukikaa hizo mita 200 utaweza kuona kinachoendelea ndani? Maana mita 200 ni viwanja viwili vya mpira.
Au mtakuwa na darubini?

Tutumie akili Vijana. Sisi bado hatujtimiza malengo yetu mengi kama hao tunaowapigania.

Ni mita mia moja, lakini kama sio ishu kusubiria matokeo mbona wamekomalia kuwa hakuna mtu kusubiria matokeo?, wewe ndiyo acha ujinga.
 
Unadhani wazazi wako wewe au wazazi wa wakati wanaotumiwa na Rais JK kuleta vurugu dhidi ya raia watakuwa wapi?

Ninyi inaonekana mna UCHUNGU sana na MBOWE NA LOWASSA Kuliko hata JOYCE MUKYA,REGINA NA FRED LOWASSA.Andamaneni MUIONE KAZI.Hivi watu wachache kama nyie mnatishia vyombo vya DOLA Kama nani??MARUFUKU KUBAKI VITUONI_AMRI
 
Back
Top Bottom