UKAWA mnafanya kosa la kiprotokali

UKAWA mnafanya kosa la kiprotokali

Umenena.UKAWA hawajui swala la ımani ya dıni ni zaidi ya mapenzi ya vyama.
 
Binafsi kama Mtanzania wa kawaida kabisa nilichukizwa sana na maneno aliyoyaporomosha Gwajima dhidi ya Karidinali Pengo Kimsingi tu hata kama kweli Pengo angekuwa na makosa hakistahili matusi ya namna ile wote tunajua Gwajima ni mdogo sana kwa Karidinali Pengo na kwa desturi ya Kitanzania mkubwa wako akikukosea kuna namna ya kumweleza na siyo kuporomosha matusi kama aliyoporomosha Gwajima

Sasa tumesikia Kauli ya Pengo akisema amemsamehe Gwajima. ni jambo la kiungwana kabisa kwa hadhi ya Pengo alichokifanya ndio kilitakiwa kufanywa na muungwana yeyote yule nina Imani atakuwa amemsamehe kiroho safi kabisa na ni matumaini yangu Gwajima naye atafanya hivyo pindi akipata nafuu Mungu amsaidie apone upesi

Kuhusu Viongozi wa UKAWA Slaa na Lipumba kumtembelea Gwajima sioni kama kuna tatizo kama watakuwa wameenda kumsalimia Gwajima kama Kiongozi wa dini na Mtanzania pia ila Shida itakuwepo iwapo wamefanya hivyo kwa ajili kumsapoti Gwajima sababu ya kumpromoshea maneno Pengo ambaye Kimsingi wanaona kama hayuko upande wao kama watakuwa na mtazamo huo wajue qamepotea ila kama wameenda kumsalimia bila kuchukua upande wowote basi mimi sioni tatizo

Labda ni kiswahili kina shida ila naomba kujua matusi hayo yakoje kwa lugha yetu kusema ni kama mtoto kafalishwa pepasy anapelekwa asiko jua anafanya asiyo jua ndiyo matusi yenyewe Pengo ameshindwa kujitambua yeye
Ninani na anacho tetea nini wakati Wa bunge la katiba jukwaa la Kikristo walisema maoni ya wananchi ya eshimiwe wakaunga mkono serekali tatu baada tamko lao Pengo akajitoza bila kuangalia anamtetea na anamwaribia nani kama mtoto akasema yeye anaunga mkono serekali mbili.
Juzi tena jukwaa lile lile wasema wanapiga kura ya hapana na kuwatangazia waumini wao wapige kura ya hapana Siku ileile madhabau na alutare zinatangazia waumini kupiga kura ya hapana ya katiba pendekezwa yeye akaibuka tena akasema wasilekese nini cha kufanya kama mtoto asiejua anacho fanya akasahau viongozi wa chama na serekali kila nafasi wanayopata wanashawishi watanzania ambao wengi wao hawajui mbele wala nyuma ya katiba kwamba wapige kura ya ndiyo hili hamlioni eti Gwajima ni mdogo mesahau watehawa in watumishi mkisahau mmoja akikosea antakiwa akemewe mbele za watu ili wengine waogope.
Paulo aliekuwa mdogo kiuduma na kiumri alimkaripia Petrol akikuwa kiongozi wa kanisa mbele watu na Petro akaona kosa lake akajirekebisha hakusema anamsamehe Bali akikuja kusifia mafundisho ya Paulo tuache kuichafua tiba aliotaoa mtumiahi wa MUNGU
 
Kwa hiyo siku hizi kujuliana hali ni makosa? Hakuna kitu kibaya kama kutanguliza mbele maslah zidi ya ubinadamu halafu pia ni kosa kulipiza baya kwa ubaya wacha apate aibu mwenyewe kingine kwa nn pengo asiwakemee viongoz wa serikal na wale wa ukawa kwa kuamuru watu wapige kura ya ndio au hapana? Unataka kutuambia wakatolik wanamaamuz makubwa ktk taifa hili kwa kuwa mpo wengi? Mbona hamjakemea maaskofu walio kula hela za escrow tena chafu kama tunataka taifa makini? Bas palipo na maslah pana mkatoliki.
 
Pengo ndie Mkuu wa Kanisa Katoliki kwa hapa Tanzania!. Anatokea mtu aliyekuwa Mkatoliki, akaasi na kuanzisha kijikanisa chake cha uchochoroni, kisha amtukane Mkuu wa Kanisa Katoliki, kisha anatokea memba mpya wa jf na kumsifu huyo mtukanaji kuwa ni shujaa!. Karibu jeiefu!.
Pasco

Pasco kwa hierachy gani Pengo ni mkuu wa kanisa katoliki Tanzania?

Nani anaripoti kwa Pengo zaidi ya Maaskofu na Mapadri wa Jimboni kwake Dar es Salaam?
Pasco usiwe mpotoshaji ...alafu unayo hii habit
 
Last edited by a moderator:
Mkuu usitufanye sisi ni watoto na hatujasikia kilichosemwa na Gwajima.

Ukawa wangejituliza vyumbani na kuacha jambo hili lipite kimya kimya.kumtembelea Gwajima ina maana mnakubaliana na yote aliyosema Gwajima kitu ambacho si sahihi.

Tusiwe wanafiki.
Wewe nae sijui unafikiri kwa kutumia nini,kumtembelea mgonjwa hospitalini ina maana kuwa unakubaliana na yote aliyoyasema??ndugu yako akikamatwa ugoni akajeruhiwa hutaenda kumsabahi hospital?na ukienda ina maana unakubaliana na ugoni?.Think big kijana
 
Ukiwa mueneza chuki kwa chadema wewe ni shujaa hilo liko wazi,we huoni viongozi wao wote watu wa jazba,hakuna naeongea bila jazba chadema.
 
Wewe nae sijui unafikiri kwa kutumia nini,kumtembelea mgonjwa hospitalini ina maana kuwa unakubaliana na yote aliyoyasema??ndugu yako akikamatwa ugoni akajeruhiwa hutaenda kumsabahi hospital?na ukienda ina maana unakubaliana na ugoni?.Think big kijana
Si makosa hata kidogo kujuliana hali.Lipumba au Slaa hajakatazwa kumjulia hali ila kwa wadhifa wao na hali ya mambo ilivyo haikuwa sahihi na haitakuwa sahihi kumjulia hali mtu aliyeropoka matusi hadharani tena dhidi ya kiongozi mkuu wa kanisa hapa nchini.

matamshi ya Gwajiba yameacha watu njia panda alikuwa na ujumbe lakini hakuufikisha kama kiongozi wa dhehebu la dini bali alitumia mistari utadhani Tupac Shakur dhidi ya BIG kwenye ule wimbo wa 'Hit em up'

Nikizungumzia makosa na madhara ya kiprotokali ninaweza kutoa mfano mmoja unaorandana kwa mbali kidogo.

mwaka 2000 waziri mkuu wa Israel Ariel Sharon punde baada ya kuchaguliwa alienda kuhuji katika eneo lijulikanalo kama Temple Mount au Msikiti wa Al Aqsa...msikiti ambao ni muhimu sana kwa waislamu wa kipalestina.

jambo hili lilileta mgogoro mkubwa(2nd Intifada) kati ya waisrael na wapelestina ...mgogoro ambao ulimalizika mwaka 2005.
Kwa wale msiolelewa maana ya kuzingatia protocal basi mnaweza kuona madhara ya mzaha mzaha wa kukiuka protocal.

Sisemi kitendo cha Slaa na Lipumba kinaweza leta vita la hasha bali nasisitiza kuwa viongozi ni lazima wajifikirie sana kabla ya kuamua na kutenda.
 
Hapo upo sawa hata mi mkatoliki sijafurahishwa na kitendo cha pengo kutukanwa n ukawa wajue wakatoliki ni wingi na wanasikiliza viongozi wao wa dini so wakifanya ujinga kwa hilo kweli watapoteza

unamaanisha lile tamko LA maaskofu haiku shirk misha wakatoliki? Kuna maaskofu wakatoliki wengi tu wasiokubaliana na upuuzi wa pengo.Hats Mimi ni mkatoliki lakini kwa hili LA pengo sitakubaliana naye na imani yangu kwake imepungua sana
 
Mkuu meningitis heshima yako..

Maandiko matakatifu yanatufinza kusamehe na si kusamehe tu bali yanatufunza kusahau pindi tunaposamehe. Umemsikia Mwadhama Pengo? Yeye mwenyewe kupitia kinywa chake kasema Amesamehe. Wich means yuko tayari akipata nafasi kumtembelea Gwajima Hospitali. Naam hivyo ndivyo tunavyohimizwa na bwana wetu Yesu Kristu. Hivi utajisikiaje pindi ukimuona Pengo kamtembelea Gwajima huko hospitali?

Halafu tambua hakuna ugomvi kati ya Gwajima na Pengo, Kanisa Catholic na Kanisa la Ufufuo na Uzima. Kilichopo ni sintofahamu iliyoibuka kati ya Gwajima na Pengo, katu si ugomvi. Hii inatokana naw kauli za wote wawili, Pengo akionekana kupingana na Tamko la Maaskofu wenzake ambao walikuwa wote wakati wa kuandaa tamko husika. Na wakati huohuo Gwajima kuonekana akitoa lugha zisizofaa kwa Askofu mwenzie. Na ndiomaana unaona licha kutukanwa huko Pengo hakuwahi kumshitako kokote Gwajima.

Kwahiyo Dr Slaa wala Lipumba hawawezi kufungwa na makosa ya Gwajima aliyomkosea Pengo. Kumkosea Pengo haina maana ya kulikosea Kanisa Catholic na waumini wake. Ikumbukwe licha ya makosa yaliyofanywa na Gwajima bado Gwajima anabaki ni mtu mkubwa ktk jamii yetu hii. Yeye anawaongoza maelfu ya waumini wake ambao katu hawahitaji kuona kiongozi wake akidhulika kwa lolote na kwakweli wanahitaji faraja ktk kipindi hiki.

Kama utakuwa umemchukia Gwajima kwa kile alichokisema kwa Pengo, ni wazi pia utakuwa umekwazika kwa Pengo kwanda kinyume na Tamko la Baraza la Wakristu hapa nchini na ni wazi pia kwamba utakuwa hujalichukia kanisa Catholic kwa makosa ya Pengo.

Tafakaru chukua hatua.

BACK TANGANYIKA
 
Last edited by a moderator:
Mimi sikuelewi. Ukawa na Pengo wapi na wapi? Wanaomtuhumu Pengo sio wanasiasa tu wa Ukawa. Hata CCM wapo na vibaraka wake. Binadamu wote wameguswa sawia na ni mchanganyiko wa mawazo. Nadhani una bifu na Ukawa.
 
Pasco kwa hierachy gani Pengo ni mkuu wa kanisa katoliki Tanzania?

Nani anaripoti kwa Pengo zaidi ya Maaskofu na Mapadri wa Jimboni kwake Dar es Salaam?
Pasco usiwe mpotoshaji ...alafu unayo hii habit
Kanisa Katoliki linaongozwa kwa majimbo, ambapo Jimbo Kuu la Dar es Salaam ndilo linaloongoza ikiwemo ku host Baraza La Maaskofu Katoliki pale Kurasini, na kiongozi mkuu wa Kanisa Katoliki ni Muadhama Polcarp Karninali Pengo, akisaidiwa na maaskofu wawili wasaidizi.

Hivi ndivyo mimi nijuavyo toka enzi za Muadhama Laurian, Kardinari Rugambwa ndio mkuu wa Kanisa akifuatiwa na Wahashamu Maaskofu wa majimbo mbalimbali.

Ni huyu pekee anayekwenda Rome kumchagua Papa na ndiye pekee mwenye daraja ya kuweza kuwa Papa.

Pasco.
 
Najitambulisha kama mkatoliki kindakindaki...na sio mara ya kwanza kufanya hivi.niliwahi kufanya hivi hapo awali na nilimtuhumu Askofu Pengo kwa tamko lake kuhusiana na mashambulizi dhidi ya mapadre wetu.inawezekana kipindi kile sikumuelewa Kadinali Pengo...nilikurupuka kumtuhumu kama alivyokurupuka Gwajima.

Nilimtuhumu kwa kupingana na msimamo wa wengi dhidi ya nani muhusika wa mashambulizi yale.nilimtuhumu kwa kutoelekeza wakatoliki tufanye nini dhidi ya ufirauni waliofanyiwa mapadre na waumini wa Kanisa katoliki,nilikasirika na kumuona ni msaliti na anasimama na serikali inayotuudhi!

Mambo yalivyoendelea nilijikuta naanza kuelewa zaidi kauli za kadinali Pengo na kuziona ni sahihi na zinazingatia ukweli au uchunguzi wa mambo.

Ndio maana kwa kauli hii ya juzi sikutaka kukurupuka.

Nimeanzisha thread zipatazo mbili kuhusu sakata na kauli ya hivi karibuni ya kadinali Pengo lengo ni kujua uhalisia na ukweli wa kile alichokisema Askofu Pengo..zote zimeishia kapuni.

madhumuni ya uzi huu ni kuwatahadharisha Ukawa juu ya kukurupuka!

Nawasihi na kuwatahadharisha Ukawa juu ya kumdharau Pengo kisa porojo na matusi ya Gwajima.

Nawatahadharisha Ukawa kutojifungamanisha na Gwajima mtu ambaye amewakosea adabu wakatoliki ...hakuna mkatoliki anayefurahishwa na matusi dhidi ya Kadinali Pengo na haitatokea kamwe hata kama angeshikwa ugoni!

Ukawa jihadharini sana!hapa ndipo mtakapopoteza!

Nawasilisha kwa uchungu!

Kardinal amesema ameshamsamehe sasa wewe mgonjwa wa mgongo usiopona unamaana gani tena kuleta porojo hizi!??? Mnafanikisha BVR kwa mgongo wa Gwajima??
 
Pengo ndie Mkuu wa Kanisa Katoliki kwa hapa Tanzania!. Anatokea mtu aliyekuwa Mkatoliki, akaasi na kuanzisha kijikanisa chake cha uchochoroni, kisha amtukane Mkuu wa Kanisa Katoliki, kisha anatokea memba mpya wa jf na kumsifu huyo mtukanaji kuwa ni shujaa!. Karibu jeiefu!.
Pasco

Mkuu Pasco with all due respect..!!!

Wewe ni mtu mkubwa sana hapa jamvini, najiaminisha kuwa pengine na Tanzania kwa ujumla hii ni kutokana na michango yako hapa jukwaani.

Lakini ktk uelewa wako wote, umeshindwa kujisumbua hata kidogo tu kumjua Mkuu wa Kanisa Catholic hapa Tanzania? Hapana wewe si yule ninayekufahamu aiseeee..!!! Umeandika kitu cha kitoto mno.

Ninahakika kama Pengo angekuwa Mkuu wa Kanisa Catholic hapa Tanzania (Siingilii maamuzi ya Mungu lkn naomba aepushie Mbali isipokuwa Mapenzi yake yatimie..!!) Basi lile Tamko la baraza la Wakristu hapa Tanzania lisingetoka..!!! Na kama lingetoka basi lisingekuwa ktk sura ile. Sitaki kukwambia ni kwanini.!!

BACK TANGANYIKA
 
Kanisa Katoliki linaongozwa kwa majimbo, ambapo Jimbo Kuu la Dar es Salaam ndilo linaloongoza ikiwemo ku host Baraza La Maaskofu Katoliki pale Kurasini, na kiongozi mkuu wa Kanisa Katoliki ni Muadhama Polcarp Karninali Pengo, akisaidiwa na maaskofu wawili wasaidizi.

Hivi ndivyo mimi nijuavyo toka enzi za Muadhama Laurian, Kardinari Rugambwa ndio mkuu wa Kanisa akifuatiwa na Wahashamu Maaskofu wa majimbo mbalimbali.

Ni huyu pekee anayekwenda Rome kumchagua Papa na ndiye pekee mwenye daraja ya kuweza kuwa Papa.

Pasco.

Kwenda kumchagua papa sio kigezo cha kuwa kiongozi wa kanisa Tanzania

Kanisa katoliki Tanzania liko chini ya TEC

Pengo ni askofu wa dar es salaam tu...hana mamlaka yoyote nje ya Dar es salaam

Kumbuka cheo cha kardinali sio kwamba ni ukuu katika nchi ...hapana...Afrika kuna nchi zina makadinali zaidi ya wawili mfano Nigeria na Ghana...na kuna nchi hakuna makadinali mfano Uganda.

Ukadinali ni daraja tu katika madaraja ya Upadri ....kuna Monsignor ......na mengineyo....

Hapa nchini Pengo anawajibika kiutawala kwa TEC.....Yeye ni askofu tu sawa na askofu wa Mbinga.

Acha hoja mfu....kwa hio kwa sababu makao makuu ya Jumuia ya Afrika Mashariki yako Arusha kwa hio Rais wa Tanzania ndiye Mkuu wa Marais wote wa Afrika Mashariki ? I believe you are better than this.
Pasco narudia tena....Umezoea kuwa mpotoshaji...acha upotoshaji...kama hujui Nyamaza...kaa kimya...pia ni busara
 
Last edited by a moderator:
Hapo upo sawa hata mi mkatoliki sijafurahishwa na kitendo cha pengo kutukanwa n ukawa wajue wakatoliki ni wingi na wanasikiliza viongozi wao wa dini so wakifanya ujinga kwa hilo kweli watapoteza

Pengo hajatukanwa na UKAWA wewe kilaza...
 
Acha uchonganishi wewe! Side wakatoliki tunapenda wema na upendo, ningekuelewa ungemuomba mhashamu amtembelee gwajima hospital na sio kutaka watu wasiende kumuona! Nawaomba wakatoliki wenzangu tumuombee afya njema gwajima, kazi ya kuhukumu watu sio yetu. Mungu halali anaona kila kitu. Amri kuu kuliko zote ni upendo, natamani kumsikia gwajima mahubiri yake punde tu akiwa na afya yake, long live gwajima. Tutetee kondoo wa bwana.

Umemaliza kila kitu. Kutokana na Imani na mafunzo yetu sisi wakatoliki, hata Pengo mwenyewe alipaswa kumtembmbelea Gwajima hospitalini.
 
Mnakuza mambo na kumuwekea maneno mdomoni mwa Mtu...
Wote tulimsikia Gwajima, akieleza kumuheshimu Ngalikumtwa.
Sasa huo ugomvi wa Catholic na Gwajima unatokea wapi??
Ngalikumtwa ni nani?

Mkuu hii thread yako imejaa hisia tu na hujaonyesha mashiko yoyote zaidi ya kutaka kutia hofu ambayo kimsingi haipo...

Pia akumbuke kwamba Gwajima alisema wazi kuwa kanisa katoliki ndio kanisa Mama la makanisa yote duniani, hivyo analikubali na kuliheshimu
 
Kanisa Katoliki linaongozwa kwa majimbo, ambapo Jimbo Kuu la Dar es Salaam ndilo linaloongoza ikiwemo ku host Baraza La Maaskofu Katoliki pale Kurasini, na kiongozi mkuu wa Kanisa Katoliki ni Muadhama Polcarp Karninali Pengo, akisaidiwa na maaskofu wawili wasaidizi.

Hivi ndivyo mimi nijuavyo toka enzi za Muadhama Laurian, Kardinari Rugambwa ndio mkuu wa Kanisa akifuatiwa na Wahashamu Maaskofu wa majimbo mbalimbali.

Ni huyu pekee anayekwenda Rome kumchagua Papa na ndiye pekee mwenye daraja ya kuweza kuwa Papa.

Pasco.

Pole sana mkuu Pasco, uelewa wako tangu utoto umekulemaza mno..!!!

Ni kweli kwamba Pengo anadaraja la kuwa Papa moja kwa moja ikiwa kura zitatosha, Pia ni kweli kwamba Pengo anamchagua Papa na nafasi yake hii automatically ndiyo inayompa nafasi ya yeye kuchaguliwa kuwa Papa. Ila nafasi zote hizo zinatokana na kuchaguliwa na Papa mwenyewe hii ikiwa sawa na kwa Askofu.

Lakini ukija kwenye msingi wa Kanisa Catholic, unakuta Kanisa linaongozwa na Majimbo ambayo kila jimbo linaaskofu wake ambaye ndiye mkuu wa Kanisa kwenye jimbo husika. Hii inamaana hata Pengo hana mamlaka yoyote kwenye jimbo letu la Sumbawanga zaidi ya heshima ya kawaida tu anayoipata kutokana na Nafasi yake kama Mkatoliki na kiongozi wa Kanisa hilo kwa jimbo la Dareslaam.

Jimbo la Dareslaa haliwezi kuwa kubwa au kuu kuliko majimbo mengine kutokana na kigezo eti lina host Maaskofu wengi ndani ya Baraza la Maaskofu (TEC) kuliko jimbo lolote hapa nchini, Kama kigezo hicho kingekuwa kweli basi haingukuwa na maana ya kufanya uchaguzi wa kiongozi waw Baraza la Maaskofu. Maana moja kwa moja kiongozi huyo angekuwa ni Mwadhama Kadinari wa jimbo hilo la Dareslaam.

Kwahiyo tunaona wazi kwamba Askofu wa Kanisa Katoliki, ni kiongozi mwenye mamlaka kwenye jimbo analoliongoza, Ukija kwa Askofu na Mkuu wa Kanisa Katoliki kwa hapa Tanzania ndipo unamkuta Mwenyekiti wa baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania. Huyu ndiye kwa hakika twaweza sema ndiye Kiongozi mkuu wa Kanisa Katoliki hapa nchini kwasababu, kwanza anachaguliwa na Maaskofu wenzake na pia chombo kinachomteua/mchagua ndicho chenye mamlaka na Maamuzi yoyote yahusuyo Kanisa Katoliki hapa nchini.

Sidhani kama haya yote ulikuwa huyajui mkuu wangu Pasco

Kwenu MTAZAMO, Otorong'ong'o

BACK TANGANYIKA
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom