UKAWA mnafanya kosa la kiprotokali

UKAWA mnafanya kosa la kiprotokali

Mkuu UKAWA wamesha poteza sifa za kuungwa mkono na wakatoliki walio wengi, kwa kiu yao ya kisiasa na kutafuta uungwaji mkono na yeyote yule, wapo tayari kumshabikia hata mwendawazimu na kumuona ni mmoja wao
Uwezo wako wa kufikiri hauna tofauti na wa Kibajaji. Hangereni kwa kumtawaza Pengo kuwa mUNGU wa wakatoliki Tanzania. Kwani yeye alivyopingana na maaskofu wengine hawezi poteza uungwaji mkono na watanzania?
 
Nyie ndo maboya kama mnajadili vipofu kwa nini mapadre wanasoma na kuhitimu vyuoni wakati mpo wa kujadili ukuu wa maria?
mkuu nikushauri kitu kimoja tu,mrudie BWANA MUNGU WAKO!!!coz yeye hana ubaguzi,hajikwezi,hajitengi na wazambi,ni Mungu wa wakosaji kama mimi,ambao machoni pa wateule kama nyinyi tunaonekana si mali kitu.WEWE SI TAYARI UMESHAMALIZA SAFARI YAKO YA KUUTAFUTA UTUKUFU WA MUNGU?TUACHIENI SISI AMBAO BADO TUNAKESHA USIKU NA MCHANA TUKIUPIGANIA UTUKUFU WAKE KWA SABABU HATUJUI SIKU WALA SAA....Mungu alimtuma mwanae mpendwa kwa ajili yetu sisi wakosefu na sio nyie watakatifu wa dunia hiii
 
Hapo upo sawa hata mi mkatoliki sijafurahishwa na kitendo cha pengo kutukanwa n ukawa wajue wakatoliki ni wingi na wanasikiliza viongozi wao wa dini so wakifanya ujinga kwa hilo kweli watapoteza

Stop misused ninyi vijana wa lumumba na chekaung'atwe.
 
Mnakuza mambo na kumuwekea maneno mdomoni mwa Mtu...
Wote tulimsikia Gwajima, akieleza kumuheshimu Ngalikumtwa.
Sasa huo ugomvi wa Catholic na Gwajima unatokea wapi??
Ngalikumtwa ni nani?

Mkuu hii thread yako imejaa hisia tu na hujaonyesha mashiko yoyote zaidi ya kutaka kutia hofu ambayo kimsingi haipo...

Kweli kabisa, hata Dr Slaa ni mkatoriki na alienda kumtembelea Gwajima. Dr Slaa ndiye mkatoriki safi maana kwenye ukristo hakuna kulipa baya kwa baya au laumu kwa laumu. Wanaomkosoa Dr Slaa kwa kwenda kumjulia hali Gwajima ni wakatoriki jina lakini sio moyoni. Yesu mwenyewe waliomtesa aliwasamehe hata Pengo kasamehe toka moyoni, sasa msamaha wake utakuwa batili kama atakuja kulipiza kwenye kura. Hakuna msamaha wa namna hiyo.
 
Ni afadhali ukiri kuwa hujui kitu, unadhani unaiponya nafsi yako kumbe unaiangamiza kabisa!!!! HUKUSOMA WEWE IMEANDIKWA "MTAKACHOKIFUNGIA DUNIANI NA MBINGUNI KIMEFUNGIWA"? Ni nini hiyo basi!!! Ya nini kubeba bango la ujinga katikati ya wajinga!!!! Mamlaka ya hukumu tunayo, hatuna mamlaka ya kuadhibu tu. (yaani kusema hili ni kosa mamlaka hayo tunayo 100%)
Unaweza kusamehewa manake wakatoliki mnasomewa biblia na padre, wenzenu wanaisoma wao wenyewe hata kama somo linasomwa kanisani nao wanafuatisha kwenye biblia zao. Sasa wewe umezoea kusomewa hiyo biblia na Pengo unawezaje kuonyeshwa mamlaka uliyonayo kama biblia inavyoonysha????!!!
Unawapigia mbuzi gitaa, wao kwao akisema Pengo ndo limefungwa Duniani si mtu mwingine, sijui amewaloga maana anatokea kwetu Sumbawanga huyu jamaa. Labda wanasubiri mtaguso sijui utakuwa wa saba!
 
Sijamdharau lakini siwezi kumpa kazi isiyo ya kwake, alikuwa binadamu kama wengine, huwezi kusema ni mama wa MUNGU na ukataka akuombee kwa MUNGU wakati hata yeye anatakiwa kuomba ya kwake.
kama Mungu mwenyewe alimwinua wakati Malaika anampelekea habari za ujauzito wa Yesu wewe ni nani hasa hata uhoji mimi kuliinua jina lake?wewe na Mungu nani zaidi.
 
mkuu nikushauri kitu kimoja tu,mrudie BWANA MUNGU WAKO!!!coz yeye hana ubaguzi,hajikwezi,hajitengi na wazambi,ni Mungu wa wakosaji kama mimi,ambao machoni pa wateule kama nyinyi tunaonekana si mali kitu.WEWE SI TAYARI UMESHAMALIZA SAFARI YAKO YA KUUTAFUTA UTUKUFU WA MUNGU?TUACHIENI SISI AMBAO BADO TUNAKESHA USIKU NA MCHANA TUKIUPIGANIA UTUKUFU WAKE KWA SABABU HATUJUI SIKU WALA SAA....Mungu alimtuma mwanae mpendwa kwa ajili yetu sisi wakosefu na sio nyie watakatifu wa dunia hiii
Now you are talking, kwa nini iwe kosa kwa watu kumtembelea "mdhambi" Gwajima? kama tunatakiwa kusameheana, kwa kuwa sisi si wakamilifu? huoni kwamba hawa ndo wanahubiri maisha ya YESU kisawasawa kuliko hawa wanaolaumu? Kwa mtazamo wangu ilikuwa bora kumuombea apone ili apate nafasi ya kutubu na kumrudia BWANA badala ya kumuombea mabaya ikiwemo kuwalaumu waliokwenda kumuona Hospital!
 
Jamani siasa ifanywe katika mambo ya siasa, kuhusianisha siasa na mambo ya imani ni unyambilisi.
 
Acheni michango ya kinafiki jamani, Mh. Komba kamtukana Warioba kuhusu hili hili suala la katiba na siku aliyokufa wanasiasa wote toka waupinzani mpaka wa chama tawala wamejazana. Mbona hamkumkataza mtu yoyote kwenda, ukiachia kwamba Pengo ni kiongozi wa dini hebu nipe tufauti yake kwa heshima kwenye nchi hii na Warioba. Kila mtu anajua Warioba aliwahi kuwa nani kwenye nchi hii achia mbali umri wake na Komba alivurumisha matusi bila mtu yoyote kujali. Hizi post zinaletwa na watu wa mlengo fulani wenye malengo fulani tena kutoka kile chama kichovu chenye kuishi kwa propaganda. Mnajifanya waromani nani kawateua kuwasema waromani? Acheni hizo nyie. Kwa hiyo kwakuwa Gwaijima kamkashifu Pengo basi asitembelewe na Ukawa lakini akifa ndio mnaenda na makamera msibani kutafut kura kwa wananchi.
True!
Huwezi kuwa mkristo kamili,huku unawaza kulipa kisasi eti kwa vile Dr Slaa kaenda kumjulia hali Gwajima. Biblia inatamka wazi kuwa 'wewe ni wa ibilisi. Wapendeni adui zenu. Usilipe baya kwa baya. Dr Slaa naye ni mkatoriki tena level ya upadiri, yeye kaonyesha ni jinsi gani mkatoriki anavyotakiwa kuwa. Hata Pengo asiishie kusamehe tu, amtembelee Gwajima hospitali, huo ndiyo Upendo. Mungu ni Pendo.
 
Mkuu UKAWA wamesha poteza sifa za kuungwa mkono na wakatoliki walio wengi, kwa kiu yao ya kisiasa na kutafuta uungwaji mkono na yeyote yule, wapo tayari kumshabikia hata mwendawazimu na kumuona ni mmoja wao

uongo utakusaidia nini ? nani mkweli kati ya pengo na waraka wa maaskofu ? kwanini pengo asiombe radhi hadharani kwa kauli yake ? au aufute ule waraka wa maaskofu basi , nakuhakikishia kwamba sisi wananchi tutampinga na kumkataa mtu yoyote yule bila kujali cheo wala wadhifa wake , hii katiba iliyoandaliwa na chenge haikubaliki hata na shetani , itakuwa ajabu sana kwa watu werevu kulifumbia macho jambo hili , pengo ni binadamu wa kawaida tu mwenye mama na baba na wajomba na mashangazi kama wewe tu , amekosea kwa makusudi ni lazima akemewe .
 
Uwezo wako wa kufikiri hauna tofauti na wa Kibajaji. Hangereni kwa kumtawaza Pengo kuwa mUNGU wa wakatoliki Tanzania. Kwani yeye alivyopingana na maaskofu wengine hawezi poteza uungwaji mkono na watanzania?

Nilikuwa sijajua uwezo wako wa kufikiri, Nimesoma quote yako hapo chini nikaona kwamba hauna tofauti na Gwajima
 
Najitambulisha kama mkatoliki kindakindaki...na sio mara ya kwanza kufanya hivi.niliwahi kufanya hivi hapo awali na nilimtuhumu Askofu Pengo kwa tamko lake kuhusiana na mashambulizi dhidi ya mapadre wetu.inawezekana kipindi kile sikumuelewa Kadinali Pengo...nilikurupuka kumtuhumu kama alivyokurupuka Gwajima.

Nilimtuhumu kwa kupingana na msimamo wa wengi dhidi ya nani muhusika wa mashambulizi yale.nilimtuhumu kwa kutoelekeza wakatoliki tufanye nini dhidi ya ufirauni waliofanyiwa mapadre na waumini wa Kanisa katoliki,nilikasirika na kumuona ni msaliti na anasimama na serikali inayotuudhi!

Mambo yalivyoendelea nilijikuta naanza kuelewa zaidi kauli za kadinali Pengo na kuziona ni sahihi na zinazingatia ukweli au uchunguzi wa mambo.

Ndio maana kwa kauli hii ya juzi sikutaka kukurupuka.

Nimeanzisha thread zipatazo mbili kuhusu sakata na kauli ya hivi karibuni ya kadinali Pengo lengo ni kujua uhalisia na ukweli wa kile alichokisema Askofu Pengo..zote zimeishia kapuni.

madhumuni ya uzi huu ni kuwatahadharisha Ukawa juu ya kukurupuka!

Nawasihi na kuwatahadharisha Ukawa juu ya kumdharau Pengo kisa porojo na matusi ya Gwajima.

Nawatahadharisha Ukawa kutojifungamanisha na Gwajima mtu ambaye amewakosea adabu wakatoliki ...hakuna mkatoliki anayefurahishwa na matusi dhidi ya Kadinali Pengo na haitatokea kamwe hata kama angeshikwa ugoni!

Ukawa jihadharini sana!hapa ndipo mtakapopoteza!

Nawasilisha kwa uchungu!
Kwanza wewe sio mkatoliki unataka kujenga chuki kati ya wakatoliki na Gwajima, haitakaa iwe.
Hakuna wakatoliki waliolalamikia maneno ya Gwajima, bali walishangazwa na maneno ya Cardinali Pengo ya kuwageuka maaskofi wenzake.
Kumbuka baraza la maaskofu ni ya Pengo peke yake, Mmoja hawezi kudhalilisha wengi akashinda.
Pengo aliamua kujitenga na atabeba mzigo wake mwenyewe.
Article yako haina maana yoyote zaidi ya kutaka kutengeneza devide and rule kati ya wakristo.
Hizo mbinu za magamba watu wako makini nazo.
Sahau hizo habari za uongo na uzushi, tafuteni kazi nyingine za kufanya.
 
Kwanza wewe sio mkatoliki unataka kujenga chuki kati ya wakatoliki na Gwajima, haitakaa iwe.
Hakuna wakatoliki waliolalamikia maneno ya Gwajima, bali walishangazwa na maneno ya Cardinali Pengo ya kuwageuka maaskofi wenzake.
Kumbuka baraza la maaskofu ni ya Pengo peke yake, Mmoja hawezi kudhalilisha wengi akashinda.
Pengo aliamua kujitenga na atabeba mzigo wake mwenyewe.
Article yako haina maana yoyote zaidi ya kutaka kutengeneza devide and rule kati ya wakristo.
Hizo mbinu za magamba watu wako makini nazo.
Sahau hizo habari za uongo na uzushi, tafuteni kazi nyingine za kufanya.

Naona unaleta ucheshi!Fuatilia threads zangu ndio utajua mimi ni gamba au la!
Wanapochemka ni lazima tuwaweke sawa kwani huu muda sio wa makosa ya kizembe.
 
uongo utakusaidia nini ? nani mkweli kati ya pengo na waraka wa maaskofu ? kwanini pengo asiombe radhi hadharani kwa kauli yake ? au aufute ule waraka wa maaskofu basi , nakuhakikishia kwamba sisi wananchi tutampinga na kumkataa mtu yoyote yule bila kujali cheo wala wadhifa wake , hii katiba iliyoandaliwa na chenge haikubaliki hata na shetani , itakuwa ajabu sana kwa watu werevu kulifumbia macho jambo hili , pengo ni binadamu wa kawaida tu mwenye mama na baba na wajomba na mashangazi kama wewe tu , amekosea kwa makusudi ni lazima akemewe .
Mkuu uongo ni upi? kushauri waumini waamue kwa utashi na maslahi yao? ujui kuwa ni vigumu na sirahisi kuwaamulia,kuwapangia na hata kuwaamuru wakatoliki?
 
Bahati mbaya umekurupuka tena......utakuja kutuomba msamaha tena wiki ijayo
 
wewe ndio ziro kabisa!!!!nani aliyekwambia kuwa wakatoliki huwa tunasomewa biblia kanisani,kwenye jumuia ndogo ndogo unafikiri huwa tunaenda kuuza sura?tatizo lenu mnajiaminisha kuwa nyie ndio mnajua zaidi ya wengine na hao wanaowafanya mazezeta ndio wanawasomea hiyo biblia nyie kazi yenu ni kusema ndiooooo au aleluyaaaaa au ameeeen upuuzi mtupu!ndio maana mnamwamini gwajima kuliko mnavyomwamini Mungu wenu coz kila akipata nafasi anawasomea mistari yenye feva kwa upande wake ili mumtegee yeye kuishi!!!ndio maana hata akifanya makosa mnamtetea coz mmeaminishwa hawezi kosea.ulivyo boya unataka kutumia biblia kuhalalisha huo uppuzi wako,KWA HIYO UKIPIGA KURA YA NDIO NA MAASKOFU WAMEKUAMRISHA UPIGE KURA YA HAPANA BASI WANAKUFUNGIA KABISA MLANGO WA KWENDA MBINGUNI SIO?wewe si unajua BIBLIA sana hebu nitajie huo mstari unakupa mamlaka ya kuhukumu na sio kutoa adhabu(siamini hata kama unajua ni nini umesema hapo).hiyo ya kusoma kufuatilizia wakati mchungaji wako anasoma biblia na baada ya kumaliza anaanza kukufafanulia atakavyo na wewe husemi neno ndio unajisifia?sisi kila siku ya jumuia tunasoma neno kutoka katika vitabu vya Injili(either Mathayo/Yahana/Marko/Luka) na tunashirikishana kila mmoja kwa jinsi anavyoelewa sio wewe unabeba Biblia jpili unafika pale kawe unasubiri gwajima akuambie fungua mstari fulani anasoma yeye we unafuatisha kwa kidole then anaanza kukufafanulia atakavyo hapa Biblia inasema usalipo usipige kelele ye anaongezea hapa walikuwa wanaongelea kama unasali chumbani kwako ndio usipige kelele lakini ukiwa barabarani we payuka uwezavyo na we kweli unaamini eti kisa umeaminishwa huyo ni mpakwa mafuta wa bwana basi anaijua biblia kuliko wewe!!!!!mko breinwoshid hadi mnajiona nyie tu ndio wateule wa Mungu wengine hawafai,HOVYOOOO

Ukristo wako una mashaka, umeshusha verse za lungha ya hovyo kuwahi kutamkwa na mtu ajiitaye mkristo, kwanza punguza jazba, halafu nakuomba sana ufungue biblia takatifu kitabu cha kutoka (exodus) 20:1-17 halafu ujipime kama haufanyi ibada ya sanamu, mimi nimesoma imeandikwa "atakaye kuiponya nafsi yake ataiangamiza, bali atakaye kuiangamiza ataiokoa" je bado wataka kukaa viti vya mbele kwenye karamu??

Ukatoliki ama uprotestant wako ni upuuzi mbele ya Bwana wa majeshi, Ni heri kuomba sana maana hilo ndio fungu jema.
 
wapi wanaonyesha ndio mkuu wa kanisa katoliki Tanzania au wewe tu kwa mamlaka yako umempa hiko cheo.nifafanulie plz hivi katika ngazi za kiutumishi kwa kanisa katoliki askofu anakuwa juu/chini ya Kadinali?kwa mfano plisi sijui kuna konstebo-sijui sajenti-sijui meja au sajenti nani sijui then.......na kwa upande wa kanisa katoliki inakuwaje?nijuavyo,kwa Tanzania kama linatokea tukio huko Vatican kama uchaguzi wa Papa huwa naona anaenda Pengo na sio mwingine,inakuwaje aende aliye mdogo kimamlaka kwa nchi?

Kama huelewi ni bora ukaenda kanisani ukaelezwa sio kupanic, cadinal ni daraja tu la kiaskofu, na si kwamba yeye ndie mkuu wa kanisa katolic tanzania, yupo Askofu ambae ndiye mkuu wa kanisa na ndiye mwenyekiti wa TEC, Pengo yeye ni askofu mkuu wa jimbo la Dar, tafadhali sana tafuta majibu kanisani kwa sasa ni hayo tu, na ni kweli Macadinal ndiyo wanamchagua Papa lakini sio kwamba wao ndio wakuu wa maaskofu nchini kwao, hata Pengo askofu wake kiongozi ni huyo niliyomtaja hapo juu, ndio mwenye kusign tamko la TEC sio Pengo. nipo tayari kusahihishwa kwani haba Duniani kila siku tunajifunza.
 
Najitambulisha kama mkatoliki kindakindaki...na sio mara ya kwanza kufanya hivi.niliwahi kufanya hivi hapo awali na nilimtuhumu Askofu Pengo kwa tamko lake kuhusiana na mashambulizi dhidi ya mapadre wetu.inawezekana kipindi kile sikumuelewa Kadinali Pengo...nilikurupuka kumtuhumu kama alivyokurupuka Gwajima.

Nilimtuhumu kwa kupingana na msimamo wa wengi dhidi ya nani muhusika wa mashambulizi yale.nilimtuhumu kwa kutoelekeza wakatoliki tufanye nini dhidi ya ufirauni waliofanyiwa mapadre na waumini wa Kanisa katoliki,nilikasirika na kumuona ni msaliti na anasimama na serikali inayotuudhi!

Mambo yalivyoendelea nilijikuta naanza kuelewa zaidi kauli za kadinali Pengo na kuziona ni sahihi na zinazingatia ukweli au uchunguzi wa mambo.

Ndio maana kwa kauli hii ya juzi sikutaka kukurupuka.

Nimeanzisha thread zipatazo mbili kuhusu sakata na kauli ya hivi karibuni ya kadinali Pengo lengo ni kujua uhalisia na ukweli wa kile alichokisema Askofu Pengo..zote zimeishia kapuni.

madhumuni ya uzi huu ni kuwatahadharisha Ukawa juu ya kukurupuka!

Nawasihi na kuwatahadharisha Ukawa juu ya kumdharau Pengo kisa porojo na matusi ya Gwajima.

Nawatahadharisha Ukawa kutojifungamanisha na Gwajima mtu ambaye amewakosea adabu wakatoliki ...hakuna mkatoliki anayefurahishwa na matusi dhidi ya Kadinali Pengo na haitatokea kamwe hata kama angeshikwa ugoni!

Ukawa jihadharini sana!hapa ndipo mtakapopoteza!

Nawasilisha kwa uchungu!


Haya mamlaka ya uwakilishi na kimaadili ya kuwasemea wakatoliki wote unayapata wapi??!!!!!!!;
wacha tabia ya kujikweza kiongozi!!! Kardinali Pengo alifanya makosa makubwa kukiuka dhana ya uwajibikaji wa pamoja na alistahili kukemewa kwa kosa hilo JAPO pia namshutumu Askofu Gwajima kwa kutumia lugha isiyo ya kistaarabu kufikisha ujumbe wake kwa Pengo; sio mfano wa kuigwa katu; Jamiii haimtegemei kiongozi wa kiroho kufanya aliyoyafanya Askofu gwajima. lakini kwa vyovyiote vile ujumbe umlifika kwa Cardinali Pengo kwamba kauli zake pia haziungwi mkono na kila mkatoliki, kila mkristo na kila mwananchi. Given a chance ningemshauri cardinali Pengo aliombe taifa msamaha kwa kuliingiza katika tashtiti na mashaka yasiyokuwa ya lazima
 
Mkuu usitufanye sisi ni watoto na hatujasikia kilichosemwa na Gwajima.

Ukawa wangejituliza vyumbani na kuacha jambo hili lipite kimya kimya.kumtembelea Gwajima ina maana mnakubaliana na yote aliyosema Gwajima kitu ambacho si sahihi.

Tusiwe wanafiki.

Mkuu,
Kwani UKAWA kukubaliana na Gwajima juu ya kuunga Mkono Maamuzi ya baraza la Maaskofu na Kwenda kinyume na Pengo kuna tatizo gani.
Mimi naona UKAWA wamekuwa Neutral katika hili,wangelaani Tamko la Gwajima wangeonakana na wao wanaenda Kinyume na Maazimio ya Baraza la Maaskofu,bifu na wa Kristo.
Pia Mkuu,Mpaka sasa haiko Clera,Gwajima amefanywa nini na Polisi Mpaka kufikia hali ile.
Tuwache kukuza mambo
 
Pengo Alitangaza Kumsamehe Bule Gwajima Na Maana Ya Kumsahe Mtu Ni Kuondoa Kinyongo Kabisa, Na Ingependeza Hata Pengo Angeenda Kumjulia Hali Gwajima, Sasa Nashangaa Kuna Watu Mnajiita Wakatolik Mmejaa Chuki Maneno Ya Kashfa, Mpaka Wengeni Mnaombea Gwajima Afe, Hivi Nyinyi Mnasoma Biblia Gani, Inayoluhusu Hasira Kukaa Vifuani Mwenu? Maana Maandiko Yanasema Hasila Hukaa Kifuani Mwa Mpumbavu, Ndio Maana Pengo Kwa Kiliona Hilo Akatangaza Msamaha.
 
Back
Top Bottom