UKAWA mnafanya kosa la kiprotokali

UKAWA mnafanya kosa la kiprotokali

Gwajima kweli ni shujaa, mpiganaji, msemakweli bila kuogopa, bora ukamuacha kuliko kumchokoza binafsi nampenda na ni mfano wa kuigwa swala la kutumia maneno ambayo hata muhusika hayamuumi. It's shame kabisa.
Maneno yanayoudhi na kuuma si lazima yawe matusi.
 
Binafsi kama Mtanzania wa kawaida kabisa nilichukizwa sana na maneno aliyoyaporomosha Gwajima dhidi ya Karidinali Pengo Kimsingi tu hata kama kweli Pengo angekuwa na makosa hakistahili matusi ya namna ile wote tunajua Gwajima ni mdogo sana kwa Karidinali Pengo na kwa desturi ya Kitanzania mkubwa wako akikukosea kuna namna ya kumweleza na siyo kuporomosha matusi kama aliyoporomosha Gwajima

Sasa tumesikia Kauli ya Pengo akisema amemsamehe Gwajima. ni jambo la kiungwana kabisa kwa hadhi ya Pengo alichokifanya ndio kilitakiwa kufanywa na muungwana yeyote yule nina Imani atakuwa amemsamehe kiroho safi kabisa na ni matumaini yangu Gwajima naye atafanya hivyo pindi akipata nafuu Mungu amsaidie apone upesi

Kuhusu Viongozi wa UKAWA Slaa na Lipumba kumtembelea Gwajima sioni kama kuna tatizo kama watakuwa wameenda kumsalimia Gwajima kama Kiongozi wa dini na Mtanzania pia ila Shida itakuwepo iwapo wamefanya hivyo kwa ajili kumsapoti Gwajima sababu ya kumpromoshea maneno Pengo ambaye Kimsingi wanaona kama hayuko upande wao kama watakuwa na mtazamo huo wajue qamepotea ila kama wameenda kumsalimia bila kuchukua upande wowote basi mimi sioni tatizo
 
Mkuu usitufanye sisi ni watoto na hatujasikia kilichosemwa na Gwajima.

Ukawa wangejituliza vyumbani na kuacha jambo hili lipite kimya kimya.kumtembelea Gwajima ina maana mnakubaliana na yote aliyosema Gwajima kitu ambacho si sahihi.

Tusiwe wanafiki.
Acha uchonganishi wewe! Side wakatoliki tunapenda wema na upendo, ningekuelewa ungemuomba mhashamu amtembelee gwajima hospital na sio kutaka watu wasiende kumuona! Nawaomba wakatoliki wenzangu tumuombee afya njema gwajima, kazi ya kuhukumu watu sio yetu. Mungu halali anaona kila kitu. Amri kuu kuliko zote ni upendo, natamani kumsikia gwajima mahubiri yake punde tu akiwa na afya yake, long live gwajima. Tutetee kondoo wa bwana.
 
kwenda kumtembelea mgonjwa sio kosa ,mimi sio mkatoliki alikuwa anapeleka ujumbe ila maneno aliyotumia hayakuwa na stahasana

Alitaka kufikisha ujumbe..hilo ni sawa lakini matusi si sawa...Kilaini hatujamtukana katika issue ya escrow lakini ujumbe ulifika.
 
Acha uchonganishi wewe! Side wakatoliki tunapenda wema na upendo, ningekuelewa ungemuomba mhashamu amtembelee gwajima hospital na sio kutaka watu wasiende kumuona! Nawaomba wakatoliki wenzangu tumuombee afya njema gwajima, kazi ya kuhukumu watu sio yetu. Mungu halali anaona kila kitu. Amri kuu kuliko zote ni upendo, natamani kumsikia gwajima mahubiri yake punde tu akiwa na afya yake, long live gwajima. Tutetee kondoo wa bwana.

Pengo kamsamehe lakini hajafika hospitali!
 
Mtamile;

Kosa sio kwenda kumsabahi...kosa ni la kiprotokali zaidi...naamini unanielewa.
 
Last edited by a moderator:
Gwajima kweli ni shujaa, mpiganaji, msemakweli bila kuogopa, bora ukamuacha kuliko kumchokoza binafsi nampenda na ni mfano wa kuigwa swala la kutumia maneno ambayo hata muhusika hayamuumi. It's shame kabisa.

Kama siyo muoga ni nini kilichompeleka mpaka ICU. Tafuta ile video yake halafu usikilize ile audio clip ndiyo utajua kama jamaa ni muoga au siyo muoga.
 
Mimi mkatoliki nimefurahishwa na maneno ya gwajima mkatoliki pia
 
Mambo yalivyoendelea nilijikuta naanza kuelewa zaidi kauli za kadinali Pengo na kuziona ni sahihi na zinazingatia ukweli wa mambo.

Ndio maana kwa kauli hii ya juzi sikutaka kukurupuka.

Nimeanzisha thread zipatazo mbili kuhusu sakata na kauli ya hivi karibuni ya kadinali Pengo lengo ni kujua uhalisia na ukweli wa kile alichokisema Askofu Pengo..zote zimeishia kapuni.

madhumuni ya uzi huu ni kuwatahadharisha Ukawa kukurupuka!

Nawasihi na kuwatahadharisha Ukawa juu ya kumdharau Pengo kisa porojo na matusi ya Gwajima.

Nawatahadharisha Ukawa kutojifungamanisha na Gwajima mtu ambaye amewakosea adabu wakatoliki ...hakuna mkatoliki anayefurahishwa na matusi dhidi ya Kadinali Pengo na haitatokea kamwe hata kama angeshikwa ugoni!

Ukawa jihadharini sana!hapa ndipo mtakapopoteza!

Nawasilisha kwa uchungu!

Mods msifute...!!

1. Hapa uansema umezisikia kauli zakee.

2. Unasema hujazisikia wewe vipi? umekuwa mshumaa au sigara kali? au wewe ni ....

3. hakuna Mkatoliki mwenye akili atakaye vumilia udhalilishaji aliofanya Pengo, pengo yeye nani mpaka ajione yupo juu hata ya Mkuu w kanisa hilo Tanzania ambaye alishiriki kikao na kutoka na maamuzi hayo ?
 
kwenda kumtembelea mgonjwa sio kosa ,mimi sio mkatoliki alikuwa anapeleka ujumbe ila maneno aliyotumia hayakuwa na stahasana

Mkuu wewe kama si mkatoliki basi hujui ni kwa nini wewe si mkatoliki, kwa kifupi waprotestant waliupinga ukatoliki miongoni mwa sababu kuu ni waumini kuzuiwa kusoma bibli, walipaswa/wanapaswa kumsikiliza padre na wao kusoma misale.

Kwa wale wanaosoma biblia watakubaliana nami kuwa Yesu alisema "mkinionea haya nami nitawaonea haya kwenye ufalme wangu"

Maneno ya Pengo kwa waumini wake hayakuwa na mustakabali mwema kiroho (ametafsirika kiroho kuwafanyia biashara wakatoliki kwa ccm)

Yesu alipinduapindua meza za wafanyabiasha na kuyatimuatimua mabanda ya njiwa alipowakuta wanafanya biashara hekaluni (kitendo kinamuhusu Pengo)

Kwa maana ya kutokumuonea aibu Yesu, yale maneno sahihi aliyoyatamka Gwajima kumlenga Pengo yalipaswa kuambatana na hatua kali zaidi ikiwa ni pamoja na kumuita shaurini mbele ya baraza la jumuia ya maaskofu (kama ipo)

Yesu haonewi aibu inapokuja swala la kuchunga kondoo zake.
 
kiukweli dhambi ya umafiki kwa viongozi wa dini itatufikisha pabaya sana hebu mjiulize maswali mlisha wahi kuona nyerere anafungua au anazindua kanisa au msikiti unafikiri alikuwa hapendi? alijua matatizo kama haya yangetokea tu.lkn siku je?
 
1. Hapa uansema umezisikia kauli zakee.

2. Unasema hujazisikia wewe vipi? umekuwa mshumaa au sigara kali? au wewe ni ....

3. hakuna Mkatoliki mwenye akili atakaye vumilia udhalilishaji aliofanya Pengo, pengo yeye nani mpaka ajione yupo juu hata ya Mkuu w kanisa hilo Tanzania ambaye alishiriki kikao na kutoka na maamuzi hayo ?
Mkuu heshima sana!
Pengo aliwahi kutoa kauli juu ya mashambulizi ya mapadre na kanisa..na alisema hayahusiani na udini.

Kauli hii ilituchefua wengi kwani tuliamini ni waislamu wanatushambulia...pengo aliitaka serikali kuchunguza zaidi na baadae tuliona mashambulizi hadi kwenye mikutano ya siasa.

Kauli ya juzi inayosemekana ni ya Pengo ati anakubaliana na mahakama ya kadhi haina kichwa wala miguu..haina chanzo kinachoeleweka na haikuwa na audio au video clip lakini tukakumbwa na ushabiki kama Gwajima!

My take...hakuna uthibitisho wa Pengo kupingana na maaskofu au tuseme Pengo kuikubali katiba mpya au mahakama ya kadhi.

Kilichothibitishwa mpaka sasa ni matusi na kejeli dhidi ya Kadinali ambaye anaweza kutawazwa kuwa PaPa au niseme alishiriki kumteua PaPa(sio kitu kidogo kama wengi tubavyokichukulia)
 
Dr Slaa na Lipumba wameshauriwa vibaya! Gwajima hakustahili sabahi kutoka kwao.

Kwa hiyo tatizo hapa ni Lipumba na Slaa kwenda kumjulia hali mgonjwa? Mbona aliyesemwa mwenyewe ameshasema kuwa amesamehe! Inakuwaje sasa suala hili ligeuzwe na kufanywa ni la Gwajima na RC?

Imeandikwa "Msihukumu wengine, ili nanyi msije mkahukumiwa, kwa maana jinsi mnavyowahukumu wengine, hivyo ndivyo nanyi pia mtakavyohukumiwa"
 
kiukweli dhambi ya umafiki kwa viongozi wa dini itatufikisha pabaya sana hebu mjiulize maswali mlisha wahi kuona nyerere anafungua au anazindua kanisa au msikiti unafikiri alikuwa hapendi? alijua matatizo kama haya yangetokea tu.lkn siku je?

Nyerere alikuwa mkatoliki safi lakini alizingatia protokali
 
Hawa Chadema na Cuf kwa style hii watakosa kura kwa wakatoliki kabisaa,hii njia wanayotumia itawapeleka pabaya hawaoni Ccm wamekauka kimya coz wanajua implication zake kwa jamii
 
Hawa Chadema na Cuf kwa style hii watakosa kura kwa wakatoliki kabisaa,hii njia wanayotumia itawapeleka pabaya hawaoni Ccm wamekauka kimya coz wanajua implication zake kwa jamii

Mkuu umenielewa vyema sana!
 
Hawa Chadema na Cuf kwa style hii watakosa kura kwa wakatoliki kabisaa,hii njia wanayotumia itawapeleka pabaya hawaoni Ccm wamekauka kimya coz wanajua implication zake kwa jamii

Hata waislamu,leo UKAWA wakiulizwa msimamo wao juu ya mahakama ya kadhi watapishana majibu lazima.
 
Back
Top Bottom