UKATA: Biashara ya maji ya kunywa yaanza kudoda

UKATA: Biashara ya maji ya kunywa yaanza kudoda

Wakuu , hii mnaweza kuiona kama Masihara vile , lakini uchunguzi nilioufanya jijini DSM , Jiji linaloaminika kuongoza kwa unywaji wa maji ya chupa ( maji safi ) , unaonyesha kwamba biashara ya maji imeanza kudoda kwa kasi ya kutisha !

Kwanza kwa kipindi cha mwaka mzima maji hayo hayajawahi kuadimika sokoni kama miaka ya nyuma , hali ni mbaya kiasi cha kusababisha magari ya makampuni karibu yote yanayotengeneza maji kupishana na kushinda mitaani yakisaka wateja , mithili ya Wanasiasa wanaoomba kura za ubunge majimboni .

Si kwamba watu hawanywi maji , la hasha ! Ugunduzi wangu umebaini kwamba watu wengi wanabeba maji ya Dawasco yaliyochemshwa ili kupunguza gharama , Hakika hali ni mbaya mno !

Ushauri wangu ni kwamba , maendeleo ya viwanda yaendane na vipato vya wananchi , viwanda vya maji vikifungwa kwa kukosa soko tutapoteza sana chanzo cha ajira ya vijana wengi mno .
Hii ilikua kwa ajili ya mvua, ila zikiisha biashara itarud pale pale kwenye peak.

Wabongo sio kwamba tunapenda kununua maji ya dukani, ila kwa kuwa maji ya bomba maeneo mengi yana chumvi sana, unakunywa km unameza dawa, so, mtu anaamua anunue tu ya dukani.

Kitonga muhimu mkuu.
 
Kuna kila dalili , enzi ya kutembea na viporo imekaribia , hali ni mbaya sana
Mara ngapi mkuu. Kuna jamaa nafanya naye kazi. Yeye huja na kiporo cha ubwabwa. Anakunywa chai kavu ya ofisi saa 4 (asbh anakunywa nyumbani) [emoji56][emoji56][emoji56]. Kiporo anapasha kwenye microwave lunch.
 
Huo utafiti umeufanyia ukiwa dar kweli? hujaona mvua zilizonyesha wiki 2 mfululizo ikiambatana na baridi kama ni chanzo?

au umekaririshwa tu neno ukata na wewe unaenda nalo hivyo hivyo?
 
MAMBO KUMI ( 10 ) WATU WALIYOJIFUNZA KIPINDI HIKI CHA MAGUFULI
1 ) Kumbe unaweza kushinda njaa bila kufa
2 )Kumbe unaweza kubeba chakula na kwenda nacho kazini.
3 )Bila bodaboda, Bila bajaji kumbe unaweza kutembea na ukafika Kazini.
4 )Tafadhali nipigie kumbe ni huduma ya msingi.
5 )Nyama ni mbaya kwa Afya yako.
6 )Jiko la mkaa kumbe linapika chakula kizuri sana.
7 )Ukisaga Mahindi yasiyokobolewa kumbe yanatoa unga safii.
8 )Maji ya kuchemsha kumbe ni matamu sana.
9 )Ugali pia kumbe ni breakfast. (kifungua kinywa).
10 )Ukioga na sabuni ya Kipande, kumbe bado unaKuwa msafi.
Umemaliza. Hapa nilikuwa nawaza kununua lunch box.......nakutana na uchambuzi huu murua kabisa
 
MAMBO KUMI ( 10 ) WATU WALIYOJIFUNZA KIPINDI HIKI CHA MAGUFULI
1 ) Kumbe unaweza kushinda njaa bila kufa
2 )Kumbe unaweza kubeba chakula na kwenda nacho kazini.
3 )Bila bodaboda, Bila bajaji kumbe unaweza kutembea na ukafika Kazini.
4 )Tafadhali nipigie kumbe ni huduma ya msingi.
5 )Nyama ni mbaya kwa Afya yako.
6 )Jiko la mkaa kumbe linapika chakula kizuri sana.
7 )Ukisaga Mahindi yasiyokobolewa kumbe yanatoa unga safii.
8 )Maji ya kuchemsha kumbe ni matamu sana.
9 )Ugali pia kumbe ni breakfast. (kifungua kinywa).
10 )Ukioga na sabuni ya Kipande, kumbe bado unaKuwa msafi.
unaambiwa hayo ndo maisha halisi tuliyotakiwa kuishi,sio maisha fake ya awamu iliyopita
 
Sio kweli mkuu, utafiti wako upo upande sana. Mi nauza vinywaji baridi hapa dar. Kutozunguka kwa biashara ya maji kunachangiwa kwa kiasi kikubwa na mvua, kwani joto hupungua na hivyo watumiaji wa kinywaji kama maji hushuka matumizi na hii ni kila kipindi cha msimu wa mvua. Wengi wanaulizia maziwa ya moto pindi wanapofika kwenye cafe yoyote au kioski. Tuacheni ushabiki.
Nimefanya utafiti huu kwa zaidi ya miezi mitatu , mvua imenyesha wiki 2 tu .
 
Na biashara ya bodaboda wale waliozoea kupanda hata sehemu fupi kwa sasa wanatumia tz 11 yaani miguu kusave badget hakuna ubishow tena kwa sasa!!!!.
Siku moja nimekodi boda boda yule dereva akasema Alhamdulirahi! Sikuamini kuwa hata dereva wa boda boda kupata abiria imekuwa ni shida kiasi hicho...
 
Nimefanya utafiti huu kwa zaidi ya miezi mitatu , mvua imenyesha wiki 2 tu .
Hahahaha [emoji1] [emoji1] [emoji1] [emoji1] upo dar ipi ambayo mvua imenyesha wiki 2. Kwa huku kwetu kwa siku mbili hizi imepumzika lakn ilikuwa imepiga mfululizo.
 
Hahahaha [emoji1] [emoji1] [emoji1] [emoji1] upo dar ipi ambayo mvua imenyesha wiki 2. Kwa huku kwetu kwa siku mbili hizi imepumzika lakn ilikuwa imepiga mfululizo.
Sawa imepiga mfululizo , lakini imeanza lini na imenyesha kwa siku ngapi ?
 
Wakuu , hii mnaweza kuiona kama Masihara vile , lakini uchunguzi nilioufanya jijini DSM , Jiji linaloaminika kuongoza kwa unywaji wa maji ya chupa ( maji safi ) , unaonyesha kwamba biashara ya maji imeanza kudoda kwa kasi ya kutisha !

Kwanza kwa kipindi cha mwaka mzima maji hayo hayajawahi kuadimika sokoni kama miaka ya nyuma , hali ni mbaya kiasi cha kusababisha magari ya makampuni karibu yote yanayotengeneza maji kupishana na kushinda mitaani yakisaka wateja , mithili ya Wanasiasa wanaoomba kura za ubunge majimboni .

Si kwamba watu hawanywi maji , la hasha ! Ugunduzi wangu umebaini kwamba watu wengi wanabeba maji ya Dawasco yaliyochemshwa ili kupunguza gharama , Hakika hali ni mbaya mno !

Ushauri wangu ni kwamba , maendeleo ya viwanda yaendane na vipato vya wananchi , viwanda vya maji vikifungwa kwa kukosa soko tutapoteza sana chanzo cha ajira ya vijana wengi mno .
Kuuzwa kwa maji ya chupa mtaani kwa wingi sio maendeleo bali ni umaskini na udhaifu Mkubwa wa serikali katika huduma ya maji. Maji yanayouzwa kwenye chupa serikali ilitakiwa iprovide majumbani mashuleni mahospitalini kwenye bustani za kupumzikia n.k hivyo kushamiri kwa biashara hii ni aibu ya serikali kwa upande wa wenye viwanda vya maji lazima wajipange kuwa kadri serikali inavyozidi kuimarisha huduma ya maji safi na salama kwa wananchi wake ndivyo biashara hii itakavyozidi kushuka. Kwa waliowahi kutembelea nchi za ulaya na marekani waje hapa watuambie kama biashara ya maji imeshamiri kama hapa bongo.
 
Hahaha! Wakuu sasa hivi hata kuzunguka na daladala ili uwahi siti tabia imeisha! Baadhi waliofanikiwa kuwa na magar kama nguo wanauza walau waweze kwenda na hali ya uchumi! tumeanza kuishi maisha kama digidigi! Its xo pain especially tuliopanga kuoa maana ndoto zimeyeyuka tumebaki kuhairisha kama vikao vya mjengoni!
Huu ni uchumi halisi unaofaa na utakaotupa maendeleo sio ule uchumi fake wataalam wanaita ghost economy
 
Wakuu , hii mnaweza kuiona kama Masihara vile , lakini uchunguzi nilioufanya jijini DSM , Jiji linaloaminika kuongoza kwa unywaji wa maji ya chupa ( maji safi ) , unaonyesha kwamba biashara ya maji imeanza kudoda kwa kasi ya kutisha !

Kwanza kwa kipindi cha mwaka mzima maji hayo hayajawahi kuadimika sokoni kama miaka ya nyuma , hali ni mbaya kiasi cha kusababisha magari ya makampuni karibu yote yanayotengeneza maji kupishana na kushinda mitaani yakisaka wateja , mithili ya Wanasiasa wanaoomba kura za ubunge majimboni .

Si kwamba watu hawanywi maji , la hasha ! Ugunduzi wangu umebaini kwamba watu wengi wanabeba maji ya Dawasco yaliyochemshwa ili kupunguza gharama , Hakika hali ni mbaya mno !

Ushauri wangu ni kwamba , maendeleo ya viwanda yaendane na vipato vya wananchi , viwanda vya maji vikifungwa kwa kukosa soko tutapoteza sana chanzo cha ajira ya vijana wengi mno .
Mkuu Kilimanjaro wamepunguza bei kudadadeki....
 
Mkuu umeeleza vizr kumbe hatua za kwenda uchumi wa kati zina changamoto!
Saana biashara nyingi zitafungwa kupungua au kufa natural death kwa mfano biashara ya vipodozi biashara ya bar biashara ya guest na hotel biashara ya toys n.k zitabakia biashara za essential goods tu. Hii ni dalili ya uchumi wa kweli uchumi imara.
 
Back
Top Bottom