Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,299
- 33,082
Picha ya kwanza inaonesha vifaranga vya ndege vikiwa hai, mama wa vifaranga hivi alitoka na kwenda huko kutafuta chakula cha kuwalisha watoto wake, lakini akiwa huko alikutana na maadui wakampiga na kumuwa. Vifaranga vikabaki vinateseka kwa njaa na baada ya muda kidogo navyo vikafa kwa njaa na kubakia mifupa kama unavyoona kwenye picha ya pili.
UJUMBE WANGU.
Unapo mfanyia mwenzio kitu kibaya ujue umewafanyia na wale wanao mtegemea. Wanaweza wakawa ni watoto, wazazi, wagonjwa ama wanafunzi wanaotegemea kulipiwa ada na mtu huyo.
Hivyo basi kabla hujamfanyia mwezio kitu kibaya kumbuka kuwa kunawatu wanamtegemea na uwepo wake ni mhimu sana kwa watu hao.