Ujumbe wa leo: Mama Mkwe

Ujumbe wa leo: Mama Mkwe

Hili ni tatizo la kufanya mahusiano / mapenzi kama battleground.., ndio maana unajikuta unatafuta allies na enemies..

Matatizo yenu wawili solve nyie wawili, ukiona imeshindikana na unahitaji msaada angalia busara ya unayemwambia sio sababu huyu ni wangu na yule ni wake
 
Mhhhhhhhh! Inaonekana kuna Tatizo hapo kwako MISS PIRATE, embu eleza tatizo tuweze kukushauri nn ufanye kuliko kuandika post iko hewani haina mashiko. PLS ELEZA TATIZO TUKUSAIDIE MAWAZO
 
Tena kwa sie wanawake, mamamkwe siyo mama mama yako hata ukimbeba mgongoni hata umwogeshe. ukiwa na matatizo yako kimbilia kwenu ukijifanya kumshitaki mumeo kwa mama yake imekula kwako. Siyo mzazi wako yule na kamwe hawezi kukuelewa. Usipoteze muda kufanya hivyo.
Cha maana ni kumheshimu imetosha na usiweke vikolombwezo vingine.

Huyu ni wa kwako ila mama mke wa kweli alieanza kama wewe na akasaidiwa na mama mkwe anajua nini maana ya mkwe na siku zote atatatua matatizo na sio kutetea mtoto wake. Mama mkwe mwenye busara hawezi kushughudia upuuzi ktk ndoa ya mwanae nae akatetea. Kama mimi ni mmeo matatizo ukaanzia kwenu na sio kwa wasimamizi wa ndoa au viongozi wa kanisa kama hao wakwe huwaamin uondoke kabisa kwani hapo umeivunjia heshima ndoa yako. Kumbuka maandiko yanasema mtaziacha familia zenu na kujenga yenu. Kifungo natafakari
 
Apana shosti sio wote,wengine wanaubinadamu na wanapenda haki,nadhani inategemea vile unavyo mchukulia kumbuka sikuzote mapenzi ndio yatamfanya hata kama anaroho mbaya basi atabadilika nakwambia haya kwa kuyaona,mie na mkwe wangu tunaelewana sana tena sana sifanyi jamboo bila kumshirikisha kama mzazi na usisahau na wewe iko siku utakua mkwe kama yeye...

Aksante kwa kuonyesha upande wa pili.
 
Baadhi wana maneno sana, ila baadhi pia ni wazuri anakupenda kama mama mzazi....
inategemea umeangukia wapi, pole mwaya!!!!

Good speak.....Pia tusisahau hata waolewaji nao wapo wenye maneno sana na wengine ni wazuri inategemea muoaji alivyobahatika.
 
Tena kwa sie wanawake, mamamkwe siyo mama mama yako hata ukimbeba mgongoni hata umwogeshe. ukiwa na matatizo yako kimbilia kwenu ukijifanya kumshitaki mumeo kwa mama yake imekula kwako. Siyo mzazi wako yule na kamwe hawezi kukuelewa. Usipoteze muda kufanya hivyo.
Cha maana ni kumheshimu imetosha na usiweke vikolombwezo vingine.


Shosti sio mama mkwe tu hata mawifi pia unatakiwa ukae nao mbali sio kujifanya mashoga, angalia kisa hiki

kuna rafiki yng mmoja alizaa na mwanaume na baada ya kutambulishwa ukweni akajichanganya na wakwe mawifi wakawa mashogaa ile mbaya, sasa akawa anawasimulia matatizo ya kaka/mtoto wao(yaani mchumba wake) kila mara yeye ni kumshitakia huyo mumewe mtarajiwa kwa mama yake.. baada ya muda akaona yule mama mkwe kabadilika, mawifi wamebadilika na huyo mume mtarajiwa amebadilika..ndoa ilikuwa ifungwe mwezi decemba mwaka jana lakini process zilisimamishwa ghafla mwezi novemba..mpaka leo hakuna kinachoendelea na huyo mume mtarajiwa amekata mawasiliano..alipokalishwa chini na kuulizwa kisa cha kusitisha harusi ghafla ni nini? akasema mama yake na dada zake wamemtonya aache(kutokana na maneno waliokuwa wakiongea wakiwa mashoga).. sasa huyo mama mkwe km ingekuwa ni binti yake ndio anaolewa angemfanyia hivyo? mama mkwe bana usijipendekeze saaana, mana wao kukugeuka ni one minute tu
 
Apana shosti sio wote,wengine wanaubinadamu na wanapenda haki,nadhani inategemea vile unavyo mchukulia kumbuka sikuzote mapenzi ndio yatamfanya hata kama anaroho mbaya basi atabadilika nakwambia haya kwa kuyaona,mie na mkwe wangu tunaelewana sana tena sana sifanyi jamboo bila kumshirikisha kama mzazi na usisahau na wewe iko siku utakua mkwe kama yeye...

mwambie huyo!!!!aibu mwanamke kuhamasisha wengine wawachukie wanawake wenzio.kesho utakuja na stori mtoto wa mwanamke mwenzio si wako,muheshimu tu lakini usimthamini na kumjali.as if u r not a woman.
 
Mtoto / Mkwe (wa leo ni mama mkwe wa kesho)...., kwahio wewe ukiwa na watoto hapo kesho ukiletewa kesi na mwenza wa mtoto wako utamtetea mwanao hata kama makosa ni yake ?
 
All in all akili kumkichwa jamani kama wako mzuri bahati yako nzuri wengine nouma kuna mama mkwe kamgeuza mjukuu wake tahira kisa kumkomoa mkwe achwee akiamini mtoto wake ataoa mwanamke mwengine atamzalia mjukuu mwengine akaona bado hawajaachana akamtia kichaaa mkwe wake kile cha kuja na kuondoka yani leo mzima kesho chizi akaona mwanae hamuachi mkewe akamtoa kizazi mkwe wake bado hawaachani akamtafutia mwanae mke wa nje bado hawaachani ss hv wapo wapo tu kama madudu ss kumbatia mama wa mwenzio ukidhani wa mama wa cku hizi niwale wa enzi hizoo mtakiona cha moto yy alee mwanae ww uje ule hivi hivi atakuua
 
Pole sana Miss Pirate ijapo si wamama wakwe wote wabaya

kwa kuwa umekubali kuishi na mwanae, mpende na umheshimu huyo bimkubwa tu shosti
 
Je na wewe ukijaliwa kupata mtoto wa kiume je mke wake asipokupenda wewe utajisikiaje?
 
hpo umesema shosty.mama mkwe sio mama ako hta.tena ukimuweka kama mamako utalia wengi sio wazuri.lkn ina2paswa 2waheshimu 2.mm mama mkwe wangu alitaka kunivuruga tena si kidog,ndoa ingekufa kma ningekuwa lele mama.mpk sawa chezea mm wewe.kingine, umpate mwanaume anaempenda mamake sana au last born bas wee utaisoma bila roho ya paka na hekima ndoa itakushinda.lastly,hyo mtto wake (wakiume)awe na vijisenti lahh?anaona kma vile unavimaliza hajui kma mnatafuta na mwanae aka.
 
Tena kwa sie wanawake, mamamkwe siyo mama mama yako hata ukimbeba mgongoni hata umwogeshe. ukiwa na matatizo yako kimbilia kwenu ukijifanya kumshitaki mumeo kwa mama yake imekula kwako. Siyo mzazi wako yule na kamwe hawezi kukuelewa.
Wewe nawe ni mkwe wa mtu?
 
Nawe unaenda kumshtaki ni mtoto mdogo huyo? Muambie nataka kuishi nawe kwa sababu tunapendana, sio kwa sababu wazazi wako wanatuamuru kama watoto! Kesi ikifika kwa wazazi ni taarifa ya kusudio la kutengana!
 
Mama mkwe ni mama ila inabidi kuwa makini sana lipi la kumshirikisha na lipi sio. Some of them ukimshirikisha wanakua msaada sana tu kuliko wazazi pengine!
 
Back
Top Bottom