Nimeona huu ujumbe sehemu facebook, kinachonishangaza ni jinsi wanawake wengi walivyomsifu aliyepost,
Chris Mauki, na kuufurahia ujumbe. Responses za wanawake ni kwamba, hata kama unagharimia ndoa/familia kwa mahitaji yote ya msingi lakini haufanyi surprises kama vile kumnunulia mwanamke vitu vidogo vidogo kama pipi, hereni basi wewe mwanaume hufai! Ameenda mbali kwa kuonyesha kumridhisha mwanamke sio issue, kikubwa ni kumjali. Kumjali kulikosisitizwa na wanawake kwa mjibu wa comments zao ni cheap surprises!
Hawa ndio wanawake wa karne hii, wakati wewe unapambana na mambo mazito yenye tija na sustainability kwa maendeleo ya familia, yeye anakupima kama unampenda kwa kusubiria surprises za pipi, chocolate, chicken burger, etc. Hajui kwamba unaweza kuwa hata hukumbuki hayo kwa sababu maisha yanakupeleka puta ili yeye aishi maisha mazuri/standard ya kupata mahitaji yote ya msingi na kufanya maendeleo!
Ujumbe wenyewe
"
HII INAUMUHIMU KWAKO
Siumeskia wenzako wanasema mwanamke anataka mtu anayejua kufanya mapenzi? Sasa wewe wekeza muda na akili yako kujenga mwili na kutafuta mbinu za kumfurahisha mkeo kimapenzi tu wakati vitu vingine vidogo vidogo vinakushinda kuvifanya au unaviona sio vyamaana. Utaachwa na mastaili yako yasio na tija. We ujuzi umewekeza tu kwenye kuijua mechi, ukiambiwa kumjali mwenzako unatoka kapa, kumshirikisha mambo yako hujui, kumprotect dhidi ya ndugu zako huwezi, mama yako na dada zako wamekuweka kiganjani na bado unaona hilo ni sawa, akiomba umsaidie kitu kidogo unaona shida, vijizawadi na vijisapraizi navyo ndio kabisaaa umefeli. Ndugu yangu hayo maujuzi yako ya mechi peleka kwenye maonyesho saba saba, huyu dada wawatu atakushindwa mapemaaa, maana haumfai kwa kulumangia wala kwa kunywa - Chris Mauki
"
Responses za wanawake ni nyingi na zimefagilia ujumbe huu, karibu kila mmoja akimalizia na kionjo "ufundi peleka maonyesho sabasaba au veta".