Ujumbe wa Dr. Chris Mauki

Ujumbe wa Dr. Chris Mauki

duh,mi sipendi kumnunulia demu zawadi wala sitaki surprise yeyote.nataka plan/great ideas.
 
images.jpg
 
Nimeona huu ujumbe sehemu facebook, kinachonishangaza ni jinsi wanawake wengi walivyomsifu aliyepost, Chris Mauki, na kuufurahia ujumbe. Responses za wanawake ni kwamba, hata kama unagharimia ndoa/familia kwa mahitaji yote ya msingi lakini haufanyi surprises kama vile kumnunulia mwanamke vitu vidogo vidogo kama pipi, hereni basi wewe mwanaume hufai! Ameenda mbali kwa kuonyesha kumridhisha mwanamke sio issue, kikubwa ni kumjali. Kumjali kulikosisitizwa na wanawake kwa mjibu wa comments zao ni cheap surprises!

Hawa ndio wanawake wa karne hii, wakati wewe unapambana na mambo mazito yenye tija na sustainability kwa maendeleo ya familia, yeye anakupima kama unampenda kwa kusubiria surprises za pipi, chocolate, chicken burger, etc. Hajui kwamba unaweza kuwa hata hukumbuki hayo kwa sababu maisha yanakupeleka puta ili yeye aishi maisha mazuri/standard ya kupata mahitaji yote ya msingi na kufanya maendeleo!

Ujumbe wenyewe

"
HII INAUMUHIMU KWAKO

Siumeskia wenzako wanasema mwanamke anataka mtu anayejua kufanya mapenzi? Sasa wewe wekeza muda na akili yako kujenga mwili na kutafuta mbinu za kumfurahisha mkeo kimapenzi tu wakati vitu vingine vidogo vidogo vinakushinda kuvifanya au unaviona sio vyamaana. Utaachwa na mastaili yako yasio na tija. We ujuzi umewekeza tu kwenye kuijua mechi, ukiambiwa kumjali mwenzako unatoka kapa, kumshirikisha mambo yako hujui, kumprotect dhidi ya ndugu zako huwezi, mama yako na dada zako wamekuweka kiganjani na bado unaona hilo ni sawa, akiomba umsaidie kitu kidogo unaona shida, vijizawadi na vijisapraizi navyo ndio kabisaaa umefeli. Ndugu yangu hayo maujuzi yako ya mechi peleka kwenye maonyesho saba saba, huyu dada wawatu atakushindwa mapemaaa, maana haumfai kwa kulumangia wala kwa kunywa - Chris Mauki
"
Responses za wanawake ni nyingi na zimefagilia ujumbe huu, karibu kila mmoja akimalizia na kionjo "ufundi peleka maonyesho sabasaba au veta".
Vizawadi na surprise kwa michepuko inawezekana. Lakini kwa mkeo inakuwa ngumu.
 
Dr. Mauki unajidhalilisha mno kwa namna unavyojipamnbanua kwenye ulimwengu wa wasomi. Yaani tunakutofautishaje na kina MC Pilipili, Gea n.k (too low). Hebu jitafakari upya tulitegemea tuki-google jina lako tuone Papers ulizopubl;ish kwenye International Journal sio hizi tambo za kinamama hapa nchini na kuitwa kwenye vipindi vya KITCHEN PARTY. Dr. Mauki aibu aibu aibu
Hivi ni msomi?
Mbona kuna mambo chanya ya kuandika kama mwana saikolojia bila kuonekana unamlenga mtu yeyote...
Ajaribu kusoma maandiko ya wenzie..
Mimi kuna rafiki yangu ana like kila anachoandika huyu jamaa...ananifanya nimfikirie ana like nini wakati ni mipasho...my conclusion ni kuwa atakuwa yuko kwenye frustrations (huyo shosti angu) maana ni aibu kwa mke wa mtu ku like baadhi ya vitu anavyoandika huyu jamaa.

Wewe mtu anaandika mwanaume hujui penda mkeo...afu una like na mmeo anaona...si kudhalilisha mmeo huko...shida sana
 
Mbona udakta hata wa kufungiwa kwenye maboksi na kupewa kama zawadi nao unatambulika vlvl………
 
Mapenzi ya maigizo haya ni upotoshaji tu.

Kama mwanamke siyo mtu wa kuridhika hutakaa umridhisha hata ukimnywesha damu yako yote.
Wengine hizo pumba za jamaa ndiyo hujifariji nazo kwa madhambi yao ya michepukoni huko
 
Sioni tatizo kama wengi wao wamekubaliana naye.

Kama wewe haujakubaliana naye sioni tatizo pia.

Tatizo lako kwa huyo Chris nadhani ni hapo unaposema kuwa "anawala" sana wanawake japo mimi bado sioni tatizo akiwala kwasababu moja ya sababu za uwepo wao ni kuliwa.
Hahaahar ndio kabisa wapo ili waliwe
 
swali no kwamba kama unaona mwanaume kukufanyia vitu vidogodogo ndo amekamilika bac mbona hamkimbilii kuolewa nao?mbona mtafute wenye hela zao bac kama nyinyi si ulafi tu na kutoridhika!mwenzako anahenya kwenye foleni na joto kali anatafuta kwa ajiri yako January mpaka Dec. ss hivo vidogo ndo vina kulisha!ndo vinakufanya upendeze?ndo vinakuweka mjini?Inahitaji moyo sana kuishi na hawa viumbe...
 
Mm wa kwangu aliniletea hizo kauli eti bila kufanya visapraizi vidogo ninafanya sawa na bure kabisa!nikamwambia ok mm siwezi kuanfaoka na vidogo kwa sabb viko ndani ya uwezo wako mm nahangaika na vikubwa ola siku nikikunasa na mchepuko kisa sikupi vidogo bac kuanzia siku hiyo ndo atakuwa mumeo muebdelee kupeana hivo vidogo
 
wee endelea kukataa, km unadhani mwanamke anatulia kwa vurugu zako za kitandani tu, utalizwa kila siku, tena basi vizawadi unavyovidharau huwa vinatekenya kweli
 
Kuna part nakubaliana na wewe.
Ufundi wa kitandani ni muhimu ila kama kwingine huwezi kubalnce kwakweli ni ngumu kuvumilia....wanaume wakituelewa mbona rahisi sana tatizo wamekariri
Mind is the first thing to be stimulated, mi hata kuwe na ufundi wa PHD kama mind haijawa stimulated sitafurahia chochote. Na hizo mind stimulators ni hayo yote anayoyaongea Dr Mauki.
sometimes vitu tunavyohitaji sio vikubwa kama ambavyo wanaume wanafikiri.
Lakini pia kila mwanaume amuelewe mwanamke wake alivyo, kuna wanaume wanajitahidi kuwaelewa wanawake zao kwa stori za wanawake wengine.
 
Criss mauki yuko right isitoshe ni mtu makini anayeelewa mahusiAno.ni counselor mzur sn.anatoa elimu nzuri ambayo naona kumtimizia mwanamke ni wajibu wako usikwepe.naona ishu ya kutoa sapraiz imekutachi sana mnunulilie bana mkeo visapraiz afurahi akifurahi ht mungu anawazidishia rizki
 
Back
Top Bottom