Jadda
JF-Expert Member
- May 20, 2019
- 31,540
- 88,485
Mkuu hivi dhambi ikifanywa na mtumishi wa Mungu maana yake ndo Mungu amaeiruhusu? Hivi unajua nini kuliwakuta hao baada ya kufanya hiyo dhambi au umeshika hapo tu pa kuwa na wake wengi? Fuatilia wote hao kuna adhabu walipata baada ya kufanya hayo na kumbuka walipofika uzeeni wote hao walitubu na Mungu akawasamehe sasa kama ingekuwa Mungu karuhusu kwanini walitubu?Yaani dada me nakuambia ukweli,wapo wenye unafuu tu. Kumbuka hata watu waliokuwa wameaminiwa na Mungu nao walichepuka. Kwenye biblia ibrahimu alichepuka,mfalme Daud hadi aliua ili amuoe mchepuko,mfalme suleimani ndo alivunja record kwa kuoa wake halali 700 na michepuko 300. Huenda Mungu mwenyewe anaruhusu tuchepuke sema sisi tu ndo tunawaogopa nyie. Lkn nadhani Mungu hana tatizo na wanaume kuhusu hilo.
Halafu kuwa mtumishi wa Mungu hakukufanyi wewe mkamilifu watu wanadhani ukiwa mtumishi wa Mungu basi umekuwa malaika hapana hata watumishi wa Mungu nao ni binadamu na wanajaribiwa vile vile na kati yao wapo ambao wanayashinda hayo majaribu na wapo wanaoyashindwa na kuwa muumini tu wa kawaida hakukufanyi ndo kuwa mdhambi sana
Kuna watu siyo watumishi wa Mungu ni waumini tu wa kawaida lakini wanaweza kujizuia dhambi za kijinga kama hizo kuliko hata watumishi wa Mungu na Mungu analielewa hilo kwamba hakuna mkamilifu chini ya jua ila tu unapofanya dhambi ukubali na ukatubu siyo kusema eti hii siyo dhambi tena kwa sababu hadi watumishi wa Mungu wanafanya
Hapana maandiko yanakataza uzinzi pia yanasema kila mwanaume awe na mke mmoja na kila mwanamke awe na mume mmoja yaani kama Adam alivyoumbiwa mke mmoja tu Evah ndivyo Mungu alivyotaka iwe haya mengine ni shetani tu kawadanganya wanadamu

