Ujenzi wa lenta kwa nondo 3 unafaa?

Ujenzi wa lenta kwa nondo 3 unafaa?

usipozifunga zile nondo ikatokea kuna nguvu, kani au force inayolazimisha kui-twist au kuinyonga ile lenta ni zege pekee yake ndiyo itatoa ukinzani kwa hiyo kani au nguvu msukumo kwa kuwa nondo hazijaunganishwa, hazina ushirikiano katika ktk hiyo aina ya force...kwa hiyo unakuwa huja-exploit vizuri msaada wa nondo ulizoweka
nilitaka ufafanue kwa kiswahili kwa faida ya wasomaji mimi binafsi naelewa maani hii ni fani yangu..kwa kuongezea tuu bangili/stirrups ndio zenye kazi ya kuzuia nyufa ikiwa tu nafasi imezingatiwa
 
Inategemea pia na life span ya nyumba... Kwa standard hizo, nyumba inaweza dumu kwa miaka 30 ivi.
Mimi nilipiga mahesabu haya.. Sasa nina miaka 36. Kama Mungu amenipa miaka 70 ya kuishi hapa Duniani ina maana nyumba inabidi iwe na uwezo wa kudumu kwa miaka 34 ijayo.. Iwapo mie nitatangulia na miaka 70 mke wangu akafuatia miaka 10 baadaye, basi nyumba iwe na uwezo angalau wa kuishi miaka 44!
Ili nyumba iweze kufikia umri huo, nimeiimarisha kwa nondo za kutosha kama unavyoweza kuiona kwenye hii picha.
Usipoimarisha nyumba vya kutosha, utahitaji kujenga tena nyumba ingine uzeeni wakati nguvu zishakwisha.View attachment 1469059
Swala la nondo 4 pia linategemea na udongo wa mahali,mimi kuna sehemu nilipiga nondo 4 ndani ya mwaka mmoja eneo lile lile kulikopita nondo nyufa zika chanja mbuga,kwahiyo hata nondo 2 kama udongo uko vizuri nyumba zinadumu...
 
Swala la nondo 4 pia linategemea na udongo wa mahali,mimi kuna sehemu nilipiga nondo 4 ndani ya mwaka mmoja eneo lile lile kulikopita nondo nyufa zika chanja mbuga,kwahiyo hata nondo 2 kama udongo uko vizuri nyumba zinadumu...
Na hii kufunga msingi haisaidii!
 
Swala la nondo 4 pia linategemea na udongo wa mahali,mimi kuna sehemu nilipiga nondo 4 ndani ya mwaka mmoja eneo lile lile kulikopita nondo nyufa zika chanja mbuga,kwahiyo hata nondo 2 kama udongo uko vizuri nyumba zinadumu...
Nyufa zilianzia wapi? kama ni za kutoka juu sawa ila hazina uhusiano na udongo,but kama zilianzia chini kutoka kwenye msingi na kupanda juu hadi kuvuka ring beam hapo ndioudongo unahusika yaani kitu inaitwa settlement so ukigundua hali hiyo unapojenga msingi lazima ulete udongo mwingine na ufunge plimth beam au underground beam ndio uendelee na kupandisha kuta za beam ya juu,pia kumbuka kuzingatia spacing ya zile rings zinaitwa stirrups
 
Ubarikiwe sana mkuu
Kitaalamu haufai kabisa.

Kwa sababu hiyo lenta(linta) ndiyo inapokea mzigo kutoka juu na kuleta msawazo wa jengo lako. Kwa sababu linta inapokea mzigo inatakiwa iipokee kwa usawa.

Kwanza kazi ya nondo ni nini kwenye linta??

Kazi ya nondo kwenye linta ni kuzuia kani(force) za mvutano ndani ya jengo lako!

Kwa nini sasa nondo tatu hazifai??
Ni kwa sababu standards zinashauri nondo lazima zifungwe symmetrically arranged. Ili zinapopokea mzigo na kuusambaza uwe sawa sawa.

Nondo tatu siyo symmetrically arranged. Sasa mzigo ukizidi kudogo tuu, jengo unaanza kuliona limeeanza nyufa na hata hiyo linta unaanza kuiona inapinda.

Suluhisho!

Ongeza nondo nyingine ziwe nne ili angalau ulete msawazo wa upokeaji wa mzigo na usambazaji wake.

Pia weka na nguzo kwenye kila kina na maungio ya jengo lako (kama ni nyumba kubwa na unataka idumu muda mrefu).

Ila kama ni banda tuu, komaa na aina ya ujenzi wako. Ila kama ni dream house, fuata hako kaushauri.
 
Spring nzuri na imara hivyo??? Kuna jamaa aliwaachia mafundi hela kumbe badala ya nondo wameweka mirunda............ALIJUAJE????....siku moja ameita mafundi waongeze rumu kwa nje kwa kuattach kwenye main house .....jamaa wamefikia usawa was lenta wanatindua ili waunganishe nondo....wanakutana na mirunda!!!!!!!!
Ni uboya kumuacha fundi afanye bila ya usimamizi japo baadhi ni waaminifu wanaoheshimu taaluma yao.
 
Duh mie nilipiga mbili kwenye kuta Ila kweny milango na madirisha nikaweka Tatu, mkuu mpaka leo kitu naona fresh tu
 
Spring nzuri na imara hivyo??? Kuna jamaa aliwaachia mafundi hela kumbe badala ya nondo wameweka mirunda............ALIJUAJE????....siku moja ameita mafundi waongeze rumu kwa nje kwa kuattach kwenye main house .....jamaa wamefikia usawa was lenta wanatindua ili waunganishe nondo....wanakutana na mirunda!!!!!!!!
Situation Kama hiyo imetokea kwenye nyumba ya rafiki yangu ..sehemu ya kibaraza..jamaa alitaka kurekebisha nguzo coz ilikua imepinda...Sasa akaita fundi aje avunje ili afunge upya aliyoyakuta Ni suprisea na kilio.
 
  • Thanks
Reactions: rr4
Situation Kama hiyo imetokea kwenye nyumba ya rafiki yangu ..sehemu ya kibaraza..jamaa alitaka kurekebisha nguzo coz ilikua imepinda...Sasa akaita fundi aje avunje ili afunge upya aliyoyakuta Ni suprisea na kilio.
Mafundi......AAA.... Acha kabisa
 
utafaa kama unaona unakufaa..ila sio rafiki kwa siku za usoni.
 
Hapo ulipoteza tu rasilimali nondo maana hakuna muunganiko wa kimuundo structurally,bora ungeweka matete au vipande vya mianzi uvifunge vizuri na bangili
...............Sijaelewa vizuri uliposema ningeweka matete but vyovyote iwavyo unadhani hayo matete au vipande vya mianzi ningevipata bure?

By the way,ulikuwa ushauri wa engineer sikuweza kubishana nae hata wewe kukubishia siwezi labda ulishawahi kufanya hivyo ukafanikiwa ila kwangu kuweka nondo ndo niliona itakuwa imara.
 
...............Sijaelewa vizuri uliposema ningeweka matete but vyovyote iwavyo unadhani hayo matete au vipande vya mianzi ningevipata bure?

By the way,ulikuwa ushauri wa engineer sikuweza kubishana nae hata wewe kukubishia siwezi labda ulishawahi kufanya hivyo ukafanikiwa ila kwangu kuweka nondo ndo niliona itakuwa imara.
swali,je nondo ulizifunga kwa bangili?
 
sijajua zina upana gani ila mi nimeweka mbili tu za milimita 12 na ipo fresh mpaka leo cha msingi usibanie saruji hakikisha unavyomwaga zege sementi iwe konki
 
Inategemea pia na life span ya nyumba... Kwa standard hizo, nyumba inaweza dumu kwa miaka 30 ivi.
Mimi nilipiga mahesabu haya.. Sasa nina miaka 36. Kama Mungu amenipa miaka 70 ya kuishi hapa Duniani ina maana nyumba inabidi iwe na uwezo wa kudumu kwa miaka 34 ijayo.. Iwapo mie nitatangulia na miaka 70 mke wangu akafuatia miaka 10 baadaye, basi nyumba iwe na uwezo angalau wa kuishi miaka 44!
Ili nyumba iweze kufikia umri huo, nimeiimarisha kwa nondo za kutosha kama unavyoweza kuiona kwenye hii picha.
Usipoimarisha nyumba vya kutosha, utahitaji kujenga tena nyumba ingine uzeeni wakati nguvu zishakwisha.View attachment 1469059
duh sio kwa nondo hizo mzee, unajenga ghorofa nini?
 
Back
Top Bottom