Ujenzi wa lenta kwa nondo 3 unafaa?

Ujenzi wa lenta kwa nondo 3 unafaa?

Mjengo wangu wa tofali za kuchoma nimepiga nondo moja tu halafu uko strong. Kwa tofali ya block ni vyema kuweka mbili ama nne.
 
Mjengo wangu wa tofali za kuchoma nimepiga nondo moja tu halafu uko strong. Kwa tofali ya block ni vyema kuweka mbili ama nne.
Hata mimi ni tofali za kuchoma
FB_IMG_1572549351084.jpeg
 
Leo nimeweza sana kusikia nondo tatu hazitoshi wakati nyumba lukuki hapa Masumbwe tena nyingine ni lodge zina nondo moja tu na matetemeko ya ardhi yamepita hii ni mara ya pili nyumba zinadunda tu.
 
Weka nondo nne mkuu ili kuweza kubalance sawasawa mzigo wa juu ya nyumba, mkuu jikaze kama umeweza kuweka tatu huwezi shindwa kuongeza hiyo moja, jenga kitu imara. Kuna jamaa yangu aliezeka bati la gauge 30 badala ya 28, kwa kubana bana hivyo hivyo matumizi wakati hela alikuwa nayo, sasa ile fundi wakati anapiga bati akikanyaga linabonyea, kamaliza kupaua huko juu kuna vidimbwi balaa hizo mvua za mwezi jana kuna sehemu kukawa kunavuja, kubadilisha hawez akabaki anajutia tu. By the way ukija kuangalia unachosave hapo hata laki 3 haifiki
 
Inategemea pia na life span ya nyumba... Kwa standard hizo, nyumba inaweza dumu kwa miaka 30 ivi.
Mimi nilipiga mahesabu haya.. Sasa nina miaka 36. Kama Mungu amenipa miaka 70 ya kuishi hapa Duniani ina maana nyumba inabidi iwe na uwezo wa kudumu kwa miaka 34 ijayo.. Iwapo mie nitatangulia na miaka 70 mke wangu akafuatia miaka 10 baadaye, basi nyumba iwe na uwezo angalau wa kuishi miaka 44!
Ili nyumba iweze kufikia umri huo, nimeiimarisha kwa nondo za kutosha kama unavyoweza kuiona kwenye hii picha.
Usipoimarisha nyumba vya kutosha, utahitaji kujenga tena nyumba ingine uzeeni wakati nguvu zishakwisha.
IMG_20200111_170503.jpg
 
Kukaa tu hata ukiweka mti unakaa tatizo mzigo unaokuja juu naona hatutaelewana Mimi ni mjenzi mtaalamu ninafahamu ninachosema bahati mbaya sifanyi kazi za nondo mbili nitakutupia kazi yako
hawa hawaelewi mantiki ya reinforcements na mbaya zaidi stirrups ndo kabisaa hawazingatii wanajua eti kazi yake ni kushikilia nondo
 
Yah itakuwa bora,nadhani wengi ndo tunavyoweka mimi niliweka mbili kwenye kiuno cha msingi lintel nikaweka tatu nyumba ilinyeshewa mvua siyo chini ya miaka saba na sehemu niliyojenga palikuwa na udongo wa mfinyanzi ila nyumba haikupata crack yoyote.
Hapo ulipoteza tu rasilimali nondo maana hakuna muunganiko wa kimuundo structurally,bora ungeweka matete au vipande vya mianzi uvifunge vizuri na bangili
 
Unazikata na kuzitandaza kabisa kule kwenye box za linter, wakati unamwaga zege ndo unazinyanyua zikae ktk umbo hilo sasa. Niliona fundi wangu anafanya hivyo.
Sawa, ila hapa kuna shida...kuzifinga kuna faida nyingi, hapa hakuna torsion, shear resistance,
 
watu wengi mara nyingi wamekuwa wakichanganya lenta(lintel) na ring beam...lenta ni kipande kifupi tu kinachofungwa kwenye uwazi(openings) kama milango na madirisha, ring beam ni ile unafungu kuzunguka nyumba kwa kuzifuata kuta zote za nje na za ndani wengine huchagua kuta zinazobeba mzigo tu(load bearing walls).

turudi kwenye mada, ufungaji wa nondo kwa level ya juu pia hutegemea sana uzito utakaobebwa kutoka juu, tu-assume mzigo ni course chache tu za tofali na paa la kawaida la mbao na bati na kama mleta maada alimaanisha lenta kwa definition niliyotoa hapo juu pamoja na ukweli kwamba standards nyingi zinataka nondo nne lkn nondo tatu za 12mm kwa sura ya mzigo niliyoelezea hapo juu zinatosha kabisa lkn zifungwe pamoja na nondo au waya angalau wa 6mm, 8mm zinaweza tumika pia.

kama mleta maada lenta alimaanisha ring beam (kama wengi wanavyoichanganya lenta na ring beam) nondo tatu kwangu ni uharibifu wa hela (is a wastage of resources), nondo mbili za 12mm is more than enough.

kumbuka zege liwe la angalau lenye mchanganyo wa ratio ya 1:2:4 cement:mchanga:kokoto...hii kwa makadirio inakupa zege lenye nguvu ya 20Mpa au grade 20 au class 20 though itategemea na ubora wa mchanga na kokoto
 
watu wengi mara nyingi wamekuwa wakichanganya lenta(lintel) na ring beam...lenta ni kipande kifupi tu kinachofungwa kwenye uwazi(openings) kama milango na madirisha, ring beam ni ile unafungu kuzunguka nyumba kwa kuzifuata kuta zote za nje na za ndani wengine huchagua kuta zinazobeba mzigo tu(load bearing walls).

turudi kwenye mada, ufungaji wa nondo kwa level ya juu pia hutegemea sana uzito utakaobebwa kutoka juu, tu-assume mzigo ni course chache tu za tofali na paa la kawaida la mbao na bati na kama mleta maada alimaanisha lenta kwa definition niliyotoa hapo juu pamoja na ukweli kwamba standards nyingi zinataka nondo nne lkn nondo tatu za 12mm kwa sura ya mzigo niliyoelezea hapo juu zinatosha kabisa lkn zifungwe pamoja na nondo au waya angalau wa 6mm, 8mm zinaweza tumika pia.

kama mleta maada lenta alimaanisha ring beam (kama wengi wanavyoichanganya lenta na ring beam) nondo tatu kwangu ni uharibifu wa hela (is a wastage of resources), nondo mbili za 12mm is more than enough.

kumbuka zege liwe la angalau lenye mchanganyo wa ratio ya 1:2:4 cement:mchanga:kokoto...hii kwa makadirio inakupa zege lenye nguvu ya 20Mpa au grade 20 au class 20 though itategemea na ubora wa mchanga na kokoto
usipozifunga kwa stirrups unapoteza tu radilimali nondo maana haitafanya kazi kusudiwa,binafsi huwa naweka nondo 4 but 8mm na nazifunga kwa stirrups za 6mm kwa spacing below 30cm nakuwa nimeachieve strength nayotaka kwa kutumia mchanganyiko wa class 20 ya zege
 
ongea lugha rahisi kwa kiswahili humu sio kila mtu kasoma civil engineering
usipozifunga zile nondo ikatokea kuna nguvu, kani au force inayolazimisha kui-twist au kuinyonga ile lenta ni zege pekee yake ndiyo itatoa ukinzani kwa hiyo kani au nguvu msukumo kwa kuwa nondo hazijaunganishwa, hazina ushirikiano katika ktk hiyo aina ya force...kwa hiyo unakuwa huja-exploit vizuri msaada wa nondo ulizoweka
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom