Baada ya kuvuka sehemu moja inayoitwa Nyancha Bukenye mida hii kuna polisi wanasimamisha kila gari linalopita barabarani na kuwalazimisha madereva kutoa hela wakidai wana speed na makosa mengine ya kulazimisha. Mmoja wao anatoa kauli chafu sana kwa madereva, anawaambia asiyetaka kutumia barabara anunue ndege apae usitumie barabara
Hawa watu wanataka hela yoyote siyo chini ya 20,000. Mimi wamenilazimishia makosa sita na kutaka 180,000 baada ya mabishani wakasema watanipunguzia iwe laki moja. Ukiwaambie wakupe risiti wanasema wanakupeleka kituoni huko utapata evidence ya speed yako huko. Ukikomaa sana, wanakupa risiti feki, lakini lazima uwape hela kwanza. Nimefanikiwa kumpata mdada anayekusanya hela ni WP 9555 PC Grace. Kamanda Siro imulike ofisi ya OCD Tarime. Watasababisha vurugu maana huu unyanganyi siyo wa kawaida. Huyo Grace aisaidie polisi kufanya uchunguzi. Wana Land rover Defender Pick up nyeupe iliyofichwa kwenye Kichaka