Logikos
JF-Expert Member
- Feb 26, 2014
- 12,475
- 19,508
HOTUBA YA NYERERE NA VIONGOZI WA DINI TABORA 27/7/70
Key Take Away:- NCHI ya Tanzania / TANU hazina Dini; Wananchi ndio Wana Dini...
- Kichama / TANU Hatujui kama Mungu yupo au hayupo (Hatuulizani); Tunaulizana Habari za Maji, Maharagwe na Mabarabara..... Lakini hatuulizi Kabisa kama ipo Pepo; kama kwenda Mbinguni ziko ngazi ngapi ? Tunaulizana ya kwetu yanataka Kura, sasa la Mungu mtalipigiaje kura ! Kwamba wengi wamekubali Mungu yupo kwahio yupo au hayupo ?
- Dini; Mimi nina yangu Karume ana yake Kawawa na Waheshimiwa wengine, Waheshimiwa mbalimbali kila mtu ana yake....., tunapokutana kwenye mikutano hatumuulizi leo Umesali ? Aa! Hiyo ni Hiari yake, kasali hakusali anajiuliza Mwenyewe
- SIASA ya UJAMAA kwa mtu anayejua Socialism ya Ulaya mtu wa Dini Inabidi Aelezewe vizuri sana sivyo atakupinga (atakuona hatari)
- Ulaya ilifika wakati watu wakasema "Kama Dini yenyewe ipo hivi Hatukubali"; Dini inatetea Mali zaidi ya mtu
- CHAMA CHETU KINASEMA - mtu mwenye Afya ambaye tumeshindwa kumpa njia halali ya kujipatia riziki yake. Nawaomba ardhi - hakuna ardhi; hamnipi ardhi, Mnasema "Ardhi hakuna". Naomba kazi ya kibarua basi, Nipeni basi ya kibarua, "Hamnipi kazi ya kibarua. Mimi niko tayari kabisa kufanya kazi au ya kulima au ya kibarua chochote nipeni. Hamnipi Chama Chetu kinasema MTANILISHA.