Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 20,922
- 30,271
HISTORIA YA KURA TATU: DUA YA MNYANJANI TANGA HADI HOTUBA YA JULIUS NYERERE PARISH HALL (UKUMBI WA KANISA KATOLIKI) TABORA 1958
Laiti kama si Sheikh Abdallah Rashid Sembe wa Tanga kukubali kuzungumza na mimi historia ya Kura Tatu isingejulikana kwa ukamilidu wake.
Waliokuwa wanaojua mkutano wa siri uliofanyika Tanga walikuwa wao viongozi wa Tanga, Mwalimu Nyerere na Amos Kisenge peke yao.
Bahati mbaya Mwalimu Nyerere hakupenda kueleza historia yake katika mengi yaliyofanywa na viongozi wenzake wa TANU wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika.
Historia hii muhimu sana katika kjupigania uhuru wa Tanganyika ingepotea na ikawa inajulikana kijuujuu kama ilivyokuwa historia ya chama cha TANU chenyewe.
Historia ya Kura Tatu nimeieleza kwa kirefu katika kitabu cha Abdul Sykes (1998) na kwa ushawishi wa mchapa vitabu mmoja kutoka Kenya akaniomba nimpatie mswada wa kitabu cha historia hii achape kitabu makhsusi kwa kaudhimisha miaka 50 ya Azimio la Busara mwaka wa 2008.
Kazi hii niliifanya na ilikuwa mapendekezo ya mchapaji huyu kitabu hiki kiandikiwe utangulizi na Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Jinsi alivyothamini historia hii mchapaji huyu alikuwa amepanga kuchapa nakala chache maalum kwa ajili ya viongozi wa nchi.
Kitabu kilichapwa lakini bila ya kuandikiwa utangulizi.
Kwa ajili hii nakala zile maalum kwa watu maalum hazikuchapwa.
Kitabu hiki kikafa kabla ya kuzaliwa lakini kilipotoka chote kilinunuliwa kwa haraka sana na sasa ni katika vitabu vinavyoitwa, ‘’out of print,’’ yaani vimekwisha sokoni havipatikani hadi vichapwe upya.
Kitabu hiki ni cha pili katika vitabu vyangu viwili vilivyochapwa na na ''publishers'' wa Kenya vinavyohusu historia ya uhuru wa Tanganyika.
Bahati mbaya sana vitabu hivi vyote viwili havikupata mafanikio Tanzania.
Havikupendwa.
Nimepokea picha ya Parish Hall Tabora palipofanyika Mkutano wa TANU wa Mwaka wa 1958, mkutano uliokuja kufahamika kama Mkutano wa Kura Tatu kwa kuwa TANU ilikuwa inajadili agenda nyeti sana ya Uchaguzi Mkuu wa kwanza kuchagua wajumbe watakaoingia katika Baraza la Kutunga Sheria (LEGCO).
Nikiwa naiangalia picha hii fikra nyingi zilipita kichwani kwangu.
Nilikuwa nawaza nchi hii ilikotoka na historia yake ya umoja wa wananchi wake na jinsi historia ilivyopotoea ikawa haijulikani.
Nachelea kuifanya makala hay kuwa ndefu sana kwa hiyo nitaeleza jambo hili ninalokusudia kwa kifupi.
Mwalimu Nyerere na Amos Kisenge walikwenda Tanga kuonana na uongozi wa TANU kutafuta kuungwa mkono kwa agenda ya TANU kuridhia kushiriki katika Kura Tatu jambo ambalo wanachama walikuwa wanapinga kiasi kuja na kauli mbiu, ''Kuingia Kura Tatu ni Sawa na Mtu Kujipaka Kinyesi Chake.''
Sababu ya upinzani huu ni yale masharti ya kupiga kura na masharti ya mpigiwa kura.
Mpiga kura alitakiwa awe na elimu ya darasa la 12 (wakashudha hadi darasa la 10), awe na kipato cha Pound za Kiingereza 400 kwa mwaka, awe na kazi ya ‘’kueleweka’’ na ampigie kura Mzungu, Muasia na Mwafrika.
Wanachama wengi wa TANU walikuwa Waislam na ukoloni uliwanyima elimu kwa kuwa elimu ilikuwa ikitolewa na wamishionari kwa kushirikiana na serikali ya Kiingereza.
Masharti haya yaliwatoa katika kupiga kura na halikadhalika kupigiwa kura kuingia katika LEGCO.
Lakini hili halikuwa likisemwa bayana.
TANU ilikuwa na hofu kubwa na hisia za dini ndani ya chama kwa kuchelea kuwagawa wananchi.
Hukumu yake kwa mwanachama atakaekiuka sharti hili ni kufukuzwa chama.
Wanachama wa TANU waliweka msimamo wao tu kuwa hawatashiriki katika uchaguzi wa Kura Tatu bila ya kueleza hayo.
Sheikh Suleiman Takadir Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa TANU akawa kiongozi wa kupinga TANU kuingia katika Kura Tatu.
Katibu Mkuu wa TANU Zuberi Mtemvu ns yeye pia alikuwa katika wapinzani wa Kura Tatu.
Majimboni kote Dodoma, Lindi, Tabora, Tanga, Kanda ya Ziwa hali ilikuwa ni hivyo.
Rais wa TANU Mwalimu Nyerere kuona hali hii ndiyo akaamua kwenda Tanga kuzungumza na uongozi wa TANU wa akina Mwalimu Kihere, Abdallah Rashid Sembe, Hamisi Heri, Mohamed Kajembe kwa kuwataja wachache kutafuta msaada kuwezesha TANU kushiriki katika Kura Tatu.
Mkutano wa Tanga ulikuwa mzito sana lakini hatimae walikubaliana kuwa lazima TANU ishiriki na wakaweka mikakati ya ushindi ndani ya chama kuwashinda wapinzania wa Kura Tatu na nje ya chama kushinda hila za Waingereza na chama chao cha United Tanganyika Party (UTP).
Baada ya kumaliza kikao hiki viongozi wa TANU Tanga wakamwambia Nyerere kwa kuwa hili jambo ni kubwa lazima ifanyike dua kumuomba nusra ya Mwenyezi Mungu.
Leo ukieleza kuwa Qur'an ilikuwa ikitangulia kusomwa katika mikutano ya TANU hakuna atakaeamini.
Kulikuwa na hofu kubwa kuwa kama hawatakufikia muafaka Tabora TANU itameguka vipande viwili na kuna hatari Julius Nyerere akajikuta yuko peke yake kundi kubwa likabaki na Sheikh Suleiman Takadir na Zuberi Mtemvu na wengine.
Dua hii ilifanyika kijiji cha Mnyanjani nje kidogo ya Tanga na Mwalimu Nyerere na Amos Kisenge walishiriki.
Kisomo kilifanyika usiku na kumalizika alfajir.
Mwalimu na Kisenge wakarudi Dar es Salaam kisha wakaenda Tabora kwenye Mkutano Mkuu wa TANU wa 1958.
Katika mkutano wa Tabora Mwalimu akawahakikishia wanachama wa TANU kuwa TANU itaingia kwenye Kura Tatu na Wazungu wake na Waasia wake wote wanaunga mkono TANU.
Ilikuwa ndani ya Parish Hall ndipo Mwalimu Nyerere alipotoa hotuba iliyobadili mwelekeo wa wanachama wa TANU wa kugomea Uchaguzi wa Kura Tatu na kukubali kushiriki.
TANU ikaja na kauli mbiu mpya kututa ile kwa kwanza, ''Tuingie Kura Tatu Tuiondoe Kura Tatu.''
Sasa angalia waasisi wa nchi hii walivyokuwa na busara.
Bila ya kujali dini zao Mwalimu Nyerere na Amos Kisenge walishiriki dua Mnyanjani dua iliyoongozwa na kufanywa na masheikh kuiombea TANU ushindi.
Ukweli ni kuwa Mwalimu alikuwa mzoefu wa haya kwani kila alipokwenda alikutana na dua ndani ya TANU.
Wanachama wa TANU wakafanya mkutano Tabora ndani ya Ukumbi wa Kanisa Katoliki (Parish Hall) na hapakuwa na ukinzani kutoka kwa Waislam kwa nini mkutano huo muhimu ufanyike pale.
Leo tumefikaje katika hali hii ya chuki inayoonekana hivi sasa?
Ukisikia anatajwa Mwarabu ni uoga tu lakini aliyekusudiwa hapo ni Muislam.
CCM ina wajibu mkubwa sana wa kusomesha historia ya kweli ya uhuru wa Tanganyika.
Huenda hawa wasiojua wapi nchi hii ilikotoka wakabadilika.
Halikadhalika huenda ikatusaidia kuleta utangamano na kurejesha msingi wa mapenzi ulipobomolewa baada ya uhuru kupatikana mwaka wa 1961.
PICHA: Jengo la Parish Hall nje na ndani, Mnara wa Julius Nyerere wa Kumbukumbu ya Kura Tatu, picha ya Mwalimu Nyerere na Hemed Mashaka wakati wa Mkutano wa Kura Tatu.
Laiti kama si Sheikh Abdallah Rashid Sembe wa Tanga kukubali kuzungumza na mimi historia ya Kura Tatu isingejulikana kwa ukamilidu wake.
Waliokuwa wanaojua mkutano wa siri uliofanyika Tanga walikuwa wao viongozi wa Tanga, Mwalimu Nyerere na Amos Kisenge peke yao.
Bahati mbaya Mwalimu Nyerere hakupenda kueleza historia yake katika mengi yaliyofanywa na viongozi wenzake wa TANU wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika.
Historia hii muhimu sana katika kjupigania uhuru wa Tanganyika ingepotea na ikawa inajulikana kijuujuu kama ilivyokuwa historia ya chama cha TANU chenyewe.
Historia ya Kura Tatu nimeieleza kwa kirefu katika kitabu cha Abdul Sykes (1998) na kwa ushawishi wa mchapa vitabu mmoja kutoka Kenya akaniomba nimpatie mswada wa kitabu cha historia hii achape kitabu makhsusi kwa kaudhimisha miaka 50 ya Azimio la Busara mwaka wa 2008.
Kazi hii niliifanya na ilikuwa mapendekezo ya mchapaji huyu kitabu hiki kiandikiwe utangulizi na Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Jinsi alivyothamini historia hii mchapaji huyu alikuwa amepanga kuchapa nakala chache maalum kwa ajili ya viongozi wa nchi.
Kitabu kilichapwa lakini bila ya kuandikiwa utangulizi.
Kwa ajili hii nakala zile maalum kwa watu maalum hazikuchapwa.
Kitabu hiki kikafa kabla ya kuzaliwa lakini kilipotoka chote kilinunuliwa kwa haraka sana na sasa ni katika vitabu vinavyoitwa, ‘’out of print,’’ yaani vimekwisha sokoni havipatikani hadi vichapwe upya.
Kitabu hiki ni cha pili katika vitabu vyangu viwili vilivyochapwa na na ''publishers'' wa Kenya vinavyohusu historia ya uhuru wa Tanganyika.
Bahati mbaya sana vitabu hivi vyote viwili havikupata mafanikio Tanzania.
Havikupendwa.
Nimepokea picha ya Parish Hall Tabora palipofanyika Mkutano wa TANU wa Mwaka wa 1958, mkutano uliokuja kufahamika kama Mkutano wa Kura Tatu kwa kuwa TANU ilikuwa inajadili agenda nyeti sana ya Uchaguzi Mkuu wa kwanza kuchagua wajumbe watakaoingia katika Baraza la Kutunga Sheria (LEGCO).
Nikiwa naiangalia picha hii fikra nyingi zilipita kichwani kwangu.
Nilikuwa nawaza nchi hii ilikotoka na historia yake ya umoja wa wananchi wake na jinsi historia ilivyopotoea ikawa haijulikani.
Nachelea kuifanya makala hay kuwa ndefu sana kwa hiyo nitaeleza jambo hili ninalokusudia kwa kifupi.
Mwalimu Nyerere na Amos Kisenge walikwenda Tanga kuonana na uongozi wa TANU kutafuta kuungwa mkono kwa agenda ya TANU kuridhia kushiriki katika Kura Tatu jambo ambalo wanachama walikuwa wanapinga kiasi kuja na kauli mbiu, ''Kuingia Kura Tatu ni Sawa na Mtu Kujipaka Kinyesi Chake.''
Sababu ya upinzani huu ni yale masharti ya kupiga kura na masharti ya mpigiwa kura.
Mpiga kura alitakiwa awe na elimu ya darasa la 12 (wakashudha hadi darasa la 10), awe na kipato cha Pound za Kiingereza 400 kwa mwaka, awe na kazi ya ‘’kueleweka’’ na ampigie kura Mzungu, Muasia na Mwafrika.
Wanachama wengi wa TANU walikuwa Waislam na ukoloni uliwanyima elimu kwa kuwa elimu ilikuwa ikitolewa na wamishionari kwa kushirikiana na serikali ya Kiingereza.
Masharti haya yaliwatoa katika kupiga kura na halikadhalika kupigiwa kura kuingia katika LEGCO.
Lakini hili halikuwa likisemwa bayana.
TANU ilikuwa na hofu kubwa na hisia za dini ndani ya chama kwa kuchelea kuwagawa wananchi.
Hukumu yake kwa mwanachama atakaekiuka sharti hili ni kufukuzwa chama.
Wanachama wa TANU waliweka msimamo wao tu kuwa hawatashiriki katika uchaguzi wa Kura Tatu bila ya kueleza hayo.
Sheikh Suleiman Takadir Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa TANU akawa kiongozi wa kupinga TANU kuingia katika Kura Tatu.
Katibu Mkuu wa TANU Zuberi Mtemvu ns yeye pia alikuwa katika wapinzani wa Kura Tatu.
Majimboni kote Dodoma, Lindi, Tabora, Tanga, Kanda ya Ziwa hali ilikuwa ni hivyo.
Rais wa TANU Mwalimu Nyerere kuona hali hii ndiyo akaamua kwenda Tanga kuzungumza na uongozi wa TANU wa akina Mwalimu Kihere, Abdallah Rashid Sembe, Hamisi Heri, Mohamed Kajembe kwa kuwataja wachache kutafuta msaada kuwezesha TANU kushiriki katika Kura Tatu.
Mkutano wa Tanga ulikuwa mzito sana lakini hatimae walikubaliana kuwa lazima TANU ishiriki na wakaweka mikakati ya ushindi ndani ya chama kuwashinda wapinzania wa Kura Tatu na nje ya chama kushinda hila za Waingereza na chama chao cha United Tanganyika Party (UTP).
Baada ya kumaliza kikao hiki viongozi wa TANU Tanga wakamwambia Nyerere kwa kuwa hili jambo ni kubwa lazima ifanyike dua kumuomba nusra ya Mwenyezi Mungu.
Leo ukieleza kuwa Qur'an ilikuwa ikitangulia kusomwa katika mikutano ya TANU hakuna atakaeamini.
Kulikuwa na hofu kubwa kuwa kama hawatakufikia muafaka Tabora TANU itameguka vipande viwili na kuna hatari Julius Nyerere akajikuta yuko peke yake kundi kubwa likabaki na Sheikh Suleiman Takadir na Zuberi Mtemvu na wengine.
Dua hii ilifanyika kijiji cha Mnyanjani nje kidogo ya Tanga na Mwalimu Nyerere na Amos Kisenge walishiriki.
Kisomo kilifanyika usiku na kumalizika alfajir.
Mwalimu na Kisenge wakarudi Dar es Salaam kisha wakaenda Tabora kwenye Mkutano Mkuu wa TANU wa 1958.
Katika mkutano wa Tabora Mwalimu akawahakikishia wanachama wa TANU kuwa TANU itaingia kwenye Kura Tatu na Wazungu wake na Waasia wake wote wanaunga mkono TANU.
Ilikuwa ndani ya Parish Hall ndipo Mwalimu Nyerere alipotoa hotuba iliyobadili mwelekeo wa wanachama wa TANU wa kugomea Uchaguzi wa Kura Tatu na kukubali kushiriki.
TANU ikaja na kauli mbiu mpya kututa ile kwa kwanza, ''Tuingie Kura Tatu Tuiondoe Kura Tatu.''
Sasa angalia waasisi wa nchi hii walivyokuwa na busara.
Bila ya kujali dini zao Mwalimu Nyerere na Amos Kisenge walishiriki dua Mnyanjani dua iliyoongozwa na kufanywa na masheikh kuiombea TANU ushindi.
Ukweli ni kuwa Mwalimu alikuwa mzoefu wa haya kwani kila alipokwenda alikutana na dua ndani ya TANU.
Wanachama wa TANU wakafanya mkutano Tabora ndani ya Ukumbi wa Kanisa Katoliki (Parish Hall) na hapakuwa na ukinzani kutoka kwa Waislam kwa nini mkutano huo muhimu ufanyike pale.
Leo tumefikaje katika hali hii ya chuki inayoonekana hivi sasa?
Ukisikia anatajwa Mwarabu ni uoga tu lakini aliyekusudiwa hapo ni Muislam.
CCM ina wajibu mkubwa sana wa kusomesha historia ya kweli ya uhuru wa Tanganyika.
Huenda hawa wasiojua wapi nchi hii ilikotoka wakabadilika.
Halikadhalika huenda ikatusaidia kuleta utangamano na kurejesha msingi wa mapenzi ulipobomolewa baada ya uhuru kupatikana mwaka wa 1961.
PICHA: Jengo la Parish Hall nje na ndani, Mnara wa Julius Nyerere wa Kumbukumbu ya Kura Tatu, picha ya Mwalimu Nyerere na Hemed Mashaka wakati wa Mkutano wa Kura Tatu.