Askofu Kilaini: Nyerere alikuwa Mtu Mwema. Mwana wa Kanisa, Baba wa Taifa na mwanadamu mwenye harufu ya Utakatifu

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,806
11,968
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akishiriki Misa Takatifu ya kumuombea Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere inayofanyika Kwenye Kanisa Kuu Katoliki Jimbo la Bukoba Mjini Mkoani Kagera leo tarehe 14 Oktoba, 2022



Misa hii inayoongozwa na Mhashamu Askofu Methodius Kilaini imehudhuriwa pia na viongozi wakuu wa Serikali akiwemo Makamu wa Rais, Mawaziri, Wakuu wa mikoa, Spika mstaafu Mhe. Anne Makinda, familia ya Hayati JK Nyerere pamoja na watu wengine wenye mapenzi mema.

Askofu Methodius Kilaini-Msimamizi wa Kitume Jimbo la Bukoba
Amesema kuwa Mwalimu Nyerere alisimama msitari wa mbele katika kupambania haki na uhuru wa Afrika, alifundisha kwa maneno na mifano yake mema.

Amesema kwenye mwaka huu tunapokumbuka miaka 23 ya kifo chake na pia miaka 100 ya kuzaliwa kwa mwana huyu wa Kanisa, ni muhimu kukumbuka maneno aliyotoa kwenye mojawapo ya hotuba zake kuwa hakuacha kubeba vitabu viwili maisha yake yote ambayo ni kitabu cha azimio la Arusha na Biblia takatifu. Hii inaonesha kuwa alikuwa ni mtu aliyeishi siasa na maisha ya Mungu.

Alikuwa mtu wa kanuni za maadili na mcha Mungu, mwanasiasa mzuri ambaye watanzania wanamuita Baba wa taifa na Kanisa likimuita mwanadamu mwenye harufu ya Utakatifu.

Aliishi maisha ya kawaida na uduni, mtu aliyeapa kutokupumzika hadi Afrika yote ibaki huru, kuanzia Afrika Kusini ya ubaguzi wa rangi hadi Angola.

Nchini Tanzania aliunganisha makabila 130 yenye dini na rangi tofauti kuwa ndugu wanaopendana. Aliheshimiwa ulimwenguni kote.

1665730488399.png

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Rais Mhe. Philip Isdor Mpango, viongozi wengine wa Chama, Serikali, pamoja na Waumini wa Kanisa hilo wakiwa kwenye Misa Takatifu

Akiwa na umri wa miaka 63 aliamua kustaafu akiamini kuwa mamlaka ni Amana kutoka kwa Mungu. Hii ni tofauti kabisa na viongozi wengine wa kiafrika wa miaka hiyo.

Kuwa mtakatifu haimaanishi kuwa hautendi dhambi kabisa. Nyerere hakuwa malaika, alikuwa binadamu wa kawaida aliyetenda dhambi. Hata Mt. Petro alimkana Yesu, kisha akafanywa kuwa Mkuu wa kanisa. Alikuwa mkosefu, lakini alikiri makosa yake, mengine hadharani.

Tuendelee kumuombea apumzike kwa amani.

Philip Mpango-Makamu wa Rais
Nawaomba watanzania wote tuendelee kumuombea mama Maria Nyerere ili apate uzee mtakatifu na afya njema.

Tumesikia sifa nyingi hapa baba Kilaini akizielezea, toka uhuru alisisitiza sana uhuru na umoja. Tunamshukuru Mungu sana watanzania sisi bado ni wamoja, tuendelee kushikamana. Alisisitiza sana amani na kweli aliitafuta hapa nchini na tunajisifu kuwa kisiwa cha amani, na nchi zingine za Afrika. Tusibweteke.

Alisisitiza sana uhuru na kazi, hili ni jambo la muhimu sana. Lazima tuendelee kufanya kazi ili kuleta maendeleo. Ni lazima tufanye kazi, na lazima kazi iendelee.

Baba wa taifa alichukia sana rushwa, sasa sisi viongozi tunatenda haki, hatuwadai rushwa wanyonge? Nakumbuka baba wa taifa aliwahi kusema mtu anayechukua rushwa yafaa atandikwe viboko, Tanzania leo hakuna rushwa? Wanyonge wanapata haki yao? Ni jukumu letu sote, viongozi na wasio viongozi.

Alisisitiza sana kuhusu elimu na sisi tuliopata elimu tuliambiwa tunao wajibu wa kurudisha kwenye nchi yetu kile tulichopata. Nawaomba sana vijana wa kitanzania mnapokuwa chuo, mfanye bidii ya kusoma. Bado tunahitaji wataalamu wa kila aina.

Na sisi ambao tunatumika katika taasisi mbalimbali za Umma na Serikali kuu tufanye kazi kwa uadilifu, Msikwapue mali za umma, ni za wanyonge.

1665730359018.png

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Makamu wa Rais Mhe. Philip Isdor Mpango Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Bukoba Methodius Kilaini, Mapadri pamoja na viongozi mbalimbali
 
Kanisa Katoliki.... Samia Muislam mwenye msimamo mkali wa Kizenj lkn naam kaingia kwa Bwana Yesu, safi sana nchi yetu maana na bwana yule alikuwa anavaa balagashia anaingia kwa wale jamaa mpaka aliwachangishia swadakar ya kujenga Masjid..mpaka alimuomba Mmorocco kujenga msikiti...


Taifa lenye amani..safi sana Mhe. Rais
 
Hakuna shida yeyote isipokuwa kuna baadhi ya mambo hatashiriki kwa ibada za kikatioliki mfano kupokea ekaristi nk.
 
Ibada ya misa hii ya wafu ya Kikatoliki kama ingalifanyika kule Butiama, sehemu alipozaliwa na hatimaye kuzikwa Hayati Mwl. J.K Nyerere ingalikuwa ni jambo la heri zaidi. Kusafirisha familia, viongozi wa kitaifa na watu wengine maarufu kwenda kuhudhuria misa hiyo huko Kagera ni kujiingiza tu katika gharama zisizokuwa na umuhimu wowote ule ambazo pia zinazoweza kuepukwa.
 
Inaelekea ule mchakato wa kumfanya Nyerere mtakatifu bado unaendelezwa na Kanisa Katoliki.

Japo, nilikuwa nikiupinga mwanzo, lakini baada ya kujua maisha ya watakatifu wengine yalikuwaje, ndipo nikagundua nilikuwa nakosea.

Mwenye kuyajua makosa ya mwanadamu na kuyasamehe ni Mungu pekee, kuleta ujuaji kwenye haya mambo ni sawa na kuingilia kazi isiyonihusu.
 
Hivi huwa tunamuombea nini mtu ambaye mema au mabaya yake yamekwishaandikwa, kwanini tusiitumie nafasi hiyo kufanya wema sisi wenyewe? Je, sisi ni wema kiasi gani mpaka tuweze kuwaombea wenzetu?
Anzisha dini yako na wengine waache na imani zao
 
Ibada ya misa hii ya wafu ya Kikatoliki kama ingalifanyika kule Butiama, sehemu alipozaliwa na hatimaye kuzikwa Hayati Mwl. J.K Nyerere ingalikuwa ni jambo la heri zaidi. Kusafirisha familia, viongozi wa kitaifa na watu wengine maarufu kwenda kuhudhuria misa hiyo huko Kagera ni kujiingiza tu katika gharama zisizokuwa na umuhimu wowote ule ambazo pia zinazoweza kuepukwa.
Khaa! Sasa hao viongozi wa kitaifa wanaishi Butiama? Si lazima wangesafiri kutoka Dar, Dom na kwengine to Butiama! Kuna mambo mengine ya kitaifa tusipende kuyajengea hoja hasi. Hili ni tukio kubwa kuhusu Baba wa Taifa letu.🙏🙏🙏
 
Nyerere - Mkatoliki aliye lelewa katika misingi ya Kanisa
Magufuli - Mkatoliki - alitaka kuwa padri

🙄 Mtoto umeleavyo ndivyo akuavyo
 
Inaelekea ule mchakato wa kumfanya Nyerere mtakatifu bado unaendelezwa na Kanisa Katoliki...
Huo mchakato wauache tu, maana viongozi wengi hawaishi maisha manyoofu wanapokuwa wanatawala.

Wakati mwingine hawatendi haki na matendo mengine mabaya ambayo hatuyaoni sisi wanaotutawala. Sisi huwa tunaangalia ya nje tu lakini MUNGU anakusanya data zetu za kila siku mpaka unapokufa.

Sasa kama kuna doa lolote wakati wa maisha yako hata kama ulikuwa unaishi vizuri kwa mtazamo wa watu wanaokuona wakati ya gizani hawayajui jehenamu inakuhusu.

Kwa MUNGU hakuna kupindishapindisha kama majaji wetu tulionao. Kule unaletewa screen ya maisha yako yote mazuri na mabaya yako unapewa hukumu yako stahiki kulingana na matendo yako.

Tumepewa akili na utashi, kuamini au kutoanini. Tengeneza maisha yako ya kimbingu ungali mzima kwa matendo mema kwa watu na kumwamini MUNGU wako.
 
Huo mchakato wauache tu,maana viongozi wengi hawaishi maisha manyoofu wanapokuwa wanatawala. Wakati mwingine hawatendi haki ...
Hilo aachiwe Mungu mwenyewe na kanisa, maandiko yanasema usihukumu ili nawe usije kuhukumiwa.
 
Hivi huwa tunamuombea nini mtu ambaye mema au mabaya yake yamekwishaandikwa, kwanini tusiitumie nafasi hiyo kufanya wema sisi wenyewe? Je, sisi ni wema kiasi gani mpaka tuweze kuwaombea wenzetu?
Mkuu upo, Ulipotea Sana.

Nakumbuka mada yako ya ufugsji wa kuku kitambo sana
 
Back
Top Bottom