UJAMAA: Mfumo rafiki kwa maendeleo ya Tanzania. China imeendelea kwa sababu ya ujamaa uliopo mpaka sasa

KARLO MWILAPWA

JF-Expert Member
Apr 10, 2019
2,590
4,601
Watanzania tuna kasumba ya kuuangalia ujamaa kwa jicho la ubepari na kuona ujamaa ni mfumo usio na maslahi yeyote kwa jamii. Vipi kuhusu ubepari unatengeza matabaka ndani ya jamii, una maslahi gani? Kushindwa kuutazama ujamaa kama ujamaa na badala yake ukatumia jicho la kipebari kuutazama ujamaa, hapo utaona kile usichokuwa nacho ni bora Zaidi kuliko ulichonacho( kwa sababu ulichonacho umekizoea)

Tunapozungumzia ujamaa duniani, tunazungumzia falsafa za Karl Marx na nchi mfano iliyofanikiwa kukuza na kuendeleza ujamaa kufikia mafanikio ya juu kabisa ni China. Ni wachache sana baina ya watanzania walioisoma historia halisi ya China, wengi historia ya china wanaisoma mitandaoni ambayo si historia ya China kweli ila ni ya Mmarekani(google na internet ni marekeni) hivyo Marekani inaweza kuitengeneza historia ya china kwa kadiri inavyojisikia. Si historia ya China tu bali hata ya Afrika inaweza kuitengeneza atakavyo.

Kusema Ujamaa hauna manufaa, mmeona China walichofanya ndani ya muda wa miaka 30 walipotoa azimio la maendeleo ya China miaka ya 1980? China leo imekuwa great power na sababu ni kuendeleza na kudumisha historia ya mchina hususani kuendelea na mfumo wa kijamaa.

Ni mfumo ambao china imeona unafaa kwa maendeleo na imethibitika ni kweli unafaa sana.
Leo mtanzania ukimuuliza CHINA ni mbepari au mjamaa? Karibu 80% watakuambia China ni mbepari, ni kwa sababu wanauangalia ujamaa kama ubepari na wameathiriwa na historia za mitandaoni ya ujamaa. Kama nilivyokwisha kusema hapo awali, mitandao na google ni mmarekani hivyo marekani itatumia kila njia kuusema vibaya ujamaa ili usienee na kuwa tishio la ubepari. Hawataki kuamini kuwa ujamaa unaweza kujenga uchumi imara na wanaogopa ujamaa unaweza kuwa tishio la ubepari.

Ili kujiridhisha ukweli wa nisemayo, kitabu cha XI JIPING- THE GOVERNANCE OF CHINA kimeeleza kila kitu na mfumo ambao china unatumia ambao ni SOCIALISM WITH CHINESE CHARACTERISTICS. Kama Rais wa China na Katibu mkuu wa CPC ( chama pekee kikubwa china) anasema ataiongoza CHINA katika ujamaa, inakuwaje mbepari aseme china ni mbepari? Hii ni hofu ya ubepari dhidi ya ujamaa.

Katika kitabu hicho XI JIPING anaendelea kusema kwamba wataendelea kuwa na mfumo wa vyama vingi kwa lengo la kuendeleza na kukuza demokrasia. Hii kauli inathibisha uongo wa mabepari na washirika wake kuwa ujamaa hakuna demokrasia. Kama demokrasia ni vyama vingi, China ina demokrasia ya mfano lakini CPC ndio chama kikuu kama ilivyo CCM kwa Tanzania.

China hakutaka kujiingiza mzimamzima katika mfumo wa kibeberu ila alikuwa anatafuta njia yake ya kupita kwa kuuboresha mfumo wa kijamaa ambao SOCIALISM WITH CHINESE CHARACTERISTICS ndio mfumo wao na ni mpya kabisa. Njia ambayo wamepita ni salama kwa maendeleo yao.

Tanzania tunaweza kujifunza kitu kutokea China, mfumo wa kibeberu umekomaa sana kiasi cha kufanya nchi za Afrika kushindwa kuendana nao. Turudi kwenye historia yetu na kurekebisha falsafa za mfumo wetu wa zamani kama walivyofanya China, Nina hakika maendeleo yatakuja kwa kasi sana. Ninaamini siku moja Afrika ikisimama na kupita njia yake nje ya ubepari na ujamaa au kufuata ujamaa kwa sababu ni mchanga na hujakomaa sana, ndio siku ubepari utakufa.

Msiangalie ujamaa kwa kuiangalia Korea Kaskazini, ule ni udikteta. Uangalie ujamaa wa China ambao umeibadilisha China kwa muda mfupi sana na kuendeleza historia ya China.
 
China ni Mabepari wanaosimamiwa na Chama cha kikomunisti. Kuwepo na mfumo wa chama kimoja cha siasa si ishara ya ujamaa. Unaweza kututofuatishia Kanuni za kibepari na zile za kijamaa na uoneshe China ya sasa inafuata kanuni zipi?
 
China ni Mabepari wanaosimamiwa na Chama cha kikomunisti. Kuwepo na mfumo wa chama kimoja cha siasa si ishara ya ujamaa. Unaweza kututofuatishia Kanuni za kibepari na zile za kijamaa na uoneshe China ya sasa inafuata kanuni zipi?
Unachosema ni chako , mimi nimesoma kwenye kitabu cha THE GOVERNANCE OF CHİNA CHA Xİ JİPİNG , rais wa sasa wa china.
 
unachosema ni chako , mimi nimesoma kwenye kitabu cha THE GOVERNANCE OF CHİNA CHA Xİ JİPİNG , rais wa sasa wa china.
Ukiona mtu anachomoa hela kwenye mfuko wa mtu mwingine bila ridhaa yake, wewe utahitaji mchomoaji ndiye akwambie kwamba anaiba ama haibi? Yaani hicho kitabu ndicho kina kanuni za kibepari ama ujamaa?

Umeleta mada kwamba China siyo nchi ya Kibepari bali ni ya kijamaa, na kwa kuwa Kila kitu kina kanuni zake ili kitambuliwe,sasa wewe weka kanuni za kijamaa na kibepari unazozifahamu wewe halafu tuone kama China ni wajamaa ama ni Mabepari.
 
Hao Wachina uchumi wao unaendeshwa kibepari kwani makampuni mengi ya Ulaya yamewekeza huko sababu ya soko kubwa ila ujamaa walionao ni kwenye siasa tu kwa chama cha kikomunisti kushika hatamu.
 
Hivi bado kuna akili zinazotetea ujamaa tu?

Nyerere mwenyewe alikufa kakubali alikosea,then wewe bado unasema eti unafaa.

Hebu acha uzembe,copy and paste USA capitalism wrapped up in a vibrant democracy and then we are Singapore!
 
Ukiona mtu anachomoa hela kwenye mfuko wa mtu mwingine bila ridhaa yake, wewe utahitaji mchomoaji ndiye akwambie kwamba anaiba ama haibi? Yaani hicho kitabu ndicho kina kanuni za kibepari ama ujamaa?

Umeleta mada kwamba China siyo nchi ya Kibepari bali ni ya kijamaa, na kwa kuwa Kila kitu kina kanuni zake ili kitambuliwe,sasa wewe weka kanuni za kijamaa na kibepari unazozifahamu wewe halafu tuone kama China ni wajamaa ama ni Mabepari.
Hizo kanuni za kutambua huu ni ubepari au ujamaa , anazo mmarekani tu? kitabu kimeandikwa na Xİ JİPİNG, Rais wa China wa sasa na mpaka kifo. ni kitabu kinachoeleza njia ambayo atatumia kuiongoza China
 
hizo kanuni za kutambua huu ni ubepari au ujamaa , anazo mmarekani tu? kitabu kimeandikwa na Xİ JİPİNG, Rais wa China wa sasa na mpaka kifo. ni kitabu kinachoeleza njia ambayo atatumia kuiongoza China
Wapi nimeitaja Marekani? Wewe taja kanuni zinazoutofautisha ujamaa na ubepari ili tuone kama China ya sasa inafuata kanuni za kibepari ama za kijamaa!!
 
Katika kitabu hicho XI JIPING anaendelea kusema kwamba wataendelea kuwa na mfumo wa vyama vingi kwa lengo la kuendeleza na kukuza demokrasia.
Huu upuzi umetoka kwa Musiba? Maana hivyo vyama vingi huko China vipo hewani visikoonekana?

Ndiyo maana huwa anawaita Pumbavu, kumbe mna huu upumbavu vichwani mwenu!!
 
Hizo kanuni za kutambua huu ni ubepari au ujamaa , anazo mmarekani tu? kitabu kimeandikwa na Xİ JİPİNG, Rais wa China wa sasa na mpaka kifo. ni kitabu kinachoeleza njia ambayo atatumia kuiongoza China
Unashindwa kuitetea mada yako?au ulitaka uipost fb?kitu Cha kufanya ni kukimbia mzee.
 
Watanzania tuna kasumba ya kuuangalia ujamaa kwa jicho la ubepari na kuona ujamaa ni mfumo usio na maslahi yeyote kwa jamii. Vipi kuhusu ubepari unatengeza matabaka ndani ya jamii, una maslahi gani? Kushindwa kuutazama ujamaa kama ujamaa na badala yake ukatumia jicho la kipebari kuutazama ujamaa, hapo utaona kile usichokuwa nacho ni bora Zaidi kuliko ulichonacho( kwa sababu ulichonacho umekizoea)

Tunapozungumzia ujamaa duniani, tunazungumzia falsafa za Karl Marx na nchi mfano iliyofanikiwa kukuza na kuendeleza ujamaa kufikia mafanikio ya juu kabisa ni China. Ni wachache sana baina ya watanzania walioisoma historia halisi ya China, wengi historia ya china wanaisoma mitandaoni ambayo si historia ya China kweli ila ni ya Mmarekani(google na internet ni marekeni) hivyo Marekani inaweza kuitengeneza historia ya china kwa kadiri inavyojisikia. Si historia ya China tu bali hata ya Afrika inaweza kuitengeneza atakavyo.

Kusema Ujamaa hauna manufaa, mmeona China walichofanya ndani ya muda wa miaka 30 walipotoa azimio la maendeleo ya China miaka ya 1980? China leo imekuwa great power na sababu ni kuendeleza na kudumisha historia ya mchina hususani kuendelea na mfumo wa kijamaa.

Ni mfumo ambao china imeona unafaa kwa maendeleo na imethibitika ni kweli unafaa sana.
Leo mtanzania ukimuuliza CHINA ni mbepari au mjamaa? Karibu 80% watakuambia China ni mbepari, ni kwa sababu wanauangalia ujamaa kama ubepari na wameathiriwa na historia za mitandaoni ya ujamaa. Kama nilivyokwisha kusema hapo awali, mitandao na google ni mmarekani hivyo marekani itatumia kila njia kuusema vibaya ujamaa ili usienee na kuwa tishio la ubepari. Hawataki kuamini kuwa ujamaa unaweza kujenga uchumi imara na wanaogopa ujamaa unaweza kuwa tishio la ubepari.

Ili kujiridhisha ukweli wa nisemayo, kitabu cha XI JIPING- THE GOVERNANCE OF CHINA kimeeleza kila kitu na mfumo ambao china unatumia ambao ni SOCIALISM WITH CHINESE CHARACTERISTICS. Kama Rais wa China na Katibu mkuu wa CPC ( chama pekee kikubwa china) anasema ataiongoza CHINA katika ujamaa, inakuwaje mbepari aseme china ni mbepari? Hii ni hofu ya ubepari dhidi ya ujamaa.

Katika kitabu hicho XI JIPING anaendelea kusema kwamba wataendelea kuwa na mfumo wa vyama vingi kwa lengo la kuendeleza na kukuza demokrasia. Hii kauli inathibisha uongo wa mabepari na washirika wake kuwa ujamaa hakuna demokrasia. Kama demokrasia ni vyama vingi, China ina demokrasia ya mfano lakini CPC ndio chama kikuu kama ilivyo CCM kwa Tanzania.

China hakutaka kujiingiza mzimamzima katika mfumo wa kibeberu ila alikuwa anatafuta njia yake ya kupita kwa kuuboresha mfumo wa kijamaa ambao SOCIALISM WITH CHINESE CHARACTERISTICS ndio mfumo wao na ni mpya kabisa. Njia ambayo wamepita ni salama kwa maendeleo yao.

Tanzania tunaweza kujifunza kitu kutokea China, mfumo wa kibeberu umekomaa sana kiasi cha kufanya nchi za Afrika kushindwa kuendana nao. Turudi kwenye historia yetu na kurekebisha falsafa za mfumo wetu wa zamani kama walivyofanya China, Nina hakika maendeleo yatakuja kwa kasi sana. Ninaamini siku moja Afrika ikisimama na kupita njia yake nje ya ubepari na ujamaa au kufuata ujamaa kwa sababu ni mchanga na hujakomaa sana, ndio siku ubepari utakufa.

Msiangalie ujamaa kwa kuiangalia Korea Kaskazini, ule ni udikteta. Uangalie ujamaa wa China ambao umeibadilisha China kwa muda mfupi sana na kuendeleza historia ya China.


Si kweli China sio wajamaa kiuchumi kuna makampuni ya US na EU kibao na kuna kampuni binafsi za China. Hakuna nchi imeendelea Duniani na ujamaa kuwa na chama kimoja sio kigezo pekee cha ujamaa. China imekuwa kiuchumi baada ya mabadiliko na kuingia kwenye soko la dunia World market
 
Watanzania tuna kasumba ya kuuangalia ujamaa kwa jicho la ubepari na kuona ujamaa ni mfumo usio na maslahi yeyote kwa jamii. Vipi kuhusu ubepari unatengeza matabaka ndani ya jamii, una maslahi gani? Kushindwa kuutazama ujamaa kama ujamaa na badala yake ukatumia jicho la kipebari kuutazama ujamaa, hapo utaona kile usichokuwa nacho ni bora Zaidi kuliko ulichonacho( kwa sababu ulichonacho umekizoea)

Tunapozungumzia ujamaa duniani, tunazungumzia falsafa za Karl Marx na nchi mfano iliyofanikiwa kukuza na kuendeleza ujamaa kufikia mafanikio ya juu kabisa ni China. Ni wachache sana baina ya watanzania walioisoma historia halisi ya China, wengi historia ya china wanaisoma mitandaoni ambayo si historia ya China kweli ila ni ya Mmarekani(google na internet ni marekeni) hivyo Marekani inaweza kuitengeneza historia ya china kwa kadiri inavyojisikia. Si historia ya China tu bali hata ya Afrika inaweza kuitengeneza atakavyo.

Kusema Ujamaa hauna manufaa, mmeona China walichofanya ndani ya muda wa miaka 30 walipotoa azimio la maendeleo ya China miaka ya 1980? China leo imekuwa great power na sababu ni kuendeleza na kudumisha historia ya mchina hususani kuendelea na mfumo wa kijamaa.

Ni mfumo ambao china imeona unafaa kwa maendeleo na imethibitika ni kweli unafaa sana.
Leo mtanzania ukimuuliza CHINA ni mbepari au mjamaa? Karibu 80% watakuambia China ni mbepari, ni kwa sababu wanauangalia ujamaa kama ubepari na wameathiriwa na historia za mitandaoni ya ujamaa. Kama nilivyokwisha kusema hapo awali, mitandao na google ni mmarekani hivyo marekani itatumia kila njia kuusema vibaya ujamaa ili usienee na kuwa tishio la ubepari. Hawataki kuamini kuwa ujamaa unaweza kujenga uchumi imara na wanaogopa ujamaa unaweza kuwa tishio la ubepari.

Ili kujiridhisha ukweli wa nisemayo, kitabu cha XI JIPING- THE GOVERNANCE OF CHINA kimeeleza kila kitu na mfumo ambao china unatumia ambao ni SOCIALISM WITH CHINESE CHARACTERISTICS. Kama Rais wa China na Katibu mkuu wa CPC ( chama pekee kikubwa china) anasema ataiongoza CHINA katika ujamaa, inakuwaje mbepari aseme china ni mbepari? Hii ni hofu ya ubepari dhidi ya ujamaa.

Katika kitabu hicho XI JIPING anaendelea kusema kwamba wataendelea kuwa na mfumo wa vyama vingi kwa lengo la kuendeleza na kukuza demokrasia. Hii kauli inathibisha uongo wa mabepari na washirika wake kuwa ujamaa hakuna demokrasia. Kama demokrasia ni vyama vingi, China ina demokrasia ya mfano lakini CPC ndio chama kikuu kama ilivyo CCM kwa Tanzania.

China hakutaka kujiingiza mzimamzima katika mfumo wa kibeberu ila alikuwa anatafuta njia yake ya kupita kwa kuuboresha mfumo wa kijamaa ambao SOCIALISM WITH CHINESE CHARACTERISTICS ndio mfumo wao na ni mpya kabisa. Njia ambayo wamepita ni salama kwa maendeleo yao.

Tanzania tunaweza kujifunza kitu kutokea China, mfumo wa kibeberu umekomaa sana kiasi cha kufanya nchi za Afrika kushindwa kuendana nao. Turudi kwenye historia yetu na kurekebisha falsafa za mfumo wetu wa zamani kama walivyofanya China, Nina hakika maendeleo yatakuja kwa kasi sana. Ninaamini siku moja Afrika ikisimama na kupita njia yake nje ya ubepari na ujamaa au kufuata ujamaa kwa sababu ni mchanga na hujakomaa sana, ndio siku ubepari utakufa.

Msiangalie ujamaa kwa kuiangalia Korea Kaskazini, ule ni udikteta. Uangalie ujamaa wa China ambao umeibadilisha China kwa muda mfupi sana na kuendeleza historia ya China.


Ww utakuwa ni mzee, na kama ni kijana basi unatokea kwenye dhiki kubwa. Watu wa makundi hayo ndio wenye mitazamo ya kijamaa.
 
Ubepari ni mfumo wa mtaji sio siasa ni mfumo wa kiuchumi. Sasa unaongelea mambo ya siasa
Ujamaa na Ubepari ni falsafa za kuendeshea uchumi zinazosimamiwa na itikadi za kisiasa. Lakini falsafa hizi za kiuchumi zina kanuni zake zisizofanana zinazosimamia uzalishaji na ugawanaji wa mapato kwa kigezo ni nani anamiliki njia Kuu za uzalishaji kati ya watu binafsi ama umma kwa ujumla.
 
Back
Top Bottom