Uislamu ungeacha kuambatana na ukatili ingelikuwa dini moja safi sana

Mhaya

JF-Expert Member
Aug 20, 2023
1,658
4,866
Uislamu ingekuwa Dini nzuri sana endapo baadhi ya Tabia zinazohusushwa na Dini zingeachwa. Siongelei huu uislamu wa gongo la mboto, waislamu jina. Naongelea wakulungwa wenyewe.

Mfano: Tabia ya kufinya haki za wanawake, kwenye dini ya uislamu mwanamke ni kiumbe kinachopewa daraja la chini sana kwenye karibia baadhi ya mambo kwenye familia hadi jamii, kuanzia kwenye maamuzi na utendaji wa kazi, ambapo mwanaume amejisimika ufalme kwenye kila mambo.

Nchi nyingi zinazoongozwa na Uislamu zinapinga uongozi wa wanawake, kuendesha magari japo juzi kati ndipo walianza kuruhusu, mtindo wa maisha na mambo kadha wa kadha yanayowahusu wanawake.

Kuchukua sheria mkononi: hapa siongelei puchu au mgalala, la ashah, hapa nazungumzia sheria nyingi za Uislamu zinaamuru kujichukulia sheria mkononi endapo mtu ataenda kinyume na matakwa ya uislamu mfano; mtu akitaka kuhama Dini ya kiislamu anaweza kuuliwa, mtu akidhini au kuchepuka apigwe mawe mpaka kufa, ukimkubatia mwanamke si wako uchapwe viboko 99.

Juzi tu umeona mchezaji mpira Cristiano Ronaldo akimkumbatia msichana mlemavu baada ya kumletea zawadi ya picha hiko Iran, lakini serikali ya Iran inayoendeshwa chini ya uislamu ikaamuru Ronaldo akirudi tena Iran atandikwe viboko 99 kwa kosa la kumkumbatia yule dada mlemavu kama shukurani. Yapo mambo mengi ya kujichukulia sheria mkononi ya kuua au kumdhuru mtu endapo hatafata sheria za Uislamu.

Wazee wa Suicide mission: Hapa sizungumzii ile Movie ya Suicide Squad ya Will Smith, hapa nazungumzia wale wakulungwa wa Imani kali wanaoanzisha vikundi vinavyojulikana kama vikundi vya Jihad kama Islamic State (IS), Balochistan Liberation Army (BLA), Al-Qaida, Al-shabab, Jumaat Nusrat Al-Islam wal Muslimeen (JNIM), Islamic State Khorasan (ISK), Islamic State Sinai (ISS) na vikundi vya namna hiyo huko Africa magharibi (Islamic State West Africa) kama Boko Haram na vinginevyo vya imani kali ambavyo lengo lao ni kusambaza Uislamu kwa nguvu na kupambana na serikali zisizo za kidini.

Hawa wazee wanajulikana kwa mashambulizi yao dhidi ya raia na serikali ikiwemo majeshi, na kuua watu bila sababu zenye mashiko, wengine wamejizolea umaarufu kwa kujitoa muhanga na kuua watu wengi bila kujali kwamba wanafamilia au hawana. Na pia Al-Qaida walikuwa wanafahamika kwa kuchinja raia wa Kimarekani na wa nchi za Ulaya, kupelekea nchi za Mashariki ya Kati kuogopwa kutembelewa na wageni kutoka nchi nyingine.

Ukijaribu kuwagusia hawa waislam wa Bonyokwa wanakwambia Uislamu unakataza mambo hayo, lakini ukifuatilia kwenye vitabu vyao ukatili wa aina hiyo umeandikwa kwenye kitabu chao kama kuchampa mtu viboko, kuua kama aendani na itikadi za kiislamu na mambo kadha wa kadha.

Hata hawa waislam wa Bonyokwa washukuru tu kwa sababu wanaishi Tanzania na sio nchi ya kidini ila wangekuwa wanaishi huko Iran au Afaghanstan, wangeelewa shoo.

Juzi kati tu ndege ya Marekani ya kijeshi ilivyokuwa inaondoka Afaghanstan, Waafaghan wengi walitaka kuondoka nayo kuonesha hawataki kubaki nchini kwao kupelekea watu wengine kuanguka na kufa, inaonesha hata nchi nyingi za Uarabuni haziruhusu wananchi wao kuondoka hovyo hovyo bila sababu, wanabanwa na kunyimwa passport.

Endapo waislamu wangeacha hayo mambo ya ukatili wangekuwa Dini moja safi sana ulimwenguni.
 
Kwanza Usilamu hauchukuli mwanamke kama kiumbe dhaifu, katika uislamu kila mtu yupo sawa mbele ya mungu, Ila uislamu unasisitiza mwanaume awe kiongozi wa mwanamke na yeye mwanaume ndio awe mtu wa mwisho kwenye kutoa na kuchukua maamuzi.

Pili hizo sheria za kislamu unazosema watu wanajichukulia mkononi zina utaratibu wake wa kutolea hawezi fanya kila muislam, kuna viongozi ambao wapo na wao ndio wenye mamlaka ya kutimiza hizo sheria, na hakuna sheria kwamba ukihama uislamu uuliwe, sijawahi iona hii.

Tatu hayo makundi uliyoyataja yana ajenda zao na hizo nchi tajawa lakini kwa sababu ni waislamu basi inakua kama washapata kivuli cha kujifichia lakini ki uhalisia HAKUNA aya yoyote katika QURAN inayosema unatakiwa utoe roho ya mtu ambae hafuati uislamu, hakuna hicho kitu na jukumu hilo ni la mungu tu

Kuhusu passport na watu wa jamii za nchi za kiarabu kuzuliwa kuondoka nchini kwao hili ni kinyume kwa sababu.
Kwanza waarabu sio watu wa kutembea sana wengi wanapenda kuwa kwao.
Na pia ukifuatilia nchi za Qatar, UAE, SAUDIA ARABIA, PAKISTAN, na nyenginezo wanarai wengi katika nchi kubwa za duniani kama MAREKANI, UK na nchi nyengine za ULAYA.

Mtoa post rudi kafanye ufuatiliaji wa kina alafu lete mrejesho, La sivyo hapa umefananisha asili ya kikundi cha watu wa ania fulani kwa sababu ni dini fulani.
 
Kitu kibaya ni kwamba hujui kuhusu uislamu na huo ndio mtazamo wako ,sikulaumu na ulichoongea hakina ukweli kwa asilimia zote.

Mbaya wengi wanaosma uislamu ndio wanasilimu, uliloongea hapo halina ukweli kabisa zote ni nadharia za kimagharibi.

Uislamu umempa mwanamke cheo hata tunaamini pepo ipo chini ya nyayo ya mama (mwanamke) na sio baba, kuna sehemu inafundisha katikq daraja nne basi tatu anabeba mwanamke katika wazazi(mama na baba) kwamba mama ana daraja 3 na baba ana moja.

Ukienda kweny kusoma hata utume alimpendelea binti ,sasa njoo kweny mirathi ndio utajua yaani mwanamke anapewa mirathi yake ila bado kaka yake anahusika kumlea kwa nguvu zake mpaka atakapoelewa huku akiwa hatumii hata thumni ya mirathi yake (Mwanamke).

Mwanamke huyo ndie ambaye hata mahari anataja yeye na sio mzazi na maamuzi ya kuolewa ni yeye. Mwanamke katika uislamu ukiangalia majukumu ya ndoa hata akizaa akinyonyesha mtoto wako wewe mwanaume unatakiwa kumlipa na hakuna sehemu imeonyesha kwamba mwanamke ni mama wa kufanya kazi za nyumbani. Ni mengi nikikutajia hapa hata nikuambia mwanamke anapewa stare ili kumpa thamni nyie mnasema haki za binadamu ila akitembea uchi ndio uhuru🙄

Hakuna ugaidi na kama hukumu zipo kisheria mbona hata bible imetoa hukumu nyingi ,bible ilisema mwanamke hawezi kuwa kiongozi wala hatakiwi kuuliza swali kanisani ila anaenda kumuuliza mmewe nyumbani 😅😅haya hamyaon?...Sababu uislamu upo practical tukichambua hapa utajua sheria nyingi zinafana ila ukristo umathirika na wazungu ndio maana kwa sababu hata vipedo kanisani havikuhusu na utashangaa sanamu la maria na masister wamevaa hijabu ila waumini hawavai😅

Hakuna hukumu uislamu kama dhambi tunasema haijalishi nan kafanya
 
Mimi ni mkristo ila nauteyea uislam. Uislam kama dini haifundishi ukatili hata siku moja, ila katika imani zote huwa kuna watu unaowaita wakatili, wapo tayari kuua, kutesa kwa sababu ya dini zao, ukristo ukiufuatilia kuna kanisa moja kubwa kuliko yote walikuwa wanachemsha watu kwenye mapipa ya mafuta, walirusha watu kwenye simba wenye njaa, walirusha watu kwenye matanuru,
Uislam ni dini ya haki. Ukiangalia ni watu wangapi hueaendea wakristo kuwaomba msaada na ni watu wangapi huwaendea waislam kuwaomba msaada utakugua jambo.
Sisi wakristo hatuna tunachojivunia
 
Mimi ni mkristo ila nauteyea uislam. Uislam kama dini haifundishi ukatili hata siku moja, ila katika imani zote huwa kuna watu unaowaita wakatili, wapo tayari kuua, kutesa kwa sababu ya dini zao, ukristo ukiufuatilia kuna kanisa moja kubwa kuliko yote walikuwa wanachemsha watu kwenye mapipa ya mafuta, walirusha watu kwenye simba wenye njaa, walirusha watu kwenye matanuru,
Uislam ni dini ya haki. Ukiangalia ni watu wangapi hueaendea wakristo kuwaomba msaada na ni watu wangapi huwaendea waislam kuwaomba msaada utakugua jambo.
Sisi wakristo hatuna tunachojivunia

Wewe si mkristo.
 
Back
Top Bottom