Uhusiano kati ya kiu ya maji na mauti

Uhusiano kati ya kiu ya maji na mauti

Maeneo ya koo ndio inapotoka roho ndio maana mtu husikia kiu kwa koo kukauka
 
KIIMANI:
Roho ya mtu inapoacha mwili huwa Mara nyingi haitaki mtu ashuhudie hivyo anapokutuma kalete hiki au kile(Mara nyingi huwa maji) ni njia/janja ya kukutoa ili uhai umtoke. Ndo maana mara nyingi unapokuwa unarud ndio utakuta anamalizikia kukata roho!.
hapana kabsa je kama amezungukwa na watu wengi inamaana wote watafuata maji??
 
Nafikiri kiu wanayokuwa nayo ni sawa na ile anayoisikia mgonjwa aliyetoka kufanyiwa operation hasa kubwa

Niliwahi kufanyiwa ya namna hiyo ile nimezinduka ile kiu niliyoisikia siyo ya mchezo ni kali sana nilikuwa naomba maji ila hawakunipa mpk baada ya muda kidogo ndiyo nikapewa tena kwenye kifuniko cha maji ya Kilimanjaro tena baada ya kulalamika sana baada ya hapo sikupewa tena na wauguzi wakawapiga biti ndugu hakuna kunipa ni kiu ya hatari hata mate yanakuwa yamekauka kabisa
Dawa za nusu kaputi husababisha kiu kali, usingizi, misuli kutanuka (smooth muscles) pia kukupumbaza usisikie maumivu kwa muda,

Hizi dawa zina deal na mfumo wa fahamu moja kwa moja,
Zinashambulia sehemu moja ambayo huratibu hayo mambo yote kwa wakati mmoja,

Ndio maana ulihisi kiu,
Kunywa maji ni kwenda kinyume na mfumo ndio maana walikuacha dawa iishe kwanza mwilini,

Hiyo ni nusu kifo

Ni kwa uelewa wangu lakini
 
KIIMANI:
Roho ya mtu inapoacha mwili huwa Mara nyingi haitaki mtu ashuhudie hivyo anapokutuma kalete hiki au kile(Mara nyingi huwa maji) ni njia/janja ya kukutoa ili uhai umtoke. Ndo maana mara nyingi unapokuwa unarud ndio utakuta anamalizikia kukata roho!.
Kuna ukweli hapo mkuu
 
Though hatuwezi kuwa na jibu kulingana na experience but we can think about it kufwatana na uelewa, imani n.k, kama kichwa kinavyoeleza si kitu kigeni masikioni mwako au pengine umewahi kushuhudia mwenyewe baadhi ya wagonjwa dakika za mwisho kabla ya umauti kuwafika huwatuma watu wanaowauguza kuwachukulia maji ya kunywa though wengi wao huwa hata hawafanikiwi kuyanywa yale maji, process ya mpaka mtu kutokwa na roho inaambatana na energy kubwa ambayo pengine hupelekea hadi mtu kuhisi kiu; najaribu tu kuwaza je mwenzangu unawaza nini??
Kupitia maji Mola ameumba uhai,yaani kupitia maji uhai huapatikana.

Ila siku yako ya kufa ikifika haichelewi hata sekunde.

Mwisho wa yote Mola ametupa kidogo sana katika elimu ya roho na umauti.

Kifo kinauma asikwambie mtu.
 
Vipi wale wanaokufa usingizini...?

Uchungu ambao huwezi kupiga yowee au kulia kwa uchungu....

Just thinking...
Nakujibu kwa mtindo huu,hivi kwani kila kinacho ongea kina mdomo ?

Au mkono wako na mkono wa birika viko sawa ? Ila yote ni mikono sio ?

Ukitafakari kwa makini maswali utapata jibu la swalo lako.
 
Kwa imani ya dini ya kiislam na mafunzo yake hili jambo limeelezwa. ...kwamba wakati wa kutoka roho mwanadam yeyote hupata kiu kikubwa sana inavyosemekana hata kama ataletewa bahari nzima kwa wakati ule haiwezi kuondosha kiu hile.

Wallahi mungu yupo na nguvu zake tunaziona .....
Umejibu vyema sana bro ?! Kifo kinauma. Ndio maana katika uislamu mtu anapokaribia kukata roho,unatakiwa kumtamkisha maneno,maneno ambayo ni machache sana,ila cha ajabu kwa kile kilevi cha roho inapotoka unakuta anashindwa kutamka maneno mpaka roho ina malizika kutoka.

Kifo ni haki na kila nafsi itaonja umauti.

Kuna wanazuoni wenye elimu kubwa na wingi wa matendo mema wanasema "Lau kama wangejua matendo yanakubaliwa na Mola wetu walau kwa chembe ndogo sana ya ngano,basi wasingetamani kufa"

Yaani uone jinsi gani mauti yanavyouma. Cha msingi tufanye mema kwani hatujui tutakufa lini na wapi tutafia.
 
Nafikiri kiu wanayokuwa nayo ni sawa na ile anayoisikia mgonjwa aliyetoka kufanyiwa operation hasa kubwa

Niliwahi kufanyiwa ya namna hiyo ile nimezinduka ile kiu niliyoisikia siyo ya mchezo ni kali sana nilikuwa naomba maji ila hawakunipa mpk baada ya muda kidogo ndiyo nikapewa tena kwenye kifuniko cha maji ya Kilimanjaro tena baada ya kulalamika sana baada ya hapo sikupewa tena na wauguzi wakawapiga biti ndugu hakuna kunipa ni kiu ya hatari hata mate yanakuwa yamekauka kabisa
Aisee Dada Jirani yangu alifanyiwa operation Kujifungua ... Akahitaji Maji Kasema kiu Sana aisee ... Akapewa Hali ikabadilika ....R.I.P


Mtoto wake now days anatimiza 1 year [emoji31][emoji31]
 
Kupitia maji Mola ameumba uhai,yaani kupitia maji uhai huapatikana.

Ila siku yako ya kufa ikifika haichelewi hata sekunde.

Mwisho wa yote Mola ametupa kidogo sana katika elimu ya roho na umauti.

Kifo kinauma asikwambie mtu.
"Kifo kinauma asikwambie mtu." hapa umeremba as if ushawahi kufariki[emoji4]
 
Nakumbuka nilichezewa rafu mbaya sana kwenye mechi wakati nikiwa nalia nimelala chini nilipatwa na kiu ya maji so niliomba maji kabla hawajanipakia kwenye gari kwenda hospital mshikaji wa karibu alihamaki akisisitiza nisipewe

Baada ya hili tukio nikikutana naye huwa ananiambia bila yeye ningekuwa nishakufa [emoji22]
Mlete uyo jamaa hapa atuambie siri ya maji na kifo
 
Though hatuwezi kuwa na jibu kulingana na experience but we can think about it kufwatana na uelewa, imani n.k, kama kichwa kinavyoeleza si kitu kigeni masikioni mwako au pengine umewahi kushuhudia mwenyewe baadhi ya wagonjwa dakika za mwisho kabla ya umauti kuwafika huwatuma watu wanaowauguza kuwachukulia maji ya kunywa though wengi wao huwa hata hawafanikiwi kuyanywa yale maji, process ya mpaka mtu kutokwa na roho inaambatana na energy kubwa ambayo pengine hupelekea hadi mtu kuhisi kiu; najaribu tu kuwaza je mwenzangu unawaza nini??
hizo movies labda
 
Back
Top Bottom