Uhusiano kati ya kiu ya maji na mauti

Uhusiano kati ya kiu ya maji na mauti

Nakumbuka nilichezewa rafu mbaya sana kwenye mechi wakati nikiwa nalia nimelala chini nilipatwa na kiu ya maji so niliomba maji kabla hawajanipakia kwenye gari kwenda hospital mshikaji wa karibu alihamaki akisisitiza nisipewe

Baada ya hili tukio nikikutana naye huwa ananiambia bila yeye ningekuwa nishakufa [emoji22]
 
SIE watu wa IMAAN unaambiwa process ya kutoka roho sawa sawa na umchukue MBUZI alafu ACHUNWE ngozi yake... akiwa HAI...

pia roho hutoka kwa uchungu wa hali ya juu sana
Hiyo ya kuchunwa ngozi ni kwa waliojaaliwa kifo chema, sijui wanaokufa kiuhalisia ipoje
 
For Catholics this is the moment if you have been reciting your rosary your mother Mary will be there to welcome you in heaven

If you have been reciting our Lady of Sorrows rosary she may be able to console her son on your judgement

If you have been reciting the chaplain of St Michael all the nine angelic choir Sherubin,Serafin ect be there to escort you
 
Kwa elimu ndogo niliyonayo wacha nishare nanyi.

Tuanze na umauti, mtu alimuuliza mtume muhammad(s.a.w) kuhusu uchungu wa umauti unakoje ama unafananaje.. Jibu alisema ni sawa na mtu uchunwe ngozi kuanzia unyayo mpaka utosini, na machungu haya aliyafananisha kwa mbali hakusema ni sawa sawa ila kwa mbali, yanausogelea uchungu wa umauti kwa mbali, kwahyo maana yake ni zaidi ya hapo.
Sasa kama ukijikwaa ukachunika ngozi ikabaki kidogo wakati unaimalizia ukakosea ukaichuna mpaka ile ambayo haijafa ganzi, au kuna vile vigozi viotavyo katika kidole ukikosea kuvichuna nadhani sote tunajua balaa lake, sasa maumivu hayo ndio uyapate kuanzia unyayoni mpaka utosini na hapo ni maumivu ya mbali sio halisi..

Katika umauti imeelezwa mtu anapata kiu isiyoelezeka, hata akapewa maji ya ulimwengu mzima hayawezi kukata kiu hiyo.
 
Nilipata ajali ya gari nikiwa na mjombaangu tuliumia sana ila yeye ndiye aliumia zaidi, alichokuwa anaomba ni maji tu tena anauliza eti mnataka nife ndiyo mnipe maji? Mbn mna roho mbaya hivo hata maji mnaninyima, waokozi hawakuwa na maji na maduka yalikuwa yamefungwa maana ilikuwa alfajiri saa 10 au 11, Mi nilikuwa nasubiri nione mtu analeta maji nimfoke kana kwamba naweza kuamka, nilishaambiwa mgonjwa akiomba maji usimpe.
 
Vipi wale wanaokufa usingizini...?

Uchungu ambao huwezi kupiga yowee au kulia kwa uchungu....

Just thinking...
kifo chochote kina KASHESHE lake... ndio maana wapo wanaokufa wanatoa macho na wapo wanaokufa wamefumba macho.. hizo ni style tu... kwa wanaokufa wakiwa wamelala huwez kuona kwa macho yako hayo bali ni kazi ya IZRAEL... ndio anaifanya na roho hutoka katika kidole gumba cha mguuni.. na kuvutwa taratibu/harakahaka kulingana na matendo yako
 
KIIMANI:
Roho ya mtu inapoacha mwili huwa Mara nyingi haitaki mtu ashuhudie hivyo anapokutuma kalete hiki au kile(Mara nyingi huwa maji) ni njia/janja ya kukutoa ili uhai umtoke. Ndo maana mara nyingi unapokuwa unarud ndio utakuta anamalizikia kukata roho!.
Real myself yamenikuta kifo cha mama yangu mzazi.
Alipokaribia kukata roho akanituma maji nakwenda kuleta maji mpaka narudi tayari siku nyingi.
 
Kwa imani ya dini ya kiislam na mafunzo yake hili jambo limeelezwa. ...kwamba wakati wa kutoka roho mwanadam yeyote hupata kiu kikubwa sana inavyosemekana hata kama ataletewa bahari nzima kwa wakati ule haiwezi kuondosha kiu hile.

Wallahi mungu yupo na nguvu zake tunaziona .....
Umesema kweli
 
Kwa imani ya dini ya kiislam na mafunzo yake hili jambo limeelezwa. ...kwamba wakati wa kutoka roho mwanadam yeyote hupata kiu kikubwa sana inavyosemekana hata kama ataletewa bahari nzima kwa wakati ule haiwezi kuondosha kiu hile.

Wallahi mungu yupo na nguvu zake tunaziona .....
Tena ulevi wa kifo kabisaa
Sakaratul maut
 
Nafikiri kiu wanayokuwa nayo ni sawa na ile anayoisikia mgonjwa aliyetoka kufanyiwa operation hasa kubwa

Niliwahi kufanyiwa ya namna hiyo ile nimezinduka ile kiu niliyoisikia siyo ya mchezo ni kali sana nilikuwa naomba maji ila hawakunipa mpk baada ya muda kidogo ndiyo nikapewa tena kwenye kifuniko cha maji ya Kilimanjaro tena baada ya kulalamika sana baada ya hapo sikupewa tena na wauguzi wakawapiga biti ndugu hakuna kunipa ni kiu ya hatari hata mate yanakuwa yamekauka kabisa
 
kifo chochote kina KASHESHE lake... ndio maana wapo wanaokufa wanatoa macho na wapo wanaokufa wamefumba macho.. hizo ni style tu... kwa wanaokufa wakiwa wamelala huwez kuona kwa macho yako hayo bali ni kazi ya IZRAEL... ndio anaifanya na roho hutoka katika kidole gumba cha mguuni.. na kuvutwa taratibu/harakahaka kulingana na matendo yako
Roho inatolewa kwenye dole gumba?? Dahh hizi Imani zingine bhana taabu kweli.
 
Nina maoni yangu tu sina ujuzi au taarifa rasmi,
Moja roho inapotoka baadhi ya watu huona aibu hivyo hukuondoa ili afe,na ukiondoka ukirudi tayari wa baridi kana kwamba sio dakika ile ile uliyokuwepo(mpa kichogo tu).pili kwa sisi wenye kujua mfumo wa damu,ni kwamba anavyoomba maji ni kwamba damu ishakauka mwilini kwa either kutoka au chumvi au lishe,sasa huhitaji maji ili kuiongezea damu mzunguko.
 
Kuna kitu kinaitwa hypothalamus, kipo ktk ubongo wa mwanadamu,
Kinaratibu matendo yasiyo ya hiari kama vile

1sleep/ usingizi
2.Thirsty/ kiu
3. Vasomotor/ kuratibu kusinyaa na kutanuka kwa moyo

Mtu anayeelekea kufa mapigo yake ya moyo huwa sio ya kawaida hupelekea hypothalamus ku be stimulated,

Hivyo basi kazi zote za hypothalamus zitafanyikr kwa wakati mmoja huku ukitaabika kukata roho,
Kazi hizo ni kama nlizozotaja hapo juu,
Ambspo mtu

Atahisi kiu
Usingizi
Mapigo ya moyo kubsdirika

Mwisho kabisa kifo,


Hayo mambo ya high energy sijui nini rejea principle of conservation of energy,
Kikawaida tunavuta oxygen na kutoa carbondioxide, ukifa unaingia kwenye mchakato mwingine wa kuoza utatoa carbondioxide itatumiwa na mimea mimea itatoa oxygen oxygen watavuta wengine cycle inaendelea
 
Back
Top Bottom