Uhuru wa wachunguzi huru

Uhuru wa wachunguzi huru

P


Ok Kifyatu basi tusubiri uchunguzi ufanywe na vyombo vya dola vya Tz i.e. mtuhumiwa anajichunguza mwenyewe!! na bado tutapata report saafi kabisa isiyoegemea upande wowote!!

Kuhusu Gadafi kwani ni lini Gadafi alikuwa anawindwa na FBI na CIA?
Kama hukujua kuhusu kuwindwa kwa Gadafi na kushambuliwa mara kadhaa na CIA basi wala sina haja ya kuuendeleza huu mjadala nawe.

M-google Gadafi halafu usome ugonvi wake na mataifa ya mangaribi kwanza ndio utajua ninachokizungumzia. Hii mada haimhusu Gadafi.
 
..Ni kweli 100%.

..lakini watu wengi zaidi wanamjua TL kuliko wale wahanga waliokuwa wakiuawa mpaka wakafika 40++.

..labda nikuulize: Je unaweza kutaja majina matatu ya wahanga wa Kibiti na shughuli walizokuwa wakifanya? Unaweza kutoa jibu bila kutafuta kwenye mtandao?

..Sasa jiulize ni Watanzania wangapi wanamfahamu TL pamoja na harakati zake.

..Lakini vilevile inawezekana kwamba wakaazi wa Kibiti wangekuwa na access ya JF kama tuliyonayo sisi huenda wangekuwa na malalamiko na kilio kama hiki tulichokuwa nacho kuhusu utendaji wa vyombo vyetu vya uchunguzi.

..Naamini ukifuata mtiririko huo utaelewa kwanini kumekuwa na taharuki kubwa kuhusu shambulizi la TL kuliko ilivyokuwa wakati wa mauaji ya Kibiti.
Sikatai kwamba TL ni maarufu na habari zake zinauza sana magazeti kuliko wale waliouawa kule Kibiti.

Kinachoniboa ni kuona kuwa inafikia hatua kwamba TL anaonekana ndio mtu pekee ambaye amekutwa na yaliyomkuta.

Wakazi zaidi ya 40 wa Kibiti kutokuwa maarufu sio kigezo cha kufikia hatua serikali inakuwa blackmailed kwa sababu tu ya TL kukoswakoswa kuuliwa. Kila mtu anaonekana mdhambi kwa sababu ya TL lakini nobody cares kuhusiana na uhai wa wananchi wengine!!.
 
Mungu huwa hana muda na watu wajinga kama wewe.

Ungejiuliza kwanza ni kwa nini wengine wakifa wanaitwa marehemu na wengine wanaitwa hayati.

Hoja za kipuuzi kama hizi hata last born wangu wa Nursery school anaweza kukujibu. Inshort wewe ni mjinga.
Mkuu Matola punguza povu. Kwa hiyo wale wa Kibiti ni marehemu na huyu mwingine kama mabaya yangemkuta angeitwa Hayati!!.

Yale yale ya waluguru kumsifia marehemu Mkude kwa kusema eti kafa zuri kwa sababu kagongwa na gari ya balozi!!.

Aliyevipiga marufuku viroba alikuwa na nia njema ya kuzikomboa akili za watu kama mkuu Matola.
 
Tokea Mh. Lissu anusurike kwenye shambulio dhidi ya uhai wake siku ashara na kitu zilizopita, kumekuwepo na sauti kadhaa zinazodai au zinazotaka tukio hilo lichunguzwe na wachunguzi 'huru' kutoka nje ya nchi.

Sababu yake kubwa ni kwamba vyombo vya ndani [ya nchi] vya usalama haviko huru kuweza kufanya uchunguzi huo kwa sababu vyenyewe ndivyo vinavyoshukiwa kupanga na kutekeleza jaribio hilo ili kutimiza matakwa ya mtu au watu wa huko serikalini na kwenye CCM.

Hisia hizo [za kuishuku na kuituhumu] nazielewa. Hivyo watu wanaotaka kuona wachunguzi huru wakichunguza nao nawaelewa.

Ila, kuna vitu vinanitatiza kidogo kuhusu huo u huru wa hao wachunguzi na utayari wa kambi ya Lissu na kambi ya serikali kuyakubali matokeo ya huo uchunguzi wao endapo utatokea.

La kwanza, ni nani atayeingia gharama za hao wachunguzi?

Tuseme CHADEMA na wafadhili wao ndiyo wataingia hizo gharama.

Kama hivyo ndo itavyokuwa, je, hao wachunguzi watakuwa huru kiasi gani ilhali wanalipwa na upande wa mnusurika wa jaribio?

CHADEMA kweli inaweza kuwalipa hao wachunguzi huru halafu hao wachunguzi watoe uchunguzi ambao ni kinyume na madai ya CHADEMA [kwamba serikali kupitia vyombo vyake vya usalama ndiye mhusika]? Kama wataletwa na CHADEMA maana yake ni kwamba wao ni waajiriwa wa hicho chama. Akili yangu haioni ni jinsi gani hao wachunguzi huru wanaweza kutoa matokeo yaliyo kinyume na hisia za watu waliowaajiri.

Je, serikali nayo ipo tayari kweli kuyakubali matokeo ya hao wachunguzi huru ambao huenda wakalipwa na hicho chama pinzani?

Na vipi kwa mfano serikali ikubali ujio wa hao wachunguzi na iingie gharama kwa kazi watayoifanya, je, CHADEMA ipo tayari kuyapokea na kuyakubali matokeo ya huo uchunguzi hata kama yakiwa tofauti na vile wao wadhaniavyo?

Kumbuka, kama serikali ndiyo itayoingia gharama za hao watu maana yake ni kwamba watakuwa wanaitumikia serikali iliyopo madarakani ambayo ni ya CCM.

Kwa mtaji huo hao wachunguzi huru watakuwa wapo huru kiasi gani?

Hili suala ni gumu kwa kweli. Kila ninapowaza na kuwazua sipati majibu.

Sijui nyie wadau mnalionaje hilo suala.

Jumapili njema.
Scotland yard walipochinguza kifo cha Ouko walifadhiliwa na serikali ya Kenya ..walifanya na wakatoa uchunguzi wao..serikali ikaukataa....
 
Kama hivyo ndo itavyokuwa, je, hao wachunguzi watakuwa huru kiasi gani ilhali wanalipwa na upande wa mnusurika wa jaribio?

...

Kwa mtaji huo hao wachunguzi huru watakuwa wapo huru kiasi gani?

Hili suala ni gumu kwa kweli. Kila ninapowaza na kuwazua sipati majibu.

Sijui nyie wadau mnalionaje hilo suala.

Cf.

"Public pressure led President Daniel arap Moi to ask British detectives from New Scotland Yard to investigate Ouko's death.[13]. The following investigation by the Kenyan police was supported by the arrival on 21 February of Detective Superintendent John Troon of Scotland Yard's International Organised Crime Branch, accompanied by two other detectives and a Home Office forensic pathologist" - Robert Ouko (politician) - Wikipedia
 
Huu ugumu unaouweka hapa kuhusu uchunguzi huru ni mwendelezo wako wa kuhakikisha muhusika anayefahamika hatajwi hadharani kwani kwako ni jambo litakalokufedhehesha sana.

Simply huna jipya zaidi ya jitihada zako za kuhakikisha ukweli haufahamiki. Usipoteze muda kile ulichoona ni sahihi kumkuta Lissu kimemkuta full stop.
Mkuu bora umemchana ukweli, hakuna kinachomtatiza hapo zaidi ya kupost unafiki mtupu! nyani ni moja kati ya kiumbe ambae ametanguliza uchama mbele na kusahau utu.
 
Kwanini hiyo akili yako inayokwambia kuwa hauoni namna ambavyo hao wachunguzi huru hawawezi kutoa matokeo ambayo ni kinyume na matakwa ya waajiri wao vile vile pia isikwambie hao wachunguzi huru endapo kama watakafanya biased investigation na kubainika, watakuwa wamejipunguzia credibility hivyo basi hili kuepuka hali hiyo isije ikatokea watajitahidi kufanya uchunguzi wa haki na kuja na majibu sahihi?
 
Walikuja kuchunguza mauaji ya padri. Kinachombwa na CDM sasa ni hao wapelele waje wachunguze vyombo vyetu vya usalama kwa sababu ndivyo vinavyoshutumiwa. Can't do that.
Kama hawahusiki tatizo liko wapi?
 
Swali gani unauliza?jambo ukilijua sana lielezee si tunaelimishana.haya labda mimi niko nyuma kuhusu usalama wa taifa nieleweshe basi.
Usalama wa taifa ndio nguzo kuu ya kuulinda utawala na uongozi wa nchi. Unataka FBI na CIA wauchunguze unavyofanya kazi?
 
Usalama wa taifa ndio nguzo kuu ya kuulinda utawala na uongozi wa nchi. Unataka FBI na CIA wauchunguze unavyofanya kazi?
kwanza ujue ni kwamba wanakuja kuchunguza tukio waliloombwa na kama serikali haihusiki basi haina cha kupoteza.
kama mpaka sasa unafikiri hao FBI na CIA wanasubiri nafasi ya kuombwa kuja ndio watuchunguze basi sawa.
 
kwanza ujue ni kwamba wanakuja kuchunguza tukio waliloombwa na kama serikali haihusiki basi haina cha kupoteza.
kama mpaka sasa unafikiri hao FBI na CIA wanasubiri nafasi ya kuombwa kuja ndio watuchunguze basi sawa.
Una matatizo ya kuelewa.

FBI na CIA ni vyombo vya kijasusi vya Kimarekani. Hawawezi kuichunguza serikali ya Tanzania bila ya kudukua mfumo wetu wa ulinzi na usslama. Wanaweza huchunguza uhalifu mwengine lakini sio vyombo vya ulinzi na usalama wa taifa letu.
 
Waafrika na waarabu bwana! yaani tunafikiri katika njia ileile waliotuchorea wazungu, Sasa hapo kwa UK na US si ndo yale yale.

MIAFRIKA NDIVYO TULIVYO by nyani ngabu.
 
Una matatizo ya kuelewa.

FBI na CIA ni vyombo vya kijasusi vya Kimarekani. Hawawezi kuichunguza serikali ya Tanzania bila ya kudukua mfumo wetu wa ulinzi na usslama. Wanaweza huchunguza uhalifu mwengine lakini sio vyombo vya ulinzi na usalama wa taifa letu.
Unataka kumaanisha nini sasa hasa?kwamba serikali inahusika?
 
Unataka kumaanisha nini sasa hasa?kwamba serikali inahusika?
Hapani. Ninachosema ni kuwa hakuna nchi yoyote ile duniani itakayoruhusu vyombo vya kijasusi vya nchi nyingine vije viichunguze mifumo ya ulinzi na usalama wa nchi yao.
 
Back
Top Bottom