Uhuru wa wachunguzi huru

Uhuru wa wachunguzi huru

..ni jambo la kawaida mikasa inapomkuta mtu MAARUFU ukilinganisha na wananchi wa kawaida

..kwa mfano msiba wa KANUMBA ulipewa coverage kubwa zaidi kuliko msiba wa MV BUKOBA ambapo wananchi 600+ walipoteza maisha.
Navyofahamu mimi kwa muumba hakuna mkubwa na mdogo, ndio maana wote tunasubiri tufukiwe futi sita kwenda chini.
 
Tokea Mh. Lissu anusurike kwenye shambulio dhidi ya uhai wake siku ashara na kitu zilizopita, kumekuwepo na sauti kadhaa zinazodai au zinazotaka tukio hilo lichunguzwe na wachunguzi 'huru' kutoka nje ya nchi.

Sababu yake kubwa ni kwamba vyombo vya ndani [ya nchi] vya usalama haviko huru kuweza kufanya uchunguzi huo kwa sababu vyenyewe ndivyo vinavyoshukiwa kupanga na kutekeleza jaribio hilo ili kutimiza matakwa ya mtu au watu wa huko serikalini na kwenye CCM.

Hisia hizo [za kuishuku na kuituhumu] nazielewa. Hivyo watu wanaotaka kuona wachunguzi huru wakichunguza nao nawaelewa.

Ila, kuna vitu vinanitatiza kidogo kuhusu huo u huru wa hao wachunguzi na utayari wa kambi ya Lissu na kambi ya serikali kuyakubali matokeo ya huo uchunguzi wao endapo utatokea.

La kwanza, ni nani atayeingia gharama za hao wachunguzi?

Tuseme CHADEMA na wafadhili wao ndiyo wataingia hizo gharama.

Kama hivyo ndo itavyokuwa, je, hao wachunguzi watakuwa huru kiasi gani ilhali wanalipwa na upande wa mnusurika wa jaribio?

CHADEMA kweli inaweza kuwalipa hao wachunguzi huru halafu hao wachunguzi watoe uchunguzi ambao ni kinyume na madai ya CHADEMA [kwamba serikali kupitia vyombo vyake vya usalama ndiye mhusika]? Kama wataletwa na CHADEMA maana yake ni kwamba wao ni waajiriwa wa hicho chama. Akili yangu haioni ni jinsi gani hao wachunguzi huru wanaweza kutoa matokeo yaliyo kinyume na hisia za watu waliowaajiri.

Je, serikali nayo ipo tayari kweli kuyakubali matokeo ya hao wachunguzi huru ambao huenda wakalipwa na hicho chama pinzani?

Na vipi kwa mfano serikali ikubali ujio wa hao wachunguzi na iingie gharama kwa kazi watayoifanya, je, CHADEMA ipo tayari kuyapokea na kuyakubali matokeo ya huo uchunguzi hata kama yakiwa tofauti na vile wao wadhaniavyo?

Kumbuka, kama serikali ndiyo itayoingia gharama za hao watu maana yake ni kwamba watakuwa wanaitumikia serikali iliyopo madarakani ambayo ni ya CCM.

Kwa mtaji huo hao wachunguzi huru watakuwa wapo huru kiasi gani?

Hili suala ni gumu kwa kweli. Kila ninapowaza na kuwazua sipati majibu.

Sijui nyie wadau mnalionaje hilo suala.

Jumapili njema.
Mkuu mbona USÀ kuna watu wengi wenye waledi wa hali ya juu sana na nchi hiyo imeendeleà sana,sasa wewe imekuwaje hata kucopy na kupaste ushiñdwe? Chadema nini mpaka ilipie gharama za uchunguzi? Au na wewe ni miongoni mwa wale watanzania wachache na serikali yao wanaoamini mtu kàmà si mwanaçcm basi si mtanzania?
 
Mkuu mbona USÀ kuna watu wengi wenye waledi wa hali ya juu sana na nchi hiyo imeendeleà sana,sasa wewe imekuwaje hata kucopy na kupaste ushiñdwe? Chadema nini mpaka ilipie gharama za uchunguzi? Au na wewe ni miongoni mwa wale watanzania wachache na serikali yao wanaoamini mtu kàmà si mwanaçcm basi si mtanzania?

Nyie watu bana.

Hivi kweli mnadhani hao wachunguzi huru watakuja tu nchini bila gharama yoyote?

Kwamba watapanda ndege bure.

Watafikia hotelini na kukaa bure.

Watakula bure.

Na watafanya kazi asubuhi mpaka jioni bure tu?

Halafu wakimaliza kazi watapanda ndege na kurudi kwao bure tu?
 
Kwa hiyo kama lissu na Dereva wake wangeuwawa pale ndo ingekuwa basi tena kwà mujibu wa akili yako? Kuna akili za ajabu dunia hii du

The situation at hand is not a hypothetical one.

Lissu and his driver are not dead.

So no need to hypothesize with what 'ifs'.
 
Navyofahamu mimi kwa muumba hakuna mkubwa na mdogo, ndio maana wote tunasubiri tufukiwe futi sita kwenda chini.


..Ni kweli 100%.

..lakini watu wengi zaidi wanamjua TL kuliko wale wahanga waliokuwa wakiuawa mpaka wakafika 40++.

..labda nikuulize: Je unaweza kutaja majina matatu ya wahanga wa Kibiti na shughuli walizokuwa wakifanya? Unaweza kutoa jibu bila kutafuta kwenye mtandao?

..Sasa jiulize ni Watanzania wangapi wanamfahamu TL pamoja na harakati zake.

..Lakini vilevile inawezekana kwamba wakaazi wa Kibiti wangekuwa na access ya JF kama tuliyonayo sisi huenda wangekuwa na malalamiko na kilio kama hiki tulichokuwa nacho kuhusu utendaji wa vyombo vyetu vya uchunguzi.

..Naamini ukifuata mtiririko huo utaelewa kwanini kumekuwa na taharuki kubwa kuhusu shambulizi la TL kuliko ilivyokuwa wakati wa mauaji ya Kibiti.
 
What benefits they get after spending their budget for this investigation?
Kwani wanavyowasaidiaga chanjo ya mabusha huwa wananufaika na nini?

Labda hujui tu bajetibya Tanzania inachangiwa na wazungu kila mwaka kwa zaidi ya 50%
 
Kuna mtu kapost mitandaoni anashangaa kwamba Kibiti wameuliwa watu zaidi ya 40 lakini hatukusikia habari za wapelelezi wa kimataifa kuja kuwatafuta wauaji!!.

Wakati wanauliwa wale wananchi wasio na hatia humu mitandaoni kulijaa kejeli nyingi za ajabu, tena nyingine kutoka kwa hawa ambao wanataka wapelelezi wa kimataifa waje kufanya uchunguzi wa jaribio la mauaji.

Yaani mauaji ya watu zaidi ya 40 hayakustahili kufanyiwa uchunguzi wa kimataifa, lakini jaribio moja tu ndilo muhimu kwa sasa kwa taifa letu!!.

Mungu na anisamehe kama nimemkwaza mtu yoyote yule, ni katika kujaribu kuchangia mawazo yangu katika jumapili ya leo.
Mungu huwa hana muda na watu wajinga kama wewe.

Ungejiuliza kwanza ni kwa nini wengine wakifa wanaitwa marehemu na wengine wanaitwa hayati.

Hoja za kipuuzi kama hizi hata last born wangu wa Nursery school anaweza kukujibu. Inshort wewe ni mjinga.
 
Kwani wachunguzi hawaruhusiwi kwenda kuwahoji wahusika huko Nairobi? Yani hii sababu wanayotoa ni ya kizwazwa.
Mwakyembe na wahuni wenzake wa kamati ya Richmond walisafiri mpaka Marekani kukusanya ushahidi, lakini shahidi muhimu/ mtuhumiwa alikuwa umbali wa mita 200 tu kutoka ofisi za Dar esbsalaam na hawakwenda kumuhoji wala hawakumuita.

Labda wewe ni mgeni Tanzania.
 
Hakuna lishindikanalo chini ya jua.
Kama ni mahakamani tayari nakufunga! ......logic and mantic is very important in reasoning,unajicommit kuwa hujui wakati mwanzo ulishaconclude!
Kumbe hata hayo ya gharama hayawezi kushindikana chini ya jua hili!

Kuna aliyesema gharama ni kikwazo?

Kwani kikwazo ndiyo hushindikana chini ya jua?

 
..Ni kweli 100%.

..lakini watu wengi zaidi wanamjua TL kuliko wale wahanga waliokuwa wakiuawa mpaka wakafika 40++.

..labda nikuulize: Je unaweza kutaja majina matatu ya wahanga wa Kibiti na shughuli walizokuwa wakifanya? Unaweza kutoa jibu bila kutafuta kwenye mtandao?

..Sasa jiulize ni Watanzania wangapi wanamfahamu TL pamoja na harakati zake.

..Lakini vilevile inawezekana kwamba wakaazi wa Kibiti wangekuwa na access ya JF kama tuliyonayo sisi huenda wangekuwa na malalamiko na kilio kama hiki tulichokuwa nacho kuhusu utendaji wa vyombo vyetu vya uchunguzi.

..Naamini ukifuata mtiririko huo utaelewa kwanini kumekuwa na taharuki kubwa kuhusu shambulizi la TL kuliko ilivyokuwa wakati wa mauaji ya Kibiti.
Naona unazunguka tu na kupoteza muda wako bure kwa watu wasiojielewa.

Kwa Mungu binadamu wote tunaweza tukawa sawa lakini duniani Tundu Lisu ni bora kuliko watu 100.

Hili Wairael wameliweka wazi kabisa thamani yao kule kwao, ukiuwa Muisrael mmoja ni sawa na Waparestina wangapi.

Ni wanafki peke yake ndio wanaweza kuhoji ni kwa nini Nyerere anapewa heshimu zaidi ya wengine, ni lazima watu wajuwe kuna majina hapa duniani ni Brand.

Usidhani umfanyie tukio Mzee Mengi response yake itakuwa sawa na mfanyabiashara mwengine, hapo mtakuwa mnajidanganya.
 
Nakubaliana na hoja za Nyani Ngabu.

Pia hebu fikirieni:

Vyombo vya kijasusi vya Marekani na/au Uingereza vije Tanzania kuchunguza kama vyombo vya dola vya TZ (polisi, usalama wa taifa, n.k.) walihusika na shambulizi la Lissu? Are you guys nuts?

Ni nchi gani duniani itaruhusu vyombo vya kijasusi vya taifa jingine waje wapeleleze mfumo wao wa ulinzi na usalama?

Halafu unawasikia viongozi wa juu kabisa wa CDM, ambao wanawania kuja kuiongoza TZ siku moja, wanaishauri serikali iruhusu huu ujinga.

CDM, you guys are not ready for prime time. Subirini miaka kadhaa ili mkomae kisiasa. Pathetic!
Mkuu una umri gàni?
 
Back
Top Bottom