Uhuru siyo kama marais wengine Afrika Mashariki, oneni

Uhuru siyo kama marais wengine Afrika Mashariki, oneni

Eti magari manne?? Jana huo msafara wa Kenyata umesababisha wamama wa watu wachelewe nyumbani ...hapakuwa na gari la kwenda Tengeru,Ngulelo na kuendelea ..barabara ya kwenda kijenge na Moshono zote zimefungwa. Nikiwa kama muhanga wa tukio la jana sioni kama ana sifa zote hizi alizotajiwa kwa kweli. Hata kama ni magari ya Tanzania yalimpokea lakini sio kuleta foleni kiasi kile cha jana. Inalindwa roho moja wakati wengine 100 hawajui hata watalala wapi..

Viongozi wenu kwa kiherehere chao ndio waliamua kufunga barabara Arusha wala sio Kenyatta. Yeye alikuwa ni mgeni na wenyeji ndio waliamua kufunga barabara sasa Kenyatta unamlaumu kwa lipi hapa?. Yeye hata kule Nairobi hatembei na msururu mrefu hata kidogo. Ulisikia kisa yeye na escort wake walipozuiliwa na traffic polisi Nairobi akafungua dirisha kumuomba traffic police awaruhusu wapite? Hapendi makuu huyu jamaa.

Tiba
 
Imekuwa ni tabia ya Uhuru Kenyatta rais wa Kenya kuishi maisha ambayo sio yaliozoeleka kwa viongozi wengine wa Africa..kwa sasa ni rais anaetembea na msafara mdogo sana kuliko wote E Africa pmoja na tishio la ugaidi kenya. Na wiki mbili zilizopita amekutwa akiwa na gari Moja na security details wanne akielekea hotelini kwenye kikao cha kifamilia, na alipo kuwa kwene trafic lights alimsalimia police, na watu wengine.

KIBOKO ni hii.
Jana amekuja tanzania kupitia Boda ya Namanga arusha na magari yasiyozidi nane (mengine ni ya serikali ya tanzania yaliyoenda kumpokea) na amesema baada ya kufungua bunge la Africa mashariki atarudi kenya kupitia boda ya Taveta ipo kilimanjaro rombo.

Ikumbukwe majuzi juzi rais huyu amejiondolea mshahara wake zaidi ya 20% na amewataka viongozi wa nyadhifa serikalini wapunguziwe 20%.

Ikumbukwe huyu rais hapendi kuzurura nchi za watu anaamini uchumi wa kenya sio yeye peke yake anaweza kuuinua ndio maana kadeligate power kwa waziri wa mashauriano ya kigeni..ana nguvu sana.

Lipo la kujifunza. Kenyatta sio limbukeni pengine ni kwa sababu ni mtoto wa aliekuwa rais wa kenya. Sijui but the guy ni gentleman hata uwezo wa kumanage diplomasia za nchi hizi masikini Tanzania, uganda, rwanda,burundi na kongo anaweza. Hana adui wa kudumu, hana rafiki wa kudumu. Ana maslahi ya kudumu.

You know why? ameelimika yeyote aliye elimika ndivyo anavyo ishi na kutumikia watu wake.
 

Kamanda acha uongo kuhusu msafara. Jana nimeshuhudia CITIZEN TV ya Kenya wakionyesha msafara wa Kenyatta toka Kenya kuja Tanzania ukiwa na Magari zaidi ya 40 yametapakaa barabara nzima.

Kibaya zaidi alisindikizwa na Makamo wake yaani Ruto hadi mpakani na magari lukuki. Jana Wakenya wamepiga mayowe wakisema kwa nini asingekuja kwa ndege. Angalia hapa Kamanda

President Kenyatta's Road Trip to Arusha - YouTube

Mkuu, kwenye ratiba yake alipashwa apite Namanga kukagua ujenzi wa jengo jipya la Customs. Sasa angesafiri kwa ndege huo ukaguzi angeufanya saa ngapi? Waliokuwa wanalaumu wala hawakujua ratiba yake ikoje.

Tiba
 
Haya wazee uhuru kenyata ndio huyo anaondoka sasa.
 
A plane was about to crash and
there were only four parachutes on
the plane. Meanwhile there were
five people on it. The first person,
Lionel Messi, said, "I'm the world's
best footballer right now, I cant die
now!"
So he took one of the parachutes
and left. The second person, Bill
Gates, said, "I'm the richest man on
Earth, I can't die now, I'm needed in
the world!"
So he took the second parachute
and left. The third was the
Tanzanian President and he said,
"I'm the smartest President in the
world, so I cant die now, my people
still need me!"
So he took one and left.
Then it was left with the Pope and a
little school girl. The Pope said to
the little girl, "Take the last one, I'll
sacrifice my life for you."
The little girl replied, "No need for
that, There are two parachutes left."
The pope asked her, "How come?"
The little girl replied, "The
Tanzanian President took my school
bag." Ndio Huyu wa kwetu???


Nimedondosha kikombe changu cha gahawa!!, mh!!! amaa kweli ngoma bado mbichi mpaka ikauke ije ipigwe tutakuwa hoi
 
Mkuu nipo Arusha, magari yenye presidency identification nimeyaona nane so far. Mkuu usifuatilie propaganda. Mkuu wa arusha alikuja na msafara mkubwa kuliko wa kenyata

Citizen ni tv ya Kenya na wametangaza kuwa Uhuru ameenda Arusha tz na msafara wa magari 40 sasa wewe juha wa mtaa Ufipa unakataa nini?
 
vijana wa ufipa simulipeleka jeshi la ardhini kumnadi Odinga!!! na kulikoni leo hii huyu mnamuona tunu wakati mnapiga vita Ridh1 kugombea charinze? au kenya mtoto wa rais kugombea ruksa ila tanzania hamtaki! hili ndo linafanya muonekane kwa jamii kuwa wala hamjui munafanya nini na tatizo ni viroba ambavyo babu yenu anaviabudu.

Huyu ni mtoto wa rais,amegombea babaye amesha staafu,je ritz babaye si bado yuko madarakani fara wewe
 
A circus.

Kasharudisha ile ardhi yote baba yake aliyopora Kenya?

Kama hajarudisha hayo mengine ni sarakasi ndogondogo tu.
 
Usichofahamu ni kwamba Kenya ilishajitangaza nje kwa sababu hiyo nchi ni jimbo (state) tu la Uingereza na Marekani. Na hata Tanzania ilipoweka vikwazo kwa South Afrika wakati Makaburu wanatawala huku, wakiendesha ubaguzi wa rangi kwa ndugu zetu, KENYA ilikuwa inaendelea kama kazi kufanya biashara na kufyata mkia mbele ya Makaburu. Hata walipoingia Somali walitumwa na Baba zao hao. Samahani kwa neno hili lakini ni nukuu toka kwa Idd Amin Dada "Mabwana wa KENYA ni Amerika na Uingereza, kila wanachoambiwa na hao hufanya"

Matunda ya Tanzania kujitangaza Duniani yamezaa matunda, mwaka jana 2013 kwa mara ya kwanza tuliongoza kwa kutembelewa na watalii wengi kuliko nchi yeyote ya Afrika mashariki. Huko nyuma Kenya ilikuwa ni kinara kwa kila mwaka. Hongera uongezi wa Rais Kikwete. Sijachimba ya uhuru wa habari! We acha tu. Itapofika wakati nitatoa mada maalim kuhusu mafanikio ya mbinu za serikali ya JK.

kIJANA FUATILIA HISTORIA UTAELEWA, KWANINI TANZANIA HAIKUFAHAMIKA NJE YA NCHI KAMA KENYA. HATUNA CHA KUNGOJA WAKATI NI HUU TUTATUMIA MBINU ZOTE KUHAKIKISHA KUWA TANZANIA INAKUWA NAMBARI ONE KATIIKA AFRIIKA MASHARIKI. BIG RESULT NOW! Mkereketwa.

kwa upuuz huo hupati hata uongoz wa nyumba 10 kama akiteua rais kwan mwenyewe anajua unamfagilia ujinga
 
Vp na suala la wabunge wa kenya kulipwa mshahara zaidi kuliko wabunge wengine afrika wakati wakenya wengi wanaishi kifukara, au hili si tatizo?
 
umesahau kuwa uhuru ameongoza kundi lake la mungiki kufanya uhalifu kenyya kwa zaidi ya miaka 10?
 
Imekuwa ni tabia ya Uhuru Kenyatta rais wa Kenya kuishi maisha ambayo sio yaliozoeleka kwa viongozi wengine wa Africa..kwa sasa ni rais anaetembea na msafara mdogo sana kuliko wote E Africa pmoja na tishio la ugaidi kenya. Na wiki mbili zilizopita amekutwa akiwa na gari Moja na security details wanne akielekea hotelini kwenye kikao cha kifamilia, na alipo kuwa kwene trafic lights alimsalimia police, na watu wengine.

KIBOKO ni hii.
Jana amekuja tanzania kupitia Boda ya Namanga arusha na magari yasiyozidi nane (mengine ni ya serikali ya tanzania yaliyoenda kumpokea) na amesema baada ya kufungua bunge la Africa mashariki atarudi kenya kupitia boda ya Taveta ipo kilimanjaro rombo.

Ikumbukwe majuzi juzi rais huyu amejiondolea mshahara wake zaidi ya 20% na amewataka viongozi wa nyadhifa serikalini wapunguziwe 20%.

Ikumbukwe huyu rais hapendi kuzurura nchi za watu anaamini uchumi wa kenya sio yeye peke yake anaweza kuuinua ndio maana kadeligate power kwa waziri wa mashauriano ya kigeni..ana nguvu sana.

Lipo la kujifunza. Kenyatta sio limbukeni pengine ni kwa sababu ni mtoto wa aliekuwa rais wa kenya. Sijui but the guy ni gentleman hata uwezo wa kumanage diplomasia za nchi hizi masikini Tanzania, uganda, rwanda,burundi na kongo anaweza. Hana adui wa kudumu, hana rafiki wa kudumu. Ana maslahi ya kudumu.



kumanege ndio nini mkuu
 
Mbona tayari ni mzigo?
Kupeleka vimada ulaya na marekani
Kuteua baraza kubwa
Kushirikiana na mafisadi kuifisidi nchi
Kwenda kurekebisha afya yake mara kwa mara.......HUU NI MZIGO MKUBWA SANA KWA WANYONGE

cc dk w slaa na f.mbowe
 
Fanyeni kazi vijana kuleni kwa jasho lenu ustegemee porojo za jf ndio zitasomesha watoto weny hivyo ni vihela vya kununulia vitumbua na poda ya siku moja tu



tumia makalio kukalia sio kufikilia
 
Viongozi wenu kwa kiherehere chao ndio waliamua kufunga barabara Arusha wala sio Kenyatta. Yeye alikuwa ni mgeni na wenyeji ndio waliamua kufunga barabara sasa Kenyatta unamlaumu kwa lipi hapa?. Yeye hata kule Nairobi hatembei na msururu mrefu hata kidogo. Ulisikia kisa yeye na escort wake walipozuiliwa na traffic polisi Nairobi akafungua dirisha kumuomba traffic police awaruhusu wapite? Hapendi makuu huyu jamaa.

Tiba
Kwa taarifa hizi utasema unalala nje maanake haupitwi na jambo

 
Robo ya uchumi wa Kenya unashikiliwa na familia yake.Maeneo mazuri ya kilimo ya kikuyu kwa kiasi kikubwa sana yanamilikiwa na familia yake.
Alipotakiwa na ICC kutaja utajiri wake na jinsi alivyoupata alikataaa katakata kuutaja.
Hivyo kupunguza asilimia 20 ya mshahara wake sio issue kubwa.
Ningemsifia sana kama angetoa robo ya ardhi anayomiliki kwa watu masikini ili nao waweze kuwa na maeneo.
 
Mleta uzi usitake kunikumbushia mateso ya ujio wa huyo Raisi chekibobu wa kenya jana! Aliniweka barabarani masaa manne kidogo niachike na mke wangu! hakuna cha kusifia ujinga hapo kwenye ujio wake wa magari hapa Arusha!!
 
Back
Top Bottom