Uhuru na Haki Haiwezi ikaleta Amani na Maendeleo ya Watu; Amani na Maendeleo ya Watu ni Tunda la Uhuru na Usawa

The Giantist

JF-Expert Member
Dec 12, 2018
214
86
Na: McWenceslaus
01/10/2020.

Habarini za muda ndugu wanabodi wenzangu! Poleni kwa kazi na majukumu mengi ya siku. Baada ya kukaa kwa muda hivi, tukiwa tunatathiminu hali ya kampeni tangu mwanzo hata hivi leo, zikiwa zimesalia siku 27 kufika siku ya kufanya maamuzi ya kamchagua Rais, wabunge na madiwani. Kila mtu atakuwa ashapata kuona uelekeo sahihi wa nani ni Rais ajaye wa Tanzania. Na bila shaka asilimia kubwa ya watanzania wengi, wanauhakika na ushindi wa kishindo wa Rais Dkt. John Magufuli dhidi ya wagombea wengine kwa nafasi ya Rais Tanzania, msioamini subirini siku inakuja nanyi mtaamini. Ni kama ilivyokuwa kwa Thomaso mmoja wa mitume wa Yesu Kristo, ambaye hakuamini mwanzo lakini mwishowe aliamini. Leo ninakuja kuwa fahamisha Siri ya kauli ya HAKI na UHURU kama ambavyo imetumiwa na CHADEMA katika kampeni zake; na ukweli kuhusu UHURU na USAWA, katika kuleta AMANI na Maendeleo ya Watu. Nikuache uendelee....

Uhuru + usawa = Amani

Haki bila usawa ni sawa na mwili uliokosa chakula na matunzo, ni lazima mifumo yake ya mwili ifarakane na mwishowe ijifie yenyewe.

Na kwamba, haki ilikuwepo hapa nchini hata kabla ya uhuru. Moja ya sababu ya msingi ya kudai uhuru katika miaka ya 1960, ilikuwa ni kupigania haki na usawa katika mambo ya kisiasa, kiuchumi na kijamii, na hatimaye kuleta amani ndani ya taifa. Na hilo lilifanikiwa mnamo 09 disemba, 1961 ambapo watanzania walitambuliwa katika usawa na huru, hata hivi leo.

Leo hii tumeanza kusikia habari ya kuwa kuna kundi la watu wanaendelea kusikika humu nchini, wakisema "Amani ni tunda la Haki!" Huu ni uongo wa mchana kweupe peee. Hivyo basi, ni lazima tukawaambie wananchi kuwa, pasipo na usawa hakutakuwepo na amani. Ili kukanusha uongo huo. Tuseme kwa mfano, Paka anayo haki ya kumfukuza na kumtafuna panya; ni katika hali hiyo Panya ameshaonekana ni mnyonge mbele ya Paka, ni kwa sababu eti Paka anaitumia haki yake hiyo! Na kwa kusema ukweli, Panya huyu hawezi kufanya lolote la kumzuia Paka asitekeleze haki yake hiyo. Ni kwa sababu, nguvu hiyo ataitoa wapi, yeye ni mdogo paka ni mkubwa.

Hivyo katika jamii ya watu wenye hali tofauti ya kiuchumi, kiafya, kisiasa, rangi, itikadi n.k mfano wa Paka na Panya huyu, ni lazima msukumo mkubwa uwepo kwenye sera ya USAWA kuliko HAKI, kwa maana HAKI kwa asili huambatana na UHURU zaidi kuliko USAWA. Maana Palipo na HAKI pana UHURU; Na kwa sababu hiyo, ndiyo ilipelekea ndani ya azimio la Arusha 1967 chini ya chama cha TANU na baadaye CCM. Chama kilihimiza na kusisitiza kuwa ujamaa na kujitegemea ni siasa yenye lengo la kujenga jamii ya watu walio SAWA na HURU. Msukumo huo uliwekwa kwa sababu ya kutambua kuwa haki alikuwa nayo mkoloni ya kumnyonya mwafrika, lakini hakukuwepo na usawa wa kutambua kwamba mwafrika ni mtu ambaye anastahili heshima ya kutambuliwa utu wake. Na ndio maana palipo UHURU na USAWA ni lazima pawepo na AMANI, lakini palipo na haki na uhuru amani haiwezi kuwepo kabisa, ni sawa na yule Panya kwa Paka. Amani hiyo ipo kwa Paka pekee, lakini ni nani atakayeweza kusema kwamba Panya yule anayo amani, ukweli hayupo mtu huyo. Kwa Panya kukosa Amani, kwa sababu ya kuwepo kwa haki yake ya kukimbizwa na kutafunwa na Paka, inaifanya Amani ikosetafasiri nzuri kwa hakika.

Kwa kumalizia; katika kampeni za mwaka huu kuna ushindani baridi baina ya siasa ya ujamaa na siasa ya kibepari. Na ndio kwa sababu hiyo, Mgombea Lissu kupitia CHADEMA, amekuja na kauli mbiu ya uhuru na haki, na anajificha kwenye kivuli cha maendeleo ya watu kwa lengo la kuficha dhamiri yake ya kuukaribisha ubepari ndani ya Tanzania. Msukumo katika siasa za kibepari upo katika HAKI maana yake ni hivi, mfanyabiashara mkubwa na mfanyabiashara mdogo wote ni wafanyabiashara hawa hivyo watalipa kodi sawa kwa jina la biashara hiyo, hiyo ni HAKI sawa kwa wote na sio USAWA kwa wote. Katika ujamaa, msukumo mkubwa upo katika USAWA kwa wote, hii maana yake ni kwamba kila mfanyabiashara atalipa kodi kwa kadiri ya mapato yake yatokanayo na biashara yake... Huu usawa unafanya kuwepo kwa AMANI kwani kila mtu atachangia kwa kadiri ya uwezo wake. Na kila mtu atamuona mwenzake kuwa ni sawa kama alivyo yeye, vivyo hivyo kwa makundi na jumuiya zingine. USAWA ni mbegu bora ya kuleta AMANI ya kweli kwa wote.

Na katika kuendeleza nia hiyo ya dhati ya kudumisha UHURU pamoja na USAWA kwa ajili ya kuimarisha AMANI ya nchi yetu, serikali chini ya CCM na uongozi imara wa viongozi wa chama pamoja na Mwenyekiti wa chama na Rais wa nchi Dkt. John P. Magufuli; imeweza kuimarisha usawa kwa makundi yote na watu wa hali zote kwa kuwapatia haki za muhimu za huduma ya jamii. Ikiwa ni pamoja na elimu bure, huduma za afya nafuu na kuimarisha huduma ya mfuko wa TASAF, upatikanaji wa maji katika meneo yote ya mijini na vijijini na maeneo yenye viwanda na yasiyokuwa na viwanda n.k. Hivyo imeweza kuendeleza hali ya AMANI nchini hata sasa.

Uhuru + usawa = Amani
#chaguaCCM
#chaguaUjamaanaKujitegemea
#chaguaUsawanaUhuru
#chaguaMagufuli

Kazi inaendelea 2020-2025

Sauti ya Mdodomia.

01/10/2020
 

Attachments

  • IMG-20200922-WA0038.jpg
    IMG-20200922-WA0038.jpg
    43.1 KB · Views: 1
Ujamaa ulisha fariki kitambo tupo kwenye Ubepari sasa ,na sijui umetumia kanuni gani kuthibitisha Hoja yako.Yani Haki ikosekane na utarajie Maendeleo !? How !?

Sana ni unafanya kampeni tu ...
 
Na: McWenceslaus
01/10/2020.

Habarini za muda ndugu wanabodi wenzangu! Poleni kwa kazi na majukumu mengi ya siku. Baada ya kukaa kwa muda hivi, tukiwa tunatathiminu hali ya kampeni tangu mwanzo hata hivi leo, zikiwa zimesalia siku 27 kufika siku ya kufanya maamuzi ya kamchagua Rais, wabunge na madiwani. Kila mtu atakuwa ashapata kuona uelekeo sahihi wa nani ni Rais ajaye wa Tanzania. Na bila shaka asilimia kubwa ya watanzania wengi, wanauhakika na ushindi wa kishindo wa Rais Dkt. John Magufuli dhidi ya wagombea wengine kwa nafasi ya Rais Tanzania, msioamini subirini siku inakuja nanyi mtaamini. Ni kama ilivyokuwa kwa Thomaso mmoja wa mitume wa Yesu Kristo, ambaye hakuamini mwanzo lakini mwishowe aliamini. Leo ninakuja kuwa fahamisha Siri ya kauli ya HAKI na UHURU kama ambavyo imetumiwa na CHADEMA katika kampeni zake; na ukweli kuhusu UHURU na USAWA, katika kuleta AMANI na Maendeleo ya Watu. Nikuache uendelee....

Uhuru + usawa = Amani

Haki bila usawa ni sawa na mwili uliokosa chakula na matunzo, ni lazima mifumo yake ya mwili ifarakane na mwishowe ijifie yenyewe.

Na kwamba, haki ilikuwepo hapa nchini hata kabla ya uhuru. Moja ya sababu ya msingi ya kudai uhuru katika miaka ya 1960, ilikuwa ni kupigania haki na usawa katika mambo ya kisiasa, kiuchumi na kijamii, na hatimaye kuleta amani ndani ya taifa. Na hilo lilifanikiwa mnamo 09 disemba, 1961 ambapo watanzania walitambuliwa katika usawa na huru, hata hivi leo.

Leo hii tumeanza kusikia habari ya kuwa kuna kundi la watu wanaendelea kusikika humu nchini, wakisema "Amani ni tunda la Haki!" Huu ni uongo wa mchana kweupe peee. Hivyo basi, ni lazima tukawaambie wananchi kuwa, pasipo na usawa hakutakuwepo na amani. Ili kukanusha uongo huo. Tuseme kwa mfano, Paka anayo haki ya kumfukuza na kumtafuna panya; ni katika hali hiyo Panya ameshaonekana ni mnyonge mbele ya Paka, ni kwa sababu eti Paka anaitumia haki yake hiyo! Na kwa kusema ukweli, Panya huyu hawezi kufanya lolote la kumzuia Paka asitekeleze haki yake hiyo. Ni kwa sababu, nguvu hiyo ataitoa wapi, yeye ni mdogo paka ni mkubwa.

Hivyo katika jamii ya watu wenye hali tofauti ya kiuchumi, kiafya, kisiasa, rangi, itikadi n.k mfano wa Paka na Panya huyu, ni lazima msukumo mkubwa uwepo kwenye sera ya USAWA kuliko HAKI, kwa maana HAKI kwa asili huambatana na UHURU zaidi kuliko USAWA. Maana Palipo na HAKI pana UHURU; Na kwa sababu hiyo, ndiyo ilipelekea ndani ya azimio la Arusha 1967 chini ya chama cha TANU na baadaye CCM. Chama kilihimiza na kusisitiza kuwa ujamaa na kujitegemea ni siasa yenye lengo la kujenga jamii ya watu walio SAWA na HURU. Msukumo huo uliwekwa kwa sababu ya kutambua kuwa haki alikuwa nayo mkoloni ya kumnyonya mwafrika, lakini hakukuwepo na usawa wa kutambua kwamba mwafrika ni mtu ambaye anastahili heshima ya kutambuliwa utu wake. Na ndio maana palipo UHURU na USAWA ni lazima pawepo na AMANI, lakini palipo na haki na uhuru amani haiwezi kuwepo kabisa, ni sawa na yule Panya kwa Paka. Amani hiyo ipo kwa Paka pekee, lakini ni nani atakayeweza kusema kwamba Panya yule anayo amani, ukweli hayupo mtu huyo. Kwa Panya kukosa Amani, kwa sababu ya kuwepo kwa haki yake ya kukimbizwa na kutafunwa na Paka, inaifanya Amani ikosetafasiri nzuri kwa hakika.

Kwa kumalizia; katika kampeni za mwaka huu kuna ushindani baridi baina ya siasa ya ujamaa na siasa ya kibepari. Na ndio kwa sababu hiyo, Mgombea Lissu kupitia CHADEMA, amekuja na kauli mbiu ya uhuru na haki, na anajificha kwenye kivuli cha maendeleo ya watu kwa lengo la kuficha dhamiri yake ya kuukaribisha ubepari ndani ya Tanzania. Msukumo katika siasa za kibepari upo katika HAKI maana yake ni hivi, mfanyabiashara mkubwa na mfanyabiashara mdogo wote ni wafanyabiashara hawa hivyo watalipa kodi sawa kwa jina la biashara hiyo, hiyo ni HAKI sawa kwa wote na sio USAWA kwa wote. Katika ujamaa, msukumo mkubwa upo katika USAWA kwa wote, hii maana yake ni kwamba kila mfanyabiashara atalipa kodi kwa kadiri ya mapato yake yatokanayo na biashara yake... Huu usawa unafanya kuwepo kwa AMANI kwani kila mtu atachangia kwa kadiri ya uwezo wake. Na kila mtu atamuona mwenzake kuwa ni sawa kama alivyo yeye, vivyo hivyo kwa makundi na jumuiya zingine. USAWA ni mbegu bora ya kuleta AMANI ya kweli kwa wote.

Na katika kuendeleza nia hiyo ya dhati ya kudumisha UHURU pamoja na USAWA kwa ajili ya kuimarisha AMANI ya nchi yetu, serikali chini ya CCM na uongozi imara wa viongozi wa chama pamoja na Mwenyekiti wa chama na Rais wa nchi Dkt. John P. Magufuli; imeweza kuimarisha usawa kwa makundi yote na watu wa hali zote kwa kuwapatia haki za muhimu za huduma ya jamii. Ikiwa ni pamoja na elimu bure, huduma za afya nafuu na kuimarisha huduma ya mfuko wa TASAF, upatikanaji wa maji katika meneo yote ya mijini na vijijini na maeneo yenye viwanda na yasiyokuwa na viwanda n.k. Hivyo imeweza kuendeleza hali ya AMANI nchini hata sasa.

Uhuru + usawa = Amani
#chaguaCCM
#chaguaUjamaanaKujitegemea
#chaguaUsawanaUhuru
#chaguaMagufuli

Kazi inaendelea 2020-2025

Sauti ya Mdodomia.

01/10/2020
Jipige kifuan mara tatu kisha sema hivi " Mimj The Giantist ni Mpumbavu kama walivyo wapumbavu wengine"



Yaan Kama Maandiko yanafai Haki kama tunda la Amani


Weee ninani ???mjinga mkubwa... Iko wapi Libya yenye maendeleo?? .
 
Pumba tupu
Vitabu vyenyewe vya dini vinakwambia
AMANI NI TUNDA LA HAKI
Ila wewe Mataga baada ya kupewa buku 7 unakuja kupinga pinga
PNC

Ijapokuwa hujasema vitabu hivyo vya dini ni vya dini gani hasa. Lakini itoshe kusema kuwa katika mtazamo wa kidini, "Tunakuwa na Amani katika Bwana, kwa maana tumehasabiwa haki katika Bwana" huo ni muungano wa Bwana na wanadamu.

Na kwa kuwa mimi naamini kuwa Mungu hafananishwi na kitu ama kiumbe cho chote kile, hivyo si sawa kusema "Tunakuwa na Amani katika Bwana, kwa maana tumehasabiwa usawa katika Bwana." Nafikiri lengo la ujumbe kwa wanadamu usingekuwa sahihi.

Katika mtazamo wa siasa za Dunia, hakuna namna ambayo itajenga Amani na utulivu katika jamii ya watu walio sawa na huru. Kama utakuwa umenisoma vizuri, ungefahamu namna ambavyo uhuru hauwezi kujitenga na haki. Kanuni za maumbile kwa mujibu misaafu binadamu ni viumbe sawa kwa kuwa vinachimbuko la moja ambaye ni Mungu Baba Muumba. Hivyo kanuni ya usawa ni ya lazima ili tuendelee kuwa na amani kati yetu.
 
Kwa nini CCM hawapendi kabisa kusikia neno HAKI ................!!?
Zero:

Kwa sababu;

Mosi, Haki inahusiana na uhuru. Maana yake ni hivi, ukiwa na huru unaweza ukasema pasipo kusimamiwa wala kuelekezwa nini cha kusema, na hivyo una kuwa na haki ya kusema pasipo kuingiliwa.

Pili, tunafahamu haki ilikuwepo hata wakati wa mkoloni. Hivyo tulitafuta uhuru ili tupate usawa. Kwamba mtu mwafrika atakuwa sawa na mtu mweupe, mtu masikini atakuwa sawa na mtu tajiri. Na hakika palipo na usawa pana amani ya kutosha.
 
Ujamaa ulisha fariki kitambo tupo kwenye Ubepari sasa ,na sijui umetumia kanuni gani kuthibitisha Hoja yako.Yani Haki ikosekane na utarajie Maendeleo !? How !?

Sana ni unafanya kampeni tu ...
Ciril:

Kwanza sio kweli kwamba ujamaa ulikwisha kufariki. Kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya 1977, kwenye ibara yake ya 3(1) na ibara ya 9. Katiba imetamka wazi juu ya ujamaa na kujitegemea, na kwamba ndio njia itakayokuwa kujenga jamii ya watu walio sawa na huru ndani ya nchi.

Hoja yangu inathibitishwa na mfano wa maisha ya Paka na Panya. Paka anayohaki ya kumla Panya, ni kwa sababu anazo nguvu kumzidi Panya, na hivyo Panya hana namna isipokuwa kukubali hali hiyo. Panya anakuwa mnyonge na hivyo Paka anaendelea kuifaidi haki yake hiyo. Katika maisha hayo Panya hawezi kuwa na amani, na kama ndivyo Basi hakuna amani mahali hapo. Maana haki ya Paka imepelekea kukosekana kwa uhuru wa Panya na hivyo kuleta Maendeleo kwa Paka na sio kwa Panya.

Basi kama Paka angeweza kuona kwamba Panya ni sawa na yeye, kwamba inamstahili Panya awe huru kutembea bila hofu ya kuliwa, Basi amani ingekuwepo kwa Panya na kwa Paka vilevile. Hatimaye maendeleo kwa Panya na Paka yangeweza kupatikana.

Uhuru na Usawa ni mbegu ya Amani!
 
Au fuatilia matukio ya kibaguzi yaliyotekelezwa hivi karibuni katika Amerika. Ni kwamba watu weusi si sawa na watu weusi, hivyo kupelekwa kukosekanika kwa amani kwa watu weusi na hasa kuwa na hofu juu ya usalama wa maisha yao. Na kwa sababu hiyo huwezi kusema Amerika Ina amani, eti kwa sababu tu watu weupe wanayo haki dhidi ya watu weusi.

Na kama watu weupe wangejiona kuwa ni sawa na watu weusi, basi kusingekuwa na hofu ya usalama wa maisha kwa watu weusi. Na hivyo kungekuwa na uhuru kamili kwa watu weusi na watu weusi. Na hiyo ndiyo amani kamili.
 
Jipige kifuan mara tatu kisha sema hivi " Mimj The Giantist ni Mpumbavu kama walivyo wapumbavu wengine"



Yaan Kama Maandiko yanafai Haki kama tunda la Amani


Weee ninani ???mjinga mkubwa... Iko wapi Libya yenye maendeleo?? .
Carlos The Jackal:

Nina tatizo la kifua hivyo siwezi kujipiga kifuani... Zaidi naomba unisaidie kwa niaba yangu, ruhusa nimekuwa.

Maandiko matakatifu ni mengi sana, ni vizuri kama ungeniambia ni ya katika uelekeo upi huo utakitifu. Ila kwa kukusaidia tu, katika msaafu wa kikristo. Maandiko yamezungumzia haki kama neema kutoka kwa Mungu, na ambayo tunapata amani katika Mungu. Sasa mimi nazungumza katika muktadha wa siasa za kidunia, ambapo wanadunia ni viumbe sawa wenye chimbuko moja kutoka kwa Mungu muumba, hivyo basi kanuno ya usawa ni yenye kumuhusu binadamu na binadamu mwenzake, ili kutawala amani katika Dunia. Haki ni neema ya Mungu kwa Mwanadamu ili apate amani katika Mungu.

Libya ni kesi tofauti na kichwa cha huu uzi. Lakini kawa faida yako. Kama Gadaffi angetambua kuwa yeye ni sawa na wanaLibya wenzake na kwamba Libya ingeweza kutawala a na Mlibya mwingine pasipo yeye wala kijana wake, Libya ingebaki salama. Lakini kwa kuwa aliamini katika haki, aliona yeye anayo haki ya kuendelea kuiongoza Libya, na ndio mpaka sasa amani imekosekana Libya kwa sababu ya haki.

Ni rahisi sana haki ikawa na ubinafsi kuliko usawa kuwa na ubinfsi. Haki ina mimi kwanza, lakini usawa una yeye kwanza.
 
Tofauti ya usawa na haki ni nini?
Je Tanzania kuna usawa? au kuna haki?
 
Chadema imejipambanua kama chama kinachosimamia sera za kibepari hivyo tegemea katika utawala wake kuona matajiri wakirudi kushika nafasi tena kama watu wenye maamuzi katika jamii zetu.

Uhuru huu watu wa kada ya chini na Kati wanaofaidi kwa sasa utapotea na tutarudi katika minyororo ya manyanyaso ya wenye nacho.

Kwa kutambua agenda hii ya siri hutasikia Chadema ikinadi Sana sera zake ili kuficha uhakisia wake kwa wananchi waje kuwashtukiza tayari wakiwa madarakani.

Baadhi ya wafanyabiashara na mabeberu ndio wanaopush agenda za Chadema ili kurejesha ufalme wao walioupoteza katika awamu hii.

Ewe mwananchi tambua kuwa kuipa kura Chadema ni kukaribisha ubepari
 
Bujibuji:

Ndio, Tanzania ni nchi ya kijamaa kwa mujibu wa katiba ya JMT. Soma ibara ya 3(1) na ibara ya 9, ya katiba ya nchi imeitamka ujamaa na kujitegemea kuwa ndio siasa za nchi, ambayo itatoa muelekeo wa kujenga jamii ya watu walio sawa na uhuru.
Ujamaa ni katiba au ujamaa ni mfumo wa uchumi na utawala?
 
Back
Top Bottom